Albert Msando
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 1,019
- 171
Wakati najadiliana na FJM kwenye thread nyingine nimejikuta nikijiuliza je Mbunge anawajibika vipi kwa wapiga kura wake? Ni uwajibikaji wa aina gani pale ambapo Mbunge anawajibishwa kwa kutochaguliwa tena? Mwananchi anakuwa amepoteza nafasi ya muhimu ya kuhoji mambo mengi wakati Mbunge huyo akiendelea kuboronga na kufanya yale ambayo hajatumwa na wananchi au kuendeleza yale ambayo chama chake kinataka.
Ni mambo gani yafanyike au utaratibu gani uwekwe wa kuwahoji na kuwawajibisha wabunge ambao wanashindwa kutekeleza wajibu wao? Je ni wapi Mbunge anakuta kipimo cha ufanisi wa kazi yake?
Hali ya sasa ni kusubiri Mkutano wa hadhara kumuuliza Mbunge maswali. Maswali ambayo mara nyingi unakuta hayamuhusu Mbunge badala yake ni wajibu wa serikali ambao haujatekelezwa. Majibu anayotoa Mbunge hayaridhishi. Pia Mbunge anatumia hadaa kuwalaghai wananchi Kwa mfano, atatoa zawadi za madawati, atasaidia kwaya, atatoa laki kwa kina mama, elfu hamsini kikundi cha vijana, madaftari kwa wasioona, walkman kwa viziwi. Pia atatoa msaada wa kompyuta moja kwa wanafunzi mia nne!!
Je anawajibika vipi? Ni chombo gani kinaweza kumwajibisha Mbunge anayeshindwa kutekeleza wajibu wake? Nini kifanyike?
Mawazo yenu yatasaidia kuanzisha mjadala mpana zaidi ili tuweze kubadili hali ya ungozi ndani ya nchi yetu. Mbunge akiwajibishwa lazima atamuwajibisha waziri na serikali kwa ujumla. Wakiendelea kuendekezwa wataendeleza porojo na usanii.
Angalizo, katika hili hakuna cha CCM, CUF wala CHADEMA, TLP au NCCR. Ni wote. Wote lazima wawajibike kwa hiyo tuchangie bila ushabiki wala ufuasi wa vyama.
Ni mambo gani yafanyike au utaratibu gani uwekwe wa kuwahoji na kuwawajibisha wabunge ambao wanashindwa kutekeleza wajibu wao? Je ni wapi Mbunge anakuta kipimo cha ufanisi wa kazi yake?
Hali ya sasa ni kusubiri Mkutano wa hadhara kumuuliza Mbunge maswali. Maswali ambayo mara nyingi unakuta hayamuhusu Mbunge badala yake ni wajibu wa serikali ambao haujatekelezwa. Majibu anayotoa Mbunge hayaridhishi. Pia Mbunge anatumia hadaa kuwalaghai wananchi Kwa mfano, atatoa zawadi za madawati, atasaidia kwaya, atatoa laki kwa kina mama, elfu hamsini kikundi cha vijana, madaftari kwa wasioona, walkman kwa viziwi. Pia atatoa msaada wa kompyuta moja kwa wanafunzi mia nne!!
Je anawajibika vipi? Ni chombo gani kinaweza kumwajibisha Mbunge anayeshindwa kutekeleza wajibu wake? Nini kifanyike?
Mawazo yenu yatasaidia kuanzisha mjadala mpana zaidi ili tuweze kubadili hali ya ungozi ndani ya nchi yetu. Mbunge akiwajibishwa lazima atamuwajibisha waziri na serikali kwa ujumla. Wakiendelea kuendekezwa wataendeleza porojo na usanii.
Angalizo, katika hili hakuna cha CCM, CUF wala CHADEMA, TLP au NCCR. Ni wote. Wote lazima wawajibike kwa hiyo tuchangie bila ushabiki wala ufuasi wa vyama.