Je, Kinachomponza Mbowe ni Anasa?

Je, Kinachomponza Mbowe ni Anasa?

Status
Not open for further replies.
....upuuzi mtupu!! nimesoma toka post ya kwanza, mpaka hiyo hapo juu, hakuna lolote zaidi ya majungu na nonsense toka kwa washabiki na attackers wa Mbowe!! wooote machizi, ngoja nijirudie zangu kwenye thread za kutoka ughaibuni......

goodluck na mpambano wenu, yetu mimacho.
 
Hapa JF, tunasema kila mtu ana uhuru wa kuta maoni (we dare to talk openly) lakini,walau kwa tafsiri yangu, hii haimaanishi:

-Kuwa unaweza kusema tu hoja zianazoonyesha kabisa hayana mashiko...kama hili la mbowe hapa,
-Naamini kuan namna nzuri ya kutoa hoja bila kulazimika kuongea kama vile tupo kwenye mipasho
-Zaidi zinaonekana juhudi za wazi za kutupotezea muda wetu hapa kujadili mambo yasiyokuwa na msingi wa kujadiliwa.....ili tusahau kidogo mambo ya EPA, BOT etc
-Ningekuwa moderator, nahisi hapa ingekuwa kivumbi.....manake saa nyingine unahitaji nguvu za ziada kuvumilia watu wenye kutoa hoja kama hizi!
 
hapo ^ ni nini hapa kabisa cha kupoteza ?? mbowe kukataa kulipa deni au ? no way bana !
 
Mimi naona hii thread mungeitenganisha kati ya huu udaku wa Chinga na hilo
la Mbowe kukpa NSSF.

Mimi naona hilo deni lake NSSF ni issue na inafaa kujadiliwa hapa. Kama tulimjadili sana Sumaye kwa hilo kwanini tushindwe kumjadili Mboye ambaye kwa mimi naona kosa lake kubwa kuliko la Sumaye?
 
Hapa JF, tunasema kila mtu ana uhuru wa kuta maoni (we dare to talk openly) lakini,walau kwa tafsiri yangu, hii haimaanishi:


-Zaidi zinaonekana juhudi za wazi za kutupotezea muda wetu hapa kujadili mambo yasiyokuwa na msingi wa kujadiliwa.....ili tusahau kidogo mambo ya EPA, BOT etc
Nani amekuzuia kwenda kujadili EPA, BOT na ishu zingine?

"Usijitie kisebusebu na kiroho ki papo"
 
Nani amekuzuia kwenda kujadili EPA, BOT na ishu zingine?

"Usijitie kisebusebu na kiroho ki papo"

i wonder ! kama mtu anaona thread hizi zitawapotezea muda, then why dont they just WALK AWAY............... Wasije hapa even though siwezi kumkataza yeyote !
 
Mimi nadahani hapa suala si kwamba eti mtu yeyote ambaye hayuko madarakani kwa sasa basi yeye hana "elements" za ufisadi, la hasha! Ufisadi (greed) ni tabia binafsi ya mtu na inaweza kuonekana hata kama hajaiba mali ya umma.

Viongozi wa vyama vya upinzani tunaweza kuhoji tabia zao kutokana na maisha wanayoishi sasa na kugundua yupi mwenye sifa za ufisadi. Ukiona mtu anapenda sana kujilimbikizia mali basi huyo siku akipata nafasi serikalini ataiba pesa ya umma mpaka mtakoma. Tena anaweza hata kubadili katiba ya nchi ili atawale milele. Take my words!

Masaki hivi watu kama Bill Gate, Rock fellar na wengine wengi wenye utajili wao ni mafisadi? Au hawajawahi kukopa? Hebu fanya tafiti halafu utapata jibu, Acha Ushabiki wa kishamba!
 
MBOWE NAYE NI KAFISADI KENGINE.....!
USAHAU NA PENSENI ZA WAZEE WETU KALA MBOWE.
HALAFU KODI ALIZOKWEPA KWENYE MATANGAZO YA WASTAFU EAST AFRICA NITAKULETEA.
UNAJUA MRAMBA ALIMPA MATANGAZO YA ZAIDI YA BILLIONI MOJA KWA NJIA ZA KIKABILA?
 
MBOWE NAYE NI KAFISADI KENGINE.....!

sio kafisadi, yeye mabilioni yote katia mfukoni peke yake na sasa anakataa kulipa, !! kwa hiyo ni JIFISADI !

Natoka mara moja jamani naenda kuangalia kitu !! Big nyuzi will be coming out soon ! na hii ni kuhusu uchaguzi mkuu (Mbowe unajua ulifanya nini)!!
 
Mimi naona hii thread mungeitenganisha kati ya huu udaku wa Chinga na hilo
la Mbowe kukpa NSSF.

Mimi naona hilo deni lake NSSF ni issue na inafaa kujadiliwa hapa. Kama tulimjadili sana Sumaye kwa hilo kwanini tushindwe kumjadili Mboye ambaye kwa mimi naona kosa lake kubwa kuliko la Sumaye?

