" Sio Kwamba Sisikii , Wala Sio Kwamba Siambiwi Yanayosemwa ! Sio Kwamba Siwezi Kusema Au Sina La Kusema Laasha ! Sijafanya Hivyo Kwasababu Sioni Faida Yake " Mh. Jakaya Mrisho Kikwete Rais Mstaafu Wa Awamu Ya Nne.


Ongeza nukuu za mzee wetu huyu mstaafu katika kiti cha urais JMT.
FB_IMG_1566471369220.jpeg
 
  1. “Chochote ambacho akili ya binadamu inaweza kuumba na kufikiri, inaweza kukikamilisha pia.”
    Napoleon Hill
  2. “Njia ya kuanza ni kuacha kuzungumza na kuanza kutenda.”
    Walt Disney
  3. “Usiruhusu jana itawale sana leo.”
    Will Rogers
  4. “Kama unafanyia kazi kitu kinachokusisimua na unachokijali kweli, hauhitaji kusukumwa. Maono yako yatakusukuma.”
    Steve Jobs
  5. “Kufahamu haitoshi, ni lazima tuweke kwenye matendo, Kutamani haitoshi, ni lazima tufanye.”
    Johann Wolfgang
  6. “Tunatengeneza hofu tunapokaa bila kufanya kitu. Tunaishinda hofu kwa matendo.”
    Dr. Henry Link
  7. “Ikiwa unafikiri unaweza au huwezi, uko sahihi.”
    Henry Ford
  8. “Mtu mwenye kujiamini ndani yake, anapata kujiamini kwa wengine.”
    Hasidic Proverb
  9. “Fanya kile unachoweza kwa vyote ulivyonavyo, popote ulipo.”
    Theodore Roosevelt
  10. “Akili ni kila kitu. Unavyofikiri ndivyo unavyokuwa.”
    Buddha
  11. “Muda mzuri wa kupanda mti ni miaka 20 iliyopita. Lakini muda mwingine mzuri wa pili ni sasa.”
    Chinese Proverb
  12. “Muda wako ni mdogo, usiupoteze kuishi maisha ya mtu mwingine.”
    Steven Jobs
  13. “Kushinda siyo kila kitu, lakini kutaka kushinda ni kila kitu.”
    Vince Lombardi
  14. “Huwezi kuvuka bahari kama huna ujasiri wa kuacha kuona ufukwe.”
    Christopher Columbus
  15. “Kisasi kizuri ni mafanikio makubwa.”
    Frank Sinatra
  16. “Kuna njia moja tu ya kuepuka kukosolewa: usifanye kitu, usiseme kitu na usiwe chochote.”
    Aristotle
  17. “Anzia ulipo. Tumia kile ulichonacho. Fanya kile unachokiweza.”
    Arthur Ashe
  18. “Anguka mara saba simama mara ya nane.”
    Japanese Proverb
  19. “Mlango mmoja wa furaha ukifungwa, mwingine unafunguliwa, lakini mara nyingi tunautazama sana ule uliofungwa na kushindwa kuona ule uliofunguliwa kwa ajili yetu.”
    Helen Keller
  20. “Kila kitu kina uzuri wake, lakini siyo kila mtu anaweza kuuona.”
    Confucius
  21. “Changamoto zinafanya maisha yavutie na kuzishinda ni kufanya maisha kuwa na maana.”
    Joshua J. Marine
  22. “Kama unataka kujiinua mwenyewe juu, mwinue mwingine juu kwanza.”
    Booker T. Washington
  23. “Ili kufanikiwa, shauku yako ya mafanikio ni lazima iwe kubwa kuliko hofu yako ya kushindwa.”
    Bill Cosby
  24. “Kila siku ninajitahidi kufanya vizuri zaidi kuliko nilivyo fanya jana.”
    Reginald Mengi
  25. “Mtu ambaye hajawahi kufanya kosa hajawahi kujaribu kitu chochote.”
