Uongozi wa Bunge umetaja aliko aliyekuwa Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa Mkoani Dodoma, Job Ndugai.

Ndugai hajaonekana katika shughuli rasmi za chombo hicho tangu taarifa za kujiuzulu kwake wadhifa huo zilipotangazwa Januari 6, 2022 kwamba aliandika barua kwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na nakala kuwasilishwa kwa Katibu wa Bunge kutoa taarifa juu ya uamuzi wa kuachia ngazi.

Alipotafutwa na Nipashe jana Aprili 7, 2022 kwa simu kuzungumzia kutoonekana huko bungeni kwa Mbunge wa Kongwa, kushiriki vikao vya Mkutano wa Bunge la Bajeti vilivyoanza Jumanne ya wiki hii, vikitanguliwa na shughuli za kamati za kudumu za Bunge, Katibu wa Bunge, Nene wa Mwihambi alisema Ndugai yuko jimboni kwake.

"Hayupo bungeni maana yake (Ndugai) yuko jimboni. Sina barua kuhusu suala hilo. Mbunge asipokuwapo bungeni, maana yake yuko jimboni kwa mujibu wa kanuni na taratibu za Bunge."

"Ni mapema mno, ndiyo kwanza kumefanyi ka vikao viwili vya Mkutano wa Bunge la Bajeti, tulianza Jumanne.. (Ndugai) ana muda wa kutosha, atakuja kuungana na wabunge wenzake kushiriki vikao vya Bunge.

Kanuni za Kudumu za Bunge zinaelekeza miongoni mwa sababu za kukoma kwa hadhi ya ubunge ni kutohudhuria mikutano mitatu mfululizo ya Bunge pasina kutoa taarifa kwa Spika, kifo, kufutwa uanachama wa chama cha siasa, kujiuzulu ubunge na kutiwa hatiani kwa makosa ya jinai yanayosababisha kifungo cha zaidi ya miezi sita gerezani.

Nipashe ilipomtafuta Ndugai kwa simu jana Aprili 7, 2022 saa 6:48 mchana, simu yake ya kiganjani iliita kwa sekunde chache, ikakatwa kisha ukatumwa ujumbe mfupi wa maandishi kutoka kwe nye simu hiyo ukiwa na neno moja linalohoji nani?

Mwandishi alijitambulisha kwa sms lakini hakujibiwa na simu haikupokelewa.

Source: Nipashe
hv kuna kosa akifukuzwa ubunge kama alivyomfukuza joshua nasari
 
Kijifungia ndani hakutakusaidia mzee wangu. Unaweza jiletea magonjwa mengi kutokana na msongo wa mawazo. Tunajua fika hukutafajia hili lililotokea lakini binadamu wote hatujui kesho yetu.
Yaliyokutokea yamekua funzo kwetu kwamba vyeo na dhamana tulizopewa si za milele. Zinaweza kukoma muda wowote tena pale tusipotarajia. Jipige moyo konde utoke hadhari maisha yaendelee.
Uliyotukosea watanzania ukiwa spika wa bunge ni makubwa kuliko kosa lililokuondoa kwenye kiti. Utafanya vizuri kama utatoka hadharani pia utuombe radhi. Ukifanya hivyo nakuhakikishia mzee wangu utaishi kwa amani zaidi kuliko hata ulipokua na cheo. Toka hadharani acha kujificha. Tumejiandaa kukupokea kwa upendo tulojaliwa.
 
Kijifungia ndani hakutakusaidia mzee wangu. Unaweza jiletea magonjwa mengi kutokana na msongo wa mawazo. Tunajua fika hukutafajia hili lililotokea lakini binadamu wote hatujui kesho yetu.
Yaliyokutokea yamekua funzo kwetu kwamba vyeo na dhamana tulizopewa si za milele. Zinaweza kukoma muda wowote tena pale tusipotarajia. Jipige moyo konde utoke hadhari maisha yaendelee.
Uliyotukosea watanzania ukiwa spika wa bunge ni makubwa kuliko kosa lililokuondoa kwenye kiti. Utafanya vizuri kama utatoka hadharani pia utuombe radhi. Ukifanya hivyo nakuhakikishia mzee wangu utaishi kwa amani zaidi kuliko hata ulipokua na cheo. Toka hadharani acha kujificha. Tumejiandaa kukupokea kwa upendo tulojaliwa.

