WanaJF,
Kwa ufahamu wangu wa mambo ni kwamba siku zote ukitaka kulinganisha vitu, huwenda kwa kufananisha au kuvipambanisha, ni lazima angalau viwe ama wawe (kama ni watu), vyenye kukalibiana.
Nimeona uzi hapa JF na baadhi ya vyanzo vingine vya mawasiliano vikiweka mashindano ya aina hii, yani kati ya Lowassa na watu aina ya Dr Slaa. Haya ni matusi wanaJF.
Hapa Tanzania, Lowassa ana historia pana na ndefu sana katika siasa zetu, hili halihitaji mjadala. Lowassa amekuwapo enzi na enzi, Lowassa anayajua mawimbi ya kila aina ya mikiki mikiki ya siasa, Lowassa anajua kupwa na kujaa kwa siasa, Lowassa anaijua saikolojia ya Watanzania vizuri. Kweli mtu wa aina hii una mlinganisha na Dr Slaa?!!!
Dr Slaa ametumia asilimia 65 - 70 ya maisha yake yote kama padre (ingawa palimshinda), mbali na hilo, ametumia asilimia 40 - 50 ya maisha yake nje ya mipaka ya Tanzania, Dr Slaa hatujui Watanzania. Iweje leo mtu wa aina hii awe na uhalali wa kupambanishwa na gwiji?
Namaliza kwa kusema kwamba, kama kuna matusi ya kumtukana Lowassa yapo basi yatumike hayo mengine, ila naombeni msimtukane Lowassa kwa kumpambanisha na Dr Slaa. Chonde chonde wana JF.