Moaja kati ya mavitu ya hovyo Nyerere kayafanya ni huu upumbavu wa Liberation of Southern Africa. Tungesaidi kiaina tu na sio kujitoa mazima at the expenses of our economy and our wellbeing.
Tungekuwa na uchumi mkubwa sana leo kama sio ujinga ule wa Nyerere. Sad, tukiwa kwenye uhitaji kama wao, haito kaa itokee wafanye tuliowafanyia, NEVER.
Tatizo la Mwalimu aliamini katika utu, undugu, umoja na mshikamano, imani ya kuaminiana katika kuijenga Afrika.
Hakujua kama wenzake, ni wabnafsi, wachoyo, wajilimbikiaji wa mali za umma, alidhani wana mtazamo sawa na yeye.
Aliamini kwamba jirani yako akiwa na matatizo usipomsaidia kwa kumaliza hilo tatizo litakuja na kwako. Nchi zote zilizokombolewa kwa msaada wa Tanzania kama zingebaki kutawaliwa hata Mwalimu na viongozi wake wasingetawala kwa amani.
Angalia political instability ya Somalia jinsi inavyowatesa Kenya, je na sisi Tanzania, Uganda, South Sudan tungekuwa kama Somalia Kenya ingekuwa na maendeleo iliyonayo hivi leo?
Gharama iliyotumika Rwanda kurejesha amani iliyopotea miaka ya 90 ni kubwa kuliko ambavyo ingetafutwa huko nyuma. Tazama pia gharama inayotumiwa na Kenya kuimarisha ulinzi na usalama baina yake na Kenya ni kubwa mno kuliko ambavyo Somalia ingekuwa peace.
Kuwa na uchumi mkubwa na maendeleo halafu nchi haina amani ni sawa na kuishi na mke mkorofi, mchafu, mchonganishi, mgomvi, mwenye mdomo ndani ya ndoa lakini huko nje unajifanya huna shida yoyote kwenye ndoa ila maumivu ya ndani ni makali na machungu kama shubiri.
Nyerere was a real and visionary leader. Ameacha utaratibu mzuri, mali, siasa safi lakini zimevurugwa na hawa hawa tuliowapa madaraka, wamejimilikisha na kujilimbikizia mali za umma, nchi inatafunwa na wachache, maendeleo tutayapata iwapo kama viongozi wetu watakuwa na utu, mapenzi mema kwa Taifa letu, kuacha choyo na ubnafsi, kutanguliza uzalendo na kuimarisha amani na utulivu katika nchi yetu.
Miradi aliyoifanya Magufuli ndani ya miaka 5 ni mingi na mikubwa na hakuna mahali Tanzania iko inakomboa nchi nyingine. Viongozi wetu wawe na utashi wa kutenda kazi pasipokuwa n visingizio vya kijinga. Tuko vizuri kama tutasimamia sera zetu za kiuchumi, vipaumbele vya Taifa, tutasimamia rasilimali zetu vizuri, kujiepusha na mikataba ya hovyo na wananchi wote tuwe wazalendo tulinde uchumi wetu. Miaka 10 mbele tutakuwa nchi ya kutamaniwa na kila mmoja.