Hapa sasa umeamua kututukana na wala siyo Facts mkuu, iweje tuna utapiamlo wakati tuna organic food kibao kila sehemu, hivi unajua kuna sehemu matunda yanadondoka tu yenyewe shambani?
Siyo kwamba hatuna chakula kwasababu tunashindwa kuafford kwasababu ya umasikini la hasha! Bali ni kutokuwa makini kwa wazazi/walezi kuwapa chakula cha aina moja watoto bila kuchanganya vyakula vyenye virutubisho.
Na hizo sehemu ni chache unakuta wazazi wengi wako busy kutafuta pesa kutokana na huo msimu kuzalisha mazao ambayo ni deal kwa wengine, so wanakimbizana na hela huku wanasahau majukumu ya malezi.
Hii imewahi kutokea Kilimanjaro;sasa hawa utasema ni masikini, Bukoba; utasema ni masikini, Nyanda za juu kusini; hawa nao siyo wanyonge ila unakuta walijisahau kwenye kilimo cha miti na kuacha lishe kwa watoto, lakini wote hawa wako vizuri sana kwenye uzalishaji.
Sisi hatuna njaa,wala shida ya chakula.Malnutrition haitokani na njaa ya chakula ila ni ukosefu wa baadhi ya virutubisho kwenye chakula.
Upande wenu kama watu wenu wanakufa kwa njaa maana yake wamekosa hata maji ya kunywa, hawana kitu chochote cha kuweka mdomoni, pia serikali yenyu haina uwezo wa kuwanunulia chakula wasio na uwezo, serikali yenyu haina uwezo wa kuhifadhi chakula cha ziada baada ya kuvuna chakula chote mmekitumia chote.
Taasisi yenu ya kudeal na majanga haina uwezo wa kifedha wala maono kutunza chakula cha ziada. Msisingizie ukame viongozi wenu ni bomu.
Kiukweli kama Tanzania tuna umasikini mpaka kukosa chakula jiulize nyinyi mtakuwa na hali gani?