    Albert Einstein
  26. “Mtu anayesema hawezi kufanya hatakiwi kumwingilia mtu anayesema ninaweza kufanya.”
    Chinese Proverb
  27. “Haujachelewa kuwa ambaye ungeweza kuwa.”
    George Eliot
  28. “Unakuwa kile unachoamini.”
    Oprah Winfrey
  29. “Jenga ndoto zako wewe mwenyewe, la sivyo mtu mwingine atakuajiri kujenga zake.”
    Farrah Gray
  30. “Ota ndoto kubwa na dhubutu kushindwa”
    Norman Vaughan
  31. “Badili kufikiri kwako na utakuwa umebadili ulimwengu.”
    Norman Vincent Peale
  32. “Andika kitu chenye manufaa kusomwa au fanya kitu chenye manufaa kuandikwa.”
    Benjamin Franklin
  33. “Njia pekee ya kufanya kazi nzuri ni kupenda kile unachokifanya.”
    Steve Jobs
  34. “Ikiwa unaweza kuliota, unaweza kulifanikisha.”
    Zig Ziglar
  35. “Ndoto zetu zote zinaweza kutokea ikiwa tuna ujasiri wa kuzifuata.”
    Wale Disney
  36. “Usilie juu ya kile ambacho huna; tumia vizuri kile ulichonacho.”
    Reginald Mengi
  37. “Mambo mazuri huja kwa watu wanaosubiri, lakini mambo bora huja kwa wale wanaoondoka na kwenda kuayachukua.”
    Hajulikani
  38. “Fursa hazitatokea, unatakiwa kuziunda.”
    Chris Grosser
  39. “Usijaribu kuwa mtu wa mafanikio, bali jaribu kuwa mtu wa thamani.”
    Albert Einstein
  40. “Akili kubwa hujadili mawazo, akili ya wastani hujadili matukio, akili ndogo huzungumzia watu.”
    Eleanor Roosevelt
  41. “Ikiwa hauthamini muda wako, hata wengine hawatauthamini. Acha kupoteza muda na vipaji vyako sasa – anza kuvifanyia kazi”
    Kim Garst
  42. “Mtu mwenye mafanikio ni yule anayeweza kujenga msingi imara kwa kutumia matofali yaliyotupwa na wengine.”
    David Brinkley
  43. “Usiinue sauti yako, boresha hoja yako.”
    Hajulikani
  44. “Ninaamini kwamba ujasiri pekee mtu yeyote anaouhitaji ni ujasiri wa kufuata ndoto zako mwenyewe.”
    Orarah Winfrey
  45. “Fursa zina aibu, zinakusubiri uzikimbilie.”
    Reginald Mengi
  46. “Ubunifu unatofautisha kati ya kiongozi na mfuasi.”
    Steve Jobs
  47. “Hofu ni mojawapo ya adui mkubwa kwa mafanikio.”
    Reginald Mengi
  48. “Wengi wetu hatuishi ndoto zetu kwa sababu tunaishi hofu zetu.”
    Less Brown
  49. “Hatua ya mwanzo ya mafanikio yoyote ni matamanio.”
    Napoleon Hill
  50. “Baadaye inamilikiwa na wale wote wanaoamini kwenye uzuri wa ndoto zao.”
    Eleanor Roosevelt
 
  1. “Ni bora kushindwa kwenye kitu halisi kuliko kufanikiwa kwenye kitu cha kuiga.”
    Herman Melville
  2. “Njia ya kufanikiwa na barabara ya kushindwa ni sawa kabisa.”
    Colin R. Davis
  3. “Mafanikio huja kwa wale ambao wanafanya bidii kubwa kuyatafuta.”
    Henry David Thoreau
  4. “Usijaribu kuwa mtu wa mafanikio. Bali jaribu kuwa mtu wa thamani.”
    Albert Einstein
  5. “Acha kukimbilia pesa bali anza kukimbilia shauku yako.”
