Je, Kinachomponza Mbowe ni Anasa?

Je, Kinachomponza Mbowe ni Anasa?

Status
Not open for further replies.
Mkuu FD,

I hope hapo juu una maana unalipa kidogo kidogo kulingana na masharti ya mikopo yako.

Kama una maana tofauti na hiyo, hilo ni jambo la hatari sana. Kukiuka masharti ya mkopo kwa sababu zozote zile si jambo la kujivunia na badala yake ni hatari mno.

Unapokuwa kiongozi wa siasa inakuwa hata hatari zaidi maana ukifilisiwa, kweli wewe unafaa hata kuongoza chama?

Ni kweli nchi haiwezi kuendelea bila wananchi wake kuweza kukopa na kuendesha biashara zao. Lakini inapotokea kwamba viongozi wanakopa sehemu kama NSSF ambako kuna nafuu kubwa na kuwaacha wananchi wanasota na mabank
ambako kuna interest rate zaidi ya 20%, kwa kweli haiwezi kuwa sawa. Matokeo yake viongozi huwa hawachukuia hatua kubadilisha sheria za mabank maana wanakuwa hawalipati hilo joto la jiwe ambalo linawakumba wananchi wa kawaida.

Wanasiasa waache kukimbilia sehemu kama NSSF na badala yake wakakope kwenye hayo mabank sawa na wananchi wengine.

Tupo pamoja mkuu. Deni langu nalipa kidogo kidogo kama tulivyokubaliana.

Ninachopinga ni watu kuongelea vitu visivyo na msingi kama kumiliki Vogue.

Pia rudi nyuma kidogo usome post ya Techmaro. Huu ni mkopo wa kibiashara, mabenki kukosa FOREX pia ni kigezo tosha cha kukaa meza moja kujadiliana na aliyekukopesha. Kuna mambo mengi hasa kama aliyekukopesha alijua nia yako ni nini, It is a business loan sio personal loan.

Mimi pia napinga Mbowe kutorejesha on time hela hizo.
 
Tupo pamoja mkuu. Deni langu nalipa kidogo kidogo kama tulivyokubaliana.

Ninachopinga ni watu kuongelea vitu visivyo na msingi kama kumiliki Vogue.

Pia rudi nyuma kidogo usome post ya Techmaro. Huu ni mkopo wa kibiashara, mabenki kukosa FOREX pia ni kigezo tosha cha kukaa meza moja kujadiliana na aliyekukopesha. Kuna mambo mengi hasa kama aliyekukopesha alijua nia yako ni nini, It is a business loan sio personal loan.

Mimi pia napinga Mbowe kutorejesha on time hela hizo.

FD,

Nakubaliana na wewe kabisa juu ya hilo. Biashara ina milima na maporomoko. Kama mfanyabiashara anaweka kila kitu wazi sio rahisi kabisa kwa bank kumfikisha mahakamani.

Mambo yote haya ni kwenda mapema kuwaona waliokukopesha na kukaa nao chini, kuwapa ushahidi wote.

Ukiona jambo limefika mahakamani lazima ujue hata hao wakopeshaji wamechoka, au hawakubaliani na sababu au wanaona kuna ubabaishaji.

Pia mimi siko happy na hili la vigogo kutumia NSSF kukopa huku wananchi wa kawaida wanasota na mabank ambayo interests zao ni kichaa. Kama NSSF inaweza kuwakopesha vigogo bila rushwa kwanini washindwe kutukopesha wananchi wa kawaida kama sisi?
 
Mwafrica wa kike, Asha Abdala Rev Kishoka and so and so mimi naomba tuwaignore hawa watu

KADA MPINZANI
MAHESABU
CHINGA

Kwanza angalieni nick name zao
Kada mpinzani ni dhahiri amekuja humu kuleta upinzani usio na msingi na sometimes anabisha na kupost vitu ambavyo haviingii akilini na wala havina ushawishi kabisa.

Mahesabu:- Huyu amekuja JF na mahesabu ya kuvuruga watu as u know kuna watu wametumwa na (WAMENUNULIWA) kwa ajili ya kuchafua watu hapa JF

Chinga:- Ni nani asiyejua matatizo wanayokutana nayo hawa kina CHINGA??

