Bay of Pigs vs Cold War: Marekani, Cuba na USSR, ulimwengu kiganjani mwa CIA, CRF na KGB - na aibu ya dunia kwenye ulingo wa kijasusi

Comred Mbwana Allyamtu

JF-Expert Member
Jun 28, 2016
348
847
BAY OF PIGS Vs COLD WAR: MAREKANI, CUBA NA USSR, ULIMWENGU KIGANJANI MWA CIA, CRF NA KGB; NA AIBU YA DUNIA KWENYE ULINGO WA KIJASUSI.

Na. Comred Mbwana Allyamtu(CMCA)
Wednesday-16/06/2021
Kilimanjaro National Park, Marangu Kilimanjaro Tanzania.

Kwenye jengo la Pentagon ghorofa ya pili upande wa kushoto yani left wing kuna chumba namba 273, chumba ambacho ndio ofisi ya mshauri mkuu wa jeshi na wizara ya ulinzi ya Marekani yani "Chiefs of Staff counselor" , asubuhi ya Tarehe 13 mwezi wa 9 mwaka 1960, Kamati Maalumu ya Viongozi wa Juu Kijeshi nchini Marekani (Joint Chiefs of Staff Committee) chini ya Bw. L.M. Lemnitzer, iliidhinisha Operesheni iliyopewa jina la "Northwoods", kwa lengo la kutafuta sababu ya kuivamia kijeshi nchi ya Cuba (pretext for military invasion of Cuba), Chini ya operesheni hiyo, kamati ilipendekeza mfululizo mashambulizi yenye taswira ya kigaidi ndani ya miji ya Miami, Washington, D.C na kwingineko, meli za mizigo na abiria za nchi ya Marekani zingelipuliwa au kuzamishwa, ndege kutekwa, mauaji ya raia kutekelezwa makusudi, utoaji wa orodha 'feki' za wahanga wa mashambulizi ili kuufanya umma wa Wamarekani kuingia taharuki na kuipigia kelele za hasira serikali kulipiza kisasi kwa kuivamia Cuba. Kwa mujibu wa mpango huo, kila shambulizi lilipangwa kuhusishwa na nchi ya Cuba.

Kuidhinishwa kwa operation hii kulifatia baada ya mapinduzi ya Cuba yaliyofanyika mwaka 1959, mapinduzi hayo hayakuungwa mkono na mataifa mengi, hasa Ulaya na Marekani kwa sababu moja kubwa kuwa utawala wa Castro ulikuwa unaweka hatari masrahi ya Marekani nchini Cuba, sababu hiyo ni kuwa uongozi wa kijeshi ulioondolewa madarakani nchini humo chini ya dikteta Fulgencio Batista ulijaa vibaraka, walioweka mbele matumbo yao kwa kuigeuza Cuba kama mali ya mabepari, hasa Marekani, hivyo Castro na wanamapinduzi wenzake muda mfupi baada ya mapinduzi hayo, waliwatimua Wamarekani, kwa kuhodhi makampuni yote ya biashara, migodi, kilimo na Njia zote za uchumi.

Kitendo cha utawala wa Castro kutaifisha makampuni ya Marekani kiliisababishia Marekani hasara kubwa kibiashara, huo ndio ukawa mwanzo wa uadui baina yao, Mipango ya kuipindua serikali ya Fidel Castro ikaanza kwa nguvu sana, na kwa namna tofauti, ntaeleza hili kwa undani kabisa huko mbeleni, serekali ya Marekani litaka kuirudisha madarakani serikali itakayo waunga mkoni huko Cuba ili waendelee kulinyonya taifa hilo, jambo ambalo Castro na wenzake hawakutaka litokee.

Jambo la kujiuliza hapa ni kwanini Marekani iliiamua kuweka uadui na Cuba, swali la kujiuliza zaidi ni kwanini Marekani ilifamya maamuzi ya kutaka kuivamia Cuba! Maswali haya na mengine kibao kuhusu masrahi ya Marekani nchini Cuba yanairudisha nyuma historia ya Marekani na Cuba miaka 70 kabla ya tukio la kuivamia Cuba asubuhi ile ya mwaka 1961 kwenye ghuba ya mapigano ya Playa Girón ambayo hufahamika kama bay of pigs.

Hivyo basi...

Historia ya nchi hizi mbili inaanzia karne ya 18, kipindi ambacho Cuba ilikuwa "shamba la Bibi" kwa himaya ya kikoloni ya Kihispania, Katika karne ya 19 mwishoni, wazalendo wanamapinduzi wa Cuba walianza kuasi dhidi ya wakaloni wa Hispania na kutaka kuitawala nchi yao wakiongozwa na Jose Mart, hivyo kupelekea kupiganwa kwa vita tatu vya kuasi utawala wa Kihispania, Vita hivyo ni vita vilivyojulikana kama vita vya miaka kumi (1868–1878), nyingine ni ile vita iliyojulikana kama vita ndogo (1879–1880) na nyingine ni vita ya kupigania Uhuru wa Cuba (1895–1898), vita ambavyo Cuba ilijitangazia Uhuru wake, na Jose Mart kuwa rais wa kwanza wa Cuba guru, huyu José Mart nchini Cuba hutazamwa kama Baba wa taifa, mwasisi na mwanamapinduzi mkuu nchini humo, falsafa yake ya "Siri, Vamia, shambulia, gawanya na miliki" ndio ilikuwa kanuni kuu ya mapigamo kwa Castro, tutaliona hilo kwenye uvamizi wa Playa Girón au Bay of Pigs huko mbeleni.

Lakini serikali ya Marekani ilianzisha vita na himaya ya utawala wa Hispania nchini Cuba, ikumbukwe kuwa Hispania bado ilikuwa inataka kuendelea kuikalia Cuba na hivyo kupelekea vita ya Hispania na Marekani mwaka 1898, vita ambayo Marekani ilitaka kuikalia Cuba, hivyo mara kwa mara Marekani ilivamia kisiwa cha Cuba na kuyafurusha majeshi ya Hispania nje ya kisiwa cha Cuba, Katika mpango maalum uliopewa jina operation Habana, Marekani walipanga kuingiza askari 375 ndani ya visiwa vya Cuba katika mapigano ya Tayacoba katika vita kati ya Hispania na Marekani, ambapo Tarehe 20 May 1902, Marekani iliishinda Uhispania na serikali mpya ilijitangaza na kuunda Jamhuri ya Cuba chini ya usimamizi wa Marekani huku gavana wa kijeshi wa Marekani Leonard Woodhanding akimuongoza Rais Tomás Estrada Palma, Mcuba mzaliwa wa Cuba mwenye uraia wa Marekani.

Ni katika vita hivyo ndio Marekani ililikalia eneo la Guantanamo bay kama sehemu ya miliki ya Marekani kama malipo ya vita dhidi ya Hispania, Taratibu idadi kubwa ya walowezi na wafanyabiashara wa Kimarekani walikuwa wanawasili Cuba na hadi kufikia mwaka 1905 asilimia 60 ya bidhaa za mashambani zilikuwa zinamilikiwa na wananchi wasio Wacuba kutoka Marekani ya Kaskazini na kati ya mwaka 1906 na 1909, wanajeshi wanamaji wapatao 5,000 wa Kimarekani waliweka kambi katika kisiwa chote cha Cuba, na walirudi tena mwaka 1912, 1917 na 1921 na kuweza kuingilia mambo ya ndani ya Cuba, wakati mwingine bila hata ridhaa ya Wacuba wenyewe, hivyo hatimae Cuba ikawa sehemu ya nje ya Marekani.

Baada ya kuona namna Marekani ilivyoingia nchini Cuba toka mwaka 1898 kwa kuwafurusha Wahispania Sasa tuendele mbele ili kupata kiini halisi cha undani wa mapinduzi yenyewe ya mwaka 1959 nchini Cuba, lakini pia kwa nini tena Wacuba waliokuwa wakiishi uhamishoni, hususan wale ambao waliokuwa wakiishi jijini Miami katika jimbo la Florida walitaka kuuangusha utawala wa Castro nchini Cuba, pia nini hasa taifa la Marekani liliamua kuwekeza fedha nyingi ili kufanikisha kuudondosha utawala wa Castro, jambo ambalo tutaona baadae ni namna gani Marekani ilivyo injini uvamizi wa Bay of Pigs.

Mwezi Machi mwaka1952, Jenerali wa Cuba na mwanasiasa, Fulgencio Batista, alitwaa madaraka katika kisiwa hicho, na kujitangaza yeye binafsi kama Rais baada ya kumpindua Rais aliyekuwa madarakani, Carlos Prío Socarrás wa chama cha Partido Auténtico.

Batista alifuta uchaguzi wa Rais uliotarajiwa kufanyika, awali Batista alipata kiasi fulani cha uungwaji mkono, lakini kwa Wacuba wengi waliona hiyo ni aina ya utawala wa kidikteta wa mtu mmoja ambao Batista anajaribu kuuanzisha, Wengi wa wapinzani wa utawala wake waliamua kuasi na kuchukua njia ya mapambano ya silaha kumpinga na kujaribu kuuondoa utawala wake, hiyo ilichochea mapinduzi ya Cuba, Mojawapo ya makundi haya lilikuwa ni kundi la The National Revolutionary Movement (Movimiento Nacional Revolucionario – MNR), kundi la muungano wa kijeshi lililojumuisha watu wengi wanachama wa daraja la kati lililoanzishwa na Profesa wa Philosofia, Rafael García Bárcena. Kundi jingine lilikuwa The Directorio Revolucionario Estudantil (DRE), ambalo lilianzishwa na muungano wa wanafunzi wa vyuo vikuu, The Federation of University Students (FEU) chini ya Rais wake José Antonio Echevarría (1932–1957).

Hata hivyo, miongoni mwa makundi yote hayo, kundi bora kabisa katika hayo yote yaliyokuwa yakimpinga Batista lilikuwa la "26th of July Movement" (MR-26-7), lililoanzishwa na Mwanasheria aliyeitwa Fidel Castro, Castro kama kiongozi mkuu wa MR-26-7, aliligawanya kundi lake katika mfumo wa vikundi vya watu kumi kumi, huku kila kikundi kikiwa hakijui uwepo wa kikundi kingine na kujua shuguli wanazozifanya kikundi kingine.

Kuanzia Desemba mwaka1956 mpaka mwaka1959, Castro aliongoza jeshi la msituni kupambana dhidi ya majeshi ya Batista kutoka katika ngome ya kambi yake kwenye milima ya Sierra Maestra, Kusambaa kwa vuguvugu la mapinduzi kulimfanya Batista kumpunguzia umaarufu, na kufikia mwaka 1958 majeshi yake yalikuwa katika uwezekano mkubwa wa kusalimu amri, hatimae Tarehe 31 Desemba mwaka 1958, Batista alijiuzuru na kukimbilia uhamishoni, huku akiondoka na kiasi kikubwa cha pesa zaidi ya dola za Kimarekani 300,000,000. Baada ya Batista kukimbia, Urais ukaangukia kwa Mwanasheria Manuel Urrutia Lleó, aliyechaguliwa na Castro, huku wanachama wa MR-26-7 wakidhibiti idadi kubwa ya nafasi katika baraza la mawaziri.

Ilipofika Tarehe 16 Februari mwaka 1959, Castro akachukua Madaraka ya kuwa Waziri Mkuu, akaondoa uwezekano wa kufanyika kwa uchaguzi, kwa siku za mwanzoni, Castro alidai kuwa utawala mpya ni mfano wa demokrasia ya moja kwa moja ambayo umma wa wacuba unaweza kujikusanya kwa pamoja na kufanya maandamano na kuelezea hisia za demokrasia wanayoitaka moja kwa moja kwake yeye binafsi, Hata hivyo wapo waliolaumu utawala mpya wakisema si utawala wa kidemokrasia, moja ya makundi walio laumu ni walowezi wa kimalekani ambao asilimia kuwa walikuwa ndio wanao miliki 95% ya uchumi wa Cuba.

Hatua hiyo ilianza kutengeneza kudorola kwa uhusiano wa Marekani na Cuba, jambo ambalo viongozi kadhaa Washington waliitazama Cuba kama adui mpya, kufatia hatua hiyo serikali ya Cuba ilitoa amri kwa makampuni ya mafuta ya Esso na Standard Oil yaliyokuwa chini ya makampuni kutoka Marekani na kampuni ya Anglo-Dutch Shell ya Kiholanzi kuanza kusafisha mafuta yaliyonunuliwa kutoka katika nchi za Umoja wa Kisoviet badala ya Marekani lakini kutokana na shinikizo kutoka serikali ya Marekani makampuni hayo yalikataa.

Castro alijibu kwa kuyazuia kusafisha mafuta kisha akayataifisha makampuni yote na kuwa chini ya usimamizi wa serikali ya Cuba, katika kujibu mapigo, nayo serikali ya Marekani ikaacha kuagiza sukari kutoka Cuba hivyo kupelekea Castro kutaifisha raslimali nyingi zaidi zilizokuwa zinamilikiwa na Marekani, ikiwemo mabenki na viwanda vya sukari.

Uhusiano zaidi wa Cuba na Marekani ukaanza kuzorota kufuatia kulipuka kwa meli ya Kifaransa iliyoitwa "Le Coubre" na kupelekea kuzama katika bandari ya Havana mnamo mwezi Machi, mwaka 1960, Chanzo cha mlipuko hakikujulikana lakini Castro aliitaja hadharani serikali ya Marekani kuwa ndiyo iliyohusika na hujuma hiyo, lakini jambo ambalo wengi awajui ni kuwa tulio hilo la kuilipua meri hiyo ya "Le Coubre" serikali ya Marekani ilihusika, ntalieleza hili kwa upana hapo mbeleni.

Asubuhi ya tarehe 13 Oktoba, mwaka1960, serikali ya Marekani ilizuia kwa sehemu kubwa bidhaa kadhaa kusafirishwa kwenda Cuba kasoro bidhaa za madawa na baadhi ya vyakula, ikiashiria kuanza rasmi kwa vikwazo vya kiuchumi, Cuba nayo katika kujibu mapigo kamati ya Taifa ya Mabadiliko iliamua kuchukua usimamizi wa biashara binafsi 383 zilizokuwa zinaendeshwa na Marekani, na siku ya tarehe 1 Oktoba na tarehe 25 Oktoba zaidi ya makampuni 166 ya Marekani ambayo yalikuwa yakifanya shughuli nchini Cuba, majengo yao yalichukuliwa na kutaifishwa ikiwemo Coca-Cola na na kampuni ya Sear Roebuck.

Tarehe 16 Desemba, Marekani tena ikaacha kuagiza robo yote ya sukari iliyokuwa ikiagiza kutoka Cuba, Serikali ya Marekani ikazidisha kuipinga serikali ya kimapinduzi ya Castro.

Hatimae Mwezi Agosti,1960 katika mkutano wa umoja wa nchi za Amerika, yaani Organization of American State (OAS) uliokuwa unafanyika Costa Rica, Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Christian Herter, hadharani alidai kwamba utawala wa Castro "kwa uaminifu mkubwa unafuata misingi ya njia za Bolshevik" kwa kukazia mfumo wa chama kimoja cha siasa kwa serikali yake kuweka vyama vya wafanyakazi chini yake, kubana uhuru wa raia na kuondoa uhuru wa kuongea na uhuru wa vyombo vya habari na akaenda mbali zaidi kwa kusema kuwa nchi za kijamaa zinaitumia Cuba kama ngome yake ya kusambaza mapinduzi katika nchi za ncha ya Kaskazini na akatoa wito kwa wanachama wengine wa umoja huo wa OAS kuilaani Cuba kwa ukiukwaji wa haki za binadamu.

Cuba nayo ikajibu mapigo, Castro alielezea namna jamii ya watu weusi inavyonyanyaswa na tofauti kubwa ya matabaka ya wafanyakazi aliyoishuhudia wakati akiwa New York, na kupiga kijembe na kudhihaki kuwa huo ndiyo "uhuru wa hali ya juu, demokrasia ya hali ya juu, utu wa hali ya juu, na kustaarabika kwa hali ya juu kwa jiji hilo." Akadai kuwa masikini wa Marekani wanaishi katika "bakuli la mabepari wanyonyaji", pia Castro aliushambulia mtiririko wa vyombo vya habari vya Marekani na kuulaumu kuwa unaendeshwa na wafanya biashara wakubwa.

Kwa namna nyingine Marekani ilikuwa inajaribu kuimarisha uhusiano wake na Cuba, Majadiliano mengi kati ya wawakilishi kutoka Cuba na Marekani yalifanyika katika kipindi hiki, Kurekebisha uhusiano wa fedha wa kimataifa ndiyo ilikuwa dira kuu ya majadiliano hayo, Mahusiano ya kisiasa ilikuwa ajenda nyingine kubwa ya mikutano hiyo, Marekani ilieleza kuwa haitaingilia aina ya serikali ya Cuba inayoitaka au mambo yake ya ndani hata hivyo Marekani ikaiaumu Cuba kufuta siasa za Umoja wa Kisovieti, walimshawishi Castro kuacha siasa za kisoviet kwa kumuhaidi miassada kibao ya kuendesha nchi, lakini Castro aligoma, hapa ndipo Marekani ikaamua kubadilisha muelekeo dhidi ya Cuba, hapa Sasa Marekani wakaingia kazini ili kuiadabisha Cuba.

Mwezi Augosti, mwaka 1960, CIA waliwasiliana na kundi la Cosa Nostra lilokuwa na makao yake jijini Chicago ili kuandaa mipango mbalimbali ya kuwaua Fidel Castro, Raúl Castro na Che Guevara, katika mpango huo Marekani ilikubaliana na kikundi hicho kuwa baada ya kupachika serikali ambayo inawaunga mkono nchini Cuba, watakubaliana kati ya CIA na kundi hilo la Mafia kupata umiliki wa michezo ya bahati nasibu, biashara ya umalaya na madawa ya kulevya ndani Cuba, hivyo mipango hiyo ikapangwa kuanza rasmi mwaka 1960, lakini mpango huo ulitakiwa lazima upate idhini ya rais wa Marekani.

Hivyo mkurugenzi mkuu wa CIA Allen Dulles, akaamdaa kikao maalumu ili kujadili namna ya kumshawishi raisi Dwight D. Eisenhower mpango wa kuivamia Cuba na kumuua Castro, Dulles akiwa na Rolando Cubela, afisa mipango wa CIA mwenyeji wa Frolida ambae alikuwa anaifahamu vizuri Cuba, akapewa kazi ya kuinjinia ramani mpango wa namna ya kuivamia Cuba, ikumbukwe kwamba Shirika la Ujasusi la Marekani yaani Central Intelligence Agency (CIA), ni shirika la kijasusi ambalo liliundwa na serikali ya Marekani mwaka 1960 kupitia sheria iliopitishwa na bunge la Congress mwaka 1947, kupitia sheria iliyoitwa "National Security Act" azimio namba 90551, CIA "ilikuwa ni zao la Vita Baridi", shirika hili lilibuniwa ili kuzikabili njama za shirika la ujasusi la Umoja wa Kisoviet la KGB.

Sasa basi...

Hatua hii ilifatia baada ya tishio la kusambaa kwa ukomunist ulimwenguni kuwa mkubwa, CIA ilipanua shughuli zake kukabiliana na mambo ya kiuchumi, kisiasa na mambo ya kijeshi katika kulinda masilahi ya Marekani, na wakati mwingine kutumia njia za hatari ili kulinda maslahi hayo ya Marekani, Mkurugenzi wa CIA kwa wakati huo, Allen Dulles, alikuwa na wajibu wa kusimamia operesheni hizo duniani kote, hivyo jioni ya tarehe 7 mwezi 8 1960 Allen Dulles alituma ujumbe wa maneno kwenda kwenye kamati maalumu ya usalama wa taifa nchini Marekani, ujumbe huo uliokuwa na code namba SO444.PO1117 ulipokelewa na mwana mama Heren McKay aliyekuwa ofisni siku hiyo, Kwenye jengo la CIA Langley kulikuwa na kikao kilefu kilichomalizika saa 5:52 usiku kikao hicho kiliwajumlisha Rolando Cubela,Desmond Fitzgerald, Robert Kennedy, Bw. L.M. Lemnitzer, na Allen Dulles mwenyewe.

Azimio la kikao hicho ilikuwa ni kumshawishi Raisi Dwight D. Eisenhower kuhusu mpango wote ulio wasilishwa mezani na Rolando Cubela wa namna ya kuivamia Cuba, azimio hilo ulikuwa na mapendekezo matatu, Mosi ni kumshawishi Raisi Eisenhower kuidhinisha uvamizi huu bila kulishirikisha bunge, maana kama wangelishirikisha bunge wabunge wasingekubali kwasababu mda mfupi nchi ya Marekani ilikuwa inajiandaa kuingia kwenye uchaguzi mkuu, hivyo wanasiasa wengi wasingekubali kujitia doa wakati wakijianda kugombea nafasi mbalimbali, lakini hapo hapo chama cha Republican kisenge unga mkono mpango huo, hivyo waliona mpango huo ungependeza kama Raisi Eisenhower mwenyewe autekeleze kwa siri.

