Kwa mujibu wa marvel endgame ni ya 2023, avengers wakagawana stones za kuenda kuchukua katika miaka tofauti tofauti na sehemu tofauti tofauti kisha wakarudi tena 2023 ili kukamilisha lengo lao la kuwarudisha watu wote waliopotea kwenye snap.
Sasa kulingana na rules za time travel walipomaliza kutumia zile stones ilibidi wazirudishe walikozitoa, ili wasije wakasababisha tatizo la time loops na change in realities ambapo ndiyo wakakubaliana captain america azirudishe halafu arudi.
Ambapo hulk wakati anaicontrol ile time machine akasema “for him he’ll take as long as he needs for us it’s going to be five seconds”, akimaanisha kwamba huko captain anakoenda kurudisha mawe atachukua muda wowote anaojisikia lakini huku 2023 alikowaacha kina hulk itakuwa ni sekunde tano sababu time works differently in the quantum realm.
Hivyo akahesabiwa hadi tano akitegemewa kurudi lakini matokeo yake hakurudi kama walivyokubaliana ndiyo wakamuona kwa pembeni akiwa ni mzee, ambapo wanasema kuwa aliporudisha yale mawe aliamua kurudi tena nyuma ya muda miaka ya 1940s ambapo mchumba wake peggy carter alikuwa hai akaenda kuishi naye.
Sasa kumbuka kilichokuwa kinamfanya asiwe mzee ni kwa sababu alikuwa kwenye barafu sasa alirudi nyuma ya muda na ule muda alioutumia kwenye barafu, badala yake akautumia kuishi na mchumba wake kwahiyo kwa hali ya kawaida akija kurudi 2023 lazima tu awe mzee sababu alienda kuishi maisha ya kawaida kama watu wengine.
Mkuu kama haujaielewa hiyo concept nzima ya time travel ya marvel basi achana nayo tu utachanganyikiwa maana marvel siyo kila kitu wamekielezea kwenye movies zao, vingine wanavielezea mitandaoni kupitia articles na documentaries zao mbalimbali ndiyo utaelewa na kuzifuatilia hizo inabidi uwe marvel fan haswa.