KWA HIYO TUNAWEZA KUWA TUNAPOTEZA MUDA KUBISHANA NA WATU AMBAO WAMEATHIRIKA KUTOKANA NA NICK NAMES ZAO WALIZOZICHAGU MFANO MDOGO TU UNAAMUA KUJIITA DUDUBAYA WHAT DO U THINK?? KILA SIKU NI MATATIZO TU GROW UP GUYS WEKENI POST ZENYE USHAWISHI SI KUVURURUGA WATU HAPA JF.
 
Hili deni lina RIBA. Na riba compounded haifanani na simple interest rate.
EPA ni kitu kingine and Richmond ni kingine. Mbowe anatakiwa alipe deni alilokopa under terms and conditions. Hakuna mtu aliyesema Mbowe ni mwizi, noo. Bali Mbowe need to pay his Bills, that is how we suppose to conduct business. Alijua Riba ina Riba, alijua madhara ya kutolipa yanasababisha adjusted rate kutokana na Inflation aliyajua yote haya.



Well,Mtanganyika nimekupa Tano kwa analysis ulizotoa hapo juu.Lakini,Mbowe anbataka kulipa deni kwa haki.

Yeye ni mwanasiasa wa upinzani na mwenye dhamana ya kupigania haki,je alipe deni ambalo anajua lina kasoro katika terms and conditions?

Pia unashindwa kuongelea suala la Management ya NSSF iliyokua chini ya mkullo kwani sasa iatabidi pia kuwe na uchunguzi mzito hapo NSSF.Yaani mtu kukaa na deni muda wote huo lakini hakuna hatua zinazochukuliwa kuhakikisha hela za walipa kodi zinarudi on time?

Pia,tujuie NSSF kuna tatizo kubwa kuliko tunavyofikiria kwani inaonekana mpaka mtu awe mwanasiasa wa Upinzani ndipo atakapokaliwa shingoni seriously kuhusu fedha za watanzania.


Sasa uchunguzi ufanywe ibainike kuna wanaCCM wangapi wamekopa huko NNSF hadi leo hawajalipa?
 
do you know the seriousness of these allegations you are making here?

Naona Chinga na kada wameamua kuuchuna.Kwa hiyo Mkullo ana walakini maanake dataz zinazomwagwa ni noma,wataanza kupiga ramli kuomba mjadala ufe na wameuanza wenyewe.

Na hizo hela za taasisi kubwa kama hiyo kama Mkullo alishindwa kuzisimamia na kuziweka kwenye mashaka hivyo,inakuaje kikwete amteue kuwa waziri wa fedha?


Je,katika utajiri alioupata Mkullo kama si wa halali,je ni nini uhusiano wa Mkullo na Kikwete,
Je,inawezekana mkullo alisaidia kampeni za kikwete kupitia hela za NSSF?

Je,kupatiwa uwaziri inawezekana kuna fadhila fulani zinalipwa?

Well,hapa kuna mashaka makubwa kama Mkullo hakua kiongozi makini kwenye taasisi hiyo na still akapewa wadhifa mkubwa kama huo.Tuanzie kule kwenye unaibu wa wizara hiyo nyeti.

Kidali po!
Ben,
kuna mtu mwenye data anipe connection ya NSSF(NPF) na SUKITA?
Nasikia kuna balaaa kubwa huko.
 
Ben,
kuna mtu mwenye data anipe connection ya NSSF(NPF) na SUKITA?
Nasikia kuna balaaa kubwa huko.

Ben na Kitina
Baada ya gazeti za Rostam kuandika habari hizi wakidhani zina madhara kwa Mbowe na kama kawaida yake ua Uzabi zabina kama vile wakati wa Mengi na Manji jana mapema Rostam alimpigia simu Mbowe na kuomba msamaha kwamba ni waandishi wake na yeye hahusiki na habari na kutaka kuwe na amani kati yao ma kumuomba amtofautishe na gazeti lake . Lakini kwa kuwa ana akili ndogo akadhani people can buy ujinga wake huo .

Habari hizi ni za Uhakika na kilicho andikwa ni ujinga mtupu mana tangia mwaka 1990m kama Mbowe angalikuwa na kosa yeye Rostam na CCM yake wasingalimwachia .Kumbeni walivyo mvamia kwamba halipi kodi .TRA walipiga hodi na kukuta vitabu vimetulia .
 
