Wazanzibari na Watanganyika wamekuwepo tangu 1964....TANZANIA SIO NCHI.

Albert Msando

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
1,019
171
Zidumu fikra za Mwenyekiti.

Nimeona ni vyema nikaanza na salamu hiyo kwa sababu kuu moja, fikra za Mwenyekiti, Marehemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere zimedumu kwa muda mrefu hatimaye tumefika mahali sasa hali si hali na wote tunajidai kushangaa yanayotokea.

Ni kwa bahati mbaya sana fikra zake zimeendelea kutuongoza mpaka leo. Huko alipo ameendelea kutuangalia jinsi ambavyo tumezivaa fikra zake kama NIRA na naamini amekuwa akitushangaa kwa nini tumeshindwa kuendeleza pale alipoachia yeye.

Binafsi nampongeza Mwenyekiti kwa jambo kubwa moja, kuweza kufikiri na kutekeleza kile alichofikiri. Pia aliweza kuaminisha umma kwamba alichofikiri ni bora kwa ustawi wa umma. Kwa sasa hivi sina wa kumpongeza kwa kufikiri na kutekeleza anachofikiri.

Lakini, fikra zake na utekelezaji wake una mambo mengi tu. Mabaya na Mazuri. Kwa wale ambao bado wanamuamini hata katika kifo mabaya ni hakuna. Kama yapo hayakuwa yake.

Ila, nina machache ya kuweka hapa jamvini.

Kuna mama mmoja ameshitaki viongozi wa kijiji fulani. Viongozi hawa walikuwa ni wajumbe wa kamati ya ugawaji ardhi miaka ya 1970 wakati wa Operation Vijiji. ardhi yake iligawanywa kwa wanakijiji wengine. Baada ya miaka zaidi ya 15 akafungua kesi. Anadai ardhi yake. Kwenye ardhi hiyo leo kuna shule mbili, makanisa mawili, kaya zaidi ya 500, barabara ya umma, dispensary. Mama huyo alishinda kesi!!! Dalali akaenda kukamata mali wananchi wakaja juu.......Operesheni Vijiji/Ujamaa na Kujitegemea.

Mpaka leo hii bado Katiba yetu inasema;


KWA HIYO, BASI, KATIBA HII IMETUNGWA NA BUNGE MAALUM LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, kwa niaba ya Wananchi, kwa madhumuni ya kujenga jamii kama hiyo, na pia kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Tanzania
inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia na ujamaa.

SURA YA KWANZA
JAMHURI YA MUUNGANO, VYAMA VYA SIASA,WATU NA SIASA YA UJAMAA NA
KUJITEGEMEA

Lengo la Katiba hii ni kuwezesha ujenzi wa Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar au wa
chochote kati ya vyombo vyake na udugu na amani kutokana na kufuata siasa ya Ujamaa na Kujitegemea, ambayo inasisitiza
utekelezaji wa misingi ya kijamaa kwa kuzingatia mazingira yaliyomo katika Jamhuri ya Muungano. Kwa hiyo, Mamlaka ya
Nchi na vyombo vyake vyote vinawajibika kuelekeza sera na shughuli zake zote katika lengo la kuhakikisha-

Fikra za Mwenyekiti zimeendelea kudumu mpaka leo. Hakuna anayethubutu kuzigusa. Eti bado ni 'nchi' ya kijamaa. Sawa.

Haya, hilo tuache. Kuna hili la Zanzibar na Tanganyika. Alifanya kazi kubwa kuziunganisha nchi mbili ili ziwe nchi moja. Wote tukaamini amefanikiwa na sisi ni wamoja. Tuliamini fikra zake. Hakuna aliyehoji kwa sauti.

Kwa miaka yote Katiba yetu inasema;

1. Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano.


Kwenye utangulizi tukatamka kwa sauti;

KWA KUWA SISI Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani:


Hapa sisi ni Watanganyika na Wazanzibari! Tuliamini hivyo.

Lakini, Wazanzibari wakaendelea na maisha yao. Wakiamini kwamba wanaonewa na kudharauliwa. Hii si kweli. Wanaonewa na nani?? Wameijenga 'nchi' katika misingi ya uhuru, haki, udugu na amani?

Hilo si la msingi kwa sasa. Tunagalie walichokuwa wanafikiria na kutekeleza.

Katiba ya Zanzibar inasema;

(9)(i) Zanzibar itakuwa ni NCHI ya kidemokrasia na haki za kijamii.

(9)(2)(a) Mamlaka ya kuendesha NCHI ni ya wananchi wenyewe …

(10) Kwa madhumuni ya kuendeleza umoja na maendeleo ya watu na ustawi wa jamii katika NCHI itakuwa ni wajibu wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar:

(10)(3) Itadhibiti uchumi wa NCHI kufuatana na misingi na madhumuni yaliyoelezwa na katiba hii.

(12)(3) Haki za raia, wajibu na maslahi ya kila mtu yatalindwa na kuamuliwa na mahkama pamoja na vyombo vya NCHI na vinginevyo vilivyowekwa na sheria.

