JamiiForums Usiku wa manane
Ni majira ya usiku saa tatu kuelekea saa nne natembea kwa miguu katika manispaa fulani hapa nchini kando ya ziwa dogo. Nakutana na kijana mmoja mwenye haiba ya mvuta bangi akiliza mlio wa fisi. Nashikwa na hasira kutaka kumuonya aache kuigiza mlio wa fisi. Ile tu napishana naye na kuachana naye fisi wakaibuka kwa kasi wakikimbilia alikoelekea huyo kijana mliza mlio wa fisi. Fisi wakatokomea kwenye shamba la mpunga wakimtafuta mwenzao aliyewaita kula mzoga wasimuone, Hicho ndicho kisa nilichokutana nacho usiku kijana kuigiza mlio wa fisi na fisi wakatokea wakidhani ni mwenzao kawaita kuja kula mzoga
Hii ishu yako hatar sana

Kwahiyo watu wanaita mafisi kama mbwa tu

Je utapita tena maeneo hayo😂😂
 
Mazungumzo ya usiku

KAA KARIBU NA WATU WANAO WEZA KUKUPA RAMANI

Ni mazungumzo ya vijana wawili wanao fahamiana...ni uwanjani katika mchezo wa soka pale kitaa cha Tabata. Jioni hiyo niliamua kwenda kucheki mazoezi ya mpira kwani kiwanja Hicho hakipo mbali Sana na ninapoishi.

Na haya ndio mazungumzo Yao:
Kijana wa Kwanza '' Kaka hiyo fani yako ya umeme vipi umeshaifanyia kazi kidogo au bado?''
Kijana wa Pili '' bado Kaka..nilikuwa mkoa lkn hakuna Mishe Mishe yoyote ndo bro kaniita huku dar nije tufanye biashara''
Kijana wa Kwanza '' kwahiyo Kaka utasomeaje kitu halafu usikifanyie kazi huoni hapo utakuwa kama umepoteza Ada ya bure Tu?''

Mpaka hapo Kwanza hawa jamaa kama wakawa wamenifanya nifuatilie mazungumzo Yao Kwa karibu kidogo. Ikanikumbusha dada yangu ambaye alisomea wild life pale Sokoine University na mapaka Leo hajafanyia chochote Ile bachelor yake..na haya huwatokea watu wengi Tu..alichosomea Sicho anachokifanyia kazi sasa!

Msemaji wa Kwanza akaendelea na darasa lake ambalo hata Mimi likanivutia..akaendelea ujue mdogo wangu ebu jitahidi kujichanganya na watu wa fani yako huenda wakakupa ramani ya kuanzia na kufanyia kazi kile ulichosomea..unaona Mimi huwa napenda kujichanganya na mabroo ambao najua kabisa huenda wakanipa ramani na muongozo wa wapi nipite na hatimaye nifanikishe mambo yangu.

Msemaji akaendelea ambaye kwasasa naomba nimuite motivational speaker maana si Kwa darasa lile '' Mimi bwana huwezi kunikuta nakaa na watu ambao hawaeleweki eleweki lazima nikae vijiwe ambavyo vina mitazamo chanya na kusaidiana tuinuke katika Maisha yetu''...daah hakika lilikuwa darasa zuri Sana kutoka Kwa yule mdau..nilifaidika Kwa mambo mawili Kwanza kucheki vijana wakifanya mazoezi na pili kupata darasa la bure ambalo huenda wengine wanalipia huko duniani.

Basi akapita muuza kahawa pale tukapiga vikombe viwili vitatu na Mda wa mazoezi pamoja na lile darasa la bure kuisha then tukachapa lapa na kuelekea majumbani kwetu.

Mlinzi wa zamu!
 
Back
Top Bottom