Iceman 3D na carbamazepine niliwambia muda fulani kuwa lilia uzuri sio bahati kwasababu:-
1.Mimi nilileta uzi wa kutafuta mwenza hapa lakini sikupata PM hata moja licha ya kuweka vigezo vya chini kabisa,kisa na mkasa nina sura ya babu yangu na umbo la mjomba wangu baunsa.
2. Nikiwa darasani nijitahidi sana kumtega mwl.wangu Nleterewa Nganengo lakini wapi...ndio kwanza hata kilinge kakikimbia kisa sina uzuri.
3. Nikaamua kumtega mwl.wangu Mwifwa kwa kila aina ya mitego lakini wapi, ndio kwanza anampaparikia mumu
4.Nikasema ngoja nijaribu bahati yangu kwa HB wa Kigogo, lol kaniacha mchana kweupe kaenda kwa Demiss
5. Nikahamia kwa dingimtoto ndo hata hakugeuka busy kumgombania Inna yeye na mjr95
6.Nikaona isiwe tabu Kichwa Kichafu atanifaa, thubutu hata jicho hakupepesa mbiombio kwa jje's
7.Nikajilengesha kwa Manga ML, duh kumbe hana habari na mimi yuko zake kwa Maserati anayemendewa na Spade 4 spade.
8. Nikasema ngoja nijichekeshe,chekeshe kwa Joseverest labda yeye atanielewa kumbe yuko kwenye list ya wanaomgombea Neybright kama mpira wa kona.
9. Nimejichetua kwa No Escape na ipogolo wapi?
10. Nikajipitisha pitisha kwa Samaritan,nikaona yeye kanielewa kanitumia mpaka muamala tobaaa alivyoiona tu sura yangu akasitisha muamala
Ndio maana nawaambia ndugu zangu kuwa lilia UZURI usililie BAHATI maana kama bahati ninayo sana tu ndio maana nashindaga tatu mzuka na biko ila mbona sigombaniwi na mimi kama mpira wa kona kama wenzangu?