Ni wazi kuwa walichofanya gazeti la RAI ni fitna ya hali ya juu. Inasikitisha sana kuona jinsi gazeti kama hili ambalo enzi fulani tulikuwa tunasisitiza wanafunzi makini kuhakikisha wanalisoma limefika kuwa hovyohovyo kama hivi.

Hata hivyo ni muhimu kukumbushana kuwa unapokuwa kiongozi wa umma una wajibu wa kuwa msafi kila mahala. Kama wewe ni mfanyabiashara basi ni wajibu wako kuwa mfano wa kuigwa na wafanyabiashara wengine kwa mazuri na sio mabaya yako kibiashara. Kulipa kodi ipasavyo na kulipa madeni yako ni moja ya vigezo ambavyo raia makini wanapaswa kuvitumia kupima nafasi yako kama kiongozi wa kisiasa.

Hilo sio jukumu kwa viongozi waliopo sasa tu lakini hata kwa wale wenye ndoto za kuwa viongozi hapo baadae. Matendo yako leo kama kijana ama mfanyabiashara ama mshikadau katika sekta yeyote ile ni lazima hapo baadae yatumike kama vigezo vya kuchambua uwezo na uhalali wako kama kiongozi bora na sio bora kiongozi.

Mbaya zaidi ni kuwa unapokuwa kiongozi wa upinzani katika jamii ambayo bado imeshindwa kujenga imani kwa upinzani, ni wajibu wako kuwa sio msafi tu bali kuonyesha usafi unaotukuka ili wale waliochoka na uozo wa watawala kujenga imani kwako na chama chako kulinganisha na waliopo madarakani.

Wakati nikiamini kuwa MBOWE ni mfanyabiashara, vilevile naamini kuwa alipaswa kuwa mfanyabiashara makini asiye fanana kabisa na wafanyabiashara wengine kama hili fedhuli linaloitwa ROSTAM AZIZ. Mbowe ana wajibu kwa watanzania kuhakikisha anakuwa msafi kwa matendo yake, kisiasa, kijamii na hata kibiashara. Kuteleza ama kuanguka kwake kutokana na udhaifu fulani unaotoa nafasi maadui wa siasa za ukombozi kutoka katika makucha ya UFISADI kumfitini kama ilivyo katika suala hili la MKOPO wa NSSF, ni kuangusha dhima nzima ya ukombozi nchini.

Ingelikuwa katika demokrasia endelevu kama wenzetu walio nje huko ughaibuni ningeshauri MBOWE ajiuzulu nafasi yake kama mwenyekiti wa CHADEMA, chama kinachoonesha dalili zote za kuwa chama makini hapo mbeleni. Hata hivyo kwa kujua hali tuliyonayo, ushauri wangu ni kuwa MBOWE anapswa kujisafisha. Sio kwa hili la NSSF lakini kwa mengine mengi, kisiasa na hata kijamii.

Kwangu mimi hata kuendesha biashara ya NIGHT CLUB kwa hali iliyopo ambapo hata vitoto vya miaka 15-18 vinajivinjari nadhani ni tatizo kwa MBOWE kama kiongozi wa kisiasa.

Ukweli ni kuwa mambo kama haya ya NSSF, BILICANAS na mengine kadhaa ndio yanayowafanya wengi wenye nia ya kujiunga na upinzani kusita na wengine hata kutotilia maanani anayoyasema MBOWE majukwaan na zaidi kuikwepa CHADEMA ambayo ukweli ni kuwa kinaweza kujengeka na kuwa chama makini kitakachoweza kuwaunganisha watanzania kujikomboa katka lindi la ufisadi lililojengwa na kulindwa na CCM.

Tanzanianjema
 
Nimefuatilia kwa makini sana thread hii inaonesha kuwa kuna tatizo mahali na tatizo lenyewe ni ukosefu wa UAMINIFU NA UADILIFU.

Facts zilizopo hapa ni kama zifuatavyo:

Bw. Mbowe kupitia kampuni yake akiwa na akili timamu alikopa Shs. 15m/= NSSF kwa mkataba halali mwaka 1990.

Bw. Mbowe na kampuni yake ameshindwa kulipa deni hilo kwa muda waliokubaliana na NSSF.

Deni hilo kwa mahesabu ya sasa limefikia karibu 1.2b/=.

