Siku iyo niseme konyagiiii ili save my Life..
Ilikua iviii mida ya saa tatu tatu ivii Nika amka oga nikawa na safari ya kwenda kunduchii ni zaidi ya 37km kutoka napo kaa nilikua na mihadi na rafiki yangu.
Nikaenda sokoni nunua kuku andaliwa na mazaga ya home kufikia saa tano piga konyagiiii nikasema nipeleke vitu home ndio niende kunduchii
Vituoni kulikua na watu wachache sana siku iyoo muitikio ulikua mdogo sana sanaa
Kufika home wife akanipa supu nikanywa mara usingiziii naamka saa 12 JIONI mtandao umezimwa wife akawa ananionyesha matukio kwa simu yake aliyo tumiwa mchana
Labda ninge enda kunduchii ningeforce kurudi yangenikuta
Vijiweni Kila mtu anasimulizi....
Kuna jamaa alienda Buguruni saa 5 ..kukaribia saa 6 mchana
Yaani kufika saa 8 mchana ni moto mkali na vurugu...akajibana sehemu mpaka saa 12 jioni
Hakuna usafiri..akaanza kutembea kuelekea Vingunguti ..akaona mbele zinakuja gari...ni ku shoot tuu ...
Yeye akajua Hawa wanashoot hewani...
Akawa anaona mbele Kuna mtu anapiga kelele ya miguu yake imevunjwa...
Akajibana pembeni kwenye uchochoro...
Akawa ameduwaa...akashangaa anaambiwa njoo huku kibarazani ndani utakufa ukikaa barabarani..
Anasema ilikuwa saa 2 usiku...alikaa hapo na kulala kibarazani mpaka Asubuhi..
Kesho yake alitembea mpaka barakuda...
Akapata usafiri mpaka Segerea...
Anasema hakujua kama usiku ule kulikuwa na risasi za kuvunja au kuua..
Yeye alijua ni mambo ya kawaida na jioni imefika wacha niende nyumbani...
Kuvutwa kwake na kuambiwa kaa hapa mpaka Asubuhi kuliokoa Maisha yake