JamiiForums Usiku wa manane
Siku hiyo nakumbuka jua lilinitwanga baraaabara, nikanunua maji kiroho safi nikagawia watu pale ilikua mida ya saa tano jua linachoma utosini, bashasha hazikupungua usoni tukiamini safari ya matumaini inaanza..kama msimamo hautabadilika, kichinjio kitaendelea kutumika kwa matumizi mengine ya ID lakini sio shughuli zozote za NEC
Siku hiyo nilitoka siku moja kabla nikasafiri nikaenda kulala sehemu karibu na kituoa cha kuchinjia, siku husika niliamuka mapema nikaanza safari kuelekea kituoni. nilipofika nikapanga foleni ilikuwa kubwa yenye kukatisha tamaa ila sikujali hadi nikafika kunako kuhalalisha jambo likiwa limeelekezwa kunako Kibla.

Nikatoa jambia yangu, kilichofuata ni kuangalia nembo bila kujali mtu husika, nikafyeka nyasi zilikuwa zimenawiri na zenye kuvutia. Hakika mwenye roho nyepesi asingeweza kuthubutu ila mimi niliweza.

Baada ya kumaliza shughuli pevu nikaanza safari tena kurejea kwenye makazi yangu huku nikiwa na shauku pamoja na kuelekeza masikio yangu kwa Lubuva ili niweze kutangaziwa safari ya matumaini.

Kilichotokea sitasahau kamwe.......

 
Back
Top Bottom