JamiiForums Usiku wa manane
Mastory ya Bey

Wahanga wa vita ya pili ya dunia pamoja na machungu makubwa waliyopata kutokana na vita,walikuja baadae kujigundua wamekuwa watu zaidi

Kuna mambo ambayo hapo awali hawakuyapa kipaumbele katika maisha,kwa lugha nyingine waliyachukulia poa huenda kwa kutoona umuhimu wake

Lakini machungu ya vita na uzoefu walio upata wakajifunza kuyathamini maisha,wakajifunza kuthamini mambo madogo madogo ambayo hapo awali yalionekana sio chochote kwao

Waliona umuhimu wa kuwa na amani katika maisha yao,huenda hapo awali walipo ona sehemu nyingine ya dunia kuna machafuka walichukulia poa tu

Na huu mfano tunaweza kujichukulia sisi wenyewe Watanzania,tunapoona machafuko ya majirani zetu Congo,wakiwa wanatembea kana kwamba wanaandamana wakiwa na mizigo yao ,tunachukulia poa kabisa,lakini hatujui machungu ambayo wenzetu wanapitia

Tunapowaona majirani zetu Kenya wakimwaga damu tunawaona mashujaa na vidume,lakini katu tusiombe haya yatukute,kwani hakika tutajua thamani ya kuwa na amani

Kwahiyo wakati wa vita vya dunia,waathirika waliona jinsi watu walivyoteswa,kubakwa na kuuwawa,hii iliwaathiri sana hasa pale kumbukumbu zilipo wajia vichwani mwao

Lakini baadae walikuja kuwa watu imara,kimtazamo,kifikra na waliyaona mambo au maisha katika tofauti kabisa

Hapa tunajifunza kwamba kwa kila machungu ambayo tunapitia nyuma yake kuna somo kubwa sana tunajifunza,kwa kila maumivu na machungu tunayopitia ni mchakato wa kufikia sehemu fulani katika maisha yetu

Tufahamu kwamba haijalishi ni hali gani tunapitia kwasasa,ni maumivu kiasi gani yanatukuta kwa sasa,lakini mwisho wa siku,tutakuja kuwa tofauti kabisa,tutakuwa watu ambao wenye uzoefu mpya na maono mapya

But don't look for trouble,let matatizo yakutafute wewe,kwa njia hiyo yatakufundisha kitu fulani maishani
 
Info :

Watu wa Urusi ndio watu pekee ambao huwa wanaongea ukweli bila kujua athari ya maneno yao

Yani wao kukwambia umeongea ujinga hata kwa mtu geni sio ishu kabisa,wamejifunza kusema juu ya hisia zao

Wao ukifanya vizur wanakwambia,ukiboronga wanakwambia mchana kweupe

Je ni nini siri ya yote haya?

Ni kwamba baada Uchumi wao kutetereka baada ya communism,waliona njia pekee ya kujikwamua katika hali hiyo ngumu ya kiuchumi ni kuwa waaminifu

Kwakuwa waaminifu kwa hisia zao na mtazamo wao ni rahisi kujua nani umuamini au nani ni mtu ambaye unaweza kumtegemea

Yani ni kawaida kwao kutoka date na mwanamke halafu ndani ya dakika tatu ya mazungumzo yako na yeye,anakwambia kwamba UMEONGEA UPUUZI,yani mwanamke ambaye wala hamjazoeana anakupa ukweli live kuwa umeongea upuuzi

Binafsi nimekutana nalo hili,nikiwa Songea,nilikuwa nakaa kwenye hosteli za misheni,hapo raia wa kigeni huja kwa wingi sana

Nikakutana na mtoto wa kirussia,nikaomba namba akanipa,lakini baadae katika mawasiliano yetu whatsapp akawa hanipi sana ushirikiano,siku moja akanitext akaniambia HANIPENDI

Umeona hakujali how i will feel,hakutaka kujipotezea mda wala kunipotezea mda

Nami nilimshukuru kwakuwa alinifanya nifokasi na mambo mengine

Hao ndio Warusi/Warussia
 
  • Thanks
Reactions: apk
Nukuu ya leo :

"Kuwa na ndoto kubwa, anza kidogo, fanya kazi kila siku."
Anonymous

Nukuu hii inakuhimiza kuanza safari ya mafanikio hatua kwa hatua, bila kuogopa ukubwa wa ndoto zako. Kila hatua ndogo ni maendeleo.
 
LEO KATIKA HISTORIA :

Leo ni Mei 22, tarehe ambayo imejaa matukio muhimu ya kihistoria duniani. Hapa ni baadhi ya matukio ya kipekee yaliyotokea siku kama ya leo:

---

🌍 Matukio Muhimu ya Kihistoria

- 1960 – Tetemeko kubwa zaidi kuwahi kurekodiwa duniani
Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 9.5 lilitikisa kusini mwa Chile, likisababisha vifo vya zaidi ya watu 1,600 na kuharibu miji kama Valdivia. Tsunami iliyofuata ilisababisha vifo zaidi katika maeneo ya mbali kama Hawaii, Japani, na Ufilipino. [1]

- 1906 – Ndugu wa Wright wapatiwa hati miliki ya ndege
Orville na Wilbur Wright walipata hati miliki ya "Flying Machine," hatua muhimu katika historia ya usafiri wa anga. [1]

- 1980 – Mchezo wa video wa Pac-Man waachiwa rasmi
Mchezo huu maarufu ulizinduliwa na kampuni ya Namco nchini Japani, na baadaye kuwa moja ya michezo maarufu zaidi duniani. [2]