    Tony Hsieh
  6. “Mafanikio ni kupita kutoka aina moja ya kushindwa hadi nyingine bila kukata tamaa.”
    Winston Churchill
  7. “Fanya kitu kimoja kila siku kinachokutisha.”
    Hajulikani
  8. “Ukitazama kwa karibu, mafanikio ya usiku mmoja huchukua muda mrefu.”
    Steve Jobs
  9. “Hakuna siri ya mafanikio, ni matokeo ya maandalizi, kufanya kazi kwa bidii, na kujifunza kutokana na kushindwa.”
    Colin Powell
  10. “Inaonekana mafanikio yameungwa na matendo. Watu waliofanikiwa wanaendelea mbele. Wanafanya makosa lakini hawaachi.”
    Conrad Hilton
  11. “Kama unataka kufanya kitu, utatafuta njia. Kama hutafanya hivyo, utatafuta kisingizio.”
    Jim Rohn
  12. “Siwezi kukupa kanuni ya mafanikio, lakini ninaweza kukupa kanuni ya kushindwa – nayo ni: Jaribu kumridhisha kila mtu.”
    Herbert Bayard Swope
  13. “Mafanikio siyo ufunguo wa furaha. Furaha ni ufunguo wa mafanikio. Kama unapenda unachokifanya, utafanikiwa.”
    Albert Schweitzer
  14. “Mafanikio siyo vitu ulivyokamilisha kwenye maisha yako, bali ni nini ulichowahamasisha wengine kufanya.”
    Hajulikani
  15. “Baadhi ya watu wengine wanaota mafanikio wakati wengine wanaamka na kufanya kazi.”
    Hajulikani
  16. “Mtu mwenye mafanikio ni yule anayeweza kujenga msingi imara kwa kutumia matofali yaliyotupwa na wengine.”
    David Brinkley
  17. “Ili kufanikiwa ni lazima tuamini kuwa tunaweza.”
    Nikos Kazantzakis
  18. “Kushindwa kwingi kwenye maisha ni watu wanaoshindwa kufahamu jinsi walivyo karibu na mafanikio wanapokata tamaa.”
    Thomas Edison
  19. “Mafanikio ni kupata unachotaka, furaha ni kutaka unachopata.”
    Dale Carnegie
  20. “Eneo baya la mafanikio ni kujaribu kutafuta mtu ambaye ana furaha kwa ajili yako.”
    Bette Midler
  21. “Usipoteze muda kupiga ukuta, ukitumaini kuubadili kuwa mlango.”
    Coco Chanel
  22. “Nimefanikiwa leo kwa sababu nilikuwa na rafiki aliyeniamini na sina moyo wa kumwangusha.”
    Abraham Lincoln
  23. “Yote unayohitaji kwenye maisha yako ni ujinga na ujasiri; kisha mafanikio ni hakika.”
    Mark Twain
  24. “Ili kufanikiwa, shauku yako ya mafanikio ni lazima iwe kubwa kuliko hofu yako ya kushindwa.”
    Bill Cosby
  25. “Changamoto kubwa baada ya kufanikiwa ni kunyamaza kuhusu mafanikio hayo.”
    Criss Jami
  26. “Mafanikio hayahusishi kutokufanya kosa bali kutokurudia kosa hilo mara ya pili.”
    George Bernard Shaw
  27. “Mafanikio ni pale ambapo maandalizi na fikra vinakutana.”
    Bobby Unser
  28. “Kila mara kujiamini na bidii kutakupa mafanikio.”
    Virat Kohli
  29. “Mafanikio siyo mwalimu mzuri, kushindwa hukufanya kuwa mnyenyekevu.”
    Shah Rukh Khan
  30. “Kabla ya kitu kingine chochote, maandalizi ni ufunguo wa kufanikiwa.”
    Alexander Graham Bell
 
Back
Top Bottom