Je, ni uchawi au saikolojia?

Je, ni uchawi au saikolojia?

Uchawi ni suala la kiimani tu. Shida ni kwamba imani za kijadi zimetengenezewa taswira mbaya na historia ya ukoloni.

Kuamini kwamba damu ya Yesu imekuponya na kwenda kwa mganga hakuna tofauti ukifikiria. Kote ni kutafuta miujiza.

Imani ni kama miwani. Tunaitazama dunia kupitia imani zetu. Kwahiyo kila mtu anoana kwamba imani yake ni halisi.
Je uchawi ni imani?
Na ukiamini kuna miujiza?
 
Hello jamii intelligence 👋

Wakuu hii habari ya uchawi nadhani sio jambo geni
Uchawi ulitajwa kwenye vitabu vya dini hasa hivi maarufu Bible&Qur'an

Kwa bible mfano Kutoka 22:18 inasema:

Usimwache mchawi kuishi
Huu ni ushahidi kua Bible inatambua uchawi



Uchawi umetajwa pia kwenye Qur’an, hasa Al-Baqarah 2:102 ambapo inazungumzia habari ya uchawi na watu kujifunza mambo hayo
Huu nao ni ushahidi Qur'an inatambua habari za uchawi

kwa mantiki hii dhana ya uchawi ni ya kale sana

Huku Africa watu bado wamekumbatia hii imani sana, sijui huko Ulaya ikoje

Utasikia mtu anasema
👇
Mtoto huyu karogwa, sio akili zake.

Hapa tunaona uchawi unatajwa kama kitu ambacho kinaweza kubadilisha hali ya mtu
Alikuwa mzima, ghafla akawa kichaa au mtu asie sawa kama alivyokua kabla

Mtu anaumwa, unaambiwa karogwa

Sasa najiuliza...

Uchawi umetengenezwa au umeundwa kwa kufanya vitu negative tu?

Hakuna namna huo uchawi kama upo unaweza kutumika kwa njia positive?

Yaani tukaamua kutumia akili ya mtu kilaza akawa genius, kama vile inavyoaminika kwamba uchawi unaweza kumbadilisha genius kuwa kilaza?

Kuna hii pia👇

Ooh, wachawi wanapaa usiku...

Kwanini sasa kama hiyo technology ipo tusiitumie kupunguza foleni?

Huo usafiri wa kupaa uwe official sasa

Nyie wachawi wa JF(jokes)
haiwezekani kuwa hivi yaani huu uchawi ukawa na tija?

Hivi uchawi unafanya kazi kweli au ni mambo ya nadharia tu?

Niliwahi kua na matatizo ya kupata maumivu ya kicwa nakizunguzungu

Basi kuna mtu akamwambia mama:

Huyu ShesRise_1 amelogwa asifanye vizuri shuleni na si haba shuleni nilikua najitahidi kwahiyo huyo mama akamuambia mama angu huenda nimelogwa ili nirudi nyuma kimasomo🤔

Heh! 🤔

Nikastuka

Nikawaza, haya yatakuwa mambo gani?

Basi nikaanza kufanyiwa zile zinazoitwa tiba za Kisunna, visomo na mambo mengine

Ajabu ni kwamba kuanzia pale ndiyo kwanza nikaanza kupata maruerue.

Usiku naogopa kulala mwenyewe.

Naota ndoto za ajabu, heh... tafrani mtindo mmoja

Kumbe ile issue ya kuanza kuota mauza uza ni kwa sababu
ya saikolojia bana
Yaani saikolojia kwa maana baada ya kusikia nimelogwa na kupelekwa kwenye visomo

Ndiyo ubongo ukaanza kuniundia mapicha picha

So nilivyoambiwa tu vile, akili yangu na ubongo wangu vikaanza kujishughulisha na hayo mambo

Mara nione hiki...

Mara nisikie kile...

Mara nianze kujiuliza, Hivi huu ni uchawi gani?

Asieee!

Nikakaa nikasema:

Hapana, hizi mbona kama fix?