(21)(i) Kila Mzanzibari anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa NCHI…

(23)(2) Kila mtu ana wajibu wa kulinda maliasili ya Zanzibar, mali ya NCHI pamoja na mali yote inayomilikiwa kwa pamoja na wananchi…

Kwa hiyo basi, Tanzania sio nchi moja kama tulivyokuwa tunaamini. Ni dhahiri hatukuungana kama nchi moja. Zanzibar ilibaki kuwa nchi. Wazanzibari waliendelea kuishi kama nchi muda wote mpaka leo.

Je, sisi wengine nchi yetu ni ipi? Tanganyika iko wapi? Zanzibar ina bendera, raisi, baraza la wawakilishi, vikosi vyake vya ulinzi nk. Sisi?

Kama wao wana maisha yao na nchi yao iweje wanatuchagulia Raisi? Je inawezekanaje raia wa nchi nyingine achague Raisi wa 'nchi' nyingine? Sawa sheria zinaruhusu hilo, je sheria hizo ziko sawa? Na sheria kuu iko sawa?

Sheria Kuu (KATIBA) inatamka kwamba Tanzania ni nchi moja. Katiba ya Zanzibar amabyo nayo ni Sheria Kuu inatamka Zanzibar ni nchi. Sasa hapa ipi ni nchi na ipi si nchi? Hii yote ilianzia kwa Mwenyekiti......MUUNGANO!

Imani yetu imetuponza au imetuponya?

Basi nimalizie na swali, Je Wazanzibari wanashiriki kwenye mchakato wa Katiba Mpya kama raia/wananchi wa nchi gani?? Tanzania au Zanzibar? Sifa ya kushiriki utungaji wa Katiba ni lazima uwe raia wa nchi. Nchi haipo, raia hawapo!

ZIDUMU FIKRA ZA MWENYEKITI. KISIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI.
 
Hakuna tija kuendelea kujadili Muungano....Katiba ndio ya msingi na ndio itaamua yote.....Go back to our major concern...mother of all things is constitution....

:rip:Mijadala inayohusu muungano.............
 
Hakuna tija kuendelea kujadili Muungano....Katiba ndio ya msingi na ndio itaamua yote.....Go back to our major concern...mother of all things is constitution....

:rip:Mijadala inayohusu muungano.............

Only 83,

Sawa, je Katiba ipi sasa? ya Jamhuri ya Muungano au ya Tanganyika? Kuwa wazi na useme unachofikiria au unachoamini ni sahihi. Katiba Mpya ya nchi gani?
 

Katiba ya Zanzibar baada ya marekebisho ya 2010..........

Zanzibar ni nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na visiwa vidogo vidogo vilivyoizunguka bahari yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya watu wa Zanzibar."

Katiba ya 'Jamhuri ya Muungano wa Tanzania' ..........

Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania inapakana nayo.
 
Hakuna tija kuendelea kujadili Muungano....Katiba ndio ya msingi na ndio itaamua yote.....Go back to our major concern...mother of all things is constitution....

:rip:Mijadala inayohusu muungano.............

Wtg wamesha amka sasa. wazenj ltakula kwenu!
Serkali1 au Muungano wa kisanii ufilie mbali!
 
Mkuu.
Nimeona waraka wa wanasheria wa "Tanzanaia bara" ambao chama chao wanakiita Tanganyika law society.
Hawa watu wangeweza kutoa ushauri mzuri kwa serikali kama wangekuwa wanajiuliza masuali kama haya unayoyauliza hapa ,mkuu.

Mkuu, mimi kwa mtazamo wangu katiba ya muungano ilipaswa kujadiliwa baada ya kuujadili muungano na muundo wake.
kwa sababu muungano huu haujawahi kufanyiwa review...na malalamiko yamekuwa yakiongezeka kila jua linapochomoza.

Lakini mkuu. mimi pia siamini kama Tanzania ni nchi moja....kama ni nchi moja kwa nini waliunganisha baadhi ya mambo tu?
Lakini pia kwa nini ilikubaliwa ziwepo serikali mbili? na mamlaka tatu za kisheria?
It was a false start at the very beginning.

Halafu pia kwa nini tuliacha kutumia Tanganyika wakati Zanzibar wanatumia jina hili kabla ya muungano na baada ya muungano?

Ukipitia hoja ya wanasheria wetu..(wewe ni mmoja wao?). Kipengele hiki:-



6. Kuhusu kifungu cha 6 cha Muswada - Uteuzi wa wajumbe wa Tume: Chama kinatoa maoni na mapendekezo yafuatayo:
  • Uwakilishi katika Tume: Muswada unapendekeza Tume iwe na uwakilishi wa Tanzania Bara na Visiwani kwa idadi sawa. Lakini kifungu hiki hakizingatii hata kidogo tofauti ya ukubwa wa idadi ya watu na kwamba Katiba ya Muungano inahusika na Zanzibar pale tu masuala ya Muungano yanapotajwa. Hivyo basi, ili kuhakikisha kuna uwiano stahikikatika Tume (yaani unaozingatia sura halisi ya mambo), idadi ya wajumbe kutoka Tanzania Bara na kutoka Visiwani izingatie idadi ya watu.
Wanaonekana kuogopa kusema kuna mambo mengi ya Tanganyika ndani ya katiba ya Muungano. Na hivyo baada ya kushauri iwepo pia katiba ya Tanganyika na Katiba ya Muungano seperate wanajiuma ulimi...au ndio unafiki tunaousemea hapa?