Pili, walipendekeza kuwa mpango huo utekelezwe na CIA wenyewe bila kushirikisha Kitengo kingine, hii ili kuwa na maana moja kubwa kuwa kwakuwa Marekani ilikuwa kwenye vita baridi na Urusi hivyo kuruhusi vyombo vingine kuhusika ingehesabika kuwa ni vita, hivyo Urusi ingeingilia kati na kuufanya mpango kuwa mgumu, swali la kujiuliza hapa ni kwanini Marekani iliiogopa Urusi kuingia kwenye vita hivyo? Lakini swali lingine zaidi la kujiuliza je ni kuwa Marekani haikuwa na uhakika na mpango huo? Yote haya nitayaeleza huko mbele.

Pendekezo la Tatu, ilikuwa ni wakati wanaivamia Cuba, lazima tukio la uvamizi lifanywe na wa Cuba wenyewe ili ulimwengu usione kuwa uvamizi huo taifa la Marekani halihusiki kwa namna yoyote ile.

Hivyo mapendekezo hayo yote matatu yaliwasilishwa na Rolando Cubela ambae alipewa kazi hiyo na Allen Dulles, kikao hicho kiliidhinisha mapendekezo hayo ambayo yalitakiwa kufika mezani kwa Raisi Eisenhower ikulu ya White house, wakati hayo yakiendelea ule ujumbe wa maneno wenye code namba SO444.PO1117 uliopokelewa na mwana mama Heren McKay aliyekuwa ofisni siku hiyo, Bi,Heren McKay ndie aliyekuwa msaidizi binafsi wa Raisi Eisenhower kwenye ikulu ya White house, mara moja akampelekea ujumbe huo raisi ofisini kwake, alimkuta Raisi Dwight D. Eisenhower akiwa na kikao na maafisa kadhaa wa ikulu, baada ya muda Raisi Dwight D. Eisenhower akakutana na Heren McKay, ambae alimkabizi ujumbe rais, ujumbe huo ulikuwa ukiomba Raisi Eisenhower kuandaa kikao maalumu na Allen Dulles, kwakuwa kikao hicho kilitakiwa kuwa na siri kubwa, utaratibu huu ulikuwa umezoeleka kati ya Allen Dulles na rais Eisenhower pale walipokuwa wanataka kuzungumzia mambo mazito yaliyoitaji siri kubwa za bila kuhusisha vyombo vingine.

Tarehe 20 mwezi wa 8, 1960...

Kwenye ofisi ya raisi wa Marekani oval office, White house Raisi Eisenhower alikutana na Allen Dulles, kujadili mapendekezo ya uvamizi wa Cuba, baada ya mazungumzo ya muda mrefu Raisi alikubali mapendekezo hayo lakini akapinga kufanyika operation hiyo bila kuishirikisha kamati maalumu ya usalama wa taifa hilo kwani Raisi Eisenhower alimtahadharisha Dulles kuwa mpango huo ungeitaji fedha katika kufanikisha mkakati huo, japo Allen Dulles alijaribu kumuonesha Raisi Eisenhower madhara ya iwapo mpango huo utahusisha vyombo vingi kungekuwepo na hatari ya mpango huo kugomewa.

Raisi Eisenhower alimuhakikishia Dulles kuwa mambo yangekwenda vizuri, tarehe 25 mwezi wa 8 1960 Raisi Eisenhower aliomba kikao na maafisa kadhaa wa Kamati Maalumu ya Viongozi wa Juu Kijeshi nchini Marekani yani Joint Chiefs of Staff Committee, ili kuweza kuwashawishi kumuunga mkono katika mpango wake wa kuivamia Cuba, Raisi Eisenhower aliwaeleza namna gani serikali ya Castro wanavyozidi kuwa tishio na kuhatarisha masrahi ya Marekani ukanda nzima wa America ya kusini, Rais Dwight D. Eisenhower aliwaomba maafisa hao kupokea mapendekezo ya shirika la CIA ya kuanza matayarisho ya kuivamiaCuba na kuupindua utawala wa Castro.

Baada ya kamati hiyo kulidhia mpango huo bado walisisitiza kuwa Raisi lazima mpango huo aupeleke mbele ya baraza la mawaziri ili uidhinishwe na kupewa baraka na serikali, hatua hiyo ilikuwa muhimu kwasababu mpango huo ulionekana kuhusisha hatua nyingi mpaka kukamilika kwake, hivyo lazima mpango huo ungeitaji fedha katika kufanikisha mkakati huo.

Rais Eisenhower alilidhia hilo na kukutana na mawaziri wake tarehe 2 mwezi wa 9 mwaka 1960, ambapo baraza la mawaziri kwa pamoja waliidhinisha mpango huo kwa azimio namba 7186 na kuiruhusi CIA kuendelea na operation hiyo, japo walitaka mpango huo kuwa na tahadhari sana, ili kuiepusha Marekani na kelele za kimataifa.

Hivyo...

Raisi Eisenhower akaikabidhi CIA faili la mapendekezo ya kuanza maandalizi ya maauji ya Castro na uvamizi wa Cuba, hatimae asubuhi ya Tarehe 13 mwezi wa 9 mwaka 1960, Kamati Maalumu ya Viongozi wa Juu Kijeshi nchini Marekani (Joint Chiefs of Staff Committee) chini ya Bw. L.M. Lemnitzer, iliidhinisha Operesheni iliyopewa jina la "Northwoods", kwa lengo la kutafuta sababu ya kuivamia kijeshi nchi ya Cuba, Chini ya operesheni hiyo, kamati ilipendekeza mfululizo mashambulizi yenye taswira ya kigaidi ndani ya miji ya Miami, Washington, D.C na kwingineko, meli za mizigo na abiria za nchi ya Marekani zingelipuliwa au kuzamishwa, ndege kutekwa, mauaji ya raia kutekelezwa makusudi, utoaji wa orodha 'feki' za wahanga wa mashambulizi ili kuufanya umma wa Wamarekani kuingia taharuki na kuipigia kelele za hasira serikali kulipiza kisasi kwa kuivamia Cuba. Kwa mujibu wa mpango huo, kila shambulizi lilipangwa kuhusishwa na nchi ya Cuba, lakini mipango yote hii ilitakiwa kusimamiwa na CIA.

CIA nao wakaandaa njia ambazo watazitumia kumuua Castro, njia hizo ziliandaliwa kwa ustadi wa hali ya juu na ubunifu wa hali ya juu, kwa mfano, vidonge vya sumu, mlipuko wa meli ya mafuta baharini, pia CIA ilitayarisha mpango maalumu wa mazumgumzo ya amani ya siri na Castro lakini lengo likiwa ni kumuua Castro kwa kumtumia mwanamapinduzi wa Cuba ambae alikuwa shushushu wa Marekani akiwa ni wakala wa CIA, wakala huyu alitwa Rolando Cubela, ambae alipangwa kumuua Castro kupitia shamburizi kwenye mkutano huo, alafu mauaji hayo yatafsirike kutekelezwa na Mcuba hivyo Marekani ijivue lawama za kuhusika, mpango huo ulipangwa na ofisa wa CIA aliyeitwa Desmond Fitzgerald, ambaye angejifanya yeye ni mwakilishi maalumu wa Robert Kennedy.

Mipango yote hiyo ikaonekana kushindwa hivyo ikafikiliwa mpango mkakati mwingine utakao leta matokeo chanya katika kufanikisha mkakati wao, ndio wakaja na mpango mpya wa kuivamia Cuba kijeshi, mpango huu ndio uliokuja kujulika kama "Uvamizi wa Bay of Pigs".

Bay of Pigs ilivyoratibiwa...

Uvamizi wa Bay of Pigs ulikuwa ni uvamizi wa taifa la Marekani kuivamia Cuba kupitia Ghuba ya nguruwe, ghuba hii ipo nchini Cuba kaskazini Magharibi mwa visiwa vya Cuba, uvamizi huu ni moja ya uvamizi mkubwa kufanywa na Marekani ambao ulishindwa kwa aibu kubwa, kwani uvamizi huu ulishindwa pamoja na kufadhiliwa na Marekani kwa fedha nyingi karibu dola billion 1.3 dhidi ya kuivamia Cuba mwaka 1961.

Uvamizi huu kwa Kiingereza unajulikana kama "The Bay of Pigs invasion" na kwa Kihispania unajulikana kama "invasión de bahía de Cochinos" wakati mwingine pia uvamizi huu huitwa "invasión de playa Girón" au "batalla de Girón", yaani mapigano ya Playa Girón.

Kama nilivyokwisha sema hako mwanzo kuwa hili lilikuwa ni jaribio la mapigano yaliyoshindwa ambapo serikali ya Marekani iliwafadhili Wacuba waliokuwa wakiishi uhamishoni kujaribu kuipindua serikali ya Cuba iliyoongozwa na Fidel Castro, uvamizi huu ulianzia kuvamia sehemu ya Kaskazini ya Cuba, Shirika la Ujasusi la Marekani CIA katika kufanikisha uvamizi huu lilifadhili kundi la waasi la Brigade 2506, ntalieleza kundi hili baadae kidogo, hivyo kundi hili ndilo lilofanya shuguri ya kuvamia Cuba tarehe 17 Aprili mwaka 1961 Katika mapigano ambayo yalichukua siku tatu.

Kundi la Brigade 2506...

Kundi hili la Brigade 2506 lilikuwa ni kundi la wapingaji wa Mapinduzi ya Cuba na serikali ya Fidel Castro ambao wengi wao walisafiri kwenda uhamishoni Marekani baada ya Castro kuwa ameitwaa Cuba baada ya kuiangusha serikali ya Dikteta Fulgencio Batista mwaka 1959, mapigano hayo pia yaliwahusisha baadhi ya wataalaamu wa kijeshi wa jeshi la Marekani.

Kundi hili likiwa wamepawa mafunzo na kufadhiliwa na CIA, kundi hili la Brigade 2506 lilikuwa ni tawi la kijeshi la chama cha Democratic Revolutionary Front (DRF) ambao walidhamiria kuipindua serikali ya Fidel Castro ambayo ilionekana inaegemea kwa kasi kwenye siasa za mrengo wa Ukomunisti, mipango yote ya kuvamia na kuipundua serekali ya Castro iliratibiwa huko nchini Guatemala na Nicaragua, majeshi ya uvamizi yaliandaliwa chini ya usimamizi wa Marekani, ambapo yakiwa huko walipokea malipo ya fedha kwa kila askali, walihaidiwa fedha zaidi na nafasi za uongozi ikiwa watayatwaa Madaraka.

Turudi nyuma kidogo ili kulifahamu kundi la "Democratic Revolutionary Front (DRF)"....

Ni kwamba mwaka 1952 nchini Cuba yalifanyika mapimduzi yaliyoongozwa na Generali Fulgencio Batista, mshirika mkubwa wa Marekani, dhidi ya Rais Carlos Prio aliyekuwa madarakani, mapinduzi hayo yalimlazimisha Rais Prio kuondoka Cuba na kwenda kuishi uhamishoni jijini Miami nchini Marekani, raisi Prio alipo fika huko uhamishoni Rais Prio, akamua kuanzisha kundi la uasi ili kuishambulia serikali ya Batista na kurejea tena Madaraka, kundi hilo likaitwa Democratic Revolutionary Front (DRF), kundi hili ndio baadae wa Marekani wakalitumia kuangusha utawal wa Castro, ikumbukwe kwamba Marekani ilimfadhili Batista kumgoa Prio pia Marekani hiyo hiyo ikaitumia kundi hilo la Prio kumgoa Castro.

January 3 mwaka 1961...

Kule Washington DC mpango wa 'kumnyoosha' Castro ulianza, Mpango huo, ulihusisha utoaji mafunzo maalumu ya kijeshi kwa vijana karibu 1400 kwa siri ndani ya kambi zilizojengwa jimboni Florida katika jiji la Miami, kusini-Mashariki mwa Marekani na nchini Guatemala, Amerika ya kati, Mafunzo hayo yaliandaliwa, kufadhiliwa na kuratibiwa kwa asilimia 100% na serikali ya Marekani kupitia Wizara yake ya Masuala ya Nje halikadhalika Shirika lake la Ujasusi (C.I.A), Wengi wa vijana walioshiriki, walikuwa ni Wa Cuba walioishi uhamishoni, waliompinga Castro na utawala wake.

Mtu aliyepewa kazi ya kusimamia mipango yote ya kuongoza uvamizi wa Bay of Pigs alikuwa ni Richard M. Bissell Jr, Naibu Mkurugenzi wa Mipango wa CIA yaani Deputy Director for Plans (DDP), jasusi huyu ndie aliyefanya kazi ya kutarisha maafisa wengine wengi tu ili kuweza kumsaidia kufanikisha mipango ya jaribio hilo, wengi wao wakiwa wale walioshiriki katika mapinduzi yaliyofanyika miaka sita nyuma yani mwaka1954 huko Guatemala, hawa ni pamoja na David Philips, Gerry Droller na E. Howard Hunt.

Bissell alimkabidhi Droller jukumu la kuwa kiongozi wa kuwakusanya Wacuba wanaompinga Castro miongoni mwa jamii ya Wacuba-Wamarekani wanaoishi uhamishoni na alimuomba Hunt kuunda kitu kama serikali iliyo uhamishoni ambayo CIA itakuwa inaidhibiti, Hunt alisafiri kwenda Havana, mji mkuu wa Cuba, huko alikutana na kuzungumza na Wacuba kutoka katika makundi mbalimbali.
Hunt aliporudi Marekani aliwataarifu Wacuba waioshio Marekani ambao alio kuwa anawakusanya kuwa wanatakiwa wahamishie harakati zao kutoka jijini Florida nchini Marekani na kwenda Mexico City nchini Mexico, kwa sababu idara ya Taifa ya Marekani kwa maana ya State Department ya Marekani imekataa kuwaruhusu CIA kupatia mafunzo yao ndani ya ardhi ya Marekani, kitendo hiki kulikuwa na maana kuu Tatu, Mosi Viongozi wengi waliona kuwa kitendo cha kuwaruhusu wakimbizi kufanya mafunzo ndani ya aridhi ya Marekani ingekiuka sheria za kimataifa ambazo ni kitendo cha uhalamia hivyo ingeichafua Marekani kwenye taswira za kimataifa.

Pili, kwakuwa Marekani ilikuwa kwenye uchaguzi mwezi November 1960, jambo lingeweza kuharibu uchabuzi na kufanya taharuki kwenye majimbo ya kusini ambapo chama cha Republican kilitegemea kupata kura huko.

Tatu, Kwakuwa taifa la Marekani lilikuwa kwenye vita baridi na Urusi, kitendo hicho kingetafsirika na Urusi kuwa uvamizi huo unafanywa na Marekani na sio wa Cuba wenyewe ambao wanaupinga utawala wa kikominist wa Castro, jambo hili serikali ya Marekani ilitaka ulimwengu uamini kuwa wao hawahusiki na chochote ambacho kingeendele huko Cuba.

Ingawa askali hao hawakuwa na furaha kusikia habari hizo, lakini waliipokea amri hiyo, hivyo vituo vya mafunzo vikaamia Mexico city, hatimae baadae wakaamia Nicaragua, Panama na Guatamala kwa mafunzo ya kuingia kuivamia Cuba.

Baada ya uchaguzi mkuu wa Marekani wa November mwaka 1960, raisi Jonh F. Kennedy alishinda uraisi, hivyo Rais Eisenhower ambae alikuwa akiratibu uvamizi wa Cuba akasimamisha mipango kwakuwa hakuwa na nguvu tena ya kisheria ya kuinjinia uvamizi wa nchini Cuba, hivyo Raisi Eisenhower alimualika Rais Kennedy aliyechaguliwa katika uchaguzi wa mwaka huo katika Ikulu ya White House tarehe 6 Desemba, mwaka 1960, na tarehe 19 Januari, mwaka 1961 ili kumshawishi atakapoingia ikulu aendelee na mpango huo ambao mtangulizi wake alikuwa ameuanzisha, katika moja ya mazungumzo yao, Eisenhower alimwelez Kennedy kuwa toka mwezi Machi, mwaka 1960, serikali ya Marekani ilikuwa inatoa "mafunzo kwa vikundi vidogo vidogo lakini hatujafanya kitu chochote" kwasababu bado sija approve uvamizi, alimueleza pia Kennedy kuwa "baadhi ya mamia ya asikali ambao ni wakimbizi" wako huko Guatemala, na "wachache wako huko Panama, na baadhi jijini Florida."

Kama nilivyo elezea huko nyuma kuwa mara tu baada ya Fidel Castro kuchukua madaraka mwaka 1959, mwaka uliofuata yaani mwaka 1960, CIA kwa ruhusa ya Rais Dwight Eisenhower ambaye alikuwa anakaribia kuondoka madarakani walianzisha mikakati ya namna gani watamuondoa madarakani Fidel Castro, Fursa kuu waliyoitumia ulikuwa ni kutumia wahamiaji walioingia Marekani kutoka Cuba kukimbia utawala wa Fidel Castro uliokuwa "unafanya usafi" dhidi ya raia waliokuwa wanamuunga mkono Fulgencio Batista, Kwa hiyo CIA wakakusanya mamia ya raia hawa kwa siri kubwa na kuwapandikizia hari na ushaiwshi wa kutaka kumpindua Fidel Castro.

Mwezi March mwaka 1960 rais Dwight Eisenhower alipitisha bajeti ya dola milioni 13.1 kwa ajili ya mpango huu wa mapinduzi, Raia hawa wa Cuba waliokimbilia uhamishoni nchini Marekani ambao walifahika kama kikosi cha Brigade 2506, wakaanza mafunzo ya kijeshi kwa mwaka mzima nchini Guatemala, Mpango huu wa kuivamia Cuba na kumpindua Fidel Castro ulipangwa ufanyike mapema mwaka 1961 na ulikuwa umekamilika kila kitu lakini raisi Eisenhower hakuupa 'approval' na aliacha jukumu hilo la kuidhinisha uvamizi huo ifanywe na atakaye kuja kumrithi yaani Rais JF Kennedy.

Kwa hiyo mara baada ya uchaguzi mkuu mwezi November, 1960 na hatimaye JF Kennedy kuapishwa January 20 mwaka 1961, kitu cha kwanza ambacho alikabiliana nacho ni CIA kumkabidhi mkakati ulioandaliwa na wao CIA chini ya Rais Dwight Eisenhower kuhusu uvamizi wa Cuba na kumpindua Fidel Castro, hivyo mwezi February tarehe 13, mwaka huo, mpango wenye sura nzima ya utekelezaji operesheni hiyo ulitua mezani kwa Rais Kennedy.

Awali ni kwamba CIA walipowasilisha mkakati wao wa mapinduzi ya Fidel Castro kuna vitu vingi vya msingi walimficha Kennedy hii ni kwasababu Kennedy hakuonesha kuunga mkomo mpango huo toka alipotaalifiwa na maafisa usalama wa Marekani na hats Raisi Eisenhower walipokutana kwa mara ya kwanza ikulu december 10, 1960, hili ndio lilopelekea hata CIA kutompatia taarifa zote Kennedy kwakuwa waliona angekwamisha mpango huo, hivyo wakaamumu kumptatia taarifa chache, Na hii inaonekana kwamba walichukua 'advantage' kwa sababu ya ugeni wa Kennedy katika wadhifa wake huu upya wa Urais na kwa hiyo kutofahamu uhalisia wa vitu vingi kwa hiyo CIA wakatumia hiyo fursa 'kum-mislead' katika vitu muhimu kuhusu mkakati huo.

Mkakati ulikuwa ni mpana sana, lakini kwa ufupi ni kwamba, wavamizi hawa wa Brigade 2506 ilikuwa imepangwa wavamie Cuba wakitokea Guatemala na Nicaragua wakiwa na askari wa miguu pekee, Kennedy hakutaka Marekani ionekane ikihusika moja kwa moja kwenye uvamizi huo ili kulinda taswira yake katika jamii ya kimataifa na pia kuepuka kuamsha hasira za Urusi ambao walikuwa ni mshirika mkubwa wa Cuba, kwahiyo kukabiliana na hili, CIA walipendekeza kuwatumia makomando wake wa SAD, ntakuelezea kidogo kuhusu hawa SAD ni wakina nani?

SAD ni nini hasa?...

SAD ni kitengo malumu ndani ya shirika la CIA ambalo wao hufanya shughuri maalumu na zenye unyeti wa maswala muhimu, hivyo idara hii ni maalumu ndani ya shrika la CIA, ambayo hujulikana kama "Special Activities Division"

Watu wengi huzani kuwa CIA ndio kufanya shuguri zote za kijasusi, lakini ukweli ambao wengi hawauelezi ni kuwa umahiri na upekee wa wa shirika la CIA hufanywa na kikosi maalumu cha kipekee kwa ajili ya kazi nyeti maalumu na kazi hizo husamiwa na maafisa wa Idara ya SAD ndani ya CIA.