Na mimi by nature nina kaubishi fulani sipendi kumezeshwa mambo japo mwanzo wali ni win

Nikaacha kabisa huo upuuzi

Nikaamua ku-clean akili yangu

Kuanzia hapo nikiambiwa

Njoo kwenye visomo

Nawaambia

Mimi sina tatizo lolote

Na kweli, nilifanya vipimo hospitali nikambiwa kicwa kilikuwa kinauma kwa sababu sikuwa na damu ya kutosha, na ndiyo maana nilikuwa naumwa kicwa na kizunguzungu

Na hata sijui ilikuaje na mama akaingia kwenye mtego wa rafiki yake akaacha kunipeleka hospital kwanza akaanzia kwenye imani huku

Nikatumia zangu dawa nikawa fresh

Sijaumwa tena kicwa, labda cha mafua tu

Sioni mauza mauza wala nini

Naishi vizuri kabisa

Ndipo nikaja kugundua kumbe mambo mengine ni saikolojia tu

Wala hakuna cha uchawi wala nini

Na kuna hii pia ya majini kutaja uchawi bila majini sio sawa ni mtu na shoga yake

Sasa imagine eti mtu anapandisha mashetani anataka dhahabu...

Heh! Dhahabu sasa inatoka wapi yani?

Mashetani wana migodi yao huko?

Nimetoa mtazamo wangu kuhusu hii dhana ya uchawi

Je, uchawi ni nguvu halisi?

Au wakati mwingine tunaita kitu uchawi kumbe kuna sababu za kiafya, kisaikolojia au mazingira ambazo hatujazijua?

Na kama kweli uchawi una uwezo wa kumbadilisha mtu kutoka kuwa genius mpaka kilaza...

Kwanini usitumike kinyume chake?

Au kama wachawi wanaweza kupaa...

Kwanini bado tunakaa kwenye foleni?

Kama hii dhana ya uchawi haina tija kwanini tuna ing'ang'ania?

ShesRise_1 ✋️
Ingawa wengi huwa wanachanganya Kati ya Uchawi na Saikolojia(Magonjwa ya kawaida kabisa ya akili) lakini haiondoi ukweli kwamba Uchawi upo na unaathiri Sana maisha ya watu kiafya, kiuchumi,kijamii n.k.

Mifano ya matukio ya kichawi ni mingi sana ambayo mimi binafsi nimeishuhudia wazi wazi
 
Ingawa wengi huwa wanachanganya Kati ya Uchawi na Saikolojia(Magonjwa ya kawaida kabisa ya akili) lakini haiondoi ukweli kwamba Uchawi upo na unaathiri Sana maisha ya watu kiafya, kiuchumi,kijamii n.k.
Unajua mkanganyiko uko wapi mkuu ni kwamba ukiacha kuamini hizo issue za uchawi wala hutouona kabisa kwenye maisha yako
Huoni hapo kama kuna walakini?
Mifano ya matukio ya kichawi ni mingi sana ambayo mimi binafsi nimeishuhudia wazi wazi
Kama ipi share basi tujifunze
 
Wakuu, tukitaka kuelewa vizuri hili suala bila kupishana lugha, lazima tukubali kuwa uchawi na saikolojia ni vitu viwili vinavyotembea barabara moja lakini kwa mitazamo tofauti. Hakuna anayeweza kubisha kwa 100% kuwa uchawi upo, na hakuna anayeweza kuthibitisha kwa 100% kuwa haupo.

Ukiangalia upande unaounga mkono kuwa uchawi upo, huwezi kupuuza shuhuda za watu mbalimbali, kuna mambo yanatokea kwenye jamii zetu ambayo sayansi haina majibu nayo kabisa mpaka sasa, na hata sayansi yenyewe imeshakubali kuwa kuna nguvu za asili na nishati katika ulimwengu huu ambazo bado hatujazielewa kikamilifu, kama nishati ya mawimbi ya simu ipo na hatuioni kwa macho lakini inatuwezesha kutuma jumbe sehemu tofauti, ni nani anayejua kama kuna negative spiritual energies ambazo wachawi wanazitumia kuathiri maisha ya watu?

Ukiangalia upande unaosema uchawi haupo, napo utaona wazi kuwa mambo mengi tunayoyasikia ni kama propaganda, hadithi za kufikirika, na uoga tu wa kurithi. Hii habari ya kwamba mchawi anaweza kupaa kwa ungo, au anaweza kumgeuza genius kuwa kilaza, kwanini isifanye kazi kinyume chake?