Na kipengele hiki:-

11. Kuhusu vipengele visivyoruhusiwa kuguswa – Kifungu cha 9 (2) na 20 (1):
Muswada unafanya vipengele vya msingi vinavyohusu ibara za msingi za Katiba visiguswe. Kwa mfano, kif. 9 (2) kinataka mambo ya Muungano na suala la ofisi ya Rais, mambo yote mawili ambayo yaliyowekwa na Katiba, yasiguswe. Kif. 20 (1) kinakinzana na Ibara 26(2) ya Katiba ambayo inalinda haki ya mwananchi kupinga uhalali wa kikatiba wa sheria za nchi. Kuviacha vifungu vibaki pia ni kukiuka utekelezaji wa Utawala wa Sheria.

Ingawaje wanasema vipengele vinakizana wao kama washauri wameshauri nini?

Kwa nini waweke lugha ya mzunguko.
Waseme wazi tu kama muungano ni off limit basi ni kuwa tutapata katiba mpya bomu, hovyo.
Na hivyo wangeshauri muswada uingize majadiliano ya muungano na Muundo wake. Huu sio wakati wa kufunika kombe, tunapoweka,tunapoficha uchafu chini ya zulia, tutapata madhara na maafa siku za mbele.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...fa-ya-dharura-juu-ya-muswada-wa-katiba-4.html
 
umesoma baba big up,kimeeleweka hapa
Mkuu.
Nimeona waraka wa wanasheria wa "Tanzanaia bara" ambao chama chao wanakiita Tanganyika law society.
Hawa watu wangeweza kutoa ushauri mzuri kwa serikali kama wangekuwa wanajiuliza masuali kama haya unayoyauliza hapa ,mkuu.

Mkuu, mimi kwa mtazamo wangu katiba ya muungano ilipaswa kujadiliwa baada ya kuujadili muungano na muundo wake.
kwa sababu muungano huu haujawahi kufanyiwa review...na malalamiko yamekuwa yakiongezeka kila jua linapochomoza.

Lakini mkuu. mimi pia siamini kama Tanzania ni nchi moja....kama ni nchi moja kwa nini waliunganisha baadhi ya mambo tu?
Lakini pia kwa nini ilikubaliwa ziwepo serikali mbili? na mamlaka tatu za kisheria?
It was a false start at the very beginning.

Halafu pia kwa nini tuliacha kutumia Tanganyika wakati Zanzibar wanatumia jina hili kabla ya muungano na baada ya muungano?

Ukipitia hoja ya wanasheria wetu..(wewe ni mmoja wao?). Kipengele hiki:-



6. Kuhusu kifungu cha 6 cha Muswada - Uteuzi wa wajumbe wa Tume: Chama kinatoa maoni na mapendekezo yafuatayo:

  • Uwakilishi katika Tume: Muswada unapendekeza Tume iwe na uwakilishi wa Tanzania Bara na Visiwani kwa idadi sawa. Lakini kifungu hiki hakizingatii hata kidogo tofauti ya ukubwa wa idadi ya watu na kwamba Katiba ya Muungano inahusika na Zanzibar pale tu masuala ya Muungano yanapotajwa. Hivyo basi, ili kuhakikisha kuna uwiano stahikikatika Tume (yaani unaozingatia sura halisi ya mambo), idadi ya wajumbe kutoka Tanzania Bara na kutoka Visiwani izingatie idadi ya watu.
Wanaonekana kuogopa kusema kuna mambo mengi ya Tanganyika ndani ya katiba ya Muungano. Na hivyo baada ya kushauri iwepo pia katiba ya Tanganyika na Katiba ya Muungano seperate wanajiuma ulimi...au ndio unafiki tunaousemea hapa?

Na kipengele hiki:-

11. Kuhusu vipengele visivyoruhusiwa kuguswa – Kifungu cha 9 (2) na 20 (1):
Muswada unafanya vipengele vya msingi vinavyohusu ibara za msingi za Katiba visiguswe. Kwa mfano, kif. 9 (2) kinataka mambo ya Muungano na suala la ofisi ya Rais, mambo yote mawili ambayo yaliyowekwa na Katiba, yasiguswe. Kif. 20 (1) kinakinzana na Ibara 26(2) ya Katiba ambayo inalinda haki ya mwananchi kupinga uhalali wa kikatiba wa sheria za nchi. Kuviacha vifungu vibaki pia ni kukiuka utekelezaji wa Utawala wa Sheria.

Ingawaje wanasema vipengele vinakizana wao kama washauri wameshauri nini?

Kwa nini waweke lugha ya mzunguko.
Waseme wazi tu kama muungano ni off limit basi ni kuwa tutapata katiba mpya bomu, hovyo.
Na hivyo wangeshauri muswada uingize majadiliano ya muungano na Muundo wake. Huu sio wakati wa kufunika kombe, tunapoweka,tunapoficha uchafu chini ya zulia, tutapata madhara na maafa siku za mbele.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...fa-ya-dharura-juu-ya-muswada-wa-katiba-4.html
 
Naona unafikiria kinyume hakuna nchi ya Zanzibar wala Tanganyika kuna nchi ya Tanzania!!!!. Inabidi tuache kuishi kwa ndoto!
 
