Search results

  1. A

    Unafiki na Uongo Wetu Viongozi: Usiyoilamba Haikuwashi!

    Wasalaam, Kwa makusudi kabisa nitaendelea kuepuka kuzungumzia mambo magumu kwa Mtanzania wa kawaida kama vile utafiti wa gesi/mafuta, ofisi za ukaguzi Malaysia, jengo la ubalozi Marekani nk. Kwa mwananchi wa Kata ya Mabogini hayo ni mambo yaliyo mbali sana. Yanamuhusu ila kwake ni sawa na...
  2. A

    Wananchi legelege ndio chanzo cha serikali legelege!

    Kelele za JK ameshindwa nchi zimezidi. Serikali haitekelezi wajibu wake na viongozi wanajifikiria wao ni maneno ambayo yamesemwa toka enzi za mababu! Watendaji wabovu wamekuwa nembo ya Taifa. Lakini bado wananchi wale wale ndio wanaowaacha madarakani. Ni wananchi hao hao ambao wanaruhusu...
  3. A

    Dua kabla ya Bunge: Umoja, Haki, Hekima kwa Raisi na mengineyo!

    Mh. Anna Makinda anaposoma dua kabla ya kikao cha Bunge huwa anaamini anachosoma? Kwa uelewa wangu anachofanya ni kusoma dua na sio kusali/kuswali. Kunatofauti kati ya kusoma dua na kusali/kuswali. Hayo yote yanayotajwa kwenye dua yanabaki ni maneno tu na sio sala. Kwa yanayotokea...
  4. A

    Watanzania na Tanzania

    Sisi ni watu wa ajabu sana. Kwa sisi namaanisha watanzania. Najiuliza; Dowans! Tumesahau! Radar! Tumesahau! Epa! Tumesahau! Migodi! Haituhusu! Iptl! Tumesahau! Mafuta! Tumesahau! Wizi wa wanyama! Tutasahau! Jairo! Tunasukuma gari lake! Tunamwimbia na kumsifu! Pinda...
  5. A

    Fikra: Wazungu na Tanzania!

    Nimefuatilia michango ya wabunge kwa makini. Jambo moja kubwa limejitokeza, wazungu wanaonekana kuwa ni chanzo cha matatizo yetu mengi! Wapo ambao wanaosema tuwafukuze, wengine wana wakebehi na kuwatukana. Wengine wanasema ni lazima tufanye nao kazi na hatuwezi kufanikiwa bila wao. Kuna...
  6. A

    Siasa zetu: Kubali kuliwa Ule!

    Nimemsikia Mh. Makala kwenye mchango wake bungeni leo akimnukuu Raisi &quot;kubali kuliwa ule&quot;. Hii ni kuelezea kwamba TANAPA watangaze biashara ya utalii ili wapate biashara!<br /> <br /> Huu unaweza kuwa msemo. Lakini unaonyesha ni jinsi gani tunavoweza kuwa 'loose' katika fikra...
  7. A

    Maandamano ya CHADEMA Mbeya yaruhusiwa

    Taarifa zilizopatikana ni kwamba RPC Mbeya amepiga marufuku maandamano ya CDM kwa sababu ya taarifa za kiintelligensia. Kwa mara nyingine tena watawala wanaingia woga na kuweweseka wakiwafikiria CDM. Kwa nini CDM wawe chanzo cha vurugu? Watu Wa-Mbeya wavuruge amani yao wenyewe? Au...
  8. A

    Siasa na Sheria: Dada na Kaka.....

    Katika hali ya kawaida na maisha ya kila siku ni vigumu kutenganisha vitu hivi viwili. Haviwezi kutenganishwa kwa sababu aidha kimoja kinasaidia kingine au kimoja kinaharibu kingine. Hapa kwetu malalamiko mengi yanatokana na aidha sheria au wanasheria au siasa na wanasiasa. Huko Uganda...
  9. A

    BAVICHA vs UvCCM: Walipo watoto wa Viongozi wa CCM na CHADEMA

    WanaJF, Kuna msemo niliwahi kuusoma zamani, 'mimi sio nyoka kwa sababu baba yangu hakuwa nyoka'... Pia, wengi wetu (sio wote) ni wakristo au waislamu kwa sababu wazazi wetu ni wakristo au waislamu. Au kwa sababu tumelelewa kwenye mazingira hayo. Hali hiyo imewakuta wengi linapokuja...
  10. A

    Uwajibikaji wa Mbunge kwa Wapiga Kura: Nini kifanyike kuleta ufanisi?