Kama uchawi ni sayansi thabiti, kwanini hauna kanuni zinazotabirika kama zilivyo sayansi nyingine? Mbona nguvu zake zinaonekana tu gizani au pale mtu anapokuwa na uoga?

Hapa ndipo suala la saikolojia linapoingia, iko hivi binadamu ana asili ya kutaka kutafuta sababu ya kila kitu kinachomtokea, mtu akifeli sehemu yoyote au biashara yake ikienda tofauti ni rahisi sana kisaikolojia kutoa lawama kuhusu uchawi kuliko kukubali kuwa pengine alifanya maamuzi mabaya.

Mwisho wa siku, mijadala ya aina hii huwa inabaki kuwa neutral kwamba uchawi upo kama nguvu halisi ya kiroho, lakini hiyo nguvu inafanya kazi kwa kutumia udhaifu wa saikolojia ya binadamu. Usipoamini na ukiiweka akili yako sawa, hiyo nguvu huwa inakosa nguvu kwa mtu husika lakini ukiamini na kuingia uoga, unaifungulia mlango hiyo nguvu mwilini wako kukuathiri.
 
Je uchawi ni imani?
Na ukiamini kuna miujiza?
Miujiza ipo. Muujiza ni msamiati wa kiimani tu ila kimsingi ni kupata bahati nzuri. Ukitokewa na jambo zuri usiloweza kulifafanua basi utaliita muujiza.

Dunia ni dhahania(abstract) sana. Kuna vitu viiingi sana vidogo vidogo vinavyoshirikiana kufanya dunia iende sawa. Mfano mwili wako; Kuanzia zile molecule za protini zinazounda seli, mpaka viungo ulivyonavyo, hiyo yote ni mifumo inayoshirikiana kukuweka hai.

Sasa kukaa chini na kuchambua tuweze kujua nini kinasababisha nini ni kazi ngumu hivyo tunaishia kukisia majibu yetu wenyewe. Huko kukisia ndo kwenye imani huko. Maji yakibandikwa motoni yanachemka. Hii ni hakika, kila mtu anaona. Hutokaa usikie mtu akisema maji kuchemka ni uchawi. Lakini jambo gumu kuelewa mfano gonjwa la saratani, litahusishwa sana na uchawi kwasababu halifafanuliki kirahisi. Kuelewa tu mifumo ya seli hai inavyoleta saratani ni kamzozo.

Mfano umeenda kwa mganga kuhusu suala la ajira. Baada ya hapo ukaomba kazi na ukapata. Vigezo unavyo. Umehangaika kutuma maombi na kufanya saili. Kwa kuwa hujui waajiri wameona nini kwako(huenda ni vigezo, huenda ni haiba, huenda ni bahati tupu) utakisia kulingana na imani(hii ni miwani tu umevishwa tokea utotoni) zako. Labda ni Mungu, labda ni mganga, labda ni nyota nk nk. Miujiza inatokea kwa namna hii.
 
Hello jamii intelligence 👋

Wakuu hii habari ya uchawi nadhani sio jambo geni
Uchawi ulitajwa kwenye vitabu vya dini hasa hivi maarufu Bible&Qur'an

Kwa bible mfano Kutoka 22:18 inasema:

Usimwache mchawi kuishi
Huu ni ushahidi kua Bible inatambua uchawi



Uchawi umetajwa pia kwenye Qur’an, hasa Al-Baqarah 2:102 ambapo inazungumzia habari ya uchawi na watu kujifunza mambo hayo
Huu nao ni ushahidi Qur'an inatambua habari za uchawi

kwa mantiki hii dhana ya uchawi ni ya kale sana

Huku Africa watu bado wamekumbatia hii imani sana, sijui huko Ulaya ikoje

Utasikia mtu anasema
👇
Mtoto huyu karogwa, sio akili zake.

Hapa tunaona uchawi unatajwa kama kitu ambacho kinaweza kubadilisha hali ya mtu
Alikuwa mzima, ghafla akawa kichaa au mtu asie sawa kama alivyokua kabla

Mtu anaumwa, unaambiwa karogwa

Sasa najiuliza...

