Ripoti ya Mwakyembe: Nia, madhumuni, utekelezaji, dharau, kejeli, kutokujali na usahaulifu!

Albert Msando

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
1,019
171
Baada ya Ndugu Bashir Mrindoko kuteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu nimelazimika kuazima andiko la MwanaJF mmoja alipotaka kutukumbusha jambo. Jambo hilo sio lingine ila ripoti ya Mwakyembe (MB) ambayo naamini kwa kiasi fulani ilisaidia sana yeye kuteuliwa kuwa Naibu Waziri kwani ripoti hiyo pamoja na mamabo mengine ilionyesha ni mtendaji kazi mzuri.

Kinachonishangaza ni pale ambapo maazimio ya ripoti hayo yanapokuwa hayana maana, yanadharaulika, yanakejeliwa na yanaonekana yamesahaulika. Ilianza kwa Hosea ikapita, ameendelea kushikilia nafasi yake. Sasa hivi imekuja kwa Ndugu Mrindoko, amepewa cheo.

Hii ni nini? Huyu bwana kama alionewa na tume ya Mwakyembe amewahi kusafishwa? Kama hakukosea je ni hatua zipi zimechukuliwa kumsafisha au ndio anasafishwa kwa kupewa cheo?

Ina maana ilikuwa lazima sana yeye ndie ashike nafasi hiyo? Hakukuwa na mtu mwingine na hakuna mtu mwingine yeyote msafi zaidi yake, mwenye uwezo zaidi yake ndani ya nchi hii?

Kwa kweli kuna maammuzi yanafanyika unabaki mdomo wazi. Kinachouma zaidi ni pale ambapo hakuna cha kufanya zaidi ya kuumia rohoni. Natamani uteuzi kama huu ungekuwa unathibitishwa na Bunge. Ila napata faraja unaweza kuhojiwa na Bunge kwa sababu ripoti hiyo ilitokana na Bunge. Hii ni dharau na kejeli kwa Bunge.

Namtakia kazi njema Ndugu Mrindoko, Mh. Mwakyembe na Mheshimiwa Raisi

AZIMIO NAMBA 14:


"Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Ibrahim Msabaha (Mb.), na Katibu Mkuu, Ndugu Arthur Mwakapugi wachukuliwe hatua kali za kinidhamu kwa kuliingiza Taifa kwa makusudi kwenye Mkataba wa Kampuni ya Mfukoni. Aidha, Kamishna wa Nishati, Ndugu Bashir Mrindoko naye achukuliwe hatua za kinidhamu kwa kushindwa kumshauri Katibu Mkuu wake mpya kuhusu udhaifu wa Richmond Development Company LLC ambao ulijulikana dhahiri na Wizara mwaka 2004 kwenye Mradi wa bomba la mafuta. Ndugu Mrindoko ndiye aliyeiandikia barua Kampuni hiyo kusitisha Mkataba wake na Serikali mwezi mmoja tu kabla ya mchakato wa Zabuni ya umeme wa dharura haujaanza."

Mungu ibariki na uilinde Tanzania.
 
Msando, kama sikosei Tume ya Mwekyembe ilitoa mapendekezo si chini ya 18. Na Prime Minister- Mizengo Pinda went on record kusema kuwa Serikali watayafanyia kazi kama ambavyo Bunge limeazia na kutoa report baada ya miezi kadhaa.

So far, bunge halijapewa taarifa yoyote kama alivyoahadi Waziri mkuu!. Madhara yake ni kwamba Bunge kama mhimili wa dola linapoteza hadhi yake pale linaposhindwa ama kwa kutojali au kwa ushabiki wa ki-itakadi kufuatilia maazio yake yenyewe.
 
Msando, kama sikosei Tume ya Mwekyembe ilitoa mapendekezo si chini ya 18. Na Prime Minister- Mizengo Pinda went on record kusema kuwa Serikali watayafanyia kazi kama ambavyo Bunge limeazia na kutoa report baada ya miezi kadhaa.

So far, bunge halijapewa taarifa yoyote kama alivyoahadi Waziri mkuu!. Madhara yake ni kwamba Bunge kama mhimili wa dola linapoteza hadhi yake pale linaposhindwa ama kwa kutojali au kwa ushabiki wa ki-itakadi kufuatilia maazio yake yenyewe.

FJM, je ahadi ya Waziri Mkuu ndio inatekelezwa sasa hivi kwa kuwapa baadhi ya waliotajwa vyeo? Na je Bunge halitahoji hili? Kama litahoji au halitahoji ni haki yetu wananchi kuhoji.

Tukiendelea hivi ipo siku tutapigana.

Jiulize mtu ambaye amekuwa mtumishi serikalini miaka nenda rudi leo hii anaona mwenzake ambaye ametuhumiwa anapewa cheo wakati yeye yupo.

Hata kama alisingiziwa basi juhudi zingefanyika umma ujue kwamba hakuwa mkosaji na anastahili kushika nafasi hiyo. Huo ndio uongozi bora. Kinachotokea sasa hivi wengi tunaona hastahili sio kwa sababu tunamjua utendaji wake bali mazingira ya uteuzi wake.
 
Tusubirini hadi 2015 ndo tutapata bunge siyo hili la sasa! Bunge letu= Serikali yetu= Mahakama zetu, hakuna wa kumhoji mwenzake zaidi ya kupeana nini cha kufanya kupindisha kanuni, utendaji na sheria za nchi.

We (Wazalendo) just need to be more smart than these people who think they own this country.
 