    Wakati najadiliana na FJM kwenye thread nyingine nimejikuta nikijiuliza je Mbunge anawajibika vipi kwa wapiga kura wake? Ni uwajibikaji wa aina gani pale ambapo Mbunge anawajibishwa kwa kutochaguliwa tena? Mwananchi anakuwa amepoteza nafasi ya muhimu ya kuhoji mambo mengi wakati Mbunge huyo...
  11. A

    Ripoti ya Mwakyembe: Nia, madhumuni, utekelezaji, dharau, kejeli, kutokujali na usahaulifu!

    Baada ya Ndugu Bashir Mrindoko kuteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu nimelazimika kuazima andiko la MwanaJF mmoja alipotaka kutukumbusha jambo. Jambo hilo sio lingine ila ripoti ya Mwakyembe (MB) ambayo naamini kwa kiasi fulani ilisaidia sana yeye kuteuliwa kuwa Naibu Waziri kwani ripoti hiyo pamoja...
  12. A

    If the dead could rise...Nyerere, the true son of Tanzania

    As am watching TBC (one of the rare moments that I do) am reflecting on Mwl. Julius Nyerere. With his failures as a human being he remains a true son of Tanzania. He is a hero in many aspects. And, he admitted to have made some mistakes. Our leaders today will not admit that. The failed...
  13. A

    Jumuiya ya Afrika Mashariki na Zanzibar

    Kwenye gazeti la Guardian la tar. 20/4/2011 ukurasa wa mbele kuna picha yenye maneno yafuatayo.... 'Heads of EAC partner states stand attention as their national anthems are played at the start of the 9th extraordinary summit in DSM yesterday. From L are President Yoweri Museveni of Uganda...
  14. A

    Mwenyekiti wa Kitongoji; Mwenyekiti wa Kjiji; Diwani; Mbunge; Raisi wa JMT:

    WanaJF, Salaam. Ni matumaini yangu kwamba mawazo yangu kwa ufupi yatasaidia kuanzisha mjadala kuhusu wapi tunapokosea kama nchi kiuongozi. Nchi yetu inakwama sehemu nyingi, kiuchumi, kijamii, kisiasa etc. Tangu kuchaguliwa kwangu kama Diwani kuna jambo ambalo limejidhihirisha. Nimekuwa...
  15. A

    Raila: Gbagbo to receive amnesty!? Am still thinking!

    Raila, I just heard. You say the crisis which resulted to deaths of innocent souls, destruction of property and many many other unthinkable sufferings is something that should just be 'forgiven'. Brother, am still amazed. Am surprised. Am puzzled. God forgive you Raila.
  16. A

    Membe vs January Makamba

    How could you not distinguish between informal language, official language and national language? Unataka wawakilishi wawe wanatembea na mashine za kutafsiri lugha na dictionary? I have confirmed once a rattle snake always a rattle snake! ======== Kilichojiri ni kwamba January...
  17. A

    Wazanzibari na Watanganyika wamekuwepo tangu 1964....TANZANIA SIO NCHI.

    Zidumu fikra za Mwenyekiti. Nimeona ni vyema nikaanza na salamu hiyo kwa sababu kuu moja, fikra za Mwenyekiti, Marehemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere zimedumu kwa muda mrefu hatimaye tumefika mahali sasa hali si hali na wote tunajidai kushangaa yanayotokea. Ni kwa bahati mbaya sana fikra...
  18. A

    CHADEMA; wanajf na mh. Zitto tetesi na utabiri mpaka lini?

    Kila kukicha tetesi. Zitto! Chadema! Sasa imekuwa upuuzi. Hakuna ushahidi wa lolote. Kila siku 'kuna taarifa'. Nguvu inayotumika kuchangia au kujibu tetesi ingetumika kuweka mipango ya ukombozi tusingesubiri miaka 50 kuendelea. Yanayozungumziwa hapa ni majungu, fitna na umbea kuhusu...
  19. A

    JK: Ajira Milioni Moja Ziko Wapi? Au Bado?

    Mh. Raisi! Habari ya siku tele? Nimeona nikukumbushe, hivi zile ajira ulishatengeneza au bado tusubiri kidogo? UVCCM hawatakuuliza wala hawatakusaidia kuzungumzia kwa vijana wenzao ambao hawana ajira. Kwao ni rahisi kushutumu na kulalamikia mambo kuongelewa nje ya vikao. Ni watu wajinga sana...
  20. A

    Je Mabango ya Maandamano ya CHADEMA Zanzibar Yasomeke Vipi?

    Najaribu kutafakari na kujiuliza, Je CDM wakienda kuandamana mabango yatakayoandaliwa yasomeke vipi? Kwa mfano; CCM-CUF punguzeni bei ya bidhaa?? Au yataelekezwa kwa CCM peke yake? Au Zanzibar hakuna ugumu wa maisha na hakuna haja ya kufanya maandamano? Labda tupate mawazo!
Back
Top Bottom