Uchawi umetengenezwa au umeundwa kwa kufanya vitu negative tu?

Hakuna namna huo uchawi kama upo unaweza kutumika kwa njia positive?

Yaani tukaamua kutumia akili ya mtu kilaza akawa genius, kama vile inavyoaminika kwamba uchawi unaweza kumbadilisha genius kuwa kilaza?

Kuna hii pia👇

Ooh, wachawi wanapaa usiku...

Kwanini sasa kama hiyo technology ipo tusiitumie kupunguza foleni?

Huo usafiri wa kupaa uwe official sasa

Nyie wachawi wa JF(jokes)
haiwezekani kuwa hivi yaani huu uchawi ukawa na tija?

Hivi uchawi unafanya kazi kweli au ni mambo ya nadharia tu?

Niliwahi kua na matatizo ya kupata maumivu ya kicwa nakizunguzungu

Basi kuna mtu akamwambia mama:

Huyu ShesRise_1 amelogwa asifanye vizuri shuleni na si haba shuleni nilikua najitahidi kwahiyo huyo mama akamuambia mama angu huenda nimelogwa ili nirudi nyuma kimasomo🤔

Heh! 🤔

Nikastuka

Nikawaza, haya yatakuwa mambo gani?

Basi nikaanza kufanyiwa zile zinazoitwa tiba za Kisunna, visomo na mambo mengine

Ajabu ni kwamba kuanzia pale ndiyo kwanza nikaanza kupata maruerue.

Usiku naogopa kulala mwenyewe.

Naota ndoto za ajabu, heh... tafrani mtindo mmoja

Kumbe ile issue ya kuanza kuota mauza uza ni kwa sababu
ya saikolojia bana
Yaani saikolojia kwa maana baada ya kusikia nimelogwa na kupelekwa kwenye visomo

Ndiyo ubongo ukaanza kuniundia mapicha picha

So nilivyoambiwa tu vile, akili yangu na ubongo wangu vikaanza kujishughulisha na hayo mambo

Mara nione hiki...

Mara nisikie kile...

Mara nianze kujiuliza, Hivi huu ni uchawi gani?

Asieee!

Nikakaa nikasema:

Hapana, hizi mbona kama fix?

Na mimi by nature nina kaubishi fulani sipendi kumezeshwa mambo japo mwanzo wali ni win

Nikaacha kabisa huo upuuzi

Nikaamua ku-clean akili yangu

Kuanzia hapo nikiambiwa

Njoo kwenye visomo

Nawaambia

Mimi sina tatizo lolote

Na kweli, nilifanya vipimo hospitali nikambiwa kicwa kilikuwa kinauma kwa sababu sikuwa na damu ya kutosha, na ndiyo maana nilikuwa naumwa kicwa na kizunguzungu

Na hata sijui ilikuaje na mama akaingia kwenye mtego wa rafiki yake akaacha kunipeleka hospital kwanza akaanzia kwenye imani huku

Nikatumia zangu dawa nikawa fresh

Sijaumwa tena kicwa, labda cha mafua tu

Sioni mauza mauza wala nini

Naishi vizuri kabisa

Ndipo nikaja kugundua kumbe mambo mengine ni saikolojia tu

Wala hakuna cha uchawi wala nini

Na kuna hii pia ya majini kutaja uchawi bila majini sio sawa ni mtu na shoga yake

Sasa imagine eti mtu anapandisha mashetani anataka dhahabu...

Heh! Dhahabu sasa inatoka wapi yani?

Mashetani wana migodi yao huko?

Nimetoa mtazamo wangu kuhusu hii dhana ya uchawi

Je, uchawi ni nguvu halisi?

Au wakati mwingine tunaita kitu uchawi kumbe kuna sababu za kiafya, kisaikolojia au mazingira ambazo hatujazijua?

Na kama kweli uchawi una uwezo wa kumbadilisha mtu kutoka kuwa genius mpaka kilaza...

Kwanini usitumike kinyume chake?

Au kama wachawi wanaweza kupaa...

Kwanini bado tunakaa kwenye foleni?

Kama hii dhana ya uchawi haina tija kwanini tuna ing'ang'ania?

