Darasa: Maadhimisho ya leo ni ya Uhuru wa Tanzania ila kumbukumbu ndio ya Uhuru wa Tanganyika!

Happy Birth day Tanzania, 60 yrs.
Tumepiga hatua kubwa sana ktk nyanja zote;

1. Elimu=Elimu bure kuanzia primary hadi kidato cha 4, hivyo sasa watoto wengi wa kitanzania wanapata elimu bila kikwazo. Mikopo kwa elimu ya juu inatolewa na serikali bila matatizo hivyo watoto wengi wa kitanzania wanapata elimu ya juu bila kikwazo. Vyumba vya madarasa vimejengwa/vinajengwa ili kukidhi ongezeko la watoto wanao jiunga.

2 Afya= zahanati za kisasa zimejengwa kila kona ya nchi, pamoja na vifaa vya kisasa.

3. Uchumi= tupo ktk uchumi wa kati.

4. Miundo mbinu tuko safi sana.

n.k n.k

Tanzania oyeeee
Utopolo tupu
 
Kwahiyo shida ni jina tu?

Tanganyika na Tanzania?

Tunamaanisha Uhuru wa nchi, naamini tungekuwa na serikali moja tungeadhimisha siku ya leo.

Hatuna Tanganyika kwa sasa, huwezi kusema uhuru wa Tanganyika it's no sense...

Anyway kuelewa inahitaji uwe great thinker.
ushahindi wa kisheria au kikatiba au mikataba wa kuifuta Tanganyika.
Kwa taarifa waziri wa TAMISEMI wa tanganyika mwisho Chumbe.
 
Tnapendaga sana kulazimisha UJINGA kwa vitu very simple yani

Hivi leo tukisimama kwenye FACT na kutambua leo ni siku ya uhuru wa TANGANYIKA tutaharibu au kupungukiwa na nini?

Iwe kama ilivyo sahihi kwa Zanzibar kutambua siku ya MAPINDUZI

Sherehe yetu ya Muungano ndio ibaki kama sherehe ya kutambua kuzaliwa kwa TANZANIA

Kwa kumbu kumbu nzuri zaidi ya viza vijavyo ni vyema zaidi tuka ainisha haya mambo vizuri na kwa ufasaha wake kuliko kulazimisha KUUA kabisa utambulisho wa TANGANYIKA kwenye historia ya kusherehekea uhuru

Mifano ya Pasco ni ya kitoto sana na haiwezi kurandana na swala hili abadani

Hakuna nchi inayoitwa Tanzania iliopata uhuru that day
Leo ni siku ya UHURU WA TANGANYIKA........ Periode
 
Hichi ulichoandika kimejaa upotoshaji mkubwa. Kuweka kumbukumbu sawa hapa JF.

1. Tanzania ni taifa lililoundwa mwaka 1964, umri wa taifa hili mpaka sasa ni miaka 57. Hivyo haliwezi kusherekea tukio la miaka 60 iliyopita likiwa kama taifa.

2. Tanzania haikuwahi kuwa koloni la taifa lolote, hivyo haiwezi kusheherekea kumbukumbu ya uhuru wake.

3. Tanzania ni muungano wa mataifa mawili tofauti (Tanganyika na Zanzibar) yenye historia tofauti sana za kupata uhuru wake. Tanganyika ilipata Uhuru wake kutokea kwa muingereza mwaka 1961 na Zanzibar ilipata 'uhuru' wake kwa njia ya mapinduzi kutoka kwa utawala wa sultan kutoka Oman mwaka 1964. Huwezi kuziweka pamoja hizo nchi mbili kihistoria unapozungumzia suala la kupata Uhuru.