Ndugai aweza kuwa mateka mahali.

Yuko wapi Moses Lijenje?
 
huyu Ndugai alimfuta ubunge Lissu kwa kile anachodai ni mtoro na hajulikani alipo sasa tulia amfute na na yeye ubunge na kunyimwa stahiki zake zote kwa utoro bungeni bila taarifa
Wala siyo yeye aliyempora Lissu ubunge bali serikali hii ambayo imempora yeye Uspika. Katiba mpya siyo kipaumbele chetu.
 
Uongozi wa Bunge umetaja aliko aliyekuwa Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa Mkoani Dodoma, Job Ndugai.

Ndugai hajaonekana katika shughuli rasmi za chombo hicho tangu taarifa za kujiuzulu kwake wadhifa huo zilipotangazwa Januari 6, 2022 kwamba aliandika barua kwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na nakala kuwasilishwa kwa Katibu wa Bunge kutoa taarifa juu ya uamuzi wa kuachia ngazi.

Alipotafutwa na Nipashe jana Aprili 7, 2022 kwa simu kuzungumzia kutoonekana huko bungeni kwa Mbunge wa Kongwa, kushiriki vikao vya Mkutano wa Bunge la Bajeti vilivyoanza Jumanne ya wiki hii, vikitanguliwa na shughuli za kamati za kudumu za Bunge, Katibu wa Bunge, Nene wa Mwihambi alisema Ndugai yuko jimboni kwake.

"Hayupo bungeni maana yake (Ndugai) yuko jimboni. Sina barua kuhusu suala hilo. Mbunge asipokuwapo bungeni, maana yake yuko jimboni kwa mujibu wa kanuni na taratibu za Bunge."

"Ni mapema mno, ndiyo kwanza kumefanyi ka vikao viwili vya Mkutano wa Bunge la Bajeti, tulianza Jumanne.. (Ndugai) ana muda wa kutosha, atakuja kuungana na wabunge wenzake kushiriki vikao vya Bunge.

Kanuni za Kudumu za Bunge zinaelekeza miongoni mwa sababu za kukoma kwa hadhi ya ubunge ni kutohudhuria mikutano mitatu mfululizo ya Bunge pasina kutoa taarifa kwa Spika, kifo, kufutwa uanachama wa chama cha siasa, kujiuzulu ubunge na kutiwa hatiani kwa makosa ya jinai yanayosababisha kifungo cha zaidi ya miezi sita gerezani.

Nipashe ilipomtafuta Ndugai kwa simu jana Aprili 7, 2022 saa 6:48 mchana, simu yake ya kiganjani iliita kwa sekunde chache, ikakatwa kisha ukatumwa ujumbe mfupi wa maandishi kutoka kwe nye simu hiyo ukiwa na neno moja linalohoji nani?

Mwandishi alijitambulisha kwa sms lakini hakujibiwa na simu haikupokelewa.

Source: Nipashe
Ameenda kumtembelea mkuu wake aliyetaka kumlazimisha kuendelea na utawala lakini Bwana akafanya yake!!

Sent from my SM-A115AZ using JamiiForums mobile app
 
Jinga tu , mtu mzima na akili zako unadanganywa na mkwere wa msoga?
Mkuu, siasa za bongo ni calculation kali sana plus figisu nyingi, ghiriba, shirki, ngebe, unafiki etc..kama unafikiri ni rahisi kiasi cha Job kuingizwa mkenge jaribu kugombea jimbo lolote 2025.
 
leta hoja ya maana sio kila siku lissu. umeanza vizuri ungeandika hivi kama bunge halina taarifa ya ndugai alipo na yenyewe ndio mhimili katika mhimili mitatu je nani atajua?kila siku lissu , mara mbowe , mara sijui nani
 
Back
Top Bottom