ShesRise_1 ✋️
Hakuna uchawi , bali ukosefu wa uelewa juu ya jambo husika.
 
Wakuu, tukitaka kuelewa vizuri hili suala bila kupishana lugha, lazima tukubali kuwa uchawi na saikolojia ni vitu viwili vinavyotembea barabara moja lakini kwa mitazamo tofauti. Hakuna anayeweza kubisha kwa 100% kuwa uchawi upo, na hakuna anayeweza kuthibitisha kwa 100% kuwa haupo.
Mimi naweza kuthibitisha kwa kusema haupo kwa sababu sijauona
Ukiangalia upande unaounga mkono kuwa uchawi upo, huwezi kupuuza shuhuda za watu mbalimbali, kuna mambo yanatokea kwenye jamii zetu ambayo sayansi haina majibu nayo kabisa mpaka sasa, na hata sayansi yenyewe imeshakubali kuwa kuna nguvu za asili na nishati katika ulimwengu huu ambazo bado hatujazielewa kikamilifu, kama nishati ya mawimbi ya simu ipo na hatuioni kwa macho lakini inatuwezesha kutuma jumbe sehemu tofauti, ni nani anayejua kama kuna negative spiritual energies ambazo wachawi wanazitumia kuathiri maisha ya watu?
Twin issue ni kwamba mbona ambao hawaamini uchawi hawapati hayo mazingaombwe🤔

Ukilinganisha na hao wanaomini hizo mambo
Ukiangalia upande unaosema uchawi haupo, napo utaona wazi kuwa mambo mengi tunayoyasikia ni kama propaganda, hadithi za kufikirika, na uoga tu wa kurithi. Hii habari ya kwamba mchawi anaweza kupaa kwa ungo, au anaweza kumgeuza genius kuwa kilaza, kwanini isifanye kazi kinyume chake?

Kama uchawi ni sayansi thabiti, kwanini hauna kanuni zinazotabirika kama zilivyo sayansi nyingine? Mbona nguvu zake zinaonekana tu gizani au pale mtu anapokuwa na uoga?
Hapa hapa yaani why
Hapa ndipo suala la saikolojia linapoingia, iko hivi binadamu ana asili ya kutaka kutafuta sababu ya kila kitu kinachomtokea, mtu akifeli sehemu yoyote au biashara yake ikienda tofauti ni rahisi sana kisaikolojia kutoa lawama kuhusu uchawi kuliko kukubali kuwa pengine alifanya maamuzi mabaya.
Naunga mkono hoja yako
haiwezekani mtu maralia imepanda kicwani waseme kwalogwa au ana mapepo
Mwisho wa siku, mijadala ya aina hii huwa inabaki kuwa neutral kwamba uchawi upo kama nguvu halisi ya kiroho, lakini hiyo nguvu inafanya kazi kwa kutumia udhaifu wa saikolojia ya binadamu. Usipoamini na ukiiweka akili yako sawa, hiyo nguvu huwa inakosa nguvu kwa mtu husika lakini ukiamini na kuingia uoga, unaifungulia mlango hiyo nguvu mwilini wako kukuathiri.
Hapa kuna kitu
 
Miujiza ipo. Muujiza ni msamiati wa kiimani tu ila kimsingi ni kupata bahati nzuri. Ukitokewa na jambo zuri usiloweza kulifafanua basi utaliita muujiza.

Dunia ni dhahania(abstract) sana. Kuna vitu viiingi sana vidogo vidogo vinavyoshirikiana kufanya dunia iende sawa. Mfano mwili wako; Kuanzia zile molecule za protini zinazounda seli, mpaka viungo ulivyonavyo, hiyo yote ni mifumo inayoshirikiana kukuweka hai.

Sasa kukaa chini na kuchambua tuweze kujua nini kinasababisha nini ni kazi ngumu hivyo tunaishia kukisia majibu yetu wenyewe. Huko kukisia ndo kwenye imani huko. Maji yakibandikwa motoni yanachemka. Hii ni hakika, kila mtu anaona. Hutokaa usikie mtu akisema maji kuchemka ni uchawi. Lakini jambo gumu kuelewa mfano gonjwa la saratani, litahusishwa sana na uchawi kwasababu halifafanuliki kirahisi. Kuelewa tu mifumo ya seli hai inavyoleta saratani ni kamzozo.

