JamiiForums Usiku wa manane
ndio mkuu nimepanda noah na nissan tu.......mabasi ya kusini bado

Kuna kipindi kukaa mbali na matatizo inasaidia sana, chukua tu ushauri wa bure kiongozi. Kaa mbali. Hii vita inapiganwa kwa nguvu za giza, atomic, nyuklia, marungu, vifaru, manati, teknolojia, mizinga, fitna na aina zote za silaha...nikikuangalia vizuri sijui hata kama unaweza kunyanyua upinde.

Kuwa mpole kwanza gavana
 
Siku hiyo nilitoka siku moja kabla nikasafiri nikaenda kulala sehemu karibu na kituoa cha kuchinjia, siku husika niliamuka mapema nikaanza safari kuelekea kituoni. nilipofika nikapanga foleni ilikuwa kubwa yenye kukatisha tamaa ila sikujali hadi nikafika kunako kuhalalisha jambo likiwa limeelekezwa kunako Kibla.

Nikatoa jambia yangu, kilichofuata ni kuangalia nembo bila kujali mtu husika, nikafyeka nyasi zilikuwa zimenawiri na zenye kuvutia. Hakika mwenye roho nyepesi asingeweza kuthubutu ila mimi niliweza.

Baada ya kumaliza shughuli pevu nikaanza safari tena kurejea kwenye makazi yangu huku nikiwa na shauku pamoja na kuelekeza masikio yangu kwa Lubuva ili niweze kutangaziwa safari ya matumaini.

Kilichotokea sitasahau kamwe.......

nadhani tangu siku hiyo uliamini msemo wa wahenga kuwa"Mipango si matumizi"
 
Back
Top Bottom