Katika ulimwengu wa kawaida wa kufanya biashara, mkopaji wa namna hii si mwaminifu na si mwadilifu. Nadhani kwa wale wanaolewa kama Mtanganyika, Mtanzania na wengine wengi hapa 'credit' imeshaharibika na hana sifa tena ya kuendelea kuaminiwa.

Hiki ni kiashiria cha dalili mbaya sana za matendo ya muhusika.

nimeona kuna wachangiaji wengine, tena huwa ni wazuri sana tu katika kukata issue hapa, lakini kwenye thread hii wameonyesha udhaifu mkubwa wa kutetea maslahi ya Taifa kwa kigezo cha kufananisha mabaya mengine ya wanasiasa wa chama Tawala, nina uhakika wamefanya hivyo kwa kuonyesha true colors zao.

Kwa upande wa CHADEMA, nadhani huu ni wakati mwafaka kabisa wa kumwambia mfalme kwamba yuko uchi ili muingie katika historia, vinginevyo tutawaona kuwa wao ni YANGA na ninyi ni SIMBA.
 
Imekuwaje tena jamani ? kwani mbowe hakusema yale maneno ? mbona mmefuta ??
 
mkuki kwenda msituni haukupotea

maana nashangaa ! jiii imefutwa ! sasa tukisema JF ni pro-CHADEMA wanakataa na kusema tunaiponda JF, how ?

Ilinilazimu nitriple check kabla ya kuandika hii thread ndipo nikaona hamna kitu, nikashangaa !

Sasa naamini UFISADI ni hadi katika uandishi, na kama chuki zenyewe ndio hivi SIDHANI KAMA WE WILL GET WHERE WE EXPECT TO GET ! Tutakuwa tunacreate vitu ambavyo tunakemea !

Maneno ni kweli mbowe kasema, sasa sijui wanafuta nini ! au alilazimishwa mbowe kusema hayo maneno ?
 
Biashara yoyote kubwa ili iendelee inaitaji mkopo, kuna aina nyingi za mikopo. Short term debt and long term debt, sasa Mbowe alikopa kwa muda gani na kwa biashara gani? Hilo ni million dollar question. Kama alikopa kwa more than 10 years ili kufinance club yake that is fine, tatizo linakuja jee alikuwa anafanya month payments?

Na kama alikuwa hafanyi payments jee ni nani alikuwa anadefend collateral alizoweka zisiuzwe? Sababu kama unapiga kelele kwenye majukwaa kwamba CCM ni wezi, na wewe unatumia same strategy za CCM katika njia nyingine, then unakila haki ya kufananishwa na Gavana wa NY.

Nilishawai kusema natofautiana sana na Mboe sababu anaonyesha ni mbabaishaji. Mikopo yote ina rules and regulation, na dawa ya kukopa ni kulipa. Rejea maneno ya Mwalim " You borrow, you pay". Hakuna sijui nilikuwa sijui hili wala lile.

Ni mategemeo yangu wana CHADEMA wataomba explaination kutoka kwa kiongozi wao, jee haoni kama huko ni kufuja mali za umma? Jee yeye anajenga picha gani kama kiongozi? Jee ni kwa asilimia ngapi kuchelewa kwake kwa loan kuna adhiri viinua mgongo vya watu?

Sababu kumbuka kwamba pesa zile zinatumika kulipa pansion za baba na mama walio staff, sasa kama kuna mtu kwa njia moja au nyingine hataki kulipa kutokana na political power yake, then what is the different na mafisadi?

This is serious, and they need to take it serious !
 