Upekee wa SAD ndani ya CIA ni nini?...

Kutokana kuongezeka kwa changamoto za kimataifa , ambazo nyingine zinatishia usalama au maslahi ya Marekani lakini marekani haiwezi kuchukua hatua zozote kutokana kujiepusha na lawama kutoka jamii ya kimataifa ndipo hapo ikaonekana kuna umuhimu wa kuwa na kitengo maalumu kwa ajili ya suala hili.

Ndipo hapa ambapo serikali ya marekani ikaagiza shirika la kijasusi la CIA kuanzisha kitengo maalumu ndani yake ambacho kitakuwa na maafisa (wanajeshi) ambao wanaweza kutekeleza oparesheni yoyote ya kijeshi kwa kujitegemea pasipo kuhusisha serikali ya marekani.

CIA wakaanzisha idara maalumu ndani yake na kuuita Special Activities Division au kwa kifupi SAD ambayo idara yenyewe ilikuwa na maafisa wa siri ambao hawabebi vitambulisho na majina yao ni siri kubwa hayawezi kupatikana hata kwenye orodha ya maafisa wa CIA.

Lengo kubwa la kuanzishwa kwa idara hii ni kutekeleza oparesheni maalumu za kijeshi au proaganda na iikitokea wakakamatwa au kushitukiwa basi serikali ya marekani wanawakana kuwa si maafisa wao (Plausible deniability).

Kwahiyo kitengo hiki kilikuwa kinafanya kazi kwa niaba ya serikali ya Marekani lakini kulikuwa hakuna uwezekano wowote wa adui kuunganisha uhusika wa kikosi hiki na serkali ya marekani.

Ndani ya Idara hii ya SAD kuna vitengo viwili;.......

Kitengo cha kwanza kinaitwa Political Action Group, kitengo hiki kazi yake kubwa ni kufanya ushawishi wa kisiasa (political influence), oparesheni za kisaikolojia (psychological operations) na vita za kiuchumi (Economic Warfares), Pia kutokana na maendeleo ya kiteknolojia, kitengo hiki kimeongezewa jukumu la vita za kimtandao (cyberwarfares).

Tuchukulie kwa mfano, katika nchi fulani kuna serikali au mwenendo wa serikalin uatishia maslahi ya Marekani basi kitengo hiki kinaingia kwa siri kubwa na kufanya mojawapo ya mambo ambayo nimeyaorodhesha hapo juu.

Moja ya matukio ambayo kitengo hiki kimehusika sana na CIA wamekiri kwenye nyaraka zilizowekwa wazi mwaka 2004 ilikuwa ni kueneza propaganda ambayo ilichangia kupinduliwa kwa Rais wa Iran mwaka 1953, Pia kitengo hiki kilitumika kuzuia chama cha kikomunisti cha Italia kushinda uchaguzi mwaka 1960.

Pia kitengo hiki kimewahi kufanya oparesheni ya siri iliyoitwa Operation Mockingbird katika taifa la marekani, Oparesheni hii ilikuwa na lengo la 'kucontrol' habari zinazoandikwa na Vyombo vya habari nchini humo, Oparesheni hii imekuja kupingwa vikali siku za karibuni na baraza la seneti kwa kuwa sheria hairuhusi CIA kufanya oparesheni yeyote ndani ya ardhi ya marekani.

Kitengo cha Pili kinaitwa Special Operations Group (SAG) na kazi yake ni kama ifuatavyo......

Kitengo hiki kinajumuisha wanajeshi wenye weledi wa hali ya juu kutekeleza malengo ya kivita pasipo kujulikana uhusika wa serikali ya marekani, Ili kulinda utambulisho wao, wanajeshi wa kikosi hiki maalumu hawavai sare za jeshi wala kubeba vitambulisho, Inasemekana kuwa hiki ndio kikosi maalumu cha oparesheni za kijeshi chenye usiri mkubwa nchini marekani.

Maafisa wa kitengo hiki wanapatikanaje?...

Maafisa wote wanaojiunga katika kitengo hiki maalumu cha SAD wanachaguliwa kutoka katika vikosi vingine vya weledi vya jeshi la marekani mfano Army Rangers, Combat controllers, Delta Force, 24 th STS, US Army Special Forces, SEALs, Force Recon n.k.

Wakishakuchaguliwa wanapelekwa katika kituo maalumu cha mafunzo ya CIA kilichopo Virginia kinachojulikana kama Camp Peary (au maarufu kama 'The Farm') ambapo miezi 18 ya kwanza wanafundisha kuhusu intelijensia na ushushushu.

Baada ya miezi 18 hiyo wanapelekwa kwenye kituo kingine cha CIA kilichopo California ambacho kinajulikana kama 'The Point', Hapa wanafundishwa mafunzo ya hali ya juu ya kijeshi ambayo hayapatikani kwa kiwango hicho katika vikosi vingine vya marekani.

Mfano wanafundishwa; mapigano ya ana kwa ana ya kiwango cha juu zaidi (special hand to hand combat), kutumia karibia aina zote za silaha na milipuko ya jeshi la marekani na nchi za kigeni, ufuatiliajj adui (tracking), Kukabiliana na hali ngumu kwenye mamzingira ya kawaida na nyikani ( extreme survival and wilderness train ing), Kumkwepa aduia, kuzuia adui na kutoroka adui (evasion, Resistance and escape - SERE) na pamoja na mafunzo hayo anaongezewa kozi maalumu ya kutambua fiziolojia ya binadamu (Udaktari).

Afisa ambaye anafuzu mafunzo haya anakabidhiwa katika idara ya SAD ndani ya CIA na anatambulika kama "Afisa Mwenye Mbinu Maalumu" (Specialized Skills Officer), Katika oparesheni zao maafisa hawa huwa wanazitekeleza katika vikundi vya watu wachache sana wasiozidi sita na oparesheni nyingine zinatekelezwa na Afisa mmoja pekee.

Katika Ofisi za CIA kitingoji cha Langley jijini Virginia kuna ukuta wa majina ya Maafisa wa CIA waliotunikiwa tuzo za heshima kutoka na utumishi wao uliotukuka ( Distinguished Intelligance Cross na Intelligence Star), Majina ya maafisa wengi kwenye ukuta huo ni ya wale waliotumikia kitengo cha SAD ndani ya CIA.

Kwa kuzingatia kwamba makala hii inalenga kuzungumzia uhusika wa CIA katika mapinduzi ya serikali ya Cuba kupitia Uvamizi wa Bay of Pigs, Hivyo basi tuone mifano michache sana ya oparesheni zilizotekelezwa na kitengo hiki cha SAD ndani ya CIA, Nitaeleza kwa ufupi ili tusitoke nje ya lengo kuu (mapinduzi ya Cuba ).

Ni idara hii maalumu ya CIA ambayo ilikabidhiwa raia wanne wa Tibet kutoka kwa kaka mkubwa wa kiongozi wa kiroho wa Tibet Mtukufu Dalai Lama ambapo idara ya SAD iliwapa mafunzo ya kikomando watibeti hao kisha wakawarudisha Tibet kutafuta raia wengine 300 ambao SAD iliwapa mafunzo ya kijeshi kwa siri katika kisiwa cha Saipan na mwezi oktoba SAD ikawaongoza wanajeshi hawa mpaka Tibet kuanzisha vuguvugi la kudai kujitenga na China.

Pia ni kikosi hiki maalumu cha idara ya SAD ambacho kilimtorosha kwa siri mtukufu Dalai Lama kwa kupita katikati ya majeshi ya China yaliyokuwa mpakani na kumpeleka India, Mpaka leo haijulikani ni namna gani waliweza kufanya tukio hili, kwakuwa tukio hili awajaliweka wazi mpaka sasa.

Ni kikosi hiki hiki cha SAD ambacho kiliusika na mauaji ya Che Guevara, hii ni kwa mujibu wa nyaraka za siri za CIA zikizowekwa wazi mwaka 2004, ambazo zinaonesha kuwa Amri ya kumpiga risasi Che Guevara miaka ya 1960 ilitoka kwa makomado wa SAD.

Ilikuwaje....

Ilikuwa hivi, Jeshi la msituni lililojiita Jeshi la Ukombozi la Bolivia (National Liberation Army of Bolivia) lilianzisha vita dhidi ya serikali ya Bolivia ambayo ilikuwa inaungwa mkono na Marekani, Jeshi hili likuwa na vifaa vya kisasa na liliungwa mkono na mwanamapinduzi Che Guevara, katika hatua za mwanzo za mapigano, jeshi hili la waasi lilionekana kushinda dhidi ya majeshi ya serikali, ndipo hapo CIA wakatuma makomando wa kitengo cha SAD ambao walienda kutoa mafunzo kwa majeshi ya Bolivia katika milima ya Camiri, Na baada ya hapo wakawaongoza kupigana na waasi na kufanikiwa kuwashinda, na kisha makomando wa SAD wakawaongoza makomando wa jeshi la Bolivia (Bolivia Special Forces) kumkamata Che Guevara ambapo Mara tu baada ya kukamatwa komando wa SAD aliyeitwa Felix Rodriguez akaamuru auwawe.

Hii ni mifano michache kati ya mifano mingi ambayo CIA kwa kutumia kitengo cha SAD wameendesha opesheni maalumu za kijeshi katika nchi nyingi duniani.

Ingawa Rais wa marekani ndiye anayetoa amri ya kufanyika kwa operesheni hizi za kuvamia kijeshi nchi nyingine au kuongoza mapinduzi ya serikali halali duniani kote lakini analindwa na sheria ya Marekani ambayo inampa Rais uwezo wa kukana uhusika wa Rais wa marekani kutoa amri au kufahamu kinachofanywa na kitengo hiki. (Plausible Deniability).

Sheria hii ilitingwa mwaka 1947 na inajulikana kama National Security Act, Pia Sheria hii ilitiliwa mkazo na tamko la rais namba 12333 (Executive Order 12333) lenye kichwa cha habari National Intelligence Activities.

Ni idara hii ya SAD ndani ya CIA ambayo ilihusika pia kuwapatia mafunzo ya kijeshi raia wa Cuba waliokuwa wanaishi uhamishoni na kuwaongoza katika jaribio la kumpindua Fidel Castro, Mapigano haya yakihistoria yalidumu kwa siku tatu na yanajulikana kwa jina maarufu la 'Bay Of Pigs Invasion'.

Jaribio hili la mapinduzi ndio lililo changia kudorara kwa mahusiano kati ya Marekani na Cuba mpaka leo hii, Lakini kutokana na umahili wa shirika hili na uhodari wao ndio maana maafisa wa CIA walimshaishi rais Kennedy kukubali mpango wa kuwatumia makomando hao kwenye uvamizi huo.

Mpaka hapa naamini sasa umeelewa vyema kuhusu hiki kitengo maalumu cha CIA cha Special Activities Division (SAD) namna kinavyofanya kazi, Sasa turejee kwenye simulizi yetu ya uvamizi wa Bay of Pigs.

Washington DC, tarehe 20, February 1961...

Maafisa CIA walipo mshauri Kennedy kuhusu uvamizi huo walimuomba sana kuidhinisha makomando wa SAD kutumika, hatimae Raisi Kennedy alikubali makomando wa SAD kuongoza wapiganaji wa Brigade 2506, lakini pamoja na hayo yote, Rais Kennedy alisisitiza sana kwamba ili kulinda taswira ya nchi ya Marekani yeye kama Rais hatoruhusu Marekani kufanya mashambulizi ya anga kusaidia katika mapambani hayo ya kumuondoa madarakani Fidel Castro, maafisa hao walikubali agizo hilo la Raisi Kennedy lakini walijua baadae wangemshawishi Raisi ili waweze kushinda vita ile.

Kwani CIA walijua fika kwamba hawawezi kushinda uvamizi huo pasipo mashambulizi ya anga wakakubaliana na sharti la Rais Kennedy kwamba hakutakuwa na mashambulizi ya anga, Walikubali hili huku wakiwa na dhamira iliyojificha kwamba mara tu vita hiyo itakapoanza watamshinikiza Rais Kennedy atoe ruhusa ya kufanyika mashambulizi ya anga, Walikuwa wanaamini kwamba lazima Rais Kennedy atakubaliana na shinikizo lao pindi atakapoonyeshwa umuhimu wa mashambulizi ya anga pindi vita ikiwa inaendelea, na lazima atafanya hivyo ili kuepusha Marekani kuaibika kushindwa vita wanayoiunga mkono ili kulinda heshima yao ya kijeshi ambayo ilikuwa inahitajika kuliko kitu chochote katika kipindi hiki cha vita baridi.

Rais Kennedy aliidhinisha rasmi uvamizi huu siku ya tarehe 4 April 1961, takribani miezi mitatu tu baada ya kuingia madarakani, Wapiganaji wapatao 1400 wa Brigade 2605 waliogawanywa katika infantry batalioni zipatazo tano na paratrooper battalion moja waliingia katika pwani ya Cuba iitwayo Playa Girón kwa kutumia boti kutokea Guatemala na Nicaragua siku ya tarehe 13 April 1961, Baada ya uvamizi tu kuanza CIA wakaanza kuweka shinikizo kwa rais Kennedy aruhusu japo shambulio moja la anga la ndege za kivita za Marekani kuharibu miundombinu ya viawanja vya ndege za kijeshi vya Cuba, Kennedy alikataa katakata lakini CIA walipozidisha shinikizo na kumpa angalizo kuwa wasipofanya hivyo kuna uwezekano wa wapiganaji hao kushindwa kutekeleza mapinduzi ya kumuondoa Fidel Castro, Kennedy alilazimika na kuruhusu mashambulio ya anga kwa awamu moja pekee.

Hivyo basi tarehe 15 April 1961 ndege za kijeshi zilizo chini ya CIA aina ya B-26, zenye marubani wavamizi walipewa ndege, ndege zile za kivita zilibadilishwa rangi na kufanana sana na zile za Jeshi la Cuba na pia zilipakwa matope ili zikiwa angani zionekane ni chakavu, kisha ziaenda kushambulia kambi ya anga za Cuba na kufanikiwa kuangamiza asilimia 80 ya ndege za Castro, Jeshi la Anga la Castro lilibakiwa na ndege sita tu na marubani saba, ndege hizo zilishambulia viwanja vya ndege za jeshi la Cuba na hatimaye tarehe 16 April wapiganaji wa Brigade 2506 walivamia rasmi Cuba, Mwanzoni mwa uvamizi huu wapiganaji wa Brigade 2506 wakiongozwa na makomando wa SAD katika CIA walionekana kulidhibiti jeshi la Cuba ambapo mwanzoni mwa mapambano haya upande wa Cuba vikosi vya kijeshi vilikuwa vinaongozwa na José Ramón Fernández.

Baada kuonekana kuwa jeshi la Cuba linazidiwa ujanja na wavamizi hawa waliokuja kufanya mapinduzi, Fidel Castro mwenyewe akaingia katika uwanja wa vita na kumuondoa José Fernández kwenye jukumu la kuongoza jeshi kwenye mapambano haya na kujipa yeye binafsi hilo jukimu la kuongoza wanajeshi, Castro alipo ingia front kuongoza mapambano alitumia mbinu ya falsafa ya mapigamo ya José Mart iitwayo "Siri, Vamia, shambulia, gawanya na miliki", mbinu hii ililifanya jeshi la Cuba kuanza kupata mafanikio.

Baada ya Castro kushikilia usukani wa kuongoza mapambano kwa upande wa jeshi la Cuba, wavamizi wa Brigade 2506 wakiongozwa na makomando wa Marekani walizidiwa ujanja na mbinu zote na wakaanza kupigwa kwa aibu kubwa, mpaka kufika tarehe 19 April, ilikuwa dhahiri kwamba ushindi uko upande wa vikosi vya Cuba, kwani walikuwa wanawapiga wavamizi kwa urahisi kana kwamba wanamsukuma mlevi, Ndipo hapa ambapo CIA wakarudi tena kwa rais Kennedy kutaka aidhinishe mashambulizi mengine ya anga, Safari hii Kennedy alikataa katakata, akidai kuwa dunia nzima itaona uvamizi huu imefanywa na Marekani na sio raia wa Cuba wanaoishi uhamishoni.

Kennedy alihofia kuwa kama Marekani itaingilia mapigano hayo kwa kiwango hicho, kulikuwa na uwezekano wa Urusi nayo kuingilia vita hiyo kusaidia upande wa Cuba, kutokana na mvutano mkubwa uliokuwepo baina yao, Kennedy alihofia kuwa ingeweza kuchochea vita nyingine kati ya Marekani na Urusi, vita ambayo ingeigharimu pande zote mbili na Dunia nzima kwa ujumla na pengine hata kusababisha vita kuu ya Tatu ya Dunia, kwa hiyo Kennedy safari hii akakataa katakata kuidhinisha mashambulio ya anga kwa kutumia jeshi la Marekani.

Joint Chiefs Of Staffs wakaja na pendekezo kwamba litengenezwe shambulio la uongo kwenye pwani ya Marekani na kisha kutupa lawama kwa Cuba ili kuhalalisha mashambulizi ya anga nchini Cuba, lakini bado pia Kennedy alishikilia msimamo wake kwamba hawezi kuidhinisha shambulio lolote la anga kufanywa na jeshi la Marekani, Hapa ndipo ambapo CIA iliumbuka, mkakati wao tangu awali ulikuwa ni lazima mashambulizi ya anga yafanyike ili kuweza kushinda mapigano na kuvishinda vikosi vya Castro na kumuondoa Madarakani, Lakini walimficha kitu hiki Rais Kennedy baada ya kumuona kuwa hasingeli idhinisha uvamizi huo kama wangemuweka wazi kuwa hawawezi kushinda pasipo mashambulio ya anga, hivyo kumficha huko na tegemeo lao la kumshawishi tena kwa mara ya pili yafanyike mashambulio ya anga ndio likawa limegonga mwamba.

Cuba ikaibuka mshindi....................

Tarehe 20 April 1961, siku tatu baada ya uvamizi, wapiganaji waliio patiwa mafunzo na kuongozwa na makomando wa Marekani, ambao waliiovamia nchini Cuba ili kumpindua Fidel Castro waliweka silaha chini na kusarenda kwa vikosi vya jeshi la Cuba, Ilikuwa ni aibu kubwa ambayo haijawahi kutokea katika historia ya jeshi la Marekani, Mateka waliokamatwa na vikosi vya Fidel Castro walihojiwa mubashara kwenye televisheni nchini Cuba na kutoa siri zote namna ambavyo Marekani ilihuiska katika uvamizi huo ambapo Marekani walikuwa wanatafuta sehemu ya kuficha nyuso zao kwa aibu, nchini Cuba taifa zima lilikuwa linasheherekea kwa shamra shamra kushangilia ushindi huo mnono, Fidel Castro aligeuka kuwa shujaa mpya wa Taifa na kujipatia heshima kubwa kimataifa kwa kushinda vita dhidi ya jeshi hatari la 'Marekani' hivyo Fidel Castro akapewa cheo cha juu jeshini cha Fidel Marshall kwa kuyashinda majeshi ya Marekani.

Huko Marekani nako...

Bado bundi alikuwa ndio kwanza ametua, Kila upande ulikuwa unamsukumia lawama upande mwingine, CIA walimuona Rais Kennedy kama ndio kisababishi cha wao kushindwa kutekeleza kwa ufanisi uvamizi na hatimaye kufanikisha kumuondoa madarakani Fidel Castro, CIA walijuta Raisi Eisenhower kutokamilisha mpango huo wa uvamizi kabla ya kuondoka ikulu.

Na kwa upande wa Rais Kennedy aliwaona CIA kama wasaliti kwa 'kumdanganya' na kutompa mkakati kamili tangu mwanzoni kwamba wasingelieweza kushinda vita ile pasipo mashambulizi ya anga, CIA wakamuona Rais Kennedy kama kiongozi ambaye si imara na shupavu au jasiri, na kwa muono wao walihisi kuwa hatoshi kuwa Rais wa Marekani.

Kwa upande wake Kennedy aliwaona CIA kama taasisi iliyopewa nguvu kiasi kwamba imelewa madaraka na kujiona wako huu ya kila kitu na kila mtu. Na moyoni mwake aliamini kuwa hilo linatakiwa kubadilika, Ikumbukwe pia kwamba hapa ilikuwa imepita miezi mitatu pekee tangu CIA wamuue Patrice Lumumba siku ya Tarehe 17 January, 1961 jimboni Katanga, Congo-Kinshasa, Kennedy anafahamika kuwa hakupendezwa na hili tukio lakini kwa kuwa lilitokea kabla hajawa Rais (siku tatu kabla) basi alilimezea mate lakini bado alibaki na kinyongo Kwa hiyo kufeli kwa uvamizi wa Bay of Pigs kuliamsha hasira zake zote alizonazo dhidi ya CIA.