Tuache unafiki kwa hili, katiba ile ambayo mimi hivi sasa naiita ya zamani haikuwa na kitu japo tumefika nayo hapa ni kwa fikra za mwenyekiti tu..

SIKU ZOTE MIMI HUSEMA SIO RAIA WA TANZANIA MIMI NI MATANGANYIKA HALISI
 
Nonda,

Nakubaliana na wewe kabisa. Nimeusoma. Kuna kila sababu ya kuacha kung'ata maneno. Zanzibar ina Sheria zake. Ina mipaka yake. Hakuna nchi, mkoa, wilaya, kata, kijiji, mtaa unaoitwa Tanzania Visiwani.
 
Mkuu.
Nimeona waraka wa wanasheria wa "Tanzanaia bara" ambao chama chao wanakiita Tanganyika law society.
Hawa watu wangeweza kutoa ushauri mzuri kwa serikali kama wangekuwa wanajiuliza masuali kama haya unayoyauliza hapa ,mkuu.

Mkuu, mimi kwa mtazamo wangu katiba ya muungano ilipaswa kujadiliwa baada ya kuujadili muungano na muundo wake.
kwa sababu muungano huu haujawahi kufanyiwa review...na malalamiko yamekuwa yakiongezeka kila jua linapochomoza.

Lakini mkuu. mimi pia siamini kama Tanzania ni nchi moja....kama ni nchi moja kwa nini waliunganisha baadhi ya mambo tu?
Lakini pia kwa nini ilikubaliwa ziwepo serikali mbili? na mamlaka tatu za kisheria?
It was a false start at the very beginning.

Halafu pia kwa nini tuliacha kutumia Tanganyika wakati Zanzibar wanatumia jina hili kabla ya muungano na baada ya muungano?

Ukipitia hoja ya wanasheria wetu..(wewe ni mmoja wao?). Kipengele hiki:-



6. Kuhusu kifungu cha 6 cha Muswada - Uteuzi wa wajumbe wa Tume: Chama kinatoa maoni na mapendekezo yafuatayo:
  • Uwakilishi katika Tume: Muswada unapendekeza Tume iwe na uwakilishi wa Tanzania Bara na Visiwani kwa idadi sawa. Lakini kifungu hiki hakizingatii hata kidogo tofauti ya ukubwa wa idadi ya watu na kwamba Katiba ya Muungano inahusika na Zanzibar pale tu masuala ya Muungano yanapotajwa. Hivyo basi, ili kuhakikisha kuna uwiano stahikikatika Tume (yaani unaozingatia sura halisi ya mambo), idadi ya wajumbe kutoka Tanzania Bara na kutoka Visiwani izingatie idadi ya watu.
Wanaonekana kuogopa kusema kuna mambo mengi ya Tanganyika ndani ya katiba ya Muungano. Na hivyo baada ya kushauri iwepo pia katiba ya Tanganyika na Katiba ya Muungano seperate wanajiuma ulimi...au ndio unafiki tunaousemea hapa?

Na kipengele hiki:-

11. Kuhusu vipengele visivyoruhusiwa kuguswa ¨C Kifungu cha 9 (2) na 20 (1):
Muswada unafanya vipengele vya msingi vinavyohusu ibara za msingi za Katiba visiguswe. Kwa mfano, kif. 9 (2) kinataka mambo ya Muungano na suala la ofisi ya Rais, mambo yote mawili ambayo yaliyowekwa na Katiba, yasiguswe. Kif. 20 (1) kinakinzana na Ibara 26(2) ya Katiba ambayo inalinda haki ya mwananchi kupinga uhalali wa kikatiba wa sheria za nchi. Kuviacha vifungu vibaki pia ni kukiuka utekelezaji wa Utawala wa Sheria.

Ingawaje wanasema vipengele vinakizana wao kama washauri wameshauri nini?

Kwa nini waweke lugha ya mzunguko.
Waseme wazi tu kama muungano ni off limit basi ni kuwa tutapata katiba mpya bomu, hovyo.
Na hivyo wangeshauri muswada uingize majadiliano ya muungano na Muundo wake. Huu sio wakati wa kufunika kombe, tunapoweka,tunapoficha uchafu chini ya zulia, tutapata madhara na maafa siku za mbele.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...fa-ya-dharura-juu-ya-muswada-wa-katiba-4.html
Swali: Ni kwa namna gani Serikali ya Tanganyika ndani ya Muungano itatuondolea ufisadi, umaskini, maradhi, ujinga, kutujengea shule, kutujengea zahanati/hospitali, kutupunguzia vifo vya mama wajawazito, kutulindia raslimali zetu dhidi ya wageni, kupunguza division 0 za f4, etc? Just let me know, au tunataka tuheshimu Wajerumani walioianzisha Tanganyika ambayo hata hivyo ilijumuisha Rwanda na Burundi? Only that? Kwa nini tusiheshimu kile tulichokitengeneza wenyewe? Mbona Zanzibar ya 1600s ilijumuisha mikoa ya Pwani na Morogoro? Nini "faida" ya kutengana anyway? Au watz wanataka vyeo tu, eti mimi Rais wa Tanganyika! Dhambi ya ubaguzi itauua Muungano, Tanganyika itakayozaliwa na hata Zanzibar!
 
