Mazungumzo ya usiku
UNAPOPATA MATATIZO HUWA UNAKIMBIA AU HUWA UNAPAMBANA NAYO
Mwaka 2008 Taliban walichukua utawala wa pakistani kimabavu na kuweka utawala wao wa sheria,ikiwemo kuzuia matangazo ya television,hakuna sinema,hakuna wanawake kutoka nje ya nyumba zao bila kuongozana na mtu wake wa karibu kama baba au kaka
Na istoshe wakazuia wanafunzi wa kike kuendelea na elimu,lakini binti mmoja anaitwa Malala mwenye umri wa miaka 11, yeye alipinga uamuzi huo,na kuamua kuhudhuria shule kama kawaida,na alikuwa mstari wa mbele kupaza sauti na kupigania haki ya watoto wa kike kwenda mashuleni
Mnamo mwaka 2012 akiwa anatoka shule na wenzake,mara paap wakasimamishwa na askari wa taliban,akiwa amebeba silaha au bunduki,na kuwauliza abiria waliokuwa mle ndani ya basi,kwamba nionyesheni Malala
Kwa mshangao mkubwa na ujasiri Malala akajitambulisha mwenyewe,na hapo hapo yule gun man akampiga Malala risasi ya kichwa,na wakasema kwamba kama binti huyo atapona basi watamuua yeye pamoja na baba yake
Lakini kwa neema ya Mwenyezi Mungu alipona na kuendelea na harakati zake kama kawaida,kwa hali ya kawaida tungetegemea angeogopa na kuacha harakati zake,lakini binti wa watu kwa ujasiri mkubwa kabisa,ndio kwanza alipata hamasa na nguvu mpya ya kupigani haki wa wanawake na kuwa msemaji wao
Kutokana na jitihada zake mnamo mwaka 2014 alipata Tuzo ya Nobel na kutambuliwa mchango wake katika jamii
Je wewe ni aina ya watu kama Malala ambao huwa hawa quit pale wanapo kutana na changamoto Au ndio changamoto kidogo unakata tamaa na kukimbia
Ngoja nikwambie kitu msomaji wangu,hii dunia inahitaji watu ambao wapo strong enough to fight back,watu ambao huwa wanasonga mbele daima na kurudi nyuma kwao ni mwiko
Hata wewe pia unaweza kuwa imara na madhubuti kama Malala.
Mlinzi wa zamu!