Japokuwa katika umma na hata alipoongea na wanahabari Kennedy alikubali kubeba lawama zote kwa kuwa yeye ndiye aliidhinisha uvamizi huo, lakini pembeni akiwa faragha na wakubwa wenzake alikuwa anaotupia lawama kubwa CIA kuwa ndio waliosbabisha aibu kubwa hii iliyoipata Marekani na jeshi lake, Baada ya hapa mwenendo wa Kennedy ukaanza kubadilika mno. Mwanzoni alipoingia madarakani alikuwa ni tegemezi mno kwa kupatiwa muhtasri wa hali ya usalama wa nchi (Daily Presidential Briefing) kutoka kwa vyombo vya Ujasusi hasa CIA, lakini baada ya tukio la kufeli kwa uvamizi wa Cuba hakutaka tena kupatiwa briefing na CIA badala yake briefings zake zote sasa alizipokea kutoka kwa washauri wa usalama wa taifa (National Security Advisors).

Lakini hakuishia hapo tu, Kennedy kuonesha ni namna gani alikasirishwa alienda mbali zaidi kufanya kitendo ambacho kilipingwa na maafisa wengi wa CIA na wanazi wao, Kennedy alimfuta kazi Mkurugenzi Mkuu wa CIA Bw. Allen Dulles, Katika ulimwengu wa Intelijensia unapomuongelea Allen Dulles hamuongelei tu jasusi, bali ni jasusi mkongwe na mzoefu na wa kiwango cha daraja la kwanza kabisa na mwenye heshima iliyotukuka, Allen Dulles ndiye Mkurugenzi wa CIA aliyetumikia kwa kipindi kirefu zaidi katika historia ya Taasisi hiyo mpaka leo hii (tangu 1953 mpaka 1961), Allen Dulles ndiye aliyesimami mapinduzi ya Waziri mkuu wa Iran miaka ya 1940s (Operation Ajax), Allen Dulles ndiye aliyesimamia mapinduzi ya Rais wa Guatemala mika 1950s, Allen Dulles ndiye aliyesimamia program ya ndege za kijeshi ya Lockheed U-2, Pia huyu ndie aliye simama operation Barracuda iliyo ratibu kifo cha Patrice Lumumba wa Kongo DRC.

Allen Dulles ni kaka wa John Dulles, waziri wa mambo ya nje wa Marekani (Secretary of State) wakati wa utawala wa Rais Dwight Eisenhower ambaye ndiye amerithiwa na Kennedy miezi mitatu iliyopita, kwa hiyo inahitaji kujitoa ufahamu kumgusa mtu kama Allen Dulles. Na Kennedy alijitoa ufahamu na kumfuta kazi Allen Dulles mtu ambaye anapendwa na kuhusudiwa na majasusi wa CIA pengine kushinda hata Kennedy mwenyewe, Karatasi ya juu ya ripoti rasmi ya CIA ambayo ndani yake kuna baadhi ya paragraph zikionyesha kuwa CIA hawakuridhishwa na namna ambavyo Kennedy alifanya maamuzi juu ya kukataa mashambulio ya anga.

Wengine huenda mbali zaidi na kusema kwamba uvamizi wa Bay of Pigs ndivyo iliyochangia kifo cha Kennedy, kutokana na madhira ya vita vyenyewe na athari ya vita kwa CIA kuipoke kwa mtazamo kuwa John F. Kennedy kama chanzo ya Marekani kushindwa vita hiyo, japo hakuna ushahidi ulio wekwa wazi kuhusu hili.

Sababu ya Cuba kushinda na Marekani kushindwa uvamizi wa Bay of Pigs...

Kuna sababu nyingi zinazotolewa juu ya ushindi huo kwa Cuba. Mosi, ni taarifa za kiintelijensia kuwafikia mapema kupitia vyanzo vyao vya ndani ya Marekani, Baadhi ya duru hubainisha kuwa vyombo vya habari nchini Marekani hasa magazeti vilikuwa vikiripoti juu ya operesheni hiyo ya mafunzo ya siri, jambo lililosababisha Havana kupata taarifa mapema na kujiandaa vilivyo, sambamba na kupenyeza mashushu watiifu wa Castro ambao walijifanya waasi wakati upande wa pili walitii serikali ya Havana na kupeleka taarifa zote kwa Castro kupitia mashushushu wa mtaani, hii ni kwamba askali hao watiifu walipokuwa kambini walitoa taarifa zote zinazoendelea kwa raia wa Cuba ambao walilikuwa wafanya biashara ambako askali hao walikuwa wakienda kupumzika baada ya mafunzo.

Pili, inadaiwa kuwa kikosi hicho kujikanganya kwenye eneo mahsusi la kuingilia kisiwani, na kujikuta wakitia nanga Playa Giron au Bay of Pigs kimakosa, mkakati wa awali ulikuwa ni kuwa ni kikosi hicho kutia Nanga eneo la Bay of Pigs upande kusini mashariki, yani kilomita 1.7 upande wa chini ambao gridi reference yake ni 27ES na 57NE, eneo ambalo kulikuwa na miinuko ya miamba ambayo ingewapa urahisi wa kutoonekana kwa urahisi kwa askali wa Cuba, kinyume chake walijikanganya na kutia nanga eneo la kusini ambalo lipo wazi hivyo ilikuwa rahisi kushambuliwa kwa uwepesi.

Tatu, na mwisho, ni kwamba hali mbaya ya hewa na uwazi kimwonekano wa eneo la Bay Of Pigs walilotia nanga, Inadaiwa kwamba ilikuwa rahisi kwa makamanda wa Cuba kuwamaliza wavamizi sababu ya eneo hilo kuwa wazi na rahisi zaidi kwenye shabaha kutokea mafichoni.

Serikali ya Marekani haikukubaliana na matokeo ya kushimdwa vita ile hivyo Raisi Kennedy akataka uchunguzi ufanyike ili kubaini sababu za Marekani kushindwa vita ile, hivyo akaitaka ofisi wa utafiti chini ya Maxwell kuendesha uchunguzi ili kubaini hasa kwanini Marekani imeshindwa vita hiyo ya uvamizi wa Bay of Pigs.

Tume ya Maxwell Taylor Commission...

Mnamo tarehe 22 Aprili mwaka 1961, Rais Jonh F. Kennedy aliunda tume na kumteua Jenerali Maxwell D. Taylor, pamoja na Mwanasheria Mkuu Robert F. Kennedy, Admiral Arleigh Burke na Mkurugenzi wa CIA Allen Dulles, tume hii ilijulikana kama Maxwell Taylor commission, tume hii iliundwa ili kutafiti sababu za Marekani kushindwa vita ile ya Cuba, baada ya tume hiyo kufanya shuguri zote za kiuchunguzi, Jenerali Taylor aliwasilisha ripoti ya tume yake ya Uchunguzi kwa Rais Kennedy mnamo tarehe 13 Juni mwaka 1961, tume hiyo ilielezea sababu za Marekani kushindwa vita ile ni kwa ukosefu wa taarifa za uhakika na za mapema kwa raisi, pia tume ilielez kuwa sababu nyingine ni operation hiyo kuendeshwa kwa njia za siri, kitu ambacho vyombo vingine vilishindwa kushirikishwa ili kutoa ushauri wa kitaalam, tume hiyo pia iliiulaumu utawala wa Kennedy kwa kushindwa kuidhinisha mashambulizi ya ndege kwa wakati, pia tume iliuulaumu uongozi wa CIA kwa kutumia ndege zisizofaa, mambo mengine ambayo tume ilieleza ni pamoja na mapungufu ya silaha, marubani ambao awakuwa na uzoefu wa kutosha na eneo la Bay of Pigs na Cuba kwa ujumla.

Pia tume ilieleza suala la mashambulizi ya angani kutokutekelezwa ipasavyo, utawala wa Kennedy kitofuata mkakati uliowekwa na mtangulizi wake.

Ripoti ya tume hiyo ilikuwa na kurasa 201, hata hivyo baada ya ripoti hiyo kutolewa na kuwekwa hadharani ilikutana na ukosolewaji mkubwa, tume hiyo ilionekana kuwa na upendeleo ulioegemea kumshambulia raisi Kennedy pamoja na Mwanasheria Mkuu Robert F. Kennedy ndugu yake Rais Kennedy.

Mika 20 baada ya riporti hiyo ya Maxwell Taylor commission, Jack Pfeiffer, ambaye alifanya kazi kama mwanahistoria wa CIA hadi katikati ya miaka ya 1980, alitoa taarifa juu ya Marekani kushindwa mapigano ya Bay of Pigs kwa kunukuu taarifa ambayo Raúl Castro, kaka wa Fidel, alikuwa ametoa kwa mwandishi wa habari wa Mexico mnamo 1975, ambayo inasema kuwa ushindi wa vita ile kwa Cuba ulitokana na hofu ya Raisi Kennedy Juu ya Urusi na uchanga wake Juu ya maswala nyeti ya nchi, Raul Castro alikili wazi kuwa kama vita ile ingefanywa na mtangulizi wa Kennedy Raisi Dwight Eisenhower ingeifanya vita ile kuwa ngumu.

Ripoti ya Siri ya CIA...

Mnamo Novemba 1961, Mkaguzi Mkuu wa CIA Lyman B Kirkpatrick aliandika ripoti juu ya Utafiti wa Operesheni ya Cuba ripoti ambayo ilibaki kuwa siri (classified) hadi mwaka 1998, miaka 37 baadae ndipo ilipo wekwa hadharani kwa umma yani disclassified, ripoti hiyo ya CIA ilionesha mambo kadhaa yaliyopelekea Marekani kushindwa vita ile ambayo ni pamoja na;

Mosi, Marekani Kushindwa kutathmini kiuhalisia hatari na kuwasiliana vya kutosha na viongozi pamoja kukosekana kwa habari sahihi juu ya operation hiyo mezani kwa Raisi Kennedy na pia upatikanaji hafifu wa maamuzi ya ndani ya CIA na wakuu wengine wa serikali.

Pili, kukosekana kwa ushiriki wa kutosha wa viongozi wa serikali ya Kennedy na askali wa brigade 2506 katika uhamishwaji.

Tatu, CIA kushindwa kuandaa mpango huu vizuri ili kuwahusisha pia upinzani wa ndani ya Cuba, ambao wangesaidia sana kuhujumu serikali ya Castro kipindi ambacho vile ikiendelea.

Nne, CIA kushindwa kukusanya taarifa kwa ufanisi na kuzichambua taarifa hizo za kijasusi kuhusu vikosi vya jeshi la Cuba.

Tano, Ukosefu wa sera thabiti au mipango ya dharura kutoka ndani ya serikali juu ya operation hiyo.

Matokeo ya Marekani kushindwa vita ile ilipelekea mgogoro mkubwa kwa viongozi wa Juu wa CIA na serikali kuu hasa kuanzia Mkurugenzi wa CIA Allen Dulles, Naibu Mkurugenzi wa CIA Charles Cabell, na Naibu Mkurugenzi wa Mipango Richard Bissell wote walilazimishwa kujiuzulu mapema mwaka wa 1962.

Baada ya vita ile uhasama baina ya Cuba na Marekani uliongezeke na Marekani ilihaidi kulipiza kisasi kufatia aibu iliyopata mwaka 1961 katika vita ile ya Bay of Pigs, kufatia hatua hiyo ya kuzorota kwa diplomasia ya mataifa hayo ilipelekea kuongezeka kwa msuguano wa vita baridi, hasa mvutano baina ya Urusi na Marekani, mivutano hii ilipelekea viongozi wa Juu wa nchi hizo kuwekeana vitisho na Urusi kuionya Marekani kuacha kuthubutu kuivamia Cuba.

Jambo hili nimelielezea huko nyuma, nilisema mara zote Marekani ilihofu kuchochea mgogoro wowote na Cuba kwa kuhofia kuibuka kwa vita baina ya Marekani na Urusi, lakini baada ya Marekani kushindwa vita ile ya Bay of Pigs ilipelekea Marekani kujitafakari upya dhidi ya usalama wake dhidi ya Cuba na hasa hasa Urusi yenyewe ambayo ndio ilikuwa kiranja mkuu wa ujamaa duniani.

Basi bwana...

Marekani ikaanza kujiimarisha na kujiimarisha katika muungano wao wa NATO, hii NATO ni muungano wa mataifa ya kibepari kujihami dhidi ya mataifa ya kijamaa, hivyo Marekani na NATO wakaanza kujiandaa ili kuidhibiti Urusi, maana walijua wakidhibiti Urusi watakuwa wameidhibiti Cuba, baada ya Urusi nao kujua hilo nao wakanza kujizatiti ili kuidhibiti Marekani, ndio Urusi wakaunda umoja wao wa Warsaw Pact.

Kufatia hilo muungano huo wa mashariki kwa kipindi hicho ulioitwa Warsaw Pact ulianza kikao chake cha dharula mwezi February mwaka 1962 na ilipofika mwezi April mwaka 1962 walifikia uamuzi wa kuingia katika vita kamili ya kujihami dhidi ya umoja wa kujihami wa nchi za magharibi NATO

Jumla ya askari 400,000 kutoka nchi mbali mbali za umoja wa kujihami wa nchi za mashariki walianza kusogea mipakani mwa nchi zao kujiandaa na vita dhidi ya umoja wa kujihami wa nchi za magharibi NATO
Ilipofika August mwaka 1962 meli za kivita za Urusi zikiwa zimebeba askari zaidi ya 100,000 pamoja nyambizi zilizobeba silaha kali za nyuklia zilitia nanga kisiwani Cuba

Dunia yataharuki...

Mwezi September mwaka huo wa 1962 Rais wa Urusi wa wakati huo Nikita Khruschev aliwahakikishia nchi washirika wake wa mashariki kuwa endapo askari hata mmoja wa NATO angevuka mpaka na kuingia katika nchi zao basi nae angejibu mapigo kwa kuangamiza sehemu kubwa ya nchi ya Marekani hususani majiji ya New York na Miami, Kwani tayari nae alikuwa ameshaweka silaha kali za nyuklia mkabala na nchi ya Marekani, Inaonekana kabisa kuwa silaha hizo zilipelekwa kwa siri katika nchi ya Cuba.

Tamko hilo la Rais Nikita Khruschev lilizua hali ya taharuki ndani ya nchi ya Marekani, Haraka sana idara ya ujasusi ya nchi hiyo CIA ilifanya upelelezi wa haraka na kugundua kuwa ni kweli kabisa silaha za nyuklia zenye uwezo wa kuangamiza taifa la Marekani zilikuwepo katika kisiwa cha Cuba mkabala na nchi ya Marekani

Vita kamili...

Tarehe 12 October 1962 bunge la Marekani lilikutana na kwa pamoja lilipitisha azimio la kuivamia nchi ya Cuba kwa haraka sana, Rais John F Kennedy Sasa alikuwa kwenye shinikizo kubwa sana la kutangaza vita ambayo kwa hakika ingekuwa ndio vita kuu ya Tatu ya Dunia, Akilihutubia taifa la Marekani usiku wa tarehe 16 October Rais Kennedy alisema kuwa kamwe taifa la Marekani halitoweza kuvumilia kitendo hicho cha kutishiwa usalama wake na akasema kuwa jeshi la Marekani litakwenda nchini Cuba kuziondoa silaha hizo kwa nguvu kwa sababu njia zote za amani zilikuwa zimeshindikana

Tayari jumla ya askari wapatao 300,000 pamoja na meli za kivita pamoja na ndege za kivita ziliwasili katika jiji la Miami kujiandaa kuivamia nchi ya Cuba, Meli kubwa kabisa za kivita za Marekani zilisogea karibu kabisa na kisiwa cha Cuba tayari kuanza mashambulizi ya kukiteka kisiwa hicho, Majeshi ya Cuba na Urusi nayo yalijibu mapigo kwa kusogeza vikosi vyake katika fukwe za kisiwa hicho mkabala na Majeshi ya Marekani

Uwanja wa mapambano...

Meli za kivita za Urusi zikiwa zimebeba silaha kali kabisa za nyuklia zikiwa Sasa zinakabiliana ana kwa ana na meli za kivita za Marekani, Tarehe 27 October 1962 ni siku ya kukumbukwa sana Duniani, Siku hiyo wizara ya ulinzi ya Marekani ilitoa amri kwa ndege zake za upelelezi za kivita kuingia katika anga ya Cuba, ndege hizo zilikuwa na kazi ya kuangalia Majeshi ya adui yamejipanga vip ili kuweza kukabiliana nayo, Ndege hizo ziliweza kuonekana na rada za Majeshi ya Urusi na mara moja walianza kuzishambulia.

Majeshi hayo ya Urusi yalifanikiwa kuangusha ndege moja ya upelelezi ya jeshi la Marekani jioni ya siku hiyo ya tarehe 27 October 1962 na kusababisha kifo cha askari wa jeshi la anga la Marekani luteni Rudolph Anderson, Kifo cha rubani mdogo mwenye umri wa miaka 34 Luteni Rudolph Anderson kilimsikitisha sana Rais John F Kennedy, Asubuhi ya tarehe 28 October 1962 Rais Kennedy alikwenda hadi nyumbani kwa familia ya marehemu kutoa salamu za rambi rambi.

Katika Hali ya kuhuzunisha sana Rais John F Kennedy alianza kulia baada ya kumuona mke wa marehemu akiwa mjamzito na pia aliwaona watoto wadogo wa marehemu mmoja akiwa na miaka 5 na mwingine akiwa na miaka 3, taarifa za kuangushwa kwa ndege ya kivita ya Marekani zilienea kwa kasi sana Duniani na Kila mtu alijua tayari Sasa Vita imeanza, Jeshi la Uingereza usiku wa siku hiyo lilituma kikosi maalum cha makomandoo kwenye mstari wa mbele wa kivita huko mashariki ya ulaya

Vasil Arkshipov aiokoa dunia...

Usiku wa siku iyo ya tarehe 27 October 1962 nyambizi ya kivita ya Urusi B-59 ikiwa imebeba silaha kali za nyuklia ikiwa chini kabisa ya bahari pasipo kuonekana na rada za Majeshi ya Marekani ilisogea karibu kabisa na pwani ya Florida ili kuanza mashambulizi endapo jeshi la Marekani lingeanzisha vita.

Nyambizi hiyo iliongozwa na Captain Savitsky pamoja na Admiral Vassil Arkhipov iliingia usiku huo karibu na Florida, Ikiwa chini kabisa ya bahari walianza kuhisi kufuatiliwa na nyambizi za jeshi la Marekani.

Wasilokuwa wakilijua askari Hawa wa Urusi ni Kwamba nyambizi hizi za jeshi la Marekani zilikuwa katika doria yake ya kawaida na wala haikuwa ikiifuatilia nyambizi hiyo ya Urusi, Kwa kuwa walikuwa chini kabisa ya bahari hawakuwa na mawasiliano yoyote na wenzao, Kulinganisha na hali waliyokuwa wameiacha Cuba Nahodha wa nyambizi hiyo Captain Savitsky alijua kabisa kuwa Sasa Vita imeshaanza na kwa maagizo waliokuwa wamepewa ni kusubiria vita ianze na kushambulia pwani za Florida kwa makombora ya nyuklia.

Haraka sana Captain Savitsky alitoa amri ya kufyatua makombora ya nyuklia kwa nyambizi za Marekani na pia kwenye fukwe za Florida zilipokuwa kambi za kijeshi na kituo cha kijeshi cha Marekani kwa wakati huo, Ili kutekeleza amri hiyo ilihitajika idhini ya Admiral Vassil Arkhipov.

Vassil alikataa kata kata kuachia makombora ya nyuklia kwa nyambizi za Marekani akisema kuwa swala zito kama hilo linahitaji amri na idhini kutoka Moscow na sio kwa yoyote yule, Askari wote wa kwenye nyambizi hiyo walikuwa wakipingana na Vassil mabishano ndani ya nyambizi hiyo yaliwachukua saa nzima na hatimaye wote wakakubali amri ya Admiral Vassil Arkhipov ya kutokupiga makombora ya nyuklia na haswa baada ya kuona nyambizi za Marekani zikiondoka bila ya kufanya shambulizi lolote kwao.

Hakika kilikuwa kitendo cha ujasiri sana kwa Vassil kuwashawishi wenzake wasishambulie nyambizi za Marekani maana endapo nyambizi zile za Marekani zingewaona na kuanza kuwashambulia wao basi ni dhahiri kuwa nyambizi hiyo ya B-59 ya Urusi ingeteketea na wote waliokuwamo ndani yake wangeuawa

Nyambizi hiyo ya B-59 iliondoka haraka sana eneo hilo na kurudi ilipokuwa ngome yao katika pwani za kisiwa cha Cuba usiku huo huo wa tarehe 27 October 1962 na vita ikawa imesimama, toka hapo Urusi na Marekani wakaanza mazungumzo ya Amani ya kuiepusha dunia kuingia kwenye uwezekano wa kutoka vita.

Copyright 2021, All Rights Reserved.

Maktaba Kuu.