Zidumu fikra za Mwenyekiti.

Nimeona ni vyema nikaanza na salamu hiyo kwa sababu kuu moja, fikra za Mwenyekiti, Marehemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere zimedumu kwa muda mrefu hatimaye tumefika mahali sasa hali si hali na wote tunajidai kushangaa yanayotokea.

Ni kwa bahati mbaya sana fikra zake zimeendelea kutuongoza mpaka leo. Huko alipo ameendelea kutuangalia jinsi ambavyo tumezivaa fikra zake kama NIRA na naamini amekuwa akitushangaa kwa nini tumeshindwa kuendeleza pale alipoachia yeye.

Binafsi nampongeza Mwenyekiti kwa jambo kubwa moja, kuweza kufikiri na kutekeleza kile alichofikiri. Pia aliweza kuaminisha umma kwamba alichofikiri ni bora kwa ustawi wa umma. Kwa sasa hivi sina wa kumpongeza kwa kufikiri na kutekeleza anachofikiri.

Lakini, fikra zake na utekelezaji wake una mambo mengi tu. Mabaya na Mazuri. Kwa wale ambao bado wanamuamini hata katika kifo mabaya ni hakuna. Kama yapo hayakuwa yake.

Ila, nina machache ya kuweka hapa jamvini.

Kuna mama mmoja ameshitaki viongozi wa kijiji fulani. Viongozi hawa walikuwa ni wajumbe wa kamati ya ugawaji ardhi miaka ya 1970 wakati wa Operation Vijiji. ardhi yake iligawanywa kwa wanakijiji wengine. Baada ya miaka zaidi ya 15 akafungua kesi. Anadai ardhi yake. Kwenye ardhi hiyo leo kuna shule mbili, makanisa mawili, kaya zaidi ya 500, barabara ya umma, dispensary. Mama huyo alishinda kesi!!! Dalali akaenda kukamata mali wananchi wakaja juu.......Operesheni Vijiji/Ujamaa na Kujitegemea.

Mpaka leo hii bado Katiba yetu inasema;


KWA HIYO, BASI, KATIBA HII IMETUNGWA NA BUNGE MAALUM LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, kwa niaba ya Wananchi, kwa madhumuni ya kujenga jamii kama hiyo, na pia kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Tanzania
inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia na ujamaa.

SURA YA KWANZA
JAMHURI YA MUUNGANO, VYAMA VYA SIASA,WATU NA SIASA YA UJAMAA NA
KUJITEGEMEA

Lengo la Katiba hii ni kuwezesha ujenzi wa Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar au wa
chochote kati ya vyombo vyake na udugu na amani kutokana na kufuata siasa ya Ujamaa na Kujitegemea, ambayo inasisitiza
utekelezaji wa misingi ya kijamaa kwa kuzingatia mazingira yaliyomo katika Jamhuri ya Muungano. Kwa hiyo, Mamlaka ya
Nchi na vyombo vyake vyote vinawajibika kuelekeza sera na shughuli zake zote katika lengo la kuhakikisha-

Fikra za Mwenyekiti zimeendelea kudumu mpaka leo. Hakuna anayethubutu kuzigusa. Eti bado ni 'nchi' ya kijamaa. Sawa.

Haya, hilo tuache. Kuna hili la Zanzibar na Tanganyika. Alifanya kazi kubwa kuziunganisha nchi mbili ili ziwe nchi moja. Wote tukaamini amefanikiwa na sisi ni wamoja. Tuliamini fikra zake. Hakuna aliyehoji kwa sauti.

Kwa miaka yote Katiba yetu inasema;

1. Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano.


Kwenye utangulizi tukatamka kwa sauti;

KWA KUWA SISI Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani:


Hapa sisi ni Watanganyika na Wazanzibari! Tuliamini hivyo.

Lakini, Wazanzibari wakaendelea na maisha yao. Wakiamini kwamba wanaonewa na kudharauliwa. Hii si kweli. Wanaonewa na nani?? Wameijenga 'nchi' katika misingi ya uhuru, haki, udugu na amani?

Hilo si la msingi kwa sasa. Tunagalie walichokuwa wanafikiria na kutekeleza.

Katiba ya Zanzibar inasema;

(9)(i) Zanzibar itakuwa ni NCHI ya kidemokrasia na haki za kijamii.

(9)(2)(a) Mamlaka ya kuendesha NCHI ni ya wananchi wenyewe …

(10) Kwa madhumuni ya kuendeleza umoja na maendeleo ya watu na ustawi wa jamii katika NCHI itakuwa ni wajibu wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar:

(10)(3) Itadhibiti uchumi wa NCHI kufuatana na misingi na madhumuni yaliyoelezwa na katiba hii.

(12)(3) Haki za raia, wajibu na maslahi ya kila mtu yatalindwa na kuamuliwa na mahkama pamoja na vyombo vya NCHI na vinginevyo vilivyowekwa na sheria.