Mfano umeenda kwa mganga kuhusu suala la ajira. Baada ya hapo ukaomba kazi na ukapata. Vigezo unavyo. Umehangaika kutuma maombi na kufanya saili. Kwa kuwa hujui waajiri wameona nini kwako(huenda ni vigezo, huenda ni haiba, huenda ni bahati tupu) utakisia kulingana na imani(hii ni miwani tu umevishwa tokea utotoni) zako. Labda ni Mungu, labda ni mganga, labda ni nyota nk nk. Miujiza inatokea kwa namna hii.
Hiyo mifumo inayoshirikiana kufanya dunia iende sawa, yenyewe ndio uchawi au miujiza yenyewe?
 
Mimi naweza kuthibitisha kwa kusema haupo kwa sababu sijauona
Kwa muktadha huu, kitu/jambo lisipoonekana kwa macho maana yake halipo?
Twin issue ni kwamba mbona ambao hawaamini uchawi hawapati hayo mazingaombwe🤔

Ukilinganisha na hao wanaomini hizo mambo
Paragraph ya mwisho kabisa, umeisoma vizuri ukaielewa Twin?
 
Miujiza ipo. Muujiza ni msamiati wa kiimani tu ila kimsingi ni kupata bahati nzuri. Ukitokewa na jambo zuri usiloweza kulifafanua basi utaliita muujiza.

Dunia ni dhahania(abstract) sana. Kuna vitu viiingi sana vidogo vidogo vinavyoshirikiana kufanya dunia iende sawa. Mfano mwili wako; Kuanzia zile molecule za protini zinazounda seli, mpaka viungo ulivyonavyo, hiyo yote ni mifumo inayoshirikiana kukuweka hai.

Sasa kukaa chini na kuchambua tuweze kujua nini kinasababisha nini ni kazi ngumu hivyo tunaishia kukisia majibu yetu wenyewe. Huko kukisia ndo kwenye imani huko. Maji yakibandikwa motoni yanachemka. Hii ni hakika, kila mtu anaona. Hutokaa usikie mtu akisema maji kuchemka ni uchawi. Lakini jambo gumu kuelewa mfano gonjwa la saratani, litahusishwa sana na uchawi kwasababu halifafanuliki kirahisi. Kuelewa tu mifumo ya seli hai inavyoleta saratani ni kamzozo.

Mfano umeenda kwa mganga kuhusu suala la ajira. Baada ya hapo ukaomba kazi na ukapata. Vigezo unavyo. Umehangaika kutuma maombi na kufanya saili. Kwa kuwa hujui waajiri wameona nini kwako(huenda ni vigezo, huenda ni haiba, huenda ni bahati tupu) utakisia kulingana na imani(hii ni miwani tu umevishwa tokea utotoni) zako. Labda ni Mungu, labda ni mganga, labda ni nyota nk nk. Miujiza inatokea kwa namna hii.
Point yako si kuwa kila kitu kina chanzo?
 
Hapo ndo penyewe sasa. Hakuna ajuaye🤷🏾‍♂️

Majibu ya uhakika hayapo. Miungu, uchawi, mizimu, vyote vinapwaya.

Binafsi naamini tunaweza kuishi vizuri tu bila hayo majibu.
Inawezekana ukawa sahihi lakini sio sana, maana kutokujua kwako majibu hakumaanishi kuwa hiyo mifumo haipo au haikuathiri Mkuu.
 
Miujiza ipo. Muujiza ni msamiati wa kiimani tu ila kimsingi ni kupata bahati nzuri. Ukitokewa na jambo zuri usiloweza kulifafanua basi utaliita muujiza.
Hakika muujiza ni jambo ulilodhani ni gumu sana lakini likawa jambo rahisi kwa namna ulikua hutarajii naamini huo ndiyo muujiza

Dunia ni dhahania(abstract) sana. Kuna vitu viiingi sana vidogo vidogo vinavyoshirikiana kufanya dunia iende sawa. Mfano mwili wako; Kuanzia zile molecule za protini zinazounda seli, mpaka viungo ulivyonavyo, hiyo yote ni mifumo inayoshirikiana kukuweka hai.

