Kuna vitu havijakaa sawa kwenye muungano hatuwezi kukaa kmy kwa kigezo cha kuchochea chuki, mm naomba kuuliza inakuaje rasilimali za zenji ziwe za kule tu lkn za bara ziwe za wote? Au labda tuwekane sawa tujue kwamba bila zenji basi hakuna Tz bara, huu muungano ni wa kipumbavu sn huu, ok usiku mwema wakuu.
Pamoja mkuu,yaani huu muungano mm unanikera Sana,mfano.
1.zanzibar walipogundua Mafuta,wakasema hayausiani na muungano,ina maana,bara SS hatumo.
2.Rais anatokea Zanzibar,anatwala pote,bara na Zanzibar,kule Zanzibar,mtu kutoka bara hawezi kuwa hata mwenyekiti wa mtaa.
3. Mtu wa bara huruhusiwi kununua ardh na kuimiliki,lakini huku bara wamejenga kila mahalo.
4. Mtu kutoka bara hawezi kupata Ajira kule hata kufagia Ofisi za serikali,Ila huku wamejaa majeshini,na tasisi nyeti.Wengi wao hawapendi kufanya kazi kwao sababu wanalipwa mishahara midogo Sana na hii imesabisha umasikini mkubwa Sana Zanzibar.
5.mtu kutoka bara ni ngumu kwake kufanya biashara kule lakini huku bara,wapemba wametapakaa kariakoo na huku mikoani na maduka ya simu na biashara zingine.
6. Ukiingiza bidhaa kutoka bara untozwa Kodi kule Zanzibar,eti ni nchi nyingine lakini huku wanaingiza vitu wanavyotaka.
Mm binafsi siutaki muunago hata kidogo,natamani uvunjwe kila mtu aishi Kwa kujitegemea. Bara hakuna tunchotegemea kutoka kule we have nothing to loose! Ila wao watapoteza vingi Sana,ule usemi kwamba muunngano ukivunjika watapata maendeleo haraka ni uwongo,Kwanza Wanaguana Sana Kati ya wapemba na waunguja. Kwa hiyo sio ajabu wakajitenga wao Kwa wao tena,pia ufisadi mkubwa Sana kule.
Muunngano unatinyonya Sana ss bara.