(21)(i) Kila Mzanzibari anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa NCHI…

(23)(2) Kila mtu ana wajibu wa kulinda maliasili ya Zanzibar, mali ya NCHI pamoja na mali yote inayomilikiwa kwa pamoja na wananchi…

Kwa hiyo basi, Tanzania sio nchi moja kama tulivyokuwa tunaamini. Ni dhahiri hatukuungana kama nchi moja. Zanzibar ilibaki kuwa nchi. Wazanzibari waliendelea kuishi kama nchi muda wote mpaka leo.

Je, sisi wengine nchi yetu ni ipi? Tanganyika iko wapi? Zanzibar ina bendera, raisi, baraza la wawakilishi, vikosi vyake vya ulinzi nk. Sisi?

Kama wao wana maisha yao na nchi yao iweje wanatuchagulia Raisi? Je inawezekanaje raia wa nchi nyingine achague Raisi wa 'nchi' nyingine? Sawa sheria zinaruhusu hilo, je sheria hizo ziko sawa? Na sheria kuu iko sawa?

Sheria Kuu (KATIBA) inatamka kwamba Tanzania ni nchi moja. Katiba ya Zanzibar amabyo nayo ni Sheria Kuu inatamka Zanzibar ni nchi. Sasa hapa ipi ni nchi na ipi si nchi? Hii yote ilianzia kwa Mwenyekiti......MUUNGANO!

Imani yetu imetuponza au imetuponya?

Basi nimalizie na swali, Je Wazanzibari wanashiriki kwenye mchakato wa Katiba Mpya kama raia/wananchi wa nchi gani?? Tanzania au Zanzibar? Sifa ya kushiriki utungaji wa Katiba ni lazima uwe raia wa nchi. Nchi haipo, raia hawapo!

ZIDUMU FIKRA ZA MWENYEKITI. KISIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI.

Kama koloni la Tanganyika! Nchi inabaki kuwa nchi hata ikiwa chini ya utawala na hilo ndilo lilioko hapa. Ni sawasawa na Jumuiya ya Kifaransa na makoloni yake wakati ule.
 
Only 83,

Sawa, je Katiba ipi sasa? ya Jamhuri ya Muungano au ya Tanganyika? Kuwa wazi na useme unachofikiria au unachoamini ni sahihi. Katiba Mpya ya nchi gani?

Ni Katiba ya ukoloni wa Tanganyika juu ya Zanzibar. Wakoloni siku zote hupanga katiba yao na kuyafanya makoloni kufuata na kwa mchongo huu wa kutoshirikishwa hali inakuja hivyohivyi ya ukoloni.
 
Mtoa mada unaonekana kuelewa kwa yale unayotaka kuyafahamu.

Nashinwa kuelewa kwanini huna hayo majibu ya maswali yako?

UNAULIZA"Kwa hiyo basi, Tanzania sio nchi moja kama tulivyokuwa tunaamini. Ni dhahiri hatukuungana kama nchi moja. Zanzibar ilibaki kuwa nchi. Wazanzibari waliendelea kuishi kama nchi muda wote mpaka leo.

Je, sisi wengine nchi yetu ni ipi? Tanganyika iko wapi? Zanzibar ina bendera, raisi, baraza la wawakilishi, vikosi vyake vya ulinzi nk. Sisi?

Kama wao wana maisha yao na nchi yao iweje wanatuchagulia Raisi? Je inawezekanaje raia wa nchi nyingine achague Raisi wa 'nchi' nyingine? Sawa sheria zinaruhusu hilo, je sheria hizo ziko sawa? Na sheria kuu iko sawa?

Sheria Kuu (KATIBA) inatamka kwamba Tanzania ni nchi moja. Katiba ya Zanzibar amabyo nayo ni Sheria Kuu inatamka Zanzibar ni nchi. Sasa hapa ipi ni nchi na ipi si nchi? Hii yote ilianzia kwa Mwenyekiti......MUUNGANO!

Imani yetu imetuponza au imetuponya?

Basi nimalizie na swali, Je Wazanzibari wanashiriki kwenye mchakato wa Katiba Mpya kama raia/wananchi wa nchi gani?? Tanzania au Zanzibar? Sifa ya kushiriki utungaji wa Katiba ni lazima uwe raia wa nchi. Nchi haipo, raia hawapo! "MWISHO.

HIVVYO HUJAJUA TU KUA MULIDANGANYWA NA NYERERE?

TANZANIA HAIWEZI KUA NCHI MOJA.NI NCHI MBILI ZILIZOUNGANA,TENA NI KWA BAADHI YA MAMBO TU.

Nadhani hili ndio tatizo watanganyika wengi hawajui kua Zanzibar haikuungano na Tanganyika kwa kila kitu.na ndio maana wamegoma kuichangia katiba mpya kwa kua Hairuhusu kujadili Muungano sasa kilicho wakutanisha wazanzibari ndani ya katiba hile ni nini? kama si muungano?
Kwabahati mbaya Tanganyika ilijigeuza kua ndio muungano,ndio ukakuta watu wanahoji uwepo wa wazanzibari ndani ya Serekali ya Muungano lakini sio Watanganyika ndani ya serekali ya SMZ.
Watanganyika mungalikua na serekali ya Tanganyika wazanzibari wasingalishiriki ila mulijifunika shuka la muungano ndio tatizo lilipo anzia.
Mukafanya Tanganyika ndio Muungano na Muungano ndio Tanganyika ndio ukaona hamuna majibu ya maswali yenu leo.
 