Habari hii ya Mbowe na madeni katika kampuni anazomiliki zinaonyesha matatizo yaliopo kwenye vyombo vyetu vya pesa ambavyo kimsingi si wakopeshaji kwa watu au kampuni Binafsi. Na si kwa mkopaji. Tatizo la NSSF kukopesha watu binafsi lilianza kusikika pale ilipogundulika kuwa Bw. Sumaye, then PM, kuwa alikopa mil. 50. Lilizimwa kwa madai kuwa angelililipa, bila shaka with compounded interest kama hizo za Mbowe na mtandao haukuwa kama ulivyo sasa.
Kwa hili sioni kama Mbowe anaweza kufananishwa na mafisadi au hata wahujumu uchumi. Ni jambo la kawaida kwa mabenki kukopesha pesa, na hili ndio jukumu lao haswa, lakini mifuko hii ya hifadhi ni ya kuwekeza katika vitega uchumi ambavyo vitawahakikishia wanachama wao usalama wa pesa zao. Kwa hiyo Mfuko kuanza kukopesha badala ya kuwekeza ilikuwa ndio mwanzo wa tatizo. Sidhani kama wanauzoefu wakutosha wa kufuatilia madeni kutoka kwa wafanya biashara la sivyo kusinekuwa na usumbufu wa kulipa wanachama pesa zao mara inapobidi. Kwa kuwa kesi ipo/ilishaamuliwa, basi mkondo wa sheria utafuatwa. Na kwa wananchi tutakuwa na angalau uwezo wa viongozi wetu wategemewa kusimamia uchumi wetu.
Maudhui ya kuiandika hoja hii kwenye magazeti ni somo ambalo Republicans wanatufundisha jinsi wanavyowashughulikia Democrats. Fuatilia suala la Spitzer,(http://harpers.org/archive/2008/03/hbc-90002589) kuwachafua wapinzani kadiri iwezekanavyo. Kwetu sisi hizi chupi zinazoanikwa tutaziona tu ziwe blu au kijani.
 
Mimi Sijaona Chochote Unaweza Kunitumia Kopy Ya Ulichotuma Katika Pm Yanu Tafadhali Kada Mpinzani ??
 
maana nashangaa ! jiii imefutwa ! sasa tukisema JF ni pro-CHADEMA wanakataa na kusema tunaiponda JF, how ?

Ilinilazimu nitriple check kabla ya kuandika hii thread ndipo nikaona hamna kitu, nikashangaa !

Sasa naamini UFISADI ni hadi katika uandishi, na kama chuki zenyewe ndio hivi SIDHANI KAMA WE WILL GET WHERE WE EXPECT TO GET ! Tutakuwa tunacreate vitu ambavyo tunakemea !

Maneno ni kweli mbowe kasema, sasa sijui wanafuta nini ! au alilazimishwa mbowe kusema hayo maneno ?
tehe....tehe...tehe......!!!
kwi.....kwi....kwi......!!!!
yaani ........au mbowe kanunua watu humu ndani.....? kama hata JF wanatenda kama RA........twafa.....!
KADA.....wameanza kufuta za MBOWE SASA HIVI WATAFUTA ZA MAFISADI WENGINE.......KAMA RA....1 LETS WATCH AND SEE THE TREND...!
 
Mwafrica wa kike, Asha Abdala Rev Kishoka and so and so mimi naomba tuwaignore hawa watu

KADA MPINZANI
MAHESABU
CHINGA

Kwanza angalieni nick name zao
Kada mpinzani ni dhahiri amekuja humu kuleta upinzani usio na msingi na sometimes anabisha na kupost vitu ambavyo haviingii akilini na wala havina ushawishi kabisa.

Mahesabu:- Huyu amekuja JF na mahesabu ya kuvuruga watu as u know kuna watu wametumwa na (WAMENUNULIWA) kwa ajili ya kuchafua watu hapa JF

Chinga:- Ni nani asiyejua matatizo wanayokutana nayo hawa kina CHINGA??

KWA HIYO TUNAWEZA KUWA TUNAPOTEZA MUDA KUBISHANA NA WATU AMBAO WAMEATHIRIKA KUTOKANA NA NICK NAMES ZAO WALIZOZICHAGU MFANO MDOGO TU UNAAMUA KUJIITA DUDUBAYA WHAT DO U THINK?? KILA SIKU NI MATATIZO TU GROW UP GUYS WEKENI POST ZENYE USHAWISHI SI KUVURURUGA WATU HAPA JF.

KAMA MMEKUWA MAKINI KIDOGO KUANGALIA MICHANGO YA HAWA WATU UTAGUNDUA KUWA HAMNA TOFAUTI HATA KIDOGO YA KIMAWAZO.
POSSIBILITIES.....
WANAKAA PAMOJA
WAMESOMA PAMOJA
NI MTU MMOJA
AU WAMETUMWA NA MTU
 
ahhh kila mmoja na speacial interest zake humu

wengine Mbowe, wengine JK wengine MEMBE wengine SALVA wengine IKULU wengine wapi zijui al muradi kunapendeza tuu
 
Wewe Mbowe kwa nini umejipendekeza kukopa fedha za NSSF milioni 15 na kuingia upinzani? Sasa tutakumaliza na hivyo vi-helikopta vyako. Rudi CCM; ona mwenzio Super Doll mtoto wa CCM; anaidaiwa zaidi ya bilioni 17 za NSSF lakini haandamwi magazetini. Utaula wa chuya kwa uvivu wa kuchagua!