Sasa kukaa chini na kuchambua tuweze kujua nini kinasababisha nini ni kazi ngumu hivyo tunaishia kukisia majibu yetu wenyewe.
Najaribu kuelewa hapa
Nitarudi
Huko kukisia ndo kwenye imani huko. Maji yakibandikwa motoni yanachemka. Hii ni hakika, kila mtu anaona. Hutokaa usikie mtu akisema maji kuchemka ni uchawi. Lakini jambo gumu kuelewa mfano gonjwa la saratani, litahusishwa sana na uchawi kwasababu halifafanuliki kirahisi. Kuelewa tu mifumo ya seli hai inavyoleta saratani ni kamzozo.

Kwa maana ya kwamba kitu watu wasichokiweza
Hukifananisha au hukiita uchawi ?
Licha ya kua huo uchawi wakiambiwa wauoneshe hawawezi
Mfano umeenda kwa mganga kuhusu suala la ajira. Baada ya hapo ukaomba kazi na ukapata. Vigezo unavyo. Umehangaika kutuma maombi na kufanya saili. Kwa kuwa hujui waajiri wameona nini kwako(huenda ni vigezo, huenda ni haiba, huenda ni bahati tupu) utakisia kulingana na imani(hii ni miwani tu umevishwa tokea utotoni) zako. Labda ni Mungu, labda ni mganga, labda ni nyota nk nk. Miujiza inatokea kwa namna hii.
🤔
 
Unajua mkanganyiko uko wapi mkuu ni kwamba ukiacha kuamini hizo issue za uchawi wala hutouona kabisa kwenye maisha yako
Huoni hapo kama kuna walakini?

Kama ipi share basi tujifunze
1.Kijana A alimtukana kijana B halafu kijana A(Mtukanaji) akapindishwa mdomo on the spot na kijana B(Mtukanwaji) tena alimwambia kabisa "Mimi huwa situkanwi"

2. Kuna mchawi mmoja mwaka huu huu alijaribu kutunishiana misuli na mimi kwa kujaribu kuniua kwa kunisababishia ajali mbaya ya gari. Ajali haikutokea kwa sababu ya Ulinzi ninaolindwa nao 24/7. Nikiri tu kwamba under normal circumstances mimi sikupaswa kuwa hai. Nimekingwa na mashambulizi ya kichawi mengi sana na mengine ni kutoka kwa ndugu zangu wa damu!

3. Mwingine alinijia usiku mnene nikiwa nimelala ili aniwangie akidhani simuoni kumbe namuona fully. Nilichofanya ni kumkata jicho tu kisha akatokomea kwa hofu

Yatosha kwa leo!

UJUMBE: Kuna tofauti kati ya kuamini uwepo wa Uchawi na kuishi kwa kuutumainia uchawi. Wengi huwa wanachanganya Kati ya haya mawili. Wapo ambao wanaamini kwamba kutoamini uwepo wa Uchawi ni Njia ya wao kuwa salama dhidi ya Uchawi jambo ambalo si kweli.

Ukweli ni kwamba kama mtu hana Ulinzi wa Kristo Yesu ndani yake basi hata ajilinde vipi hayupo 100% safe dhidi ya hatari mbalimbali za kiroho ukiwemo Uchawi na za kimwili pia

ZABURI 91
10 Mabaya hayatakupata wewe, Wala tauni haitaikaribia hema yako.

11 Kwa kuwa atakuagizia malaika zake Wakulinde katika njia zako zote.

12 Mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.

13 Utawakanyaga simba na nyoka, Mwana-simba na joka utawaseta kwa miguu.

14 Kwa kuwa amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, Kwa kuwa amenijua Jina langu.

15 Ataniita nami nitamwitikia; Nitakuwa pamoja naye taabuni, Nitamwokoa na kumtukuza;

16 Kwa siku nyingi nitamshibisha, Nami nitamwonyesha wokovu wangu.

YOHANA 10
10 Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.
 
Tatizo hamjui ya kuwa kwanza kabisa hamna free will
Kila kitu kiko controlled na Mungu

Hata hivyo vitu mnacyoviita uchawi ni Mungu
 
Back
Top Bottom