Nonda,

Nakubaliana na wewe kabisa. Nimeusoma. Kuna kila sababu ya kuacha kung'ata maneno. Zanzibar ina Sheria zake. Ina mipaka yake. Hakuna nchi, mkoa, wilaya, kata, kijiji, mtaa unaoitwa Tanzania Visiwani.

So what? Why bothering with nomenclature? Let them call whatever names they want, let them legislate in whatever manner they want, provided that they concur with the Articles of the Union, it doesn't add or remove anything potential!
 

Katiba ya Zanzibar baada ya marekebisho ya 2010..........

Zanzibar ni nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na visiwa vidogo vidogo vilivyoizunguka bahari yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya watu wa Zanzibar."

Katiba ya 'Jamhuri ya Muungano wa Tanzania' ..........

Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania inapakana nayo.

Hali hapa ndiyo ileile ya ukoloni na kama nilivyokwishasema Wakoloni walikuwa wakitambua mipaka ya makoloni yao na ndio maana mipaka ya Kenya, Uganda, Tanganyika na Zanzibar ilikuwa ikitambuliwa na Muingereza ndani ya himaya yake ya nchi za Afrika Mashariki.
 
Vueni Nguo ya Muungano mutapata majibu ya maswali yenu?

Kama ingalikueko Tanganyika wazanzibari wasingewesa kuwachagulia Ras lakini mulipo jivalisha koti la muungano ndio wazanzibari wakalazimika kuwachagulia viongozi kwa sababu Muungano unawahusu.
 
Ni Katiba ya ukoloni wa Tanganyika juu ya Zanzibar. Wakoloni siku zote hupanga katiba yao na kuyafanya makoloni kufuata na kwa mchongo huu wa kutoshirikishwa hali inakuja hivyohivyi ya ukoloni.

Ibara gani ya Katiba inayotaja mambo ya ukoloni? Na unavyodai kushirikishwa kuko kwa aina mbili kwa Zanzibar: 1. Ndani ya Bunge la Muungano Wazanzibari wamo na pia, wanaweza kukataa kwa mujibu wa Ibara ya 98 ya Katiba ya JMT, 2. Ndani ya BLW Muswada unaweza usiridhiwe kutumika Zanzibar and it becomes the end of the story! Usiweke dhana ambayo haipo!
 
Mkuu.
Nimeona waraka wa wanasheria wa "Tanzanaia bara" ambao chama chao wanakiita Tanganyika law society.
Hawa watu wangeweza kutoa ushauri mzuri kwa serikali kama wangekuwa wanajiuliza masuali kama haya unayoyauliza hapa ,mkuu.

Mkuu, mimi kwa mtazamo wangu katiba ya muungano ilipaswa kujadiliwa baada ya kuujadili muungano na muundo wake.
kwa sababu muungano huu haujawahi kufanyiwa review...na malalamiko yamekuwa yakiongezeka kila jua linapochomoza.

Lakini mkuu. mimi pia siamini kama Tanzania ni nchi moja....kama ni nchi moja kwa nini waliunganisha baadhi ya mambo tu?
Lakini pia kwa nini ilikubaliwa ziwepo serikali mbili? na mamlaka tatu za kisheria?
It was a false start at the very beginning.

Halafu pia kwa nini tuliacha kutumia Tanganyika wakati Zanzibar wanatumia jina hili kabla ya muungano na baada ya muungano?

Ukipitia hoja ya wanasheria wetu..(wewe ni mmoja wao?). Kipengele hiki:-



6. Kuhusu kifungu cha 6 cha Muswada - Uteuzi wa wajumbe wa Tume: Chama kinatoa maoni na mapendekezo yafuatayo:
  • Uwakilishi katika Tume: Muswada unapendekeza Tume iwe na uwakilishi wa Tanzania Bara na Visiwani kwa idadi sawa. Lakini kifungu hiki hakizingatii hata kidogo tofauti ya ukubwa wa idadi ya watu na kwamba Katiba ya Muungano inahusika na Zanzibar pale tu masuala ya Muungano yanapotajwa. Hivyo basi, ili kuhakikisha kuna uwiano stahikikatika Tume (yaani unaozingatia sura halisi ya mambo), idadi ya wajumbe kutoka Tanzania Bara na kutoka Visiwani izingatie idadi ya watu.
Wanaonekana kuogopa kusema kuna mambo mengi ya Tanganyika ndani ya katiba ya Muungano. Na hivyo baada ya kushauri iwepo pia katiba ya Tanganyika na Katiba ya Muungano seperate wanajiuma ulimi...au ndio unafiki tunaousemea hapa?

