mvua

  1. Kaka yake shetani

    JamiiForums Tanzania Dubai wana kituo cha kusababisha mvua kwa kumwaga nchunvi kwa kutumia ndege.Sisi huku tukimtanguliza mungu na kununua V8 new model

    Yani sijui tuna kwama wapi yani ukikaona kandege kenyewe utazani kakupeleka watalii mbugani.yani wenzetu wasio na kitu kwenye ardhi wanajaribu kisicho kuwa kitu kuwa kitu. bado na kazia ma ubongo yetu yana tumia masanturi
  2. Roving Journalist

    JamiiForums Tanzania Ruvuma: Barabara kuu ya Mangaka - Tunduru yafungwa kwa muda. Ni kutokana na mvua zinazonyesha

    Tunduru - Ruvuma Kutokana na mvua kubwa zinazonyesha ukanda wa Morogoro na Selous, daraja kubwa la Mto Muhuwesi lililoko hapa Tunduru limejaa maji hadi juu ya daraja na kwa hiyo tumechukua uamuzi wa haraka wa kufunga barabara kuu ya Mangaka - Tunduru Mjini kwa muda. Eneo la barabara...
  3. ndege JOHN

    JamiiForums Tanzania February mvua huwa zinazingua Tanzania kote

    Kama ni mfuatiliaji wa mwenendo wa mvua nchini utagundua mwezi wa pili kuna shida sana ya mvua za uhakika watu wengi naona wanashangaa mvua ku stop ghafla ila hii ni kawaida kabisa kwa mwezi wa pili. Mwezi wa pili mvua huwa Inakata na kama zitakuwepo basi za rasharasha.
  4. Roving Journalist

    JamiiForums Tanzania TRC: Tunaendelea kusitisha safari za Treni kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha

    Dar es Salaam, Tarehe 30 Januari 2024 Shirika la Reli Tanzania - TRC linautaarifu umma kuwa linaendelea kusitisha huduma ya usafiri wa treni kutoka Dar es Salaam kuelekea mikoa ya Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga, Mwanza, Katavi, Kigoma na njia ya Kaskazini kuelekea mkoani Tanga...
  5. BARD AI

    JamiiForums Tanzania TMA: Mvua za El-Nino kuendelea hadi Aprili 2024

    Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema bado kuna viashiria vya uwepo wa El-Nino hadi Aprili mwaka huu. El-nino ni mfumo wa hali ya hewa unaosababishwa na ongezeko la joto la bahari katika eneo la kati la Kitropiki kwenye Bahari ya Pasifiki. Mwaka jana, TMA ilieleza kuwepo kwa El-Nino...
  6. haszu

    JamiiForums Tanzania Mvua kubwa ilioambatana na upepo imenyesha Kibaha

    Nimetubu sala zote asikwambie mtu, upepo ni mkali sana pamoja na radi.
  7. BARD AI

    JamiiForums Tanzania Mikoa 8 kukumbwa na Mvua kubwa kwa siku 5 kuanzia Januari 30, 2024

    Mikoa ya Lindi, Iringa, Mtwara, Mbeya, Songwe, Njombe na Ruvuma inatarajiwa kupata Mvua za Juu ya Wastani kuanzia Januari 30, 2024 ikiwa ni siku chache tangu Mikoa ya Dar na Morogoro ikumbwe na Mafuriko. Kwa mujibu wa taarifa ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Mvua hizo zinaweza...
  8. Influenza

    JamiiForums Tanzania Kutokana na kuendelea kuharibika kwa miundombinu ya barabara kwa mvua, Waziri wa TAMISEMI aagiza marekebisho kwa fedha za dharura

    Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa ameuelekeza Wakala wa barabara Vijijini na Mijini (TARURA) kutumia Bilioni 40 fedha za dharura kukarabati miundombinu ya madaraja na barabara zilizoharibiwa na mvua za Elinino zinazoendelea kunyesha...
  9. X men

    JamiiForums Tanzania Maji ya Mvua meusi

    Wilayani Nzega, mkoani Tabora siku 2 zilizopita ilinyesha mvua kubwa kiasi, kama kawaida sisi wa Uswahilini lazima tukinge maji kwenye ndoo, masufuria na mabeseni. Cha ajabu sasa yale maji ya mvua yalikua ni meusi, tukajua labda kwa siku mbili tatu ambapo haikunyesha itakua bati limechafuka...
  10. excel

    JamiiForums Tanzania Wakati mvua zikiendelea kuutesa mkoa Dar, mkumbuke maji yanarudi mahala pake tu Serikali haina makosa

    Unaambiwa enzi hizo Dar es Salaam kulikuwa na mito mikubwa kabisa pamoja na maziwa(lakes) Tazama hii ramani ya beberu mjerumani inakupa picha kamili Kulikuwa na ziwa Tandale😅 Ziwa Mwananyamala😂 Ziwa Magomeni😅 Mto Sinza😅 Dar es Salaaam inahitaji MKOLONI arudi tena kuipanga upya maana yeye...
  11. S

