JamiiForums Usiku wa manane

JamiiForums Usiku wa manane

Mastory ya Bey

Leo bwana nikiwa town nikajikuta huyu hapa kwa fundi viatu,four angle yangu ilihitaji kuzungushiwa uzi maana sori kama ilianza kubanduka hivi

Kama unavyojua wabongo hatuna baya linapokuja swala la kupiga mastory,tukaongelea mada mbali mbali,mwisho wa siku tukaangukia kwenye No reforms No election

Kikubwa ambacho wadau kwa kauli moja,wamepinga sana majirani zetu wa Kenya kutaka kuingilia maswala yetu ya ndani

Wadau walihoji ya kwao yana washinda iweje waje kwetu kutaka kutuchafulia amani ya nchi yetu

Wao hawapati haki yao yoyote kwanza lazima wamwage damu,je hiyo ndio siasa? Alihoji mwamba mmoja

Mwamba mwingine akasema unajua wakenya wengi wamesoma lakini hawana kazi,ndio maana wanastress sana,hivyo hawana raha na nchi yao na wako wako confused,so wanaona tuko hapi pamoja na kula ugali na tembele lkn mwisho wa siku tunaishi kwa amani bila machafuko

Akaendelea kusema kama kuna watu wana msoto wa maisha basi ni Wakenya,wengi wao wanaishi kwenye mabanda ya bati,nadhani machakosi ni mfano mmoja wapo

Wadau wakaendelea kusema si unaona wenzetu Wakongo,kutwa kuchwa wanatembea na magodoro,hiyo yote ni kutokana na machafuko nchini mwao,kwahiyo tujifunze kutoka kwa wenzetu

Wadau wakaendelea kusema ifike kipindi Viongozi wa dini waache kuzungumzia mambo ya siasa,kwasababu wataanza kutugawa kutokana na dini zetu,na kila familia ya Watanzania tumechanganya,je si tutaanza kubaguana ndugu kwa ndugu kwasababu kuna waislamu na wakristo

Vile vile wakasema wenzetu wanabaguana kwa makabila huko kwao Kenya,ndio maana fujo na kumwaga damu ni sehemu ya maisha yao

Hivyo Watanzania tusiingie kwenye mtego wao,wapambane na shida zao watuache na maisha yetu

Wadau wakasema Watanzania tuache kabisa kushabikia hao Wakenya na kuwaona ni mashujaa,hao wako na shida mingi sana

Ni bora tuonekane ni waoga lakini mwisho wa siku watoto wetu na familia zetu waendelee kuishi kwa amani
Hivyo vijiwe vya town sio vya kukaa wamejaa mashushu wa nchi hii
 
4_unchoose17.0.png
ndo kilichobaki😂
 
secretarybird unacheka nini? Muome 😅😅😅😅
Halafu kabla ya ID hii ulikuwa unatumia ipi? Maana kuna ID kama 5 nilijua zote za mtu mmoja, maana sizielewi ikiwemo hii yako.
Wanaume mnabadili ID kwasababu gani? Au mmeunganisha mabehewa humu? 😁😁😁😁😁
 
secretarybird unacheka nini? Muome 😅😅😅😅
Halafu kabla ya ID hii ulikuwa unatumia ipi? Maana kuna ID kama 5 nilijua zote za mtu mmoja, maana sizielewi ikiwemo hii yako.
Wanaume mnabadili ID kwasababu gani? Au mmeunganisha mabehewa humu? 😁😁😁😁😁
Wana minyororo... 😂😂😂 Maana ukisema cheni itaonekana ni fupi😂😂
 
secretarybird unacheka nini? Muome 😅😅😅😅
Halafu kabla ya ID hii ulikuwa unatumia ipi? Maana kuna ID kama 5 nilijua zote za mtu mmoja, maana sizielewi ikiwemo hii yako.
Wanaume mnabadili ID kwasababu gani? Au mmeunganisha mabehewa humu? 😁😁😁😁😁
ID yangu ya zamani sitaitaja maana imefanya mambo makubwa na ya ajabu ajabu😀
 
Back
Top Bottom