Watanzania hebu niwaulize kwa heshima na unyenyekevu ni kwa nini huwa mnakataa kukubali kwamba Kenya ina uchumi mkubwa (wa sita Afrika kwa ukubwa wa uchumi) eti kwa sababu kuna Wakenya wachache kaskazini mwa Kenya ambao wanalala njaa? Kwa hivyo kama kuna Wakenya wanaolala njaa hio inamaanisha kwamba Kenya ina uchumi mdogo? Mbona hata Angola ilikuwa inapigana vita in the 1960s and 70s lakini bado ilikuwa na uchumi wa nne kwa ukubwa barani Afrika? Mbona Nigeria ilipigana vita in the 1960s (Biafran war) na wakati huo wa vita bado ilikuwa na uchumi wa pili kwa ukubwa barani Afrika na watu zaidi ya milioni mbili Nigeria wenye asili ya Igbo walikufa njaa kufuatia ukame mkali uliotokea eneo hilo? Licha ya majanga haya yote, uchumi wa Nigeria bado ulibakia kuwa wa pili barani Afrika kwa ukubwa.