- 2012 – Mnara wa Tokyo Skytree wafunguliwa kwa umma
Mnara huu wenye urefu wa mita 634 ni mnara mrefu zaidi duniani na jengo la pili kwa urefu baada ya Burj Khalifa. [2]

- 2010 – Ajali mbaya ya ndege ya Boeing 737
Ndege ya Air India Express Flight 812 iliteleza kwenye njia ya kutua katika uwanja wa ndege wa Mangalore, India, na kusababisha vifo vya watu 158. [2]

- 2017 – Shambulio la bomu katika tamasha la Ariana Grande

Watu 22 waliuawa katika shambulio la kujitoa mhanga lililotokea kwenye ukumbi wa Manchester Arena nchini Uingereza. [3]

---

🎉 Maadhimisho ya Kumbukumbu

- Harvey Milk Day
Inaadhimishwa kila Mei 22 kwa heshima ya Harvey Milk, mwanaharakati wa haki za LGBTQ+ na mwanasiasa wa kwanza waziwazi kuwa shoga kuchaguliwa kushika wadhifa wa umma nchini Marekani. [4]

- Siku ya Kitaifa ya Bahari nchini Marekani (National Maritime Day)
Inaadhimishwa kuanzia mwaka 1933 kwa kumbukumbu ya safari ya kwanza ya kuvuka bahari kwa kutumia nguvu ya mvuke ya meli ya Savannah mnamo Mei 22, 1819. [5]

---
 
Ila ubwabwa wa hashimu rungwe una maajabu watu wanahamia kula biriani samaki alafu uchaguzi ukiisha wanarudi kula makande 🤣🤣🤣🤣🤣.
Mbu wanang'ata sana huku lindo wajameni mnisamehe 😂🤣🤣
 
Mastory ya Bey

Dukani kwa Mangi nakutana na kijana mmoja barobaro hivi,anamwambia Mangi nipimie maharage,karanga, njugu mawe na nafaka nyingine mbali mbali huku anaendelea kuangalia orodha ambayo ametumiwa na mzazi mwenzake,ilikuwa na maandalizi ya kutengeneza unga WA lishe WA mtoto wao.

Kilichonipeleka Kwa Mangi ni kutuma hela sehemu kwahiyo nikiwa katika kusubiri nihudumiwe nikabahatika kupata mawili matatu.

Kijana akasema hawa watoto ambao tunawahudumia na Kula vizuri mara nyingi huwa Wajinga Wajinga Sana,tofauti na watoto ambao wanakulia katika shida Sana.

Kwa kawaida huwa napenda ukweli kwahiyo ikabidi nimuweke Sawa bwana mdogo Kwa kumuuliza,je hayo mambo umesikia wapi kuwa mtoto akila vizur anakuwa mjinga mjinga?

Akajibu huyu bwana mdogo kwakusema " unajua bro Sisi ambao tumekulia kwenye shida sio Wajinga Wajinga kama watoto wa siku hizi"

Nikamwambia hapana ujinga unatokana na malezi na si Kula vizuri ,kila mtoto anastahili Kula vizuri kwani ni msingi WA afya Bora.
Pembeni yetu alikuwepo mrembo mmoja amejistiri Kwa kuvalia baibui jeusi pamoja na mtandio wake kichwani,Akaona isiwe tabu ngoja nae achangie chochote.

Yule mrembo akasema "kwakuwa ulikulia kwenye shida haimaanishi na mwanao pia akulie kwenye shida,mbona Sisi zamani tulikuwa tunaenda shule hatupewi hela yoyote ya kula tunaenda na tunarudi lakini siku hizi watoto wetu hata WA primary lazima utampa walau shilingi Mia tano kila siku"

Kijana baro baro akaona isiwe tabu akafungua code;

" Mimi bwana nimeishi Kwa shida Sana,mama yangu amenilea yeye Peke yake,na kila nilipo muuliza kuhusu Baba yangu,aliniambia Baba yako amekufa"

Aliendele kijana kusema "kila nilipokuwa namuuliza mama yangu anionyeshe Baba yangu alikuwa ananijibu Baba yako amekufa,basi ikabidi niamini hivyo Tu,kwahiyo mama ndio alipambana na kunilea Kwa shida Sana. Lakini nilipo fikia kidato cha nne nilikuja kukutana na Baba yangu mzazi,na tunaenda Sawa vizuri mpaka Leo"

Nikamuuliza je Baba yako alikwambia nini kuhusu kutowajibika kwake kukulea mpaka umekuwa kijana mkubwa Tu? Kijana akasema Baba aliniambia kuwa upande wa mama ndio walizingua na hawakutaka kumuona kabisa.

Nikamwambia anyways huenda anajitetea Tu au anasema ukweli,lakini mwisho wa siku ukweli wanaujua wazazi wako.

Mimi na Yule mrembo aliyevaa baibui jeusi tukamwambia unafanya vizuri kumhudumia mwanao,kwakuwa wewe uliishi Kwa shida haimaanishi pia mwanao naye anapaswa kuishi Kwa shida,badilisha iyo ciycle na mtunze mwanao Kwa nguvu zako na mapenzi yako yote.

Mimi na mrembo Yule kila mtu akaondoka na kumwacha kijana anakusanya mazagazaga yake.
 
Nukuu ya leo :


"Usikate tamaa. Mwanzo huwa mgumu, lakini kila hatua inaongeza nguvu."
Methali ya Kiswahili

Nukuu hii inakutia moyo kuendelea kusonga mbele hata kama changamoto ni nyingi mwanzoni. Kila juhudi ina thamani.
 
Back
Top Bottom