4. Nchi ya Tanganyika ndio ilipata Uhuru wake tarehe 9 ya mwezi Desemba, 1961, na ndio ingepaswa kusheherekea kumbukumbu ya miaka 60 ya uhuru wake leo.
Zanzibar ilipata uhuru wake December 1963 kutoka kwa mwingereza. Uhuru ulikabidhiwa kwa Sultan wa Zanzibar aliyewakilisha Monarch ya Oman Sultanate.
Mapinduzi ya Zanzibar ya April 1964 ni Matokeo tu ya janja janja iliyofanyika kati ya viongozi wa Tanganyika na Zanzibar.
 
Ndio maana kuna swali nilijiuliza, hivi hii siku yetu ya uhuru na Zanzibar inasherehekewa? na kule kwao ni mapumziko kama huku bara? kama na Zanzibar wanasherehekea, vipi yale mapinduzi yao "matukufu" wanayaweka kwenye nafasi ipi?

Au ndio maana nasi huwa tunasherekea siku ya mapinduzi ya Zanzibar? kwamba tuko ndugu moja, lako langu... langu lako? anyway, hata kama ndio hivyo, sioni kosa kwanini hii siku ya uhuru isiitwe siku ya uhuru wa Tanganyika, sio Tanzania, naona iitwe hivyo hata kama itasherehekewa pande zote mbili.

Kumbe huwa kuna kosa la kiufundi linarudiwa kila mwaka kwenye maadhimisho ya hii siku, ni vyema sasa wahusika waamke.
Zanzibar ni kwa heri ukoloni ,kwa heri uhuru.Uhuru wa Zanzibar ungeadhimishwa kesho yaan 10/12/2021,Ila kwakuwa uhuru huo ulipinduliwa ndo maana hata hiyo tarehe tu haitajwi.Waliopindua wanalinda uhalali wa udhalimu walioufanya kwa sababu wazijuao wao.
 
Wanabodi
leo tunapo sherehekea maadhimisho ya miaka 60 ya uhuru, ni maadhimisho ya Tanzania, japo iliyopata uhuru ile Desemba 9, ni Tanganyika na sio Tanzania, maadhimisho ya leo ni maadhimisho ya Tanzania, yaani Tanzanian National Day, na sio Tanganyika. Kumbukumbu ndio ya Uhuru wa Tanganyika lakini maadhimisho na sherehe ni ya uhuru wa Tanzania!.

Kufuatia baadhi ya watu kuwa kwenye sintofahamu ni maadhimisho ya miaka 60 ya uhuru wa Tanganyika ama Tanzania?.

Hivyo nimejitolea kutoa somo hili ambalo naamini litakuwa ni very benefisho kwako.


Wajameni ni katika kukumbushana tuu kuwa maadhimisho ya leo ni ya Uhuru wa Tanzania, na sio wa Tanganyika!.
Nawatakia sikukuu njema ya Uhuru na Jamhuri.
Paskali
Tanzania ilipata uhuru lini
 
Katiba iliyoipa Zanzibar uhuru 10/12/1963 ilijadiliwa na serikali ya mseto wa ZNP na ZPPP kwa upande mmoja na serikali ya Uingereza kwa upande mwingine.Vyama vyote pamoja na ASP vikimtambua sultan kama mkuu wa nchi na ndo maana vilisajiriwa na kufanya siasa.ASP walipopata support ya jamaa fulani wa kashirikiana na wahuni wakaipindua serikali halali.Katiba ikafutwa na Karume akatoa amri hakuna Uchaguzi Zanzibar hadi 2030.
 
Ni Uhuru wa Tanganyika.

Tanzania ni pamoja na Zanzibar ambao wao wanasherehekea 12 January.

Tanzania haijawahi kupata Uhuru bali ilipata katiba yake mwaka 1977
Hizo sherehe zote ni Feki,hata hiyo ya Zanzibar siyo ya kusherehekea uhuru wa Zanzibar,tarehe 12/1/1964,ni siku mbaya kabisa kwa taifa la Zanzibar,ni siku ya uvamizi na iliyochafua kabisa taifa huru la Zanzibar.
 
Watu ukweli wanaujua, Ila kwa vile hatuko HURU ndiyo maana tunaogopa kusema ukweli. Leo Ni Uhuru wa Tanganyika. Kuna siku tutasherehekea UHURU wa Tanganyika. Huu ipuuzi wa leo ni mauzauza ya wanasiasa. KUNA SIKU UKWELI UTASIMAMA NA TANGANYIKA ITASHEREHEKEA UHURU WAKE
 
Wanabodi
leo tunapo sherehekea maadhimisho ya miaka 60 ya uhuru, ni maadhimisho ya Tanzania, japo iliyopata uhuru ile Desemba 9, ni Tanganyika na sio Tanzania, maadhimisho ya leo ni maadhimisho ya Tanzania, yaani Tanzanian National Day, na sio Tanganyika. Kumbukumbu ndio ya Uhuru wa Tanganyika lakini maadhimisho na sherehe ni ya uhuru wa Tanzania!.

Kufuatia baadhi ya watu kuwa kwenye sintofahamu ni maadhimisho ya miaka 60 ya uhuru wa Tanganyika ama Tanzania?.

Hivyo nimejitolea kutoa somo hili ambalo naamini litakuwa ni very benefisho kwako.


Wajameni ni katika kukumbushana tuu kuwa maadhimisho ya leo ni ya Uhuru wa Tanzania, na sio wa Tanganyika!.
Nawatakia sikukuu njema ya Uhuru na Jamhuri.
Paskali
Hujui kitu chochote ina wezekana wew ni kima
 
Mdogo wangu Paschal nimeona unaungana na hoja ya Uhuru wa Tanzania SIYO Tanganyika. Naomba utusaidie kujua mambo yafutayo;

1. 9/12/1961 kulikuwepo na Tanzania?

2. Je Tanganyika au Tanzania Bara imewahi kubadili jina ikajiita Tanzania? If yes,lini na kwa hati gani?

3. Tukisema Uhuru wa Tanzania tunamaanisha hata Zanzibar walipata Uhuru wao 9/12/1961?

4. Kama Zanzibar inatarehe yake yakupata Uhuru ambayo naamini ni siku ya Mapinduzi, tunasemaje Tanzania ilipata Uhuru mwaka 1961 tukijua kilichopata Uhuru ni sehemu tu ya Tanzania ambayo ni Tanganyika?

5. Kwa uelewa wako Mapinduzi ya Zanzibar yanaweza kutambua kama siku ya Uhuru ya Zanzibar?

6. Hoja Yako ya kusherekea ya Sasa ( present) umeitoa kwenye nyaraka gani?

Nauliza haya baada ya kuona mada zako zote zimeacha lakuna kwenye maeneo hayo: Nikutakie siku njema ya Uhuru wa Watanganyika
Beatrice umeeleweka, sijui ni kwa nini watu tena wasomi wabobezi wanatumia nguvu nyingi, ulaghai na hila lukuki kutaka kuipoteza Tanganyika kwenye uso wa dunia wakati ilijipata uhuru wake tar 09 Disemba 1961. Kwani iliwakosea nini Tanganyika yetu!
 
Kitu najifunza hadi sasa ni kuwa tumepoteza historia yetu kwa ujinga wetu wenyewe, leo mzee wangu Mayalla anasema ni uhuru wa Tanzania taifa ambalo halijawahi kuwa koloni la mtu.

Ni kama tulivyosoma na wanavyosoma vizazi kuwa Tanganyika ilikuwa koloni la muingereza, kitu ambacho sio kweli, ni makusudi tu zimetumika.

Wapo waliokuja na wakasema bendera ya Tanzania ina rangi nyeudi, kijani, bluu na njano, wakati hakuna rangi ya njano kwenye bendera ya Tanzania, na hawa wameaminika hadi na watawala, inashangaza sana. Ukiwaambia bendera ina rangi ya dhahabu/gold na sio njano watakukatalia, ila uzuri sheria ya Bendera inaeleza wazi wazi.

Kuna kila sababu yakurudi nyuma kuangalia mitahala yetu.
 
Back
Top Bottom