800px-Flag_of_Cuba.svg.jpg
800px-BahiadeCochinos40b.jpg
800px-BahiadeCochinos40b.jpg

View attachment 1820653View attachment 1820654View attachment 1820655View attachment 1820656View attachment 1820657View attachment 1820658View attachment 1820659View attachment 1820660View attachment 1820661View attachment 1820662View attachment 1820663
 
BAY OF PIGS Vs COLD WAR: MAREKANI, CUBA NA USSR, ULIMWENGU KIGANJANI MWA CIA, CRF NA KGB; NA AIBU YA DUNIA KWENYE ULINGO WA KIJASUSI.

Na. Comred Mbwana Allyamtu(CMCA)
Wednesday-16/06/2021
Kilimanjaro National Park, Marangu Kilimanjaro Tanzania.

Kwenye jengo la Pentagon ghorofa ya pili upande wa kushoto yani left wing kuna chumba namba 273, chumba ambacho ndio ofisi ya mshauri mkuu wa jeshi na wizara ya ulinzi ya Marekani yani "Chiefs of Staff counselor" , asubuhi ya Tarehe 13 mwezi wa 9 mwaka 1960, Kamati Maalumu ya Viongozi wa Juu Kijeshi nchini Marekani (Joint Chiefs of Staff Committee) chini ya Bw. L.M. Lemnitzer, iliidhinisha Operesheni iliyopewa jina la "Northwoods", kwa lengo la kutafuta sababu ya kuivamia kijeshi nchi ya Cuba (pretext for military invasion of Cuba), Chini ya operesheni hiyo, kamati ilipendekeza mfululizo mashambulizi yenye taswira ya kigaidi ndani ya miji ya Miami, Washington, D.C na kwingineko, meli za mizigo na abiria za nchi ya Marekani zingelipuliwa au kuzamishwa, ndege kutekwa, mauaji ya raia kutekelezwa makusudi, utoaji wa orodha 'feki' za wahanga wa mashambulizi ili kuufanya umma wa Wamarekani kuingia taharuki na kuipigia kelele za hasira serikali kulipiza kisasi kwa kuivamia Cuba. Kwa mujibu wa mpango huo, kila shambulizi lilipangwa kuhusishwa na nchi ya Cuba.

Kuidhinishwa kwa operation hii kulifatia baada ya mapinduzi ya Cuba yaliyofanyika mwaka 1959, mapinduzi hayo hayakuungwa mkono na mataifa mengi, hasa Ulaya na Marekani kwa sababu moja kubwa kuwa utawala wa Castro ulikuwa unaweka hatari masrahi ya Marekani nchini Cuba, sababu hiyo ni kuwa uongozi wa kijeshi ulioondolewa madarakani nchini humo chini ya dikteta Fulgencio Batista ulijaa vibaraka, walioweka mbele matumbo yao kwa kuigeuza Cuba kama mali ya mabepari, hasa Marekani, hivyo Castro na wanamapinduzi wenzake muda mfupi baada ya mapinduzi hayo, waliwatimua Wamarekani, kwa kuhodhi makampuni yote ya biashara, migodi, kilimo na Njia zote za uchumi.

Kitendo cha utawala wa Castro kutaifisha makampuni ya Marekani kiliisababishia Marekani hasara kubwa kibiashara, huo ndio ukawa mwanzo wa uadui baina yao, Mipango ya kuipindua serikali ya Fidel Castro ikaanza kwa nguvu sana, na kwa namna tofauti, ntaeleza hili kwa undani kabisa huko mbeleni, serekali ya Marekani litaka kuirudisha madarakani serikali itakayo waunga mkoni huko Cuba ili waendelee kulinyonya taifa hilo, jambo ambalo Castro na wenzake hawakutaka litokee.

Jambo la kujiuliza hapa ni kwanini Marekani iliiamua kuweka uadui na Cuba, swali la kujiuliza zaidi ni kwanini Marekani ilifamya maamuzi ya kutaka kuivamia Cuba! Maswali haya na mengine kibao kuhusu masrahi ya Marekani nchini Cuba yanairudisha nyuma historia ya Marekani na Cuba miaka 70 kabla ya tukio la kuivamia Cuba asubuhi ile ya mwaka 1961 kwenye ghuba ya mapigano ya Playa Girón ambayo hufahamika kama bay of pigs.

Hivyo basi...

Historia ya nchi hizi mbili inaanzia karne ya 18, kipindi ambacho Cuba ilikuwa "shamba la Bibi" kwa himaya ya kikoloni ya Kihispania, Katika karne ya 19 mwishoni, wazalendo wanamapinduzi wa Cuba walianza kuasi dhidi ya wakaloni wa Hispania na kutaka kuitawala nchi yao wakiongozwa na Jose Mart, hivyo kupelekea kupiganwa kwa vita tatu vya kuasi utawala wa Kihispania, Vita hivyo ni vita vilivyojulikana kama vita vya miaka kumi (1868–1878), nyingine ni ile vita iliyojulikana kama vita ndogo (1879–1880) na nyingine ni vita ya kupigania Uhuru wa Cuba (1895–1898), vita ambavyo Cuba ilijitangazia Uhuru wake, na Jose Mart kuwa rais wa kwanza wa Cuba guru, huyu José Mart nchini Cuba hutazamwa kama Baba wa taifa, mwasisi na mwanamapinduzi mkuu nchini humo, falsafa yake ya "Siri, Vamia, shambulia, gawanya na miliki" ndio ilikuwa kanuni kuu ya mapigamo kwa Castro, tutaliona hilo kwenye uvamizi wa Playa Girón au Bay of Pigs huko mbeleni.

Lakini serikali ya Marekani ilianzisha vita na himaya ya utawala wa Hispania nchini Cuba, ikumbukwe kuwa Hispania bado ilikuwa inataka kuendelea kuikalia Cuba na hivyo kupelekea vita ya Hispania na Marekani mwaka 1898, vita ambayo Marekani ilitaka kuikalia Cuba, hivyo mara kwa mara Marekani ilivamia kisiwa cha Cuba na kuyafurusha majeshi ya Hispania nje ya kisiwa cha Cuba, Katika mpango maalum uliopewa jina operation Habana, Marekani walipanga kuingiza askari 375 ndani ya visiwa vya Cuba katika mapigano ya Tayacoba katika vita kati ya Hispania na Marekani, ambapo Tarehe 20 May 1902, Marekani iliishinda Uhispania na serikali mpya ilijitangaza na kuunda Jamhuri ya Cuba chini ya usimamizi wa Marekani huku gavana wa kijeshi wa Marekani Leonard Woodhanding akimuongoza Rais Tomás Estrada Palma, Mcuba mzaliwa wa Cuba mwenye uraia wa Marekani.

Ni katika vita hivyo ndio Marekani ililikalia eneo la Guantanamo bay kama sehemu ya miliki ya Marekani kama malipo ya vita dhidi ya Hispania, Taratibu idadi kubwa ya walowezi na wafanyabiashara wa Kimarekani walikuwa wanawasili Cuba na hadi kufikia mwaka 1905 asilimia 60 ya bidhaa za mashambani zilikuwa zinamilikiwa na wananchi wasio Wacuba kutoka Marekani ya Kaskazini na kati ya mwaka 1906 na 1909, wanajeshi wanamaji wapatao 5,000 wa Kimarekani waliweka kambi katika kisiwa chote cha Cuba, na walirudi tena mwaka 1912, 1917 na 1921 na kuweza kuingilia mambo ya ndani ya Cuba, wakati mwingine bila hata ridhaa ya Wacuba wenyewe, hivyo hatimae Cuba ikawa sehemu ya nje ya Marekani.

Baada ya kuona namna Marekani ilivyoingia nchini Cuba toka mwaka 1898 kwa kuwafurusha Wahispania Sasa tuendele mbele ili kupata kiini halisi cha undani wa mapinduzi yenyewe ya mwaka 1959 nchini Cuba, lakini pia kwa nini tena Wacuba waliokuwa wakiishi uhamishoni, hususan wale ambao waliokuwa wakiishi jijini Miami katika jimbo la Florida walitaka kuuangusha utawala wa Castro nchini Cuba, pia nini hasa taifa la Marekani liliamua kuwekeza fedha nyingi ili kufanikisha kuudondosha utawala wa Castro, jambo ambalo tutaona baadae ni namna gani Marekani ilivyo injini uvamizi wa Bay of Pigs.

Mwezi Machi mwaka1952, Jenerali wa Cuba na mwanasiasa, Fulgencio Batista, alitwaa madaraka katika kisiwa hicho, na kujitangaza yeye binafsi kama Rais baada ya kumpindua Rais aliyekuwa madarakani, Carlos Prío Socarrás wa chama cha Partido Auténtico.

Batista alifuta uchaguzi wa Rais uliotarajiwa kufanyika, awali Batista alipata kiasi fulani cha uungwaji mkono, lakini kwa Wacuba wengi waliona hiyo ni aina ya utawala wa kidikteta wa mtu mmoja ambao Batista anajaribu kuuanzisha, Wengi wa wapinzani wa utawala wake waliamua kuasi na kuchukua njia ya mapambano ya silaha kumpinga na kujaribu kuuondoa utawala wake, hiyo ilichochea mapinduzi ya Cuba, Mojawapo ya makundi haya lilikuwa ni kundi la The National Revolutionary Movement (Movimiento Nacional Revolucionario – MNR), kundi la muungano wa kijeshi lililojumuisha watu wengi wanachama wa daraja la kati lililoanzishwa na Profesa wa Philosofia, Rafael García Bárcena. Kundi jingine lilikuwa The Directorio Revolucionario Estudantil (DRE), ambalo lilianzishwa na muungano wa wanafunzi wa vyuo vikuu, The Federation of University Students (FEU) chini ya Rais wake José Antonio Echevarría (1932–1957), Hata hivyo, miongoni mwa makundi yote hayo, kundi bora kabisa katika hayo yote yaliyokuwa yakimpinga Batista lilikuwa la "26th of July Movement" (MR-26-7), lililoanzishwa na Mwanasheria aliyeitwa Fidel Castro, Castro kama kiongozi mkuu wa MR-26-7, aliligawanya kundi lake katika mfumo wa vikundi vya watu kumi kumi, huku kila kikundi kikiwa hakijui uwepo wa kikundi kingine na kujua shuguli wanazozifanya kikundi kingine.

Kuanzia Desemba mwaka1956 mpaka mwaka1959, Castro aliongoza jeshi la msituni kupambana dhidi ya majeshi ya Batista kutoka katika ngome ya kambi yake kwenye milima ya Sierra Maestra, Kusambaa kwa vuguvugu la mapinduzi kulimfanya Batista kumpunguzia umaarufu, na kufikia mwaka 1958 majeshi yake yalikuwa katika uwezekano mkubwa wa kusalimu amri, hatimae Tarehe 31 Desemba mwaka 1958, Batista alijiuzuru na kukimbilia uhamishoni, huku akiondoka na kiasi kikubwa cha pesa zaidi ya dola za Kimarekani 300,000,000. Baada ya Batista kukimbia, Urais ukaangukia kwa Mwanasheria Manuel Urrutia Lleó, aliyechaguliwa na Castro, huku wanachama wa MR-26-7 wakidhibiti idadi kubwa ya nafasi katika baraza la mawaziri.

Ilipo fika Tarehe 16 Februari mwaka 1959, Castro akachukua Madaraka ya kuwa Waziri Mkuu, akaondoa uwezekano wa kufanyika kwa uchaguzi, kwa siku za mwanzoni, Castro alidai kuwa utawala mpya ni mfano wa demokrasia ya moja kwa moja ambayo umma wa wacuba unaweza kujikusanya kwa pamoja na kufanya maandamano na kuelezea hisia za demokrasia wanayoitaka moja kwa moja kwake yeye binafsi, Hata hivyo wapo waliolaumu utawala mpya wakisema si utawala wa kidemokrasia, moja ya makundi walio laumu ni walowezi wa kimalekani ambao asilimia kuwa walikuwa ndio wanao miliki 95% ya uchumi wa Cuba.

Hatua hiyo ilianza kutengeneza kudorola kwa uhusiano wa Marekani na Cuba, jambo ambalo viongozi kadhaa Washington waliitazama Cuba kama adui mpya, kufatia hatua hiyo serikali ya Cuba ilitoa amri kwa makampuni ya mafuta ya Esso na Standard Oil yaliyokuwa chini ya makampuni kutoka Marekani na kampuni ya Anglo-Dutch Shell ya Kiholanzi kuanza kusafisha mafuta yaliyonunuliwa kutoka katika nchi za Umoja wa Kisoviet badala ya Marekani lakini kutokana na shinikizo kutoka serikali ya Marekani makampuni hayo yalikataa.

Castro alijibu kwa kuyazuia kusafisha mafuta kisha akayataifisha makampuni yote na kuwa chini ya usimamizi wa serikali ya Cuba, katika kujibu mapigo, nayo serikali ya Marekani ikaacha kuagiza sukari kutoka Cuba hivyo kupelekea Castro kutaifisha raslimali nyingi zaidi zilizokuwa zinamilikiwa na Marekani, ikiwemo mabenki na viwanda vya sukari.

Uhusiano zaidi wa Cuba na Marekani ukaanza kuzorota kufuatia kulipuka kwa meli ya Kifaransa iliyoitwa "Le Coubre" na kupelekea kuzama katika bandari ya Havana mnamo mwezi Machi, mwaka 1960, Chanzo cha mlipuko hakikujulikana lakini Castro aliitaja hadharani serikali ya Marekani kuwa ndiyo iliyohusika na hujuma hiyo, lakini jambo ambalo wengi awajui ni kuwa tulio hilo la kuilipua meri hiyo ya "Le Coubre" serikali ya Marekani ilihusika, ntalieleza hili kwa upana hapo mbeleni.

Asubuhi ya tarehe 13 Oktoba, mwaka1960, serikali ya Marekani ilizuia kwa sehemu kubwa bidhaa kadhaa kusafirishwa kwenda Cuba kasoro bidhaa za madawa na baadhi ya vyakula, ikiashiria kuanza rasmi kwa vikwazo vya kiuchumi, Cuba nayo katika kujibu mapigo kamati ya Taifa ya Mabadiliko iliamua kuchukua usimamizi wa biashara binafsi 383 zilizokuwa zinaendeshwa na Marekani, na siku ya tarehe 1 Oktoba na tarehe 25 Oktoba zaidi ya makampuni 166 ya Marekani ambayo yalikuwa yakifanya shughuli nchini Cuba, majengo yao yalichukuliwa na kutaifishwa ikiwemo Coca-Cola na na kampuni ya Sear Roebuck.

Tarehe 16 Desemba, Marekani tena ikaacha kuagiza robo yote ya sukari iliyokuwa ikiagiza kutoka Cuba, Serikali ya Marekani ikazidisha kuipinga serikali ya kimapinduzi ya Castro.

Hatimae Mwezi Agosti,1960 katika mkutano wa umoja wa nchi za Amerika, yaani Organization of American State (OAS) uliokuwa unafanyika Costa Rica, Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Christian Herter, hadharani alidai kwamba utawala wa Castro "kwa uaminifu mkubwa unafuata misingi ya njia za Bolshevik" kwa kukazia mfumo wa chama kimoja cha siasa kwa serikali yake kuweka vyama vya wafanyakazi chini yake, kubana uhuru wa raia na kuondoa uhuru wa kuongea na uhuru wa vyombo vya habari na akaenda mbali zaidi kwa kusema kuwa nchi za kijamaa zinaitumia Cuba kama ngome yake ya kusambaza mapinduzi katika nchi za ncha ya Kaskazini na akatoa wito kwa wanachama wengine wa umoja huo wa OAS kuilaani Cuba kwa ukiukwaji wa haki za binadamu.

Cuba nayo ikajibu mapigo, Castro alielezea namna jamii ya watu weusi inavyonyanyaswa na tofauti kubwa ya matabaka ya wafanyakazi aliyoishuhudia wakati akiwa New York, na kupiga kijembe na kudhihaki kuwa huo ndiyo "uhuru wa hali ya juu, demokrasia ya hali ya juu, utu wa hali ya juu, na kustaarabika kwa hali ya juu kwa jiji hilo." Akadai kuwa masikini wa Marekani wanaishi katika "bakuli la mabepari wanyonyaji", pia Castro aliushambulia mtiririko wa vyombo vya habari vya Marekani na kuulaumu kuwa unaendeshwa na wafanya biashara wakubwa.

Kwa namna nyingine Marekani ilikuwa inajaribu kuimarisha uhusiano wake na Cuba, Majadiliano mengi kati ya wawakilishi kutoka Cuba na Marekani yalifanyika katika kipindi hiki, Kurekebisha uhusiano wa fedha wa kimataifa ndiyo ilikuwa dira kuu ya majadiliano hayo, Mahusiano ya kisiasa ilikuwa ajenda nyingine kubwa ya mikutano hiyo, Marekani ilieleza kuwa haitaingilia aina ya serikali ya Cuba inayoitaka au mambo yake ya ndani hata hivyo Marekani ikaiaumu Cuba kufuta siasa za Umoja wa Kisovieti, walimshawishi Castro kuacha siasa za kisoviet kwa kumuhaidi miassada kibao ya kuendesha nchi, lakini Castro aligoma, hapa ndipo Marekani ikaamua kubadilisha muelekeo dhidi ya Cuba, hapa Sasa Marekani wakaingia kazini ili kuiadabisha Cuba.

Mwezi Augosti, mwaka 1960, CIA waliwasiliana na kundi la Cosa Nostra lilokuwa na makao yake jijini Chicago ili kuandaa mipango mbalimbali ya kuwaua Fidel Castro, Raúl Castro na Che Guevara, katika mpango huo Marekani ilikubaliana na kikundi hicho kuwa baada ya kupachika serikali ambayo inawaunga mkono nchini Cuba, watakubaliana kati ya CIA na kundi hilo la Mafia kupata umiliki wa michezo ya bahati nasibu, biashara ya umalaya na madawa ya kulevya ndani Cuba, hivyo mipango hiyo ikapangwa kuanza rasmi mwaka 1960, lakini mpango huo ulitakiwa lazima upate idhini ya rais wa Marekani.

Hivyo mkurugenzi mkuu wa CIA Allen Dulles, akaamdaa kikao maalumu ili kujadili namna ya kumshawishi raisi Dwight D. Eisenhower mpango wa kuivamia Cuba na kumuua Castro, Dulles akiwa na Rolando Cubela, afisa mipango wa CIA mwenyeji wa Frolida ambae alikuwa anaifahamu vizuri Cuba, akapewa kazi ya kuinjinia ramani mpango wa namna ya kuivamia Cuba, ikumbukwe kwamba Shirika la Ujasusi la Marekani yaani Central Intelligence Agency (CIA), ni shirika la kijasusi ambalo liliundwa na serikali ya Marekani mwaka 1960 kupitia sheria iliopitishwa na bunge la Congress mwaka 1947, kupitia sheria iliyoitwa "National Security Act" azimio namba 90551, CIA "ilikuwa ni zao la Vita Baridi", shirika hili lilibuniwa ili kuzikabili njama za shirika la ujasusi la Umoja wa Kisoviet la KGB.

Sasa basi...

Hatua hii ilifatia baada ya tishio la kusambaa kwa ukomunist ulimwenguni kuwa mkubwa, CIA ilipanua shughuli zake kukabiliana na mambo ya kiuchumi, kisiasa na mambo ya kijeshi katika kulinda masilahi ya Marekani, na wakati mwingine kutumia njia za hatari ili kulinda maslahi hayo ya Marekani, Mkurugenzi wa CIA kwa wakati huo, Allen Dulles, alikuwa na wajibu wa kusimamia operesheni hizo duniani kote, hivyo jioni ya tarehe 7 mwezi 8 1960 Allen Dulles alituma ujumbe wa maneno kwenda kwenye kamati maalumu ya usalama wa taifa nchini Marekani, ujumbe huo uliokuwa na code namba SO444.PO1117 ulipokelewa na mwana mama Heren McKay aliyekuwa ofisni siku hiyo, Kwenye jengo la CIA Langley kulikuwa na kikao kilefu kilichomalizika saa 5:52 usiku kikao hicho kiliwajumlisha Rolando Cubela,Desmond Fitzgerald, Robert Kennedy, Bw. L.M. Lemnitzer, na Allen Dulles mwenyewe.

Azimio la kikao hicho ilikuwa ni kumshawishi Raisi Dwight D. Eisenhower kuhusu mpango wote ulio wasilishwa mezani na Rolando Cubela wa namna ya kuivamia Cuba, azimio hilo ulikuwa na mapendekezo matatu, Mosi ni kumshawishi Raisi Eisenhower kuidhinisha uvamizi huu bila kulishirikisha bunge, maana kama wangelishirikisha bunge wabunge wasingekubali kwasababu mda mfupi nchi ya Marekani ilikuwa inajiandaa kuingia kwenye uchaguzi mkuu, hivyo wanasiasa wengi wasingekubali kujitia doa wakati wakijianda kugombea nafasi mbalimbali, lakini hapo hapo chama cha Republican kisenge unga mkono mpango huo, hivyo waliona mpango huo ungependeza kama Raisi Eisenhower mwenyewe autekeleze kwa siri.

