Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,445
7,813
Leo bunge limetengua kanuni kuruhusu wageni wasioruhusiwa kuingia ndani ya ukumbi wa Bunge wakati wa hotuba ya Rais Samia Suluhu, miongoni mwao ni Makamu wa Rais, Philip Mpango na Rais wa Zanzibar, Hussein Mwinyi.

Pia spika Ndugai aliwashauri wabunge wasivae tai nyekundu kwasababu ni kwaajili ya mwenye mamlaka, ushauri wa Ndugai baade ukaondoka kwenye hiyari na kusema watakaovaa wataishia geti la nje. Rais Samia Suluhu anatarajiwa kuhutubia bunge leo saa kumi baada ya kuchukua madaraka ya Urais kutoka kwa hayati John Magufuli.

"Ningependa kuwakumbusha wabunge siku anapokuja kiongozi, mkuu wa nchi haishauriwi sana kwa wenzangu na mimi kuvaa tai nyekundu, nadhani tumekubali ile red inabakia na mwenye mamlaka, ni vizuri kuyajua hayo mambo, jioni tutakaporudi tai nyekundu utarudia geti la nje" Alisema spika Spika Job Ndugai.

 
"Ningependa kuwakumbusha wabunge siku anapokuja kiongozi, mkuu wa nchi haishauriwi sana kwa wenzangu na mimi kuvaa tai nyekundu, nadhani tumekubali ile red inabakia na mwenye mamlaka, ni vizuri kuyajua hayo mambo, jioni tutakaporudi tai nyekundu utarudia geti la nje"- Spika Job Ndugai

#Bungeni
 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama ametoa hoja ungeni ya kuvunja kanuni ya 160 kanuni ndogo ya kwanza ya Kanuni za Bunge ambayo inaelekeza wageni wataoruhusiwa kuingia bungeni watakaa maeneo maalumu yaliyotengwa kwa ajili yao

Bunge limelazimika kutengua kanuni hizo ili kuruhusu baadhi ya viongozi walioalikwa na Spika wa Bunge kuingia ndani ya Ukumbi wa Bunge, Aprili 22, 2021 ambapo Rais wa Tanzania, Samia Suluhu atazungumza na Bunge

Wageni watakao ruhusiwa ni Makamu wa Rais wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango, Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi, Makamu wa Kwanza na wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Jaji Mkuu wa Tanzania, Jaji Mkuu wa Zanzibar, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar na Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki

Hoja hiyo ilikubaliwa na wabunge, Hivyo wageni hao hawatakaa katika maeneo maalumu ya wageni kama ilivyokuwa awali bali wataingia ndani ya ukumbi wa bunge
 
Joe Biden siku ya uzinduzi wake alivaa tai ya Blue, na hata mara kibao katika shughuli zake anavaa tai aina tofauti tofauti, and yet ni the most powerful man on earth, ana mamlaka kweli kweli ya kutisha tena.

Sasa hawa watu mambo ya kukataza kuvaa tai nyekundu wanatoa wapi? Sio ulozi kweli?
 
Back
Top Bottom