Tarehe 23 Desemba 2014, Mwana Chadema mmoja anayetumia akaunti ya CHADEMA In Blood aliweka kwenye mtandao wa facebook, picha mbili za watu ambao iliaminika sana kuwa wangeweza kupeperusha bendera ya Vyama vyao kwenye nafasi ya urais katika uchaguzi uliofanyika mwezi oktoba 2015 ili majina hayo yaweze kupigiwa kura kujua nani anakubalika, moja ya majina ya hayo ni la aliyekuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dr. Wilbroad Slaa na nyingine ilikuwa ya Kada wa CCM na Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya Richmond, Edward Lowassa.
Matokeo ya kura hizo yalikuwa ni kama yanavyoonekana hapo chini.
Swali langu watu hawa hawa walioonesha kwa kiasi kikubwa kuwa Dr. Slaa ni zaidi na kiukweli ndivyo ilivyokuwa, ndivyo ilivyo sasa na ndivyo itakavyobaki kuwa, leo ndiyo wanaoongoza kumtukana, kumdhihaki na kumfedhehesha Dr. Slaa kupitia mtandao huu huu ambao kupitia kwake walionesha kuwa na imani naye na siyo Lowassa? Wamerogwa na nini? Tunajifunza nini kuhusu mfano huu?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.