Pili, walipendekeza kuwa mpango huo utekelezwe na CIA wenyewe bila kushirikisha Kitengo kingine, hii ili kuwa na maana moja kubwa kuwa kwakuwa Marekani ilikuwa kwenye vita baridi na Urusi hivyo kuruhusi vyombo vingine kuhusika ingehesabika kuwa ni vita, hivyo Urusi ingeingilia kati na kuufanya mpango kuwa mgumu, swali la kujiuliza hapa ni kwanini Marekani iliiogopa Urusi kuingia kwenye vita hivyo? Lakini swali lingine zaidi la kujiuliza je ni kuwa Marekani haikuwa na uhakika na mpango huo? Yote haya nitayaeleza huko mbele.

Pendekezo la Tatu, ilikuwa ni wakati wanaivamia Cuba, lazima tukio la uvamizi lifanywe na wa Cuba wenyewe ili ulimwengu usione kuwa uvamizi huo taifa la Marekani halihusiki kwa namna yoyote ile.

Hivyo mapendekezo hayo yote matatu yaliwasilishwa na Rolando Cubela ambae alipewa kazi hiyo na Allen Dulles, kikao hicho kiliidhinisha mapendekezo hayo ambayo yalitakiwa kufika mezani kwa Raisi Eisenhower ikulu ya White house, wakati hayo yakiendelea ule ujumbe wa maneno wenye code namba SO444.PO1117 uliopokelewa na mwana mama Heren McKay aliyekuwa ofisni siku hiyo, Bi,Heren McKay ndie aliyekuwa msaidizi binafsi wa Raisi Eisenhower kwenye ikulu ya White house, mara moja akampelekea ujumbe huo raisi ofisini kwake, alimkuta Raisi Dwight D. Eisenhower akiwa na kikao na maafisa kadhaa wa ikulu, baada ya muda Raisi Dwight D. Eisenhower akakutana na Heren McKay, ambae alimkabizi ujumbe rais, ujumbe huo ulikuwa ukiomba Raisi Eisenhower kuandaa kikao maalumu na Allen Dulles, kwakuwa kikao hicho kilitakiwa kuwa na siri kubwa, utaratibu huu ulikuwa umezoeleka kati ya Allen Dulles na rais Eisenhower pale walipokuwa wanataka kuzungumzia mambo mazito yaliyoitaji siri kubwa za bila kuhusisha vyombo vingine.

Tarehe 20 mwezi wa 8, 1960...

Kwenye ofisi ya raisi wa Marekani oval office, White house Raisi Eisenhower alikutana na Allen Dulles, kujadili mapendekezo ya uvamizi wa Cuba, baada ya mazungumzo ya muda mrefu Raisi alikubali mapendekezo hayo lakini akapinga kufanyika operation hiyo bila kuishirikisha kamati maalumu ya usalama wa taifa hilo kwani Raisi Eisenhower alimtahadharisha Dulles kuwa mpango huo ungeitaji fedha katika kufanikisha mkakati huo, japo Allen Dulles alijaribu kumuonesha Raisi Eisenhower madhara ya iwapo mpango huo utahusisha vyombo vingi kungekuwepo na hatari ya mpango huo kugomewa.

Raisi Eisenhower alimuhakikishia Dulles kuwa mambo yangekwenda vizuri, tarehe 25 mwezi wa 8 1960 Raisi Eisenhower aliomba kikao na maafisa kadhaa wa Kamati Maalumu ya Viongozi wa Juu Kijeshi nchini Marekani yani Joint Chiefs of Staff Committee, ili kuweza kuwashawishi kumuunga mkono katika mpango wake wa kuivamia Cuba, Raisi Eisenhower aliwaeleza namna gani serikali ya Castro wanavyozidi kuwa tishio na kuhatarisha masrahi ya Marekani ukanda nzima wa America ya kusini, Rais Dwight D. Eisenhower aliwaomba maafisa hao kupokea mapendekezo ya shirika la CIA ya kuanza matayarisho ya kuivamiaCuba na kuupindua utawala wa Castro.

Baada ya kamati hiyo kulidhia mpango huo bado walisisitiza kuwa Raisi lazima mpango huo aupeleke mbele ya baraza la mawaziri ili uidhinishwe na kupewa baraka na serikali, hatua hiyo ilikuwa muhimu kwasababu mpango huo ulionekana kuhusisha hatua nyingi mpaka kukamilika kwake, hivyo lazima mpango huo ungeitaji fedha katika kufanikisha mkakati huo.

Rais Eisenhower alilidhia hilo na kukutana na mawaziri wake tarehe 2 mwezi wa 9 mwaka 1960, ambapo baraza la mawaziri kwa pamoja waliidhinisha mpango huo kwa azimio namba 7186 na kuiruhusi CIA kuendelea na operation hiyo, japo walitaka mpango huo kuwa na tahadhari sana, ili kuiepusha Marekani na kelele za kimataifa.

Hivyo...

Raisi Eisenhower akaikabidhi CIA faili la mapendekezo ya kuanza maandalizi ya maauji ya Castro na uvamizi wa Cuba, hatimae asubuhi ya Tarehe 13 mwezi wa 9 mwaka 1960, Kamati Maalumu ya Viongozi wa Juu Kijeshi nchini Marekani (Joint Chiefs of Staff Committee) chini ya Bw. L.M. Lemnitzer, iliidhinisha Operesheni iliyopewa jina la "Northwoods", kwa lengo la kutafuta sababu ya kuivamia kijeshi nchi ya Cuba, Chini ya operesheni hiyo, kamati ilipendekeza mfululizo mashambulizi yenye taswira ya kigaidi ndani ya miji ya Miami, Washington, D.C na kwingineko, meli za mizigo na abiria za nchi ya Marekani zingelipuliwa au kuzamishwa, ndege kutekwa, mauaji ya raia kutekelezwa makusudi, utoaji wa orodha 'feki' za wahanga wa mashambulizi ili kuufanya umma wa Wamarekani kuingia taharuki na kuipigia kelele za hasira serikali kulipiza kisasi kwa kuivamia Cuba. Kwa mujibu wa mpango huo, kila shambulizi lilipangwa kuhusishwa na nchi ya Cuba, lakini mipango yote hii ilitakiwa kusimamiwa na CIA.

CIA nao wakaandaa njia ambazo watazitumia kumuua Castro, njia hizo ziliandaliwa kwa ustadi wa hali ya juu na ubunifu wa hali ya juu, kwa mfano, vidonge vya sumu, mlipuko wa meli ya mafuta baharini, pia CIA ilitayarisha mpango maalumu wa mazumgumzo ya amani ya siri na Castro lakini lengo likiwa ni kumuua Castro kwa kumtumia mwanamapinduzi wa Cuba ambae alikuwa shushushu wa Marekani akiwa ni wakala wa CIA, wakala huyu alitwa Rolando Cubela, ambae alipangwa kumuua Castro kupitia shamburizi kwenye mkutano huo, alafu mauaji hayo yatafsirike kutekelezwa na Mcuba hivyo Marekani ijivue lawama za kuhusika, mpango huo ulipangwa na ofisa wa CIA aliyeitwa Desmond Fitzgerald, ambaye angejifanya yeye ni mwakilishi maalumu wa Robert Kennedy.

Mipango yote hiyo ikaonekana kushindwa hivyo ikafikiliwa mpango mkakati mwingine utakao leta matokeo chanya katika kufanikisha mkakati wao, ndio wakaja na mpango mpya wa kuivamia Cuba kijeshi, mpango huu ndio uliokuja kujulika kama "Uvamizi wa Bay of Pigs".

Bay of Pigs ilivyoratibiwa...

Uvamizi wa Bay of Pigs ulikuwa ni uvamizi wa taifa la Marekani kuivamia Cuba kupitia Ghuba ya nguruwe, ghuba hii ipo nchini Cuba kaskazini Magharibi mwa visiwa vya Cuba, uvamizi huu ni moja ya uvamizi mkubwa kufanywa na Marekani ambao ulishindwa kwa aibu kubwa, kwani uvamizi huu ulishindwa pamoja na kufadhiliwa na Marekani kwa fedha nyingi karibu dola billion 1.3 dhidi ya kuivamia Cuba mwaka 1961.

Uvamizi huu kwa Kiingereza unajulikana kama "The Bay of Pigs invasion" na kwa Kihispania unajulikana kama "invasión de bahía de Cochinos" wakati mwingine pia uvamizi huu huitwa "invasión de playa Girón" au "batalla de Girón", yaani mapigano ya Playa Girón.

Kama nilivyokwisha sema hako mwanzo kuwa hili lilikuwa ni jaribio la mapigano yaliyoshindwa ambapo serikali ya Marekani iliwafadhili Wacuba waliokuwa wakiishi uhamishoni kujaribu kuipindua serikali ya Cuba iliyoongozwa na Fidel Castro, uvamizi huu ulianzia kuvamia sehemu ya Kaskazini ya Cuba, Shirika la Ujasusi la Marekani CIA katika kufanikisha uvamizi huu lilifadhili kundi la waasi la Brigade 2506, ntalieleza kundi hili baadae kidogo, hivyo kundi hili ndilo lilofanya shuguri ya kuvamia Cuba tarehe 17 Aprili mwaka 1961 Katika mapigano ambayo yalichukua siku tatu.

Kundi la Brigade 2506...

Kundi hili la Brigade 2506 lilikuwa ni kundi la wapingaji wa Mapinduzi ya Cuba na serikali ya Fidel Castro ambao wengi wao walisafiri kwenda uhamishoni Marekani baada ya Castro kuwa ameitwaa Cuba baada ya kuiangusha serikali ya Dikteta Fulgencio Batista mwaka 1959, mapigano hayo pia yaliwahusisha baadhi ya wataalaamu wa kijeshi wa jeshi la Marekani.

Kundi hili likiwa wamepawa mafunzo na kufadhiliwa na CIA, kundi hili la Brigade 2506 lilikuwa ni tawi la kijeshi la chama cha Democratic Revolutionary Front (DRF) ambao walidhamiria kuipindua serikali ya Fidel Castro ambayo ilionekana inaegemea kwa kasi kwenye siasa za mrengo wa Ukomunisti, mipango yote ya kuvamia na kuipundua serekali ya Castro iliratibiwa huko nchini Guatemala na Nicaragua, majeshi ya uvamizi yaliandaliwa chini ya usimamizi wa Marekani, ambapo yakiwa huko walipokea malipo ya fedha kwa kila askali, walihaidiwa fedha zaidi na nafasi za uongozi ikiwa watayatwaa Madaraka.

Turudi nyuma kidogo ili kulifahamu kundi la "Democratic Revolutionary Front (DRF)"....

Ni kwamba mwaka 1952 nchini Cuba yalifanyika mapimduzi yaliyoongozwa na Generali Fulgencio Batista, mshirika mkubwa wa Marekani, dhidi ya Rais Carlos Prio aliyekuwa madarakani, mapinduzi hayo yalimlazimisha Rais Prio kuondoka Cuba na kwenda kuishi uhamishoni jijini Miami nchini Marekani, raisi Prio alipo fika huko uhamishoni Rais Prio, akamua kuanzisha kundi la uasi ili kuishambulia serikali ya Batista na kurejea tena Madaraka, kundi hilo likaitwa Democratic Revolutionary Front (DRF), kundi hili ndio baadae wa Marekani wakalitumia kuangusha utawal wa Castro, ikumbukwe kwamba Marekani ilimfadhili Batista kumgoa Prio pia Marekani hiyo hiyo ikaitumia kundi hilo la Prio kumgoa Castro.

January 3 mwaka 1961...

Kule Washington DC mpango wa 'kumnyoosha' Castro ulianza, Mpango huo, ulihusisha utoaji mafunzo maalumu ya kijeshi kwa vijana karibu 1400 kwa siri ndani ya kambi zilizojengwa jimboni Florida katika jiji la Miami, kusini-Mashariki mwa Marekani na nchini Guatemala, Amerika ya kati, Mafunzo hayo yaliandaliwa, kufadhiliwa na kuratibiwa kwa asilimia 100% na serikali ya Marekani kupitia Wizara yake ya Masuala ya Nje halikadhalika Shirika lake la Ujasusi (C.I.A), Wengi wa vijana walioshiriki, walikuwa ni Wa Cuba walioishi uhamishoni, waliompinga Castro na utawala wake.

Mtu aliyepewa kazi ya kusimamia mipango yote ya kuongoza uvamizi wa Bay of Pigs alikuwa ni Richard M. Bissell Jr, Naibu Mkurugenzi wa Mipango wa CIA yaani Deputy Director for Plans (DDP), jasusi huyu ndie aliyefanya kazi ya kutarisha maafisa wengine wengi tu ili kuweza kumsaidia kufanikisha mipango ya jaribio hilo, wengi wao wakiwa wale walioshiriki katika mapinduzi yaliyofanyika miaka sita nyuma yani mwaka1954 huko Guatemala, hawa ni pamoja na David Philips, Gerry Droller na E. Howard Hunt.

Bissell alimkabidhi Droller jukumu la kuwa kiongozi wa kuwakusanya Wacuba wanaompinga Castro miongoni mwa jamii ya Wacuba-Wamarekani wanaoishi uhamishoni na alimuomba Hunt kuunda kitu kama serikali iliyo uhamishoni ambayo CIA itakuwa inaidhibiti, Hunt alisafiri kwenda Havana, mji mkuu wa Cuba, huko alikutana na kuzungumza na Wacuba kutoka katika makundi mbalimbali.
Hunt aliporudi Marekani aliwataarifu Wacuba waioshio Marekani ambao alio kuwa anawakusanya kuwa wanatakiwa wahamishie harakati zao kutoka jijini Florida nchini Marekani na kwenda Mexico City nchini Mexico, kwa sababu idara ya Taifa ya Marekani kwa maana ya State Department ya Marekani imekataa kuwaruhusu CIA kupatia mafunzo yao ndani ya ardhi ya Marekani, kitendo hiki kulikuwa na maana kuu Tatu, Mosi Viongozi wengi waliona kuwa kitendo cha kuwaruhusu wakimbizi kufanya mafunzo ndani ya aridhi ya Marekani ingekiuka sheria za kimataifa ambazo ni kitendo cha uhalamia hivyo ingeichafua Marekani kwenye taswira za kimataifa.

Pili, kwakuwa Marekani ilikuwa kwenye uchaguzi mwezi November 1960, jambo lingeweza kuharibu uchabuzi na kufanya taharuki kwenye majimbo ya kusini ambapo chama cha Republican kilitegemea kupata kura huko.

Tatu, Kwakuwa taifa la Marekani lilikuwa kwenye vita baridi na Urusi, kitendo hicho kingetafsirika na Urusi kuwa uvamizi huo unafanywa na Marekani na sio wa Cuba wenyewe ambao wanaupinga utawala wa kikominist wa Castro, jambo hili serikali ya Marekani ilitaka ulimwengu uamini kuwa wao hawahusiki na chochote ambacho kingeendele huko Cuba.

Ingawa askali hao hawakuwa na furaha kusikia habari hizo, lakini waliipokea amri hiyo, hivyo vituo vya mafunzo vikaamia Mexico city, hatimae baadae wakaamia Nicaragua, Panama na Guatamala kwa mafunzo ya kuingia kuivamia Cuba.

Baada ya uchaguzi mkuu wa Marekani wa November mwaka 1960, raisi Jonh F. Kennedy alishinda uraisi, hivyo Rais Eisenhower ambae alikuwa akiratibu uvamizi wa Cuba akasimamisha mipango kwakuwa hakuwa na nguvu tena ya kisheria ya kuinjinia uvamizi wa nchini Cuba, hivyo Raisi Eisenhower alimualika Rais Kennedy aliyechaguliwa katika uchaguzi wa mwaka huo katika Ikulu ya White House tarehe 6 Desemba, mwaka 1960, na tarehe 19 Januari, mwaka 1961 ili kumshawishi atakapoingia ikulu aendelee na mpango huo ambao mtangulizi wake alikuwa ameuanzisha, katika moja ya mazungumzo yao, Eisenhower alimwelez Kennedy kuwa toka mwezi Machi, mwaka 1960, serikali ya Marekani ilikuwa inatoa "mafunzo kwa vikundi vidogo vidogo lakini hatujafanya kitu chochote" kwasababu bado sija approve uvamizi, alimueleza pia Kennedy kuwa "baadhi ya mamia ya asikali ambao ni wakimbizi" wako huko Guatemala, na "wachache wako huko Panama, na baadhi jijini Florida."

Kama nilivyo elezea huko nyuma kuwa mara tu baada ya Fidel Castro kuchukua madaraka mwaka 1959, mwaka uliofuata yaani mwaka 1960, CIA kwa ruhusa ya Rais Dwight Eisenhower ambaye alikuwa anakaribia kuondoka madarakani walianzisha mikakati ya namna gani watamuondoa madarakani Fidel Castro, Fursa kuu waliyoitumia ulikuwa ni kutumia wahamiaji walioingia Marekani kutoka Cuba kukimbia utawala wa Fidel Castro uliokuwa "unafanya usafi" dhidi ya raia waliokuwa wanamuunga mkono Fulgencio Batista, Kwa hiyo CIA wakakusanya mamia ya raia hawa kwa siri kubwa na kuwapandikizia hari na ushaiwshi wa kutaka kumpindua Fidel Castro.

Mwezi March mwaka 1960 rais Dwight Eisenhower alipitisha bajeti ya dola milioni 13.1 kwa ajili ya mpango huu wa mapinduzi, Raia hawa wa Cuba waliokimbilia uhamishoni nchini Marekani ambao walifahika kama kikosi cha Brigade 2506, wakaanza mafunzo ya kijeshi kwa mwaka mzima nchini Guatemala, Mpango huu wa kuivamia Cuba na kumpindua Fidel Castro ulipangwa ufanyike mapema mwaka 1961 na ulikuwa umekamilika kila kitu lakini raisi Eisenhower hakuupa 'approval' na aliacha jukumu hilo la kuidhinisha uvamizi huo ifanywe na atakaye kuja kumrithi yaani Rais JF Kennedy.

Kwa hiyo mara baada ya uchaguzi mkuu mwezi November, 1960 na hatimaye JF Kennedy kuapishwa January 20 mwaka 1961, kitu cha kwanza ambacho alikabiliana nacho ni CIA kumkabidhi mkakati ulioandaliwa na wao CIA chini ya Rais Dwight Eisenhower kuhusu uvamizi wa Cuba na kumpindua Fidel Castro, hivyo mwezi February tarehe 13, mwaka huo, mpango wenye sura nzima ya utekelezaji operesheni hiyo ulitua mezani kwa Rais Kennedy.

Awali ni kwamba CIA walipowasilisha mkakati wao wa mapinduzi ya Fidel Castro kuna vitu vingi vya msingi walimficha Kennedy hii ni kwasababu Kennedy hakuonesha kuunga mkomo mpango huo toka alipotaalifiwa na maafisa usalama wa Marekani na hats Raisi Eisenhower walipokutana kwa mara ya kwanza ikulu december 10, 1960, hili ndio lilopelekea hata CIA kutompatia taarifa zote Kennedy kwakuwa waliona angekwamisha mpango huo, hivyo wakaamumu kumptatia taarifa chache, Na hii inaonekana kwamba walichukua 'advantage' kwa sababu ya ugeni wa Kennedy katika wadhifa wake huu upya wa Urais na kwa hiyo kutofahamu uhalisia wa vitu vingi kwa hiyo CIA wakatumia hiyo fursa 'kum-mislead' katika vitu muhimu kuhusu mkakati huo.

Mkakati ulikuwa ni mpana sana, lakini kwa ufupi ni kwamba, wavamizi hawa wa Brigade 2506 ilikuwa imepangwa wavamie Cuba wakitokea Guatemala na Nicaragua wakiwa na askari wa miguu pekee, Kennedy hakutaka Marekani ionekane ikihusika moja kwa moja kwenye uvamizi huo ili kulinda taswira yake katika jamii ya kimataifa na pia kuepuka kuamsha hasira za Urusi ambao walikuwa ni mshirika mkubwa wa Cuba, kwahiyo kukabiliana na hili, CIA walipendekeza kuwatumia makomando wake wa SAD, ntakuelezea kidogo kuhusu hawa SAD ni wakina nani?

SAD ni nini hasa?...

SAD ni kitengo malumu ndani ya shirika la CIA ambalo wao hufanya shughuri maalumu na zenye unyeti wa maswala muhimu, hivyo idara hii ni maalumu ndani ya shrika la CIA, ambayo hujulikana kama "Special Activities Division"

Watu wengi huzani kuwa CIA ndio kufanya shuguri zote za kijasusi, lakini ukweli ambao wengi hawauelezi ni kuwa umahiri na upekee wa wa shirika la CIA hufanywa na kikosi maalumu cha kipekee kwa ajili ya kazi nyeti maalumu na kazi hizo husamiwa na maafisa wa Idara ya SAD ndani ya CIA.

Upekee wa SAD ndani ya CIA ni nini?...

Kutokana kuongezeka kwa changamoto za kimataifa , ambazo nyingine zinatishia usalama au maslahi ya Marekani lakini marekani haiwezi kuchukua hatua zozote kutokana kujiepusha na lawama kutoka jamii ya kimataifa ndipo hapo ikaonekana kuna umuhimu wa kuwa na kitengo maalumu kwa ajili ya suala hili.

Ndipo hapa ambapo serikali ya marekani ikaagiza shirika la kijasusi la CIA kuanzisha kitengo maalumu ndani yake ambacho kitakuwa na maafisa (wanajeshi) ambao wanaweza kutekeleza oparesheni yoyote ya kijeshi kwa kujitegemea pasipo kuhusisha serikali ya marekani.

CIA wakaanzisha idara maalumu ndani yake na kuuita Special Activities Division au kwa kifupi SAD ambayo idara yenyewe ilikuwa na maafisa wa siri ambao hawabebi vitambulisho na majina yao ni siri kubwa hayawezi kupatikana hata kwenye orodha ya maafisa wa CIA.

Lengo kubwa la kuanzishwa kwa idara hii ni kutekeleza oparesheni maalumu za kijeshi au proaganda na iikitokea wakakamatwa au kushitukiwa basi serikali ya marekani wanawakana kuwa si maafisa wao (Plausible deniability).

Kwahiyo kitengo hiki kilikuwa kinafanya kazi kwa niaba ya serikali ya Marekani lakini kulikuwa hakuna uwezekano wowote wa adui kuunganisha uhusika wa kikosi hiki na serkali ya marekani.

Ndani ya Idara hii ya SAD kuna vitengo viwili;.......

Kitengo cha kwanza kinaitwa Political Action Group, kitengo hiki kazi yake kubwa ni kufanya ushawishi wa kisiasa (political influence), oparesheni za kisaikolojia (psychological operations) na vita za kiuchumi (Economic Warfares), Pia kutokana na maendeleo ya kiteknolojia, kitengo hiki kimeongezewa jukumu la vita za kimtandao (cyberwarfares).

Tuchukulie kwa mfano, katika nchi fulani kuna serikali au mwenendo wa serikalin uatishia maslahi ya Marekani basi kitengo hiki kinaingia kwa siri kubwa na kufanya mojawapo ya mambo ambayo nimeyaorodhesha hapo juu.

Moja ya matukio ambayo kitengo hiki kimehusika sana na CIA wamekiri kwenye nyaraka zilizowekwa wazi mwaka 2004 ilikuwa ni kueneza propaganda ambayo ilichangia kupinduliwa kwa Rais wa Iran mwaka 1953, Pia kitengo hiki kilitumika kuzuia chama cha kikomunisti cha Italia kushinda uchaguzi mwaka 1960.

Pia kitengo hiki kimewahi kufanya oparesheni ya siri iliyoitwa Operation Mockingbird katika taifa la marekani, Oparesheni hii ilikuwa na lengo la 'kucontrol' habari zinazoandikwa na Vyombo vya habari nchini humo, Oparesheni hii imekuja kupingwa vikali siku za karibuni na baraza la seneti kwa kuwa sheria hairuhusi CIA kufanya oparesheni yeyote ndani ya ardhi ya marekani.

Kitengo cha Pili kinaitwa Special Operations Group (SAG) na kazi yake ni kama ifuatavyo......

Kitengo hiki kinajumuisha wanajeshi wenye weledi wa hali ya juu kutekeleza malengo ya kivita pasipo kujulikana uhusika wa serikali ya marekani, Ili kulinda utambulisho wao, wanajeshi wa kikosi hiki maalumu hawavai sare za jeshi wala kubeba vitambulisho, Inasemekana kuwa hiki ndio kikosi maalumu cha oparesheni za kijeshi chenye usiri mkubwa nchini marekani.

Maafisa wa kitengo hiki wanapatikanaje?...

Maafisa wote wanaojiunga katika kitengo hiki maalumu cha SAD wanachaguliwa kutoka katika vikosi vingine vya weledi vya jeshi la marekani mfano Army Rangers, Combat controllers, Delta Force, 24 th STS, US Army Special Forces, SEALs, Force Recon n.k.

Wakishakuchaguliwa wanapelekwa katika kituo maalumu cha mafunzo ya CIA kilichopo Virginia kinachojulikana kama Camp Peary (au maarufu kama 'The Farm') ambapo miezi 18 ya kwanza wanafundisha kuhusu intelijensia na ushushushu.

Baada ya miezi 18 hiyo wanapelekwa kwenye kituo kingine cha CIA kilichopo California ambacho kinajulikana kama 'The Point', Hapa wanafundishwa mafunzo ya hali ya juu ya kijeshi ambayo hayapatikani kwa kiwango hicho katika vikosi vingine vya marekani.

Mfano wanafundishwa; mapigano ya ana kwa ana ya kiwango cha juu zaidi (special hand to hand combat), kutumia karibia aina zote za silaha na milipuko ya jeshi la marekani na nchi za kigeni, ufuatiliajj adui (tracking), Kukabiliana na hali ngumu kwenye mamzingira ya kawaida na nyikani ( extreme survival and wilderness train ing), Kumkwepa aduia, kuzuia adui na kutoroka adui (evasion, Resistance and escape - SERE) na pamoja na mafunzo hayo anaongezewa kozi maalumu ya kutambua fiziolojia ya binadamu (Udaktari).

Afisa ambaye anafuzu mafunzo haya anakabidhiwa katika idara ya SAD ndani ya CIA na anatambulika kama "Afisa Mwenye Mbinu Maalumu" (Specialized Skills Officer), Katika oparesheni zao maafisa hawa huwa wanazitekeleza katika vikundi vya watu wachache sana wasiozidi sita na oparesheni nyingine zinatekelezwa na Afisa mmoja pekee.

Katika Ofisi za CIA kitingoji cha Langley jijini Virginia kuna ukuta wa majina ya Maafisa wa CIA waliotunikiwa tuzo za heshima kutoka na utumishi wao uliotukuka ( Distinguished Intelligance Cross na Intelligence Star), Majina ya maafisa wengi kwenye ukuta huo ni ya wale waliotumikia kitengo cha SAD ndani ya CIA.

Kwa kuzingatia kwamba makala hii inalenga kuzungumzia uhusika wa CIA katika mapinduzi ya serikali ya Cuba kupitia Uvamizi wa Bay of Pigs, Hivyo basi tuone mifano michache sana ya oparesheni zilizotekelezwa na kitengo hiki cha SAD ndani ya CIA, Nitaeleza kwa ufupi ili tusitoke nje ya lengo kuu (mapinduzi ya Cuba ).

Ni idara hii maalumu ya CIA ambayo ilikabidhiwa raia wanne wa Tibet kutoka kwa kaka mkubwa wa kiongozi wa kiroho wa Tibet Mtukufu Dalai Lama ambapo idara ya SAD iliwapa mafunzo ya kikomando watibeti hao kisha wakawarudisha Tibet kutafuta raia wengine 300 ambao SAD iliwapa mafunzo ya kijeshi kwa siri katika kisiwa cha Saipan na mwezi oktoba SAD ikawaongoza wanajeshi hawa mpaka Tibet kuanzisha vuguvugi la kudai kujitenga na China.

Pia ni kikosi hiki maalumu cha idara ya SAD ambacho kilimtorosha kwa siri mtukufu Dalai Lama kwa kupita katikati ya majeshi ya China yaliyokuwa mpakani na kumpeleka India, Mpaka leo haijulikani ni namna gani waliweza kufanya tukio hili, kwakuwa tukio hili awajaliweka wazi mpaka sasa.

Ni kikosi hiki hiki cha SAD ambacho kiliusika na mauaji ya Che Guevara, hii ni kwa mujibu wa nyaraka za siri za CIA zikizowekwa wazi mwaka 2004, ambazo zinaonesha kuwa Amri ya kumpiga risasi Che Guevara miaka ya 1960 ilitoka kwa makomado wa SAD.

Ilikuwaje....

Ilikuwa hivi, Jeshi la msituni lililojiita Jeshi la Ukombozi la Bolivia (National Liberation Army of Bolivia) lilianzisha vita dhidi ya serikali ya Bolivia ambayo ilikuwa inaungwa mkono na Marekani, Jeshi hili likuwa na vifaa vya kisasa na liliungwa mkono na mwanamapinduzi Che Guevara, katika hatua za mwanzo za mapigano, jeshi hili la waasi lilionekana kushinda dhidi ya majeshi ya serikali, ndipo hapo CIA wakatuma makomando wa kitengo cha SAD ambao walienda kutoa mafunzo kwa majeshi ya Bolivia katika milima ya Camiri, Na baada ya hapo wakawaongoza kupigana na waasi na kufanikiwa kuwashinda, na kisha makomando wa SAD wakawaongoza makomando wa jeshi la Bolivia (Bolivia Special Forces) kumkamata Che Guevara ambapo Mara tu baada ya kukamatwa komando wa SAD aliyeitwa Felix Rodriguez akaamuru auwawe.

Hii ni mifano michache kati ya mifano mingi ambayo CIA kwa kutumia kitengo cha SAD wameendesha opesheni maalumu za kijeshi katika nchi nyingi duniani.

Ingawa Rais wa marekani ndiye anayetoa amri ya kufanyika kwa operesheni hizi za kuvamia kijeshi nchi nyingine au kuongoza mapinduzi ya serikali halali duniani kote lakini analindwa na sheria ya Marekani ambayo inampa Rais uwezo wa kukana uhusika wa Rais wa marekani kutoa amri au kufahamu kinachofanywa na kitengo hiki. (Plausible Deniability).

Sheria hii ilitingwa mwaka 1947 na inajulikana kama National Security Act, Pia Sheria hii ilitiliwa mkazo na tamko la rais namba 12333 (Executive Order 12333) lenye kichwa cha habari National Intelligence Activities.

Ni idara hii ya SAD ndani ya CIA ambayo ilihusika pia kuwapatia mafunzo ya kijeshi raia wa Cuba waliokuwa wanaishi uhamishoni na kuwaongoza katika jaribio la kumpindua Fidel Castro, Mapigano haya yakihistoria yalidumu kwa siku tatu na yanajulikana kwa jina maarufu la 'Bay Of Pigs Invasion'.

Jaribio hili la mapinduzi ndio lililo changia kudorara kwa mahusiano kati ya Marekani na Cuba mpaka leo hii, Lakini kutokana na umahili wa shirika hili na uhodari wao ndio maana maafisa wa CIA walimshaishi rais Kennedy kukubali mpango wa kuwatumia makomando hao kwenye uvamizi huo.

Mpaka hapa naamini sasa umeelewa vyema kuhusu hiki kitengo maalumu cha CIA cha Special Activities Division (SAD) namna kinavyofanya kazi, Sasa turejee kwenye simulizi yetu ya uvamizi wa Bay of Pigs.

Washington DC, tarehe 20, February 1961...

Maafisa CIA walipo mshauri Kennedy kuhusu uvamizi huo walimuomba sana kuidhinisha makomando wa SAD kutumika, hatimae Raisi Kennedy alikubali makomando wa SAD kuongoza wapiganaji wa Brigade 2506, lakini pamoja na hayo yote, Rais Kennedy alisisitiza sana kwamba ili kulinda taswira ya nchi ya Marekani yeye kama Rais hatoruhusu Marekani kufanya mashambulizi ya anga kusaidia katika mapambani hayo ya kumuondoa madarakani Fidel Castro, maafisa hao walikubali agizo hilo la Raisi Kennedy lakini walijua baadae wangemshawishi Raisi ili waweze kushinda vita ile.

Kwani CIA walijua fika kwamba hawawezi kushinda uvamizi huo pasipo mashambulizi ya anga wakakubaliana na sharti la Rais Kennedy kwamba hakutakuwa na mashambulizi ya anga, Walikubali hili huku wakiwa na dhamira iliyojificha kwamba mara tu vita hiyo itakapoanza watamshinikiza Rais Kennedy atoe ruhusa ya kufanyika mashambulizi ya anga, Walikuwa wanaamini kwamba lazima Rais Kennedy atakubaliana na shinikizo lao pindi atakapoonyeshwa umuhimu wa mashambulizi ya anga pindi vita ikiwa inaendelea, na lazima atafanya hivyo ili kuepusha Marekani kuaibika kushindwa vita wanayoiunga mkono ili kulinda heshima yao ya kijeshi ambayo ilikuwa inahitajika kuliko kitu chochote katika kipindi hiki cha vita baridi.

Rais Kennedy aliidhinisha rasmi uvamizi huu siku ya tarehe 4 April 1961, takribani miezi mitatu tu baada ya kuingia madarakani, Wapiganaji wapatao 1400 wa Brigade 2605 waliogawanywa katika infantry batalioni zipatazo tano na paratrooper battalion moja waliingia katika pwani ya Cuba iitwayo Playa Girón kwa kutumia boti kutokea Guatemala na Nicaragua siku ya tarehe 13 April 1961, Baada ya uvamizi tu kuanza CIA wakaanza kuweka shinikizo kwa rais Kennedy aruhusu japo shambulio moja la anga la ndege za kivita za Marekani kuharibu miundombinu ya viawanja vya ndege za kijeshi vya Cuba, Kennedy alikataa katakata lakini CIA walipozidisha shinikizo na kumpa angalizo kuwa wasipofanya hivyo kuna uwezekano wa wapiganaji hao kushindwa kutekeleza mapinduzi ya kumuondoa Fidel Castro, Kennedy alilazimika na kuruhusu mashambulio ya anga kwa awamu moja pekee.

Hivyo basi tarehe 15 April 1961 ndege za kijeshi zilizo chini ya CIA aina ya B-26, zenye marubani wavamizi walipewa ndege, ndege zile za kivita zilibadilishwa rangi na kufanana sana na zile za Jeshi la Cuba na pia zilipakwa matope ili zikiwa angani zionekane ni chakavu, kisha ziaenda kushambulia kambi ya anga za Cuba na kufanikiwa kuangamiza asilimia 80 ya ndege za Castro, Jeshi la Anga la Castro lilibakiwa na ndege sita tu na marubani saba, ndege hizo zilishambulia viwanja vya ndege za jeshi la Cuba na hatimaye tarehe 16 April wapiganaji wa Brigade 2506 walivamia rasmi Cuba, Mwanzoni mwa uvamizi huu wapiganaji wa Brigade 2506 wakiongozwa na makomando wa SAD katika CIA walionekana kulidhibiti jeshi la Cuba ambapo mwanzoni mwa mapambano haya upande wa Cuba vikosi vya kijeshi vilikuwa vinaongozwa na José Ramón Fernández.

Baada kuonekana kuwa jeshi la Cuba linazidiwa ujanja na wavamizi hawa waliokuja kufanya mapinduzi, Fidel Castro mwenyewe akaingia katika uwanja wa vita na kumuondoa José Fernández kwenye jukumu la kuongoza jeshi kwenye mapambano haya na kujipa yeye binafsi hilo jukimu la kuongoza wanajeshi, Castro alipo ingia front kuongoza mapambano alitumia mbinu ya falsafa ya mapigamo ya José Mart iitwayo "Siri, Vamia, shambulia, gawanya na miliki", mbinu hii ililifanya jeshi la Cuba kuanza kupata mafanikio.

Baada ya Castro kushikilia usukani wa kuongoza mapambano kwa upande wa jeshi la Cuba, wavamizi wa Brigade 2506 wakiongozwa na makomando wa Marekani walizidiwa ujanja na mbinu zote na wakaanza kupigwa kwa aibu kubwa, mpaka kufika tarehe 19 April, ilikuwa dhahiri kwamba ushindi uko upande wa vikosi vya Cuba, kwani walikuwa wanawapiga wavamizi kwa urahisi kana kwamba wanamsukuma mlevi, Ndipo hapa ambapo CIA wakarudi tena kwa rais Kennedy kutaka aidhinishe mashambulizi mengine ya anga, Safari hii Kennedy alikataa katakata, akidai kuwa dunia nzima itaona uvamizi huu imefanywa na Marekani na sio raia wa Cuba wanaoishi uhamishoni.

Kennedy alihofia kuwa kama Marekani itaingilia mapigano hayo kwa kiwango hicho, kulikuwa na uwezekano wa Urusi nayo kuingilia vita hiyo kusaidia upande wa Cuba, kutokana na mvutano mkubwa uliokuwepo baina yao, Kennedy alihofia kuwa ingeweza kuchochea vita nyingine kati ya Marekani na Urusi, vita ambayo ingeigharimu pande zote mbili na Dunia nzima kwa ujumla na pengine hata kusababisha vita kuu ya Tatu ya Dunia, kwa hiyo Kennedy safari hii akakataa katakata kuidhinisha mashambulio ya anga kwa kutumia jeshi la Marekani.

Joint Chiefs Of Staffs wakaja na pendekezo kwamba litengenezwe shambulio la uongo kwenye pwani ya Marekani na kisha kutupa lawama kwa Cuba ili kuhalalisha mashambulizi ya anga nchini Cuba, lakini bado pia Kennedy alishikilia msimamo wake kwamba hawezi kuidhinisha shambulio lolote la anga kufanywa na jeshi la Marekani, Hapa ndipo ambapo CIA iliumbuka, mkakati wao tangu awali ulikuwa ni lazima mashambulizi ya anga yafanyike ili kuweza kushinda mapigano na kuvishinda vikosi vya Castro na kumuondoa Madarakani, Lakini walimficha kitu hiki Rais Kennedy baada ya kumuona kuwa hasingeli idhinisha uvamizi huo kama wangemuweka wazi kuwa hawawezi kushinda pasipo mashambulio ya anga, hivyo kumficha huko na tegemeo lao la kumshawishi tena kwa mara ya pili yafanyike mashambulio ya anga ndio likawa limegonga mwamba.

Cuba ikaibuka mshindi....................

Tarehe 20 April 1961, siku tatu baada ya uvamizi, wapiganaji waliio patiwa mafunzo na kuongozwa na makomando wa Marekani, ambao waliiovamia nchini Cuba ili kumpindua Fidel Castro waliweka silaha chini na kusarenda kwa vikosi vya jeshi la Cuba, Ilikuwa ni aibu kubwa ambayo haijawahi kutokea katika historia ya jeshi la Marekani, Mateka waliokamatwa na vikosi vya Fidel Castro walihojiwa mubashara kwenye televisheni nchini Cuba na kutoa siri zote namna ambavyo Marekani ilihuiska katika uvamizi huo ambapo Marekani walikuwa wanatafuta sehemu ya kuficha nyuso zao kwa aibu, nchini Cuba taifa zima lilikuwa linasheherekea kwa shamra shamra kushangilia ushindi huo mnono, Fidel Castro aligeuka kuwa shujaa mpya wa Taifa na kujipatia heshima kubwa kimataifa kwa kushinda vita dhidi ya jeshi hatari la 'Marekani' hivyo Fidel Castro akapewa cheo cha juu jeshini cha Fidel Marshall kwa kuyashinda majeshi ya Marekani.

Huko Marekani nako...

Bado bundi alikuwa ndio kwanza ametua, Kila upande ulikuwa unamsukumia lawama upande mwingine, CIA walimuona Rais Kennedy kama ndio kisababishi cha wao kushindwa kutekeleza kwa ufanisi uvamizi na hatimaye kufanikisha kumuondoa madarakani Fidel Castro, CIA walijuta Raisi Eisenhower kutokamilisha mpango huo wa uvamizi kabla ya kuondoka ikulu.

Na kwa upande wa Rais Kennedy aliwaona CIA kama wasaliti kwa 'kumdanganya' na kutompa mkakati kamili tangu mwanzoni kwamba wasingelieweza kushinda vita ile pasipo mashambulizi ya anga, CIA wakamuona Rais Kennedy kama kiongozi ambaye si imara na shupavu au jasiri, na kwa muono wao walihisi kuwa hatoshi kuwa Rais wa Marekani.

Kwa upande wake Kennedy aliwaona CIA kama taasisi iliyopewa nguvu kiasi kwamba imelewa madaraka na kujiona wako huu ya kila kitu na kila mtu. Na moyoni mwake aliamini kuwa hilo linatakiwa kubadilika, Ikumbukwe pia kwamba hapa ilikuwa imepita miezi mitatu pekee tangu CIA wamuue Patrice Lumumba siku ya Tarehe 17 January, 1961 jimboni Katanga, Congo-Kinshasa, Kennedy anafahamika kuwa hakupendezwa na hili tukio lakini kwa kuwa lilitokea kabla hajawa Rais (siku tatu kabla) basi alilimezea mate lakini bado alibaki na kinyongo Kwa hiyo kufeli kwa uvamizi wa Bay of Pigs kuliamsha hasira zake zote alizonazo dhidi ya CIA.

