JamiiForums Usiku wa manane
To yeye siku hizi hatukuoni hata kwa bahati mbaya mtaa wa usiku wa maneno...au kwako wewe kila siku ni mchana😂😂
 
2333

Najipa ukatibu wa ulinzi,ili niratibu taratibu za ulinzi katika mtaa wa usiku wa manane

Mwenyekiti Rayns faili utalikuta kwa secretary wako
 
Ni majira ya usiku saa tatu kuelekea saa nne natembea kwa miguu katika manispaa fulani hapa nchini kando ya ziwa dogo. Nakutana na kijana mmoja mwenye haiba ya mvuta bangi akiliza mlio wa fisi. Nashikwa na hasira kutaka kumuonya aache kuigiza mlio wa fisi. Ile tu napishana naye na kuachana naye fisi wakaibuka kwa kasi wakikimbilia alikoelekea huyo kijana mliza mlio wa fisi. Fisi wakatokomea kwenye shamba la mpunga wakimtafuta mwenzao aliyewaita kula mzoga wasimuone, Hicho ndicho kisa nilichokutana nacho usiku kijana kuigiza mlio wa fisi na fisi wakatokea wakidhani ni mwenzao kawaita kuja kula mzoga
 
Ni saa nane usiku wa manane usingizi umekata, nachukua kiredio kidogo kando ya kitanda nafungulia TBC taifa nakutana na historia ya Waziri mkuu na makamu wa kwanza wa Rais hayati Cleoopa David Msuya. Wachambuzi wa mambo ya siasa wanamchambua alivyofanya akiwa waziri mkuu. Mzee John Samwel Malecela maziri mkuu mstaafu naye anasikika akimuelezea vema hayati Msuya enzi za uhai wake. Mkononi mwangu usiku huu nachukua chombo changu cha mawasiliano na kuwasha data kisha nafungua JF/JA kuperuzi yaliyojiri. Nazama moja kwa moja kwenye uzi wa usiku wa manane. Ni usiku tulivu
 
Back
Top Bottom