Mtanzania kuwa makini mkuu wangu .Angalia historia ni lini Mbowe alikopa pesa na jinsi ambayo amekuwa vocal kuwa chachafya akina JK .Kama kweli alikuwa na serious issue na pesa hii ya NSSF Chadema na Mbowe wameshiriki kampeni ngani na hujawahi kusikia CCM wanatafuta pa kufia ? Jamaa alikopa pesa na wao wanaleta usanii mkubwa na ndiyo issue imekuwa inaenda kisheria .Mbowe si mjinga kiasi hicho kwamba angaliweza kujiingiza kichwa kichwa . Lamwai waliingia kichwa kichwa na akina Mtemvu leo wamerudi CCM kwa kubanwa .Bado hili swala nasema kuna upuuzi wa watu kutuhamisha kweney mada za maana na tunakalia majungu. I hope this man will come forward na kueleza Mkasa na kumaliza mzozo ambao si mzozo ni RA na kundi lake wanatapatapa .
 
Ninaamini kabisa hayo MABILIONI yangetumiwa on other constructive,beneficial ways kuliko huyo mbowe kukataa kulipa na kuajiri ndugu zake ! holy crap !

MBOWE RUDISHA MABILIONI HAYO, WATANZANIA TUNUFAIKE !
 
KAMA WEWE MARA MWANAKIJIJI,MWAFRIKA WA KIKE, UKIZIDIWA UNAKUWA MADELA WA MADILU NA PEMBENI KUNA KOBA.

HALAFU MWANACHAMA MWANDAMIZI MWENZAKO ANAINGIA NA ASHA ABDALLAH. AJABU MWALIMU MZIMA ANADANGANYA KWENYE JF.
Chinga akutukanaye hakuchagulii tusi hata siku moja.

Nasikitika kwa sna jinsi upeo wako ulivyo jibanabana na wembamba wa hewa kiasi cha kushindwa kutofautisha Natural Signature za waandishi mabali mbali hapa JF.

Kuunganisha mawazo ya watu wanne tofauti na kusum up kuwa mwanakijiji ni dalili ya kupungukiwa na hoja pia kujawa na hofu ya mapambano wakati mapambano yenyewe hajaanza.

Mimi MADELA WA- MADILU ni mtu Tofauti kabisa dhidi ya wote watatu uliowataja.

Hoja zote zenye anuani ya Madela ni mali ya Madela na kamwe hazina uhusiano na watu wote uwadhanio.

Mawazo yangu kama Madela hayatokani na woga, ukali wa hoja za watua walio kinyume changu, wala hayatokani na nia ya kutaka kuleta mlolongo wa ubishi katika jamvi hili la JF kama ulivyo anza kubuni.

Mawazo yangu ni matokeo ya kukerwa na siasa za ubabaishaji za chama cha SISIEMU zilizo anza kunikera miaka kibao tangu nikiwa A Level.

Nimekuja hapa uwanjani kwa jina la MADELA WA- MADILU jina la uficho,sina haja ya kujificha kwa mara ya pili ya tatu na ya nne ili kuifanya hoja yangu ieleweke vyema.
Hoja zangu siku zote ziko wazi kabisa na mwelekeo wangu uko wazi.

Nishindwacho kuelewa kutoka katika hoja yako ya kuunganisha personality za watu ni kitu kimoja;
hoja yako kwamba mimi wakati fulani hujificha katika majina mengine matatu tofauti umeitafiti, umeibuni au mbashiri(mpiga lamuli) wako kakwambia hivyo?

Ningefurahi sana kusikia utetezi wako.

Kuna njia za kisasa kabisa za kumtambua mtu nyuma ya hoja kimaandishi na kivibwagizo.
Lakini wewe Chinga umeamua kuacha kila kitu na kushikiria maamuzi ya mbashiri wako kwa sababu unazozijua wewe.

Siwezi kukukatalia kuendelea kunihusisha na watu wengine watatu ambao kila mmoja ni mtu binafsi.
Nina uhakika kwa 100% kwamba watu hao pia wanashangaa jinsi wembamba wa upeo wako unavyozidi kukonda na kuuzidi wembamba wa hewa.

Alamsiki
 
Ninaamini kabisa hayo MABILIONI yangetumiwa on other constructive,beneficial ways kuliko huyo mbowe kukataa kulipa na kuajiri ndugu zake ! holy crap !

MBOWE RUDISHA MABILIONI HAYO, WATANZANIA TUNUFAIKE !

Kada,
You are either blowing this issue out of proportion, trying to make a big meal out of it or hujasoma story ya hii kesi. Kwa taarifa tu ni kwamba Mh.Mbowe alikopeshwa milioni 15 (na si mabilioni)!
 
Kada,
You are either blowing this issue out of proportion, trying to make a big meal out of it or hujasoma story ya hii kesi. Kwa taarifa tu ni kwamba Mh.Mbowe alikopeshwa milioni 15 (na si mabilioni)!

Mbowe aifilisi NSSF
::Adaiwa milioni 1200, hataki kulipa
::Atumia sheria kukwepa asifungwe
::Adai iliyokopa ni kampuni si yeye

na mwandishi wetu

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, anakalia kiasi kikubwa cha fedha za Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), kwa kukataa kulipa deni alilokopa.

