Ni majira ya usiku saa tatu kuelekea saa nne natembea kwa miguu katika manispaa fulani hapa nchini kando ya ziwa dogo. Nakutana na kijana mmoja mwenye haiba ya mvuta bangi akiliza mlio wa fisi. Nashikwa na hasira kutaka kumuonya aache kuigiza mlio wa fisi. Ile tu napishana naye na kuachana naye fisi wakaibuka kwa kasi wakikimbilia alikoelekea huyo kijana mliza mlio wa fisi. Fisi wakatokomea kwenye shamba la mpunga wakimtafuta mwenzao aliyewaita kula mzoga wasimuone, Hicho ndicho kisa nilichokutana nacho usiku kijana kuigiza mlio wa fisi na fisi wakatokea wakidhani ni mwenzao kawaita kuja kula mzoga