Na kipengele hiki:-

11. Kuhusu vipengele visivyoruhusiwa kuguswa – Kifungu cha 9 (2) na 20 (1):
Muswada unafanya vipengele vya msingi vinavyohusu ibara za msingi za Katiba visiguswe. Kwa mfano, kif. 9 (2) kinataka mambo ya Muungano na suala la ofisi ya Rais, mambo yote mawili ambayo yaliyowekwa na Katiba, yasiguswe. Kif. 20 (1) kinakinzana na Ibara 26(2) ya Katiba ambayo inalinda haki ya mwananchi kupinga uhalali wa kikatiba wa sheria za nchi. Kuviacha vifungu vibaki pia ni kukiuka utekelezaji wa Utawala wa Sheria.

Ingawaje wanasema vipengele vinakizana wao kama washauri wameshauri nini?

Kwa nini waweke lugha ya mzunguko.
Waseme wazi tu kama muungano ni off limit basi ni kuwa tutapata katiba mpya bomu, hovyo.
Na hivyo wangeshauri muswada uingize majadiliano ya muungano na Muundo wake. Huu sio wakati wa kufunika kombe, tunapoweka,tunapoficha uchafu chini ya zulia, tutapata madhara na maafa siku za mbele.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...fa-ya-dharura-juu-ya-muswada-wa-katiba-4.html


Nonda nami niliposoma hayo maoni ya Wanasheria kitu cha mwanzo kilichonifungua macho kilikuwa hicho cha uwakilishi. Nashangaa kama wanasharia wanakuwa namna hivi sisi wa" Madrasat" tutakuwa vipi?
Unaposema eti kuna watu wengi na hivyo vitu vingi na kutaka uwakilishi mkubwa jee wakati yakizungumzwa mambo yanayowahusu hao kidogo (Zanzibar) huo wingi wa upande wa walio wengi (Tanganyika) utakaa upande kwa vile linalozungumzwa ni la walio kidogo?
Hapana bali njia rahisi ni kama unavyosema ni kila mmoja aunde Katiba yake na baadae kuwe na Katiba ya mambo ya pamoj.

Hili la wanasheria linareflex mtizamo halisi wa wengi wa upande wa Tanganyiika na kwa vile upande wa pili una msimamo tofauti, kinachoonyesha hapa ni ukweli kuwa hata siku moja hatuwezi kuendelea na mfumo wa sasa wa Muungano.
 
Mtoa mada unaonekana kuelewa kwa yale unayotaka kuyafahamu.

Nashinwa kuelewa kwanini huna hayo majibu ya maswali yako?

UNAULIZA"Kwa hiyo basi, Tanzania sio nchi moja kama tulivyokuwa tunaamini. Ni dhahiri hatukuungana kama nchi moja. Zanzibar ilibaki kuwa nchi. Wazanzibari waliendelea kuishi kama nchi muda wote mpaka leo.

Je, sisi wengine nchi yetu ni ipi? Tanganyika iko wapi? Zanzibar ina bendera, raisi, baraza la wawakilishi, vikosi vyake vya ulinzi nk. Sisi?

Kama wao wana maisha yao na nchi yao iweje wanatuchagulia Raisi? Je inawezekanaje raia wa nchi nyingine achague Raisi wa 'nchi' nyingine? Sawa sheria zinaruhusu hilo, je sheria hizo ziko sawa? Na sheria kuu iko sawa?

Sheria Kuu (KATIBA) inatamka kwamba Tanzania ni nchi moja. Katiba ya Zanzibar amabyo nayo ni Sheria Kuu inatamka Zanzibar ni nchi. Sasa hapa ipi ni nchi na ipi si nchi? Hii yote ilianzia kwa Mwenyekiti......MUUNGANO!

Imani yetu imetuponza au imetuponya?

Basi nimalizie na swali, Je Wazanzibari wanashiriki kwenye mchakato wa Katiba Mpya kama raia/wananchi wa nchi gani?? Tanzania au Zanzibar? Sifa ya kushiriki utungaji wa Katiba ni lazima uwe raia wa nchi. Nchi haipo, raia hawapo! "MWISHO.

HIVVYO HUJAJUA TU KUA MULIDANGANYWA NA NYERERE?

TANZANIA HAIWEZI KUA NCHI MOJA.NI NCHI MBILI ZILIZOUNGANA,TENA NI KWA BAADHI YA MAMBO TU.

Nadhani hili ndio tatizo watanganyika wengi hawajui kua Zanzibar haikuungano na Tanganyika kwa kila kitu.na ndio maana wamegoma kuichangia katiba mpya kwa kua Hairuhusu kujadili Muungano sasa kilicho wakutanisha wazanzibari ndani ya katiba hile ni nini? kama si muungano?
Kwabahati mbaya Tanganyika ilijigeuza kua ndio muungano,ndio ukakuta watu wanahoji uwepo wa wazanzibari ndani ya Serekali ya Muungano lakini sio Watanganyika ndani ya serekali ya SMZ.
Watanganyika mungalikua na serekali ya Tanganyika wazanzibari wasingalishiriki ila mulijifunika shuka la muungano ndio tatizo lilipo anzia.
Mukafanya Tanganyika ndio Muungano na Muungano ndio Tanganyika ndio ukaona hamuna majibu ya maswali yenu leo.

Huu Muungano wetu mbona bomba tu wandugu? Mbona mnapenda sana kuchonga?
 
Back
Top Bottom