    JamiiForums Tanzania Nimepita sehemu nikakuta watu wanaomba Mungu kukemea mvua isinyeshe! Nimewashangaa sana

    Nimewaza sana leo! Yaani watu kabisa wanamuomba Mungu kukemea Mvua isinyeshe! Kwamba mvua inaleta uharibifu! Bahati mbaya kwenye hayo maombi kulikuwa na watu wazima, wazee hadi watoto wadogo! Sikatai wao kufanya maombi! Lakini kinachonitisha ni hao watoto watakuwa na mentality ya kukemea vitu...
  12. Shining Light

    JamiiForums Tanzania Mvua kuwa kilio kwetu

    Jiji la Dar es Salaam la Lia baada ya kukumbwa na changamoto kubwa ya maji ya mvua kufurika katika mitaa na nyumba za watu, na madhara ya mvua yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara. Tatizo kuu linapatikana katika mifumo ya maji taka na miundombinu ya mji. Mitaro mingi imejaa maji na kushindwa...
  13. Pdidy

    JamiiForums Tanzania Msije kusingizia mvua, Wana usafi ratiba yetu iko palepale hata mvua ikinyesha

    Wale tuliojiandaa kufanya usafi tafadhali msikose, tumeamua hata mvua ikinyesha tutasafisha kila kitu kinachosafishiika. Wale wapendwa wenzetu waliotutangazia kuungana na sisi kwenye usafi niwakumbushe msisingize mvua mnakaribishwa kwa pamoja kuliweka jiji letu safi. Mkuu wetu wa mkoa...
  14. U

    JamiiForums Tanzania Mvua nyingi, kwanini bwawa la Stiglers halijai

    Moja kati ya mabwawa makubwa kuwahi kutokea Africa mashariki, man made lake , the Stiglers Gorge dam, au bwawa la Mwalimu Nyerere au Ziwa Nyerere kutokana na ukubwa wake. Bwawa hili mpaka kujaa linatakiwa kufika MITA 186 kutoka usawa wa bahari, Cha ajabu pamoja na mageti kufungwa December 2022...
  15. 5 Nyingi

    JamiiForums Tanzania TANESCO Walalamikia Mvua kubwa, wasema ni chanzo cha mgao

    Shirika la Umeme nchini (TANESCO), limesema hali ya upatikanaji wa Umeme katika baadhi ya maeneo nchini, imekuwa duni kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali, iliyosababisha miundombinu ya umeme, zikiwemo nguzo na transfoma kuanguka. Kupitia taarifa iliyotolewa na...
  16. Melki Wamatukio

    JamiiForums Tanzania Kuna Mmasai aliniingiza mjini asubuhi ya jana kwenye mvua

    We Mmasai uliyeniadaa na madawa yako ya mitishamba siku ya jana kwenye mvua, nasemaje, sisi ni Pipo, one day tutameet Alianza kwa kunitandika dawa ya mvuto wa biashara, akafuatia dawa ya mvuto wa wanawake, akamalizia dawa ya kulifanya pembe la ndovu liwe na hasira kali kwa muda mrefu. "Rafiki...
  17. Heparin

    JamiiForums Tanzania SI KWELI Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha zasababisha kudondoka kwa Mawingu Mkoani Morogoro

    Inadaiwa kuwa kuna mawingu yamedondoka huko Morogoro kutokana na mvua kubwa zinazonyesha. Wataalam, imekaaje hii? Video ikionesha kile kinachodaiwa kuwa ni Mawingu yaliyodondoka, Morogoro
  18. BigTall

    JamiiForums Tanzania KERO Barabara za Jimbo la Kibaha Mjini (Pwani) hali ni mbaya, mvua ikinyesha Wananchi wanateseka

    Hivi ndivyo ilivyo maeneo ya mitaa ya Kibaha, Maili Moja Mkoani Pwani, mvua zikinyesha tu basi miundombinu hasa barabara hazipitiki kirahisi kama hivi inavyoonekana. Mbunge wa Jimbo hilo la Kibaha Mjini ni Silvestry Fransis Koka ambaye amekuwepo katika nafasi hiyo kwa muda mrefu lakini suala la...
  19. Light Saber Imetosha Sasa

    JamiiForums Tanzania Video: Mvua zinazoendelea kunyesha Nchini, mvua ya mawe iliyonyesha Tarafa ya Machame, Katika wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro

    Video zikionyesha baadhi ya athari zilizotokana na Mvua kubwa ya mawe iliyonyesha Mkoani Kilimanjaro, Wilaya ya Hai Tarafa ya Machame Mashariki. Jogoo mbegu Hannah TODAYS
  20. profesawaaganojipya

    JamiiForums Tanzania Msaada: Kuondoa utelezi maji ya mvua

    Wakuu, kutokana na maji ya bomba ya dawasa kutoka kwa muda wa lisaa limoja tu kwa kila miezi 3, nimeona nihifadhi maji ya mvua Tatizo yana utelezi fulani mwilini mimi napooga, je njia rahisi ya kuondoa huo utelezi ni ipi? Msaada tafadhali.
Back
Top Bottom