PM
 
Mbowe awaponda wenzake
*Asema wapo kwa maslahi ya tumbo
*Kuungana sawa na kufika mbinguni


Na Eliya Mbonea, Iramba

MGOMBEA urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bw. Freeman Mbowe (CHADEMA), amesema uwezekano wa viongozi wa kambi ya Upinzani nchini kuungana ni mgumu sawa na tajiri kuona ufalme wa Mbingu.

Alitoa kauli hiyo jana, alipokuwa akihutubia wakazi na wanafunzi wa chuo na sekondari ya Kinampanda mjini hapa, baada ya kuulizwa swali lililotaka kujua sababu ya wagombea urais wa kambi hiyo kutoungana na kuwa kitu kimoja.

Bw. Mbowe alisema chama chake kimekuwa cha kwanza katika historia ya upinzani nchini kuweka mbele dhana ya ushirikiano baina ya wapinzani.

"Vyama vichache vimepandikizwa na CCM kwa maslahi ya tumbo, CHADEMA mwaka 1995 haikusimamisha mgombea, badala yake iliungana na NCCR-Mageuzi, mwaka 2000 tukawaunga mkono CUF, jitihada zetu zote za kushirikiana zimekuwa hazizai matunda, hivyo mwaka huu tumesimamisha mgombea," alisema.

Aliongeza kuwa viongozi wengi wa Upinzani hawawezi kuungana kwa dhamira ya kuwatetea Watanzania, kwani wapo kwa ajili ya maslahi binafsi.

"Msifikirie kuwa kila mgombea urais au Mwenyekiti wa chama yupo kwa ajili ya kupigania mustakabali wa nchi, wamegeuza siasa kama biashara na wanaitumia kama vyanzo vya mapato," alisema mgombea huyo.

Alisema lazima CCM ikubali lawama za kulifikisha Taifa katika hali mbaya na ya kutisha, na kuwafanya wananchi wajione kuwa matatizo yao ni tofauti ya rangi za bendera badala ya kuwaeleza kuwa tatizo kubwa ni umasikini.

Akizungumzia nafsi yake, Bw. Mbowe aliwaeleza wananchi kuwa hakuingia kwenye siasa kwa ajili ya kutafuta ajira, kwani anachopigania si maslahi ya CHADEMA bali ya wananchi wote. "CHADEMA si mama yangu naweza kuiacha wakati wowote," alisisitiza msimamo wake.

Alisema kamwe hataacha kutumia busara na hekima za Mwalimu Nyerere katika kujenga utaifa, kwani kipindi chote cha miaka 44 bado misingi ya utaifa aliyoicha Mwalimu haijatekelezwa.

NAULIZA :
(1) Kama anajua fika kwamba vyama vya upinzani (ukiondo chadema) vimepandikizwa na ccm, iweje aungane nao wakati wamepandikiza na ccm ?
(2)Pili alisema kwamba wapinzani (chadema excluded)kwamba wapo kwa ajili ya matumbo yao, DOESNT THAT TECHNICALLY INCLUDE HIMSELF AS WELL kwa kuungana nao ??
(3) Je yupo tayari kueleza watanzania wakiwemo wapiga kura wake kwamba chama chake (CHADEMA) kimepandikizwa na CCM ?
(4) Na yeye binafsi kaungana na wenzake ili tumbo lake lipate rizki ?
(5)Kasema kwamba hayupo kwenye siasa kama ajira, ila hapo hapo alisema kwamba "wenzake"(wapinzani) DOESNT THIS EVEN RAISE MORE QUESTIONS THAN ANSWERS ?????????????


JAMANI NAOMBENI HII MUIACHE HAPA NA MSIIFUTE ! INAELEWEKA WAZEE WENYEWE NI PRO-CHADEMA, NA NAJUA YOU MIGHT BE GOING THRU A ROUGHT TIME, ACHENI TU IKAE HAPA !