Mbowe anadaiwa wastani wa sh milioni 1200 (sh bilioni 1.2), kutokana na deni alilochukua mwaka 1990 kwa nia ya kufanya upanuzi wa Mbowe Hotel ya jijini Dar es Salaam, maarufu kama Bilcanas.
 
Mbowe aifilisi NSSF
::Adaiwa milioni 1200, hataki kulipa
::Atumia sheria kukwepa asifungwe
::Adai iliyokopa ni kampuni si yeye

na mwandishi wetu

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, anakalia kiasi kikubwa cha fedha za Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), kwa kukataa kulipa deni alilokopa.

Mbowe anadaiwa wastani wa sh milioni 1200 (sh bilioni 1.2), kutokana na deni alilochukua mwaka 1990 kwa nia ya kufanya upanuzi wa Mbowe Hotel ya jijini Dar es Salaam, maarufu kama Bilcanas.

Uko very selective katika kujenga hoja yako.

Kwa hiyo mwaka 1990 alikopa 1.2 Billion kwa interest ya 31% kwa miaka 18?
Kwa hiyo sasa hivi anadaiwa ngapi? 1.2 Billion au 1.2Bill+31% interest?

Au alikopa 15,000,000.00 kwa interest ya 31% ambayo imekua sasa anadaiwa 1.2Bill?

Usahihi ni upi?

Hapa tunazungumzia kukopa kwa mktaba na siyo kuchota fedha kwa siri kwa kuunda kampuni Hewa kama DeepGreen au Green Deep na kuliza kisha kushinda uchaguzi halafu kujifanya fedha zinarudishwa au zimetumika usalama wa taifa???
 
The usual stuff from wana ccm. Tumewazoea. Amekopa atarudisha hakuwaibia wananchi. bank ni taasisi binafsi. Leave the guy alone.


P'se sema kuwa hawa wanaomsakama Mbowe ni CCM pumbavu maana, kuna watu wengi ambao ni CCM lakini hawakubaliani na upuuzi unaoendelea kwenye sirikali ya JK halafu kutaka kuifanya a legitimate business transaction ya Mbowe kuwa sawa na za kwao za Kifisadi
 
Kada,
You are either blowing this issue out of proportion, trying to make a big meal out of it or hujasoma story ya hii kesi. Kwa taarifa tu ni kwamba Mh.Mbowe alikopeshwa milioni 15 (na si mabilioni)!

hela hizo ni madafu (shilingi) au dala (dollars) ?? Nadhani hapo ndipo utakapostuka !
 
Chinga Na Kada,

Asilimia ya watu wengi walioendelea kimaisha wamekopa hela benki/taasisi za fedha. Ndio source pekee halali ya uhakika ukitaka "kutoka" ki uchumi.

Mbowe hajafanya kosa. Amekopa na atarudisha.

Vipi ukilinganisha Mbowe aliyekopa 15 Million Tshs mwaka 1990 na mpaka 2008 amerudisha 65 million Tshs na MAFISADI wa BOT walio IBA fedha billion 133 Mwka 2005/6 na mwaka 2008 wamerudisha only 50 Billion Tsh BILA RIBA?

Mimi mwenyewe benki za bongo zinanidai karibu 200 million Tshs na tunalipana kidogo kidogo hivyohivyo.

Wabongo kukopa ni muhimu sana. kama hutaki kukopa nenda KAIBE. Na ndio maana UFISADI hauwezi kuisha kwasababu ya imani zenu potofu!
 
Biashara yoyote kubwa ili iendelee inaitaji mkopo, kuna aina nyingi za mikopo. Short term debt and long term debt, sasa Mbowe alikopa kwa muda gani na kwa biashara gani? Hilo ni million dollar question. Kama alikopa kwa more than 10 years ili kufinance club yake that is fine, tatizo linakuja jee alikuwa anafanya month payments?

Na kama alikuwa hafanyi payments jee ni nani alikuwa anadefend collateral alizoweka zisiuzwe? Sababu kama unapiga kelele kwenye majukwaa kwamba CCM ni wezi, na wewe unatumia same strategy za CCM katika njia nyingine, then unakila haki ya kufananishwa na Gavana wa NY.

Nilishawai kusema natofautiana sana na Mboe sababu anaonyesha ni mbabaishaji. Mikopo yote ina rules and regulation, na dawa ya kukopa ni kulipa. Rejea maneno ya Mwalim " You borrow, you pay". Hakuna sijui nilikuwa sijui hili wala lile.

Ni mategemeo yangu wana CHADEMA wataomba explaination kutoka kwa kiongozi wao, jee haoni kama huko ni kufuja mali za umma? Jee yeye anajenga picha gani kama kiongozi? Jee ni kwa asilimia ngapi kuchelewa kwake kwa loan kuna adhiri viinua mgongo vya watu?

Sababu kumbuka kwamba pesa zile zinatumika kulipa pansion za baba na mama walio staff, sasa kama kuna mtu kwa njia moja au nyingine hataki kulipa kutokana na political power yake, then what is the different na mafisadi?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom