Wanawake tujikumbushie vituko vya leba

Wanawake tujikumbushie vituko vya leba

Kwa uchungu ulivyo naupitaga huu uzi km ukoma

Hii ni laana kwa hakika

Hapo kwenye ukali huyo mkeo kama mimi tu nakuwaga kama simba au chui jike hadi kuunguruma huku nikiuma vyuma vya kitanda

Kuna stage manesi wanasema lalia ubavu na pumulia mdomoni wakati huo ukinywa chai ya moto......ebwana ndio
Naonaga hainisaidiii huwa hakuna unafuu jamani
 
Kwa uchungu ulivyo naupitaga huu uzi km ukoma

Hii ni laana kwa hakika

Hapo kwenye ukali huyo mkeo kama mimi tu nakuwaga kama simba au chui jike hadi kuunguruma huku nikiuma vyuma vya kitanda

Kuna stage manesi wanasema lalia ubavu na pumulia mdomoni wakati huo ukinywa chai ya moto......ebwana ndio

Nimekusoma mkuu
 
nakumbuka niliingia leba na mme wangu asa uchungu ulipokolea nikawa kama nataka kuwa chizi
yani namwambia mme wangu nasikia kama nataka kuwehuka basi akaanza maombi yani ile anaaza tu nikambinya mkono adi akatoa sauti nusu anikabe
yani niliona kama ananipigia kelele kisa maombi!
jamani uchungu unauma aisee
baadae nikamwambia kwa nguvu kibofu kinapasukaaaa dk 5 mtoto huyu
sijui kwanini eva alimshawishi adamu wale tunda jamani !popote alipo eva adhabu aongezewe yani moto ukolezwe zaidi
 
Uzi nauogopaga huu hapa nilicomment km mkimbizi as if ni rahisi vile!!
 
Hili ndo jibu lililosababisha niufufue uzi huu

Mtu anabisha eti uchungu hauleti bond kati ya mama na mtoto

Hapo kwenye mtoto akipata tatizo unahisi tumbo kuuma

Mwaka jana mwanangu mdogo alipotea kwenye michezo na wenzie akanogewa mpaka jioni narudi home mtoto hayupo tafuta mtaa mzima sikumpata kigiza kikaanza hata nguvu za kumtafuta sikuwa nazo tumbo likaanza kunitetemeka nilishaanza kupiga na ukunga majirani zangu kama wanne wakaanza kumtafuta ...

Alipatikana mida ya saa mbili na nusu na wenzie kumbe walikuwa wameenda beach kuogelea
Nini zetu walikua wanarudiil mara 12 mama zetu mara nne hadi sita
Wa siku hizi mara moja yenyewe wanaogopaaaa


Pia nimewahi kusikia Maongezi ya watu wazima wamama Maana wako hapa wanaongelea dawa ya kupunguzaa uchungu kuchomwaa mgongoni au kisu

Je kuna tofauti yeyote ya mapenzi kwa mtooto kati ya mama ambaye kajifungua mtoto Ndani ya nusu kaputi yaani hakusikia lolote au kisu na mama Huyu aliyesukuma kwa jasho la damu?

Wamama hawa walikua wakisema ni muhimu Sana kuzaaa Kwa uchungu kama maandiko ilivyosema , kisu kiwe option ya mwisho baada ya kutapatapa
Yale maumivu ndio sadaka na gharama ya kumpata mtoto iweje wamama wa leo wengine wanayakimbia tena makusudiii ??!

Wanasema mama aliyepata uchungu Ana connection Kubwa na mwanaye kama “mungu” na anaweza hata kuhisi jambo haya Kwa mwanaye akiwa mbali Kwa tumbo kuuma , mwanamke aliyepata uchungu akimuona mwanaye anaumia au pengine bahati Mbaya kafariki annapata hisia za uchungu tumboni na ndio maaana anafungwa tumboooo ni kama a nakumbuka uzazi....

Mama aliyepata uchungu hawezi muacha mwanaye akiwa na mwezi na housegal akaenda disco au akalataaa kumnyonyesha
Hata kama Alikuwa kashindikana hatulii Nyumbani hiyo Tabia hupungua kwa kiasi kikubwa
Mama aliyejifungua kwa kisu hataweza kuchangia lolote kwenye Ushujaa wa kinamama hawa japo naye ni mama

Inahimizwa kuwatia Moyo wamama wajawazito wakifungue kwa njia Mungu aliyoagiza kama hawana tatizo la kitabibu linalotishia uhai wake na mtoto
 
WAIFU alinisimulia alivyomkojolea DOKTA...waifu kamwambia dokta mkojo umenibana,dokta akamwambia hapa huendi chooni Kojoa tukuone...WAIFU AKALIACHIA KOJO KOOOOO
 
Ni kweli lakini inataka mjasiri yaani moyo mgumu kama wa jiwe wanawake wote hatuna hiyo

Kuna mmoja alizalishwa na mtawa wakati wa uchungu ilibidi amuulize mtawa, hivi na nyie huwa mkizaa mnaumwa hivi kama mimi,,,, ukumbuke mtawa hawazai
Wengi ni videko na wabishi hawataki kuwasikiliza maelekezo ya wakunga!