Tusubirini hadi 2015 ndo tutapata bunge siyo hili la sasa! Bunge letu= Serikali yetu= Mahakama zetu, hakuna wa kumhoji mwenzake zaidi ya kupeana nini cha kufanya kupindisha kanuni, utendaji na sheria za nchi.
We (Wazalendo) just need to be more smart than these people who think they own this country.

RedDevil, ina maana viongozi wetu wanafanya anachofanya 'avatar' yako?
 
Bado tupotupo tunajivua magamba..................muwe wavumilivu mtafurahi tu! Mambo mazuri hayataki haraka
 
Ujinga uliopindukia, upumbavu wa kimaksudi, na kiwango kidogo cha kufikiria ndo kilimchompelekea muhusika kumchagua huyo mwehu
 
FJM, je ahadi ya Waziri Mkuu ndio inatekelezwa sasa hivi kwa kuwapa baadhi ya waliotajwa vyeo? Na je Bunge halitahoji hili? Kama litahoji au halitahoji ni haki yetu wananchi kuhoji.

Tukiendelea hivi ipo siku tutapigana.

Jiulize mtu ambaye amekuwa mtumishi serikalini miaka nenda rudi leo hii anaona mwenzake ambaye ametuhumiwa anapewa cheo wakati yeye yupo.

Hata kama alisingiziwa basi juhudi zingefanyika umma ujue kwamba hakuwa mkosaji na anastahili kushika nafasi hiyo. Huo ndio uongozi bora. Kinachotokea sasa hivi wengi tunaona hastahili sio kwa sababu tunamjua utendaji wake bali mazingira ya uteuzi wake.
Msando tuko pamoja kwenye huu mshangao.

Na niseme tu nchi hii bado inaendeshwa kwa 'mazoea' kwamba kashfa inatokea, tume inaundwa kuchunguza kashfa, report inapelekwa kwa wakubwa ambao bila haya watatuambia serikali itayafanyia kazi mapendekezo ya tume! Tofauti kwenye hii tume ya Mwakyembe ni kwamba Bunge nalo linaonekana kupalilia hii 'culture' ya kutowajibika.

Binafsi nadhani muda umefika kwa sisi wananchi tuanze kuwahoji wabunge wetu wanapokuwa kwenye majimbo juu ya mambo muhimu kama hili la maazimio ya tume ya Mwakyembe.
 
RedDevil, ina maana viongozi wetu wanafanya anachofanya 'avatar' yako?

avatar15498_6.gif
RedDevil, ina maana viongozi wetu wanafanya anachofanya 'avatar' yako?
100% correct,lets wait what those in the so called Mjengo has to say!
 
Msando tuko pamoja kwenye huu mshangao.

Na niseme tu nchi hii bado inaendeshwa kwa 'mazoea' kwamba kashfa inatokea, tume inaundwa kuchunguza kashfa, report inapelekwa kwa wakubwa ambao bila haya watatuambia serikali itayafanyia kazi mapendekezo ya tume! Tofauti kwenye hii tume ya Mwakyembe ni kwamba Bunge nalo linaonekana kupalilia hii 'culture' ya kutowajibika.

Binafsi nadhani muda umefika kwa sisi wananchi tuanze kuwahoji wabunge wetu wanapokuwa kwenye majimbo juu ya mambo muhimu kama hili la maazimio ya tume ya Mwakyembe.

I agree 100%. Kwa sasa hivi Mbunge hawezi kuhojiwa mpaka aitishe mkutano wa hadhara. Kwenye mkutano wa hadhara majibu yake ni yakubaisha tu hayana mshiko wowote.

Ni vizuri tukapendekeza utaratibu gani utumike kuwawajibisha wabunge na madiwani kwenye majimbo na kata zao baada ya uchaguzi.
 
Kama ilipendekezwa hatua za kinidhamu zichukuliwe lakini badala yake mtu anapewa unaibu katibu mkuu.

Sishangai tena kwa nini Raisi alienda kufungua hoteli halafu kesho yake asubuhi ikavunjiwa ukuta. Nilikuwa nashangaa, hajaelezwa kuhusu ubomoaji? Hakujua imeingilia hifadhi ya barabara?
 
Anichague mimi kufanya nini ambacho hao waliochaguliwa wanaenda kufanya? Nadhani wewe ungefaa zaidi. Kwa michango yako naona kua kipaji kinapotea
 
Bado hawajajua gamba ni nini! Gamba ni kichwa hivyo wanaogopa wakitoa kichwa chama kitakufa. Hawa wasichaguliwe tena. Natamani kama 2015 ingekuwa leo. Kweli wangekoma.
 
Kwa maoni yangu ni dharau kwa kamati ya Bunge na Bunge lililoridhia maazimio ya kamati.

Hii ndiyo Tanzania ya CCM, wale wanaofanya vibaya wanazawadiwa na waadilifu wanawekwa kando.... so chaotic!
 
Mtemi,

Ni kweli kabisa uteuzi kama huo ni dharau kwa Bunge na watanzania kwa ujumla. Imefika mahali viongozi hawajali maoni wala mawazo ya wananchi. Wanajiona wao ndio watawala na wanaweza kuamua lolote bila kuhojiwa.
 
Mimi namuomba Mheshimiwa Dr. Mwakyembe ajiudhulu huo unaibu waziri; kuonyesha KUPINGA hiyo dharau kubwa ilyoonyeshwa kwake na mkuu wakeJK.
 
Hawezi,bado anaangalia tumbo lake kwanza. Pale waliingilianaga maslahi tu

CCM haina wapiganaji wa ukweli
 
Back
Top Bottom