Sasa kilichobaki ni kuungana na wazee wakuu kama muonavyo hapo chini !
jkchadema.jpg
 
Mbowe awaponda wenzake
*Asema wapo kwa maslahi ya tumbo
*Kuungana sawa na kufika mbinguni


Na Eliya Mbonea, Iramba

MGOMBEA urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bw. Freeman Mbowe (CHADEMA), amesema uwezekano wa viongozi wa kambi ya Upinzani nchini kuungana ni mgumu sawa na tajiri kuona ufalme wa Mbingu.

Alitoa kauli hiyo jana, alipokuwa akihutubia wakazi na wanafunzi wa chuo na sekondari ya Kinampanda mjini hapa, baada ya kuulizwa swali lililotaka kujua sababu ya wagombea urais wa kambi hiyo kutoungana na kuwa kitu kimoja.

Bw. Mbowe alisema chama chake kimekuwa cha kwanza katika historia ya upinzani nchini kuweka mbele dhana ya ushirikiano baina ya wapinzani.

"Vyama vichache vimepandikizwa na CCM kwa maslahi ya tumbo, CHADEMA mwaka 1995 haikusimamisha mgombea, badala yake iliungana na NCCR-Mageuzi, mwaka 2000 tukawaunga mkono CUF, jitihada zetu zote za kushirikiana zimekuwa hazizai matunda, hivyo mwaka huu tumesimamisha mgombea," alisema.

Aliongeza kuwa viongozi wengi wa Upinzani hawawezi kuungana kwa dhamira ya kuwatetea Watanzania, kwani wapo kwa ajili ya maslahi binafsi.

"Msifikirie kuwa kila mgombea urais au Mwenyekiti wa chama yupo kwa ajili ya kupigania mustakabali wa nchi, wamegeuza siasa kama biashara na wanaitumia kama vyanzo vya mapato," alisema mgombea huyo.

Alisema lazima CCM ikubali lawama za kulifikisha Taifa katika hali mbaya na ya kutisha, na kuwafanya wananchi wajione kuwa matatizo yao ni tofauti ya rangi za bendera badala ya kuwaeleza kuwa tatizo kubwa ni umasikini.

Akizungumzia nafsi yake, Bw. Mbowe aliwaeleza wananchi kuwa hakuingia kwenye siasa kwa ajili ya kutafuta ajira, kwani anachopigania si maslahi ya CHADEMA bali ya wananchi wote. "CHADEMA si mama yangu naweza kuiacha wakati wowote," alisisitiza msimamo wake.

Alisema kamwe hataacha kutumia busara na hekima za Mwalimu Nyerere katika kujenga utaifa, kwani kipindi chote cha miaka 44 bado misingi ya utaifa aliyoicha Mwalimu haijatekelezwa.

NAULIZA :
(1) Kama anajua fika kwamba vyama vya upinzani (ukiondo chadema) vimepandikizwa na ccm, iweje aungane nao wakati wamepandikiza na ccm ?
(2)Pili alisema kwamba wapinzani (chadema excluded)kwamba wapo kwa ajili ya matumbo yao, DOESNT THAT TECHNICALLY INCLUDE HIMSELF AS WELL kwa kuungana nao ??
(3) Je yupo tayari kueleza watanzania wakiwemo wapiga kura wake kwamba chama chake (CHADEMA) kimepandikizwa na CCM ?
(4) Na yeye binafsi kaungana na wenzake ili tumbo lake lipate rizki ?
(5)Kasema kwamba hayupo kwenye siasa kama ajira, ila hapo hapo alisema kwamba "wenzake"(wapinzani) DOESNT THIS EVEN RAISE MORE QUESTIONS THAN ANSWERS ?????????????


JAMANI NAOMBENI HII MUIACHE HAPA NA MSIIFUTE ! INAELEWEKA WAZEE WENYEWE NI PRO-CHADEMA, NA NAJUA YOU MIGHT BE GOING THRU A ROUGHT TIME, ACHENI TU IKAE HAPA !

Sasa kilichobaki ni kuungana na wazee wakuu kama muonavyo hapo chini !
jkchadema.jpg

Kada, jamani, amesema, VYAMA VICHACHE VIMEPANDIKIZWA NA CCM, hajasema ni vyote. Kwani nani hajui hilo?
Pili, huyu tusimuite FISADI, bado ni MKOPAJI ALIYECHELEWA KULIPA DENI!
Give the man a break! Its like u r going all out to paint a bad pic
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom