Uchaguzi 2020 NEC isipomuengua Tundu Lissu, ni go-ahead ya kuipoteza CCM Zanzibar. Je, Muungano utasalimika?

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,339
51,884
NEC isipomuegua Tundu Lissu, ni go-ahead ya kuipoteza CCM Zanzibar. Je, muungano utasalimika?


Na, Robert Heriel

Jambo kubwa linaloendelea katika vichwa vya wafuatiliaji wa masuala ya kisiasa ni pamoja na Tundu Lisu kupenya NEC. Hofu kubwa ipo miongoni mwa wafuasi wa Mgombea huyo wa CHADEMA wapo katika fukuto la wasiwasi kwa mgombea wao kuenguliwa. Pengine ni hofu ya uzushi kuwa Tundu Lisu ataenguliwa, lakini pengine sio uzushi bali ni jambo halisi kutoka kwa vyanzo walivyonavyo CHADEMA.

Tundu Lisu naye siku ya jana tarehe 23/08/2020 alielezea hofu yake ya kuenguliwa na NEC kugombea Nafasi ya Urais kupitia CHADEMA. Je hii ni njama na hila za CCM kuhakikisha Tundu Lisu hatoboi? Je, ni kwa nini njama hii itumike? Je, CCM wanaogopa kushindwa na Tundu Lisu? Lakini Maswali haya yanaweza yakamezwa na swali moja; kwani NEC ni CCM? Jibu, ni hapana. Kama NEC sio CCM Kwa nini Tundu Lisu aogope kukatwa? Labda tuseme kuwa Huenda CCM inamkono wake Huko NEC, Lakini nani ataweza kuthibitisha hayo? Je matendo ya NEC ni kiashiria cha hofu kwa Lissu?

Binafsi naamini kuwa Tundu Lisu hata apewe nafasi ya kugombea Urais kamwe hataweza kushinda, ingawaje anaweza kufurukuta na kujipatia kura nyingi tuu. Niliwahi kusema siku 60 ni nyingi sana kwa mtu mwenye uwezo wa kushawishi watu kama Tundu Lissu. Naufahamu uwezo wa Lisu katika kujenga hoja.

Kwa muono wangu, CCM hawana hofu na Tundu Lissu kushindwa, bali wanahofu ya kushindwa huko visiwani Zanzibar. Jicho langu linaniambia kuwa Tundu Lisu atapata 40% za kura huku Mhe Rais aliyemadarakani John Magufuli akipata kura 50%. Hata hivyo hilo ni jicho langu na linategemea na usawa katika mchakato wa uchaguzi. Jicho langu linaniambia kuwa hofu ya CCM ipo Zanzibar zaidi kuliko Bara.

Ili CCM iendelee kuwepo Zanzibar itabidi Tundu Lissu aenguliwe hivi Leo 25/08/2020. Kwa muono wangu, ACT- WAZALENDO itachukua Zanzibar licha ya kuwepo kwa Figisu Figisu. Maalimu Seif ananafasi kubwa ya kushinda huko Zanzibar, atakachohitaji na Backup kutoka bara ambayo ataipata kwa Tundu Lissu na Zito Kabwe.

Kutokana na Tabia ya Msimamo wa Tundu Lissu, kama hataenguliwa, najua atakubali kushindwa hiyo october 28 kama atakuwa ameshindwa halali na atashindwa halali. Lakini atampa nguvu Maalimu Seifu ambaye ataibuka kidedea huko Zanzibar.

Na ikiwa CCM itakuwa imepoteza Zanzibar ni wazi kuwa yatakuwa maandalizi ya 2025 kutolewa huku bara. Njia rahisi wanayoweza kuitumia Wapinzani ni kuiondoa CCM Zanzibar kwani kule ndio rahisi kutokana na udogo wa eneo na uchache wa watu. Kisha waje waiondoe huku bara.

Swali kubwa linalopiga kichwa changu ni je, usalama wa Muungano upo kwa kiasi gani mara tuu CCM itakapofungasha virago huko Zanzibar? Kwa jicho langu, naona muungano hautabaki salama. kulingana na viongozi wa Upinzani wanaogombea mwaka huu kote bara na visiwani. Tundu Lissu niliwahi kumsikia akizungumzia suala la Muungano alipokuwa akihutubia huko Zanzibar. Maneno yake nayakumbuka kiasi, ni kama alikuwa akiwaambia Wanzanzibar wanatawaliwa na Wabara, hivyo wanatakiwa wajikomboe. Lakini Pia ukimuangalia Maalimu Seif yeye naye anamsimamo wa namna hiyo ingawaje hapendi kuuonyesha.

Seif anachoshindwa mara nyingi kwenye uchaguzi huko Zanzibar ni Backup kutoka Bara. Mwaka 2015 hakupata Backup nzuri kutoka kwa Edward Lowasa, hii ni kutokana na tabia ya upole wa Lowasa wa kumuachia Mungu. Lakini mwaka huu, Tundu Lissu na Zito Kabwe watampa Backup ya kutosha endapo atashinda.

Nina uhakika CCM hawana Hofu kubwa na Tundu Lissu kushinda bara kwani wanajua hatashinda, lakini hofu ipo visiwani.

Muhimu: NEC izingatie haki kwa kila mgombea, asiwepo wa kuonewa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
 
Mwaka 2015 MAGUFULI/ mnyapara aliyechoka na muoga alipata kura 54000 tu kwa jiji lote la dar.
Amekuwa akiitwa kiongozi wa wanyonge japp sio kweli.
Hajaongeza mishahara kwa watumishi.
Amefurusha watumishi hewa huku akiwaacha kina Bashir wakidunda na kuongeza ukubwa wa makalio.
Alipora Korosho za watu huko Kusini, Kauai zoo la mbaazi,pamba na tumbaku.
Aliahidi kujenga viwands matokeo YAke anahubiri ndege na Barbara.
Aliahidi Ajira mpaka Leo hakuna kitu vijana wapo mitaani.
Anapiga watu risasi mcshane kweupe
 
I agree with you partly. Nzanzibar is the major worry for CCM. Lakini nasmini pia kama TUME ikifanya kazi ya TUME na siyo kufanya kazi ya ccm kama ambavyo imekuwa inafanya miaka yote, inawezekana kabisa Tundu lisu akashinda.
Wawe huru na wahesabu kura Kama zilivyopigwa na wasitumie nafasi yao kuwazuia wapinzani kupita.

Wasiwasi wangu, ambao naamini Niko sahihi Ni kwamba time yetu hii haiwezi kamwe kuwa huru na kutenda Haki, kwani Hawa Ni waajiriwa was CCM.
 
Nipo njiani naelekea tume ya uchaguzi nitawafahamisha kitakachokuwa kikiendelea ndani ya Tume, hata hivyo in brief Yeye hatakuwa mgombea mwaka 2020 kwani maagizo kutoka kwa bwana yule ashatufikia nasi hatuna budi isipokuwa kuungama kwa bwana.
 
NEC jaji kaijage ni ukumbi wa CCM na jaji kaijage kwa siku anaongea na viongozi wa CCM zaidi ya mara 30, week hii Jaji kaijage amekuwa na vikao mfululizo na IGP, Lipumba, Shibuda, polepole na viongozi wengi wa CCM wakipanga njama jinsi ya kumkomoa kumhujumu Tundu lisu na pia kuidhoofisha chadema kwa ujumla.

NEC ni Sumu mbaya iliyoandaliwa kuwaua chadema kuteketeza upinzani wenye nguvu, wafanyakazi wote wa NEC ni makada wa CCM ni Tumeccm ni Tume ya uchaguzi mbaya kuliko Tume zote Duniani.
 
Hivikwanini NEC isimuengua mgombea wa CCM!?

Kwa kufanya kampeni miaka 5 kabla ya wakati, kunyamazia risasi 38 alizopigwa mbunge hadharani n.k?
Mtukufu kaanza kampeni tokea 2016 alikuwa akipita anafanya mikutano anagawa pesa cash huku akiwa amepiga marufuku mikutano ya wapinzani, juzi juzi pia kafanya kampeni kabla ya mda kwa kununua jogoo ( Rushwa) kwa tshs laki moja na kumtafutia mama yake mzazi mchumba huko Rufiji.
 
Tume ipitishe wagombea wrote wenye sifa, tunataka haki itendeke kwenye sanduku LA kura..
Shibuda na Lipumba baada ya kupewa Advance na CCM sasa wanashinda na kukesha na viongozi NEC kupanga njama za kuwahujumu chadema na ACT yafaa kuanzia sasa nyendo za Shibuda na Lipumba zifuatiliwe mguu kwa mguu mwisho wa siku waje kuchezea kichapo waache uchawi wao wa kifala.
 
Nipo njiani naelekea tume ya uchaguzi nitawafahamisha kitakachokuwa kikiendelea ndani ya Tume, hata hivyo in brief Yeye hatakuwa mgombea mwaka 2020 kwani maagizo kutoka kwa bwana yule ashatufikia nasi hatuna budi isipokuwa kuungama kwa bwana.
Tanzania hakuna Tume huru ya uchaguzi bali kuna Tumeccm inayoigiza kuwa ni ya uchaguzi.
 
Shida mpka muweke namba za simu

Sent from my Infinix HOT 4 Pro using JamiiForums mobile app
au unataka tuweke namba za cyprian Musiba na Le mutuz madalali wa siasa watesi wakubwa wanaotafuna pesa za umma kwa njia haramu kwa kisingizio kuwa wanaisaidia CCM kutokomeza chadema na kurejesha mfumo wa chama kimoja.
 
Back
Top Bottom