Japokuwa katika umma na hata alipoongea na wanahabari Kennedy alikubali kubeba lawama zote kwa kuwa yeye ndiye aliidhinisha uvamizi huo, lakini pembeni akiwa faragha na wakubwa wenzake alikuwa anaotupia lawama kubwa CIA kuwa ndio waliosbabisha aibu kubwa hii iliyoipata Marekani na jeshi lake, Baada ya hapa mwenendo wa Kennedy ukaanza kubadilika mno. Mwanzoni alipoingia madarakani alikuwa ni tegemezi mno kwa kupatiwa muhtasri wa hali ya usalama wa nchi (Daily Presidential Briefing) kutoka kwa vyombo vya Ujasusi hasa CIA, lakini baada ya tukio la kufeli kwa uvamizi wa Cuba hakutaka tena kupatiwa briefing na CIA badala yake briefings zake zote sasa alizipokea kutoka kwa washauri wa usalama wa taifa (National Security Advisors).

Lakini hakuishia hapo tu, Kennedy kuonesha ni namna gani alikasirishwa alienda mbali zaidi kufanya kitendo ambacho kilipingwa na maafisa wengi wa CIA na wanazi wao, Kennedy alimfuta kazi Mkurugenzi Mkuu wa CIA Bw. Allen Dulles, Katika ulimwengu wa Intelijensia unapomuongelea Allen Dulles hamuongelei tu jasusi, bali ni jasusi mkongwe na mzoefu na wa kiwango cha daraja la kwanza kabisa na mwenye heshima iliyotukuka, Allen Dulles ndiye Mkurugenzi wa CIA aliyetumikia kwa kipindi kirefu zaidi katika historia ya Taasisi hiyo mpaka leo hii (tangu 1953 mpaka 1961), Allen Dulles ndiye aliyesimami mapinduzi ya Waziri mkuu wa Iran miaka ya 1940s (Operation Ajax), Allen Dulles ndiye aliyesimamia mapinduzi ya Rais wa Guatemala mika 1950s, Allen Dulles ndiye aliyesimamia program ya ndege za kijeshi ya Lockheed U-2, Pia huyu ndie aliye simama operation Barracuda iliyo ratibu kifo cha Patrice Lumumba wa Kongo DRC.

Allen Dulles ni kaka wa John Dulles, waziri wa mambo ya nje wa Marekani (Secretary of State) wakati wa utawala wa Rais Dwight Eisenhower ambaye ndiye amerithiwa na Kennedy miezi mitatu iliyopita, kwa hiyo inahitaji kujitoa ufahamu kumgusa mtu kama Allen Dulles. Na Kennedy alijitoa ufahamu na kumfuta kazi Allen Dulles mtu ambaye anapendwa na kuhusudiwa na majasusi wa CIA pengine kushinda hata Kennedy mwenyewe, Karatasi ya juu ya ripoti rasmi ya CIA ambayo ndani yake kuna baadhi ya paragraph zikionyesha kuwa CIA hawakuridhishwa na namna ambavyo Kennedy alifanya maamuzi juu ya kukataa mashambulio ya anga.

Wengine huenda mbali zaidi na kusema kwamba uvamizi wa Bay of Pigs ndivyo iliyochangia kifo cha Kennedy, kutokana na madhira ya vita vyenyewe na athari ya vita kwa CIA kuipoke kwa mtazamo kuwa John F. Kennedy kama chanzo ya Marekani kushindwa vita hiyo, japo hakuna ushahidi ulio wekwa wazi kuhusu hili.

Sababu ya Cuba kushinda na Marekani kushindwa uvamizi wa Bay of Pigs...

Kuna sababu nyingi zinazotolewa juu ya ushindi huo kwa Cuba. Mosi, ni taarifa za kiintelijensia kuwafikia mapema kupitia vyanzo vyao vya ndani ya Marekani, Baadhi ya duru hubainisha kuwa vyombo vya habari nchini Marekani hasa magazeti vilikuwa vikiripoti juu ya operesheni hiyo ya mafunzo ya siri, jambo lililosababisha Havana kupata taarifa mapema na kujiandaa vilivyo, sambamba na kupenyeza mashushu watiifu wa Castro ambao walijifanya waasi wakati upande wa pili walitii serikali ya Havana na kupeleka taarifa zote kwa Castro kupitia mashushushu wa mtaani, hii ni kwamba askali hao watiifu walipokuwa kambini walitoa taarifa zote zinazoendelea kwa raia wa Cuba ambao walilikuwa wafanya biashara ambako askali hao walikuwa wakienda kupumzika baada ya mafunzo.

Pili, inadaiwa kuwa kikosi hicho kujikanganya kwenye eneo mahsusi la kuingilia kisiwani, na kujikuta wakitia nanga Playa Giron au Bay of Pigs kimakosa, mkakati wa awali ulikuwa ni kuwa ni kikosi hicho kutia Nanga eneo la Bay of Pigs upande kusini mashariki, yani kilomita 1.7 upande wa chini ambao gridi reference yake ni 27ES na 57NE, eneo ambalo kulikuwa na miinuko ya miamba ambayo ingewapa urahisi wa kutoonekana kwa urahisi kwa askali wa Cuba, kinyume chake walijikanganya na kutia nanga eneo la kusini ambalo lipo wazi hivyo ilikuwa rahisi kushambuliwa kwa uwepesi.

Tatu, na mwisho, ni kwamba hali mbaya ya hewa na uwazi kimwonekano wa eneo la Bay Of Pigs walilotia nanga, Inadaiwa kwamba ilikuwa rahisi kwa makamanda wa Cuba kuwamaliza wavamizi sababu ya eneo hilo kuwa wazi na rahisi zaidi kwenye shabaha kutokea mafichoni.

Serikali ya Marekani haikukubaliana na matokeo ya kushimdwa vita ile hivyo Raisi Kennedy akataka uchunguzi ufanyike ili kubaini sababu za Marekani kushindwa vita ile, hivyo akaitaka ofisi wa utafiti chini ya Maxwell kuendesha uchunguzi ili kubaini hasa kwanini Marekani imeshindwa vita hiyo ya uvamizi wa Bay of Pigs.

Tume ya Maxwell Taylor Commission...

Mnamo tarehe 22 Aprili mwaka 1961, Rais Jonh F. Kennedy aliunda tume na kumteua Jenerali Maxwell D. Taylor, pamoja na Mwanasheria Mkuu Robert F. Kennedy, Admiral Arleigh Burke na Mkurugenzi wa CIA Allen Dulles, tume hii ilijulikana kama Maxwell Taylor commission, tume hii iliundwa ili kutafiti sababu za Marekani kushindwa vita ile ya Cuba, baada ya tume hiyo kufanya shuguri zote za kiuchunguzi, Jenerali Taylor aliwasilisha ripoti ya tume yake ya Uchunguzi kwa Rais Kennedy mnamo tarehe 13 Juni mwaka 1961, tume hiyo ilielezea sababu za Marekani kushindwa vita ile ni kwa ukosefu wa taarifa za uhakika na za mapema kwa raisi, pia tume ilielez kuwa sababu nyingine ni operation hiyo kuendeshwa kwa njia za siri, kitu ambacho vyombo vingine vilishindwa kushirikishwa ili kutoa ushauri wa kitaalam, tume hiyo pia iliiulaumu utawala wa Kennedy kwa kushindwa kuidhinisha mashambulizi ya ndege kwa wakati, pia tume iliuulaumu uongozi wa CIA kwa kutumia ndege zisizofaa, mambo mengine ambayo tume ilieleza ni pamoja na mapungufu ya silaha, marubani ambao awakuwa na uzoefu wa kutosha na eneo la Bay of Pigs na Cuba kwa ujumla.

Pia tume ilieleza suala la mashambulizi ya angani kutokutekelezwa ipasavyo, utawala wa Kennedy kitofuata mkakati uliowekwa na mtangulizi wake.

Ripoti ya tume hiyo ilikuwa na kurasa 201, hata hivyo baada ya ripoti hiyo kutolewa na kuwekwa hadharani ilikutana na ukosolewaji mkubwa, tume hiyo ilionekana kuwa na upendeleo ulioegemea kumshambulia raisi Kennedy pamoja na Mwanasheria Mkuu Robert F. Kennedy ndugu yake Rais Kennedy.

Mika 20 baada ya riporti hiyo ya Maxwell Taylor commission, Jack Pfeiffer, ambaye alifanya kazi kama mwanahistoria wa CIA hadi katikati ya miaka ya 1980, alitoa taarifa juu ya Marekani kushindwa mapigano ya Bay of Pigs kwa kunukuu taarifa ambayo Raúl Castro, kaka wa Fidel, alikuwa ametoa kwa mwandishi wa habari wa Mexico mnamo 1975, ambayo inasema kuwa ushindi wa vita ile kwa Cuba ulitokana na hofu ya Raisi Kennedy Juu ya Urusi na uchanga wake Juu ya maswala nyeti ya nchi, Raul Castro alikili wazi kuwa kama vita ile ingefanywa na mtangulizi wa Kennedy Raisi Dwight Eisenhower ingeifanya vita ile kuwa ngumu.

Ripoti ya Siri ya CIA...

Mnamo Novemba 1961, Mkaguzi Mkuu wa CIA Lyman B Kirkpatrick aliandika ripoti juu ya Utafiti wa Operesheni ya Cuba ripoti ambayo ilibaki kuwa siri (classified) hadi mwaka 1998, miaka 37 baadae ndipo ilipo wekwa hadharani kwa umma yani disclassified, ripoti hiyo ya CIA ilionesha mambo kadhaa yaliyopelekea Marekani kushindwa vita ile ambayo ni pamoja na;

Mosi, Marekani Kushindwa kutathmini kiuhalisia hatari na kuwasiliana vya kutosha na viongozi pamoja kukosekana kwa habari sahihi juu ya operation hiyo mezani kwa Raisi Kennedy na pia upatikanaji hafifu wa maamuzi ya ndani ya CIA na wakuu wengine wa serikali.

Pili, kukosekana kwa ushiriki wa kutosha wa viongozi wa serikali ya Kennedy na askali wa brigade 2506 katika uhamishwaji.

Tatu, CIA kushindwa kuandaa mpango huu vizuri ili kuwahusisha pia upinzani wa ndani ya Cuba, ambao wangesaidia sana kuhujumu serikali ya Castro kipindi ambacho vile ikiendelea.

Nne, CIA kushindwa kukusanya taarifa kwa ufanisi na kuzichambua taarifa hizo za kijasusi kuhusu vikosi vya jeshi la Cuba.

Tano, Ukosefu wa sera thabiti au mipango ya dharura kutoka ndani ya serikali juu ya operation hiyo.

Matokeo ya Marekani kushindwa vita ile ilipelekea mgogoro mkubwa kwa viongozi wa Juu wa CIA na serikali kuu hasa kuanzia Mkurugenzi wa CIA Allen Dulles, Naibu Mkurugenzi wa CIA Charles Cabell, na Naibu Mkurugenzi wa Mipango Richard Bissell wote walilazimishwa kujiuzulu mapema mwaka wa 1962.

Baada ya vita ile uhasama baina ya Cuba na Marekani uliongezeke na Marekani ilihaidi kulipiza kisasi kufatia aibu iliyopata mwaka 1961 katika vita ile ya Bay of Pigs, kufatia hatua hiyo ya kuzorota kwa diplomasia ya mataifa hayo ilipelekea kuongezeka kwa msuguano wa vita baridi, hasa mvutano baina ya Urusi na Marekani, mivutano hii ilipelekea viongozi wa Juu wa nchi hizo kuwekeana vitisho na Urusi kuionya Marekani kuacha kuthubutu kuivamia Cuba.

Jambo hili nimelielezea huko nyuma, nilisema mara zote Marekani ilihofu kuchochea mgogoro wowote na Cuba kwa kuhofia kuibuka kwa vita baina ya Marekani na Urusi, lakini baada ya Marekani kushindwa vita ile ya Bay of Pigs ilipelekea Marekani kujitafakari upya dhidi ya usalama wake dhidi ya Cuba na hasa hasa Urusi yenyewe ambayo ndio ilikuwa kiranja mkuu wa ujamaa duniani.

Basi bwana...

Marekani ikaanza kujiimarisha na kujiimarisha katika muungano wao wa NATO, hii NATO ni muungano wa mataifa ya kibepari kujihami dhidi ya mataifa ya kijamaa, hivyo Marekani na NATO wakaanza kujiandaa ili kuidhibiti Urusi, maana walijua wakidhibiti Urusi watakuwa wameidhibiti Cuba, baada ya Urusi nao kujua hilo nao wakanza kujizatiti ili kuidhibiti Marekani, ndio Urusi wakaunda umoja wao wa Warsaw Pact.

Kufatia hilo muungano huo wa mashariki kwa kipindi hicho ulioitwa Warsaw Pact ulianza kikao chake cha dharula mwezi February mwaka 1962 na ilipofika mwezi April mwaka 1962 walifikia uamuzi wa kuingia katika vita kamili ya kujihami dhidi ya umoja wa kujihami wa nchi za magharibi NATO

Jumla ya askari 400,000 kutoka nchi mbali mbali za umoja wa kujihami wa nchi za mashariki walianza kusogea mipakani mwa nchi zao kujiandaa na vita dhidi ya umoja wa kujihami wa nchi za magharibi NATO
Ilipofika August mwaka 1962 meli za kivita za Urusi zikiwa zimebeba askari zaidi ya 100,000 pamoja nyambizi zilizobeba silaha kali za nyuklia zilitia nanga kisiwani Cuba

Dunia yataharuki...

Mwezi September mwaka huo wa 1962 Rais wa Urusi wa wakati huo Nikita Khruschev aliwahakikishia nchi washirika wake wa mashariki kuwa endapo askari hata mmoja wa NATO angevuka mpaka na kuingia katika nchi zao basi nae angejibu mapigo kwa kuangamiza sehemu kubwa ya nchi ya Marekani hususani majiji ya New York na Miami, Kwani tayari nae alikuwa ameshaweka silaha kali za nyuklia mkabala na nchi ya Marekani, Inaonekana kabisa kuwa silaha hizo zilipelekwa kwa siri katika nchi ya Cuba.

Tamko hilo la Rais Nikita Khruschev lilizua hali ya taharuki ndani ya nchi ya Marekani, Haraka sana idara ya ujasusi ya nchi hiyo CIA ilifanya upelelezi wa haraka na kugundua kuwa ni kweli kabisa silaha za nyuklia zenye uwezo wa kuangamiza taifa la Marekani zilikuwepo katika kisiwa cha Cuba mkabala na nchi ya Marekani

Vita kamili...

Tarehe 12 October 1962 bunge la Marekani lilikutana na kwa pamoja lilipitisha azimio la kuivamia nchi ya Cuba kwa haraka sana, Rais John F Kennedy Sasa alikuwa kwenye shinikizo kubwa sana la kutangaza vita ambayo kwa hakika ingekuwa ndio vita kuu ya Tatu ya Dunia, Akilihutubia taifa la Marekani usiku wa tarehe 16 October Rais Kennedy alisema kuwa kamwe taifa la Marekani halitoweza kuvumilia kitendo hicho cha kutishiwa usalama wake na akasema kuwa jeshi la Marekani litakwenda nchini Cuba kuziondoa silaha hizo kwa nguvu kwa sababu njia zote za amani zilikuwa zimeshindikana

Tayari jumla ya askari wapatao 300,000 pamoja na meli za kivita pamoja na ndege za kivita ziliwasili katika jiji la Miami kujiandaa kuivamia nchi ya Cuba, Meli kubwa kabisa za kivita za Marekani zilisogea karibu kabisa na kisiwa cha Cuba tayari kuanza mashambulizi ya kukiteka kisiwa hicho, Majeshi ya Cuba na Urusi nayo yalijibu mapigo kwa kusogeza vikosi vyake katika fukwe za kisiwa hicho mkabala na Majeshi ya Marekani

Uwanja wa mapambano...

Meli za kivita za Urusi zikiwa zimebeba silaha kali kabisa za nyuklia zikiwa Sasa zinakabiliana ana kwa ana na meli za kivita za Marekani, Tarehe 27 October 1962 ni siku ya kukumbukwa sana Duniani, Siku hiyo wizara ya ulinzi ya Marekani ilitoa amri kwa ndege zake za upelelezi za kivita kuingia katika anga ya Cuba, ndege hizo zilikuwa na kazi ya kuangalia Majeshi ya adui yamejipanga vip ili kuweza kukabiliana nayo, Ndege hizo ziliweza kuonekana na rada za Majeshi ya Urusi na mara moja walianza kuzishambulia.

Majeshi hayo ya Urusi yalifanikiwa kuangusha ndege moja ya upelelezi ya jeshi la Marekani jioni ya siku hiyo ya tarehe 27 October 1962 na kusababisha kifo cha askari wa jeshi la anga la Marekani luteni Rudolph Anderson, Kifo cha rubani mdogo mwenye umri wa miaka 34 Luteni Rudolph Anderson kilimsikitisha sana Rais John F Kennedy, Asubuhi ya tarehe 28 October 1962 Rais Kennedy alikwenda hadi nyumbani kwa familia ya marehemu kutoa salamu za rambi rambi.

Katika Hali ya kuhuzunisha sana Rais John F Kennedy alianza kulia baada ya kumuona mke wa marehemu akiwa mjamzito na pia aliwaona watoto wadogo wa marehemu mmoja akiwa na miaka 5 na mwingine akiwa na miaka 3, taarifa za kuangushwa kwa ndege ya kivita ya Marekani zilienea kwa kasi sana Duniani na Kila mtu alijua tayari Sasa Vita imeanza, Jeshi la Uingereza usiku wa siku hiyo lilituma kikosi maalum cha makomandoo kwenye mstari wa mbele wa kivita huko mashariki ya ulaya

Vasil Arkshipov aiokoa dunia...

Usiku wa siku iyo ya tarehe 27 October 1962 nyambizi ya kivita ya Urusi B-59 ikiwa imebeba silaha kali za nyuklia ikiwa chini kabisa ya bahari pasipo kuonekana na rada za Majeshi ya Marekani ilisogea karibu kabisa na pwani ya Florida ili kuanza mashambulizi endapo jeshi la Marekani lingeanzisha vita.

Nyambizi hiyo iliongozwa na Captain Savitsky pamoja na Admiral Vassil Arkhipov iliingia usiku huo karibu na Florida, Ikiwa chini kabisa ya bahari walianza kuhisi kufuatiliwa na nyambizi za jeshi la Marekani.

Wasilokuwa wakilijua askari Hawa wa Urusi ni Kwamba nyambizi hizi za jeshi la Marekani zilikuwa katika doria yake ya kawaida na wala haikuwa ikiifuatilia nyambizi hiyo ya Urusi, Kwa kuwa walikuwa chini kabisa ya bahari hawakuwa na mawasiliano yoyote na wenzao, Kulinganisha na hali waliyokuwa wameiacha Cuba Nahodha wa nyambizi hiyo Captain Savitsky alijua kabisa kuwa Sasa Vita imeshaanza na kwa maagizo waliokuwa wamepewa ni kusubiria vita ianze na kushambulia pwani za Florida kwa makombora ya nyuklia.

Haraka sana Captain Savitsky alitoa amri ya kufyatua makombora ya nyuklia kwa nyambizi za Marekani na pia kwenye fukwe za Florida zilipokuwa kambi za kijeshi na kituo cha kijeshi cha Marekani kwa wakati huo, Ili kutekeleza amri hiyo ilihitajika idhini ya Admiral Vassil Arkhipov.

Vassil alikataa kata kata kuachia makombora ya nyuklia kwa nyambizi za Marekani akisema kuwa swala zito kama hilo linahitaji amri na idhini kutoka Moscow na sio kwa yoyote yule, Askari wote wa kwenye nyambizi hiyo walikuwa wakipingana na Vassil mabishano ndani ya nyambizi hiyo yaliwachukua saa nzima na hatimaye wote wakakubali amri ya Admiral Vassil Arkhipov ya kutokupiga makombora ya nyuklia na haswa baada ya kuona nyambizi za Marekani zikiondoka bila ya kufanya shambulizi lolote kwao.

Hakika kilikuwa kitendo cha ujasiri sana kwa Vassil kuwashawishi wenzake wasishambulie nyambizi za Marekani maana endapo nyambizi zile za Marekani zingewaona na kuanza kuwashambulia wao basi ni dhahiri kuwa nyambizi hiyo ya B-59 ya Urusi ingeteketea na wote waliokuwamo ndani yake wangeuawa

Nyambizi hiyo ya B-59 iliondoka haraka sana eneo hilo na kurudi ilipokuwa ngome yao katika pwani za kisiwa cha Cuba usiku huo huo wa tarehe 27 October 1962 na vita ikawa imesimama, toka hapo Urusi na Marekani wakaanza mazungumzo ya Amani ya kuiepusha dunia kuingia kwenye uwezekano wa kutoka vita.

Copyright 2021, All Rights Reserved.

Maktaba Kuu.
Screenshot_20210616-162535.jpg
Screenshot_20210616-162358.jpg
A4D-2_Skyhawks_of_VA-34_in_flight_over_USS_Essex_(CVS-9)_during_the_Bay_of_Pigs_Invasion_in_Ap...jpg
FB_IMG_1623844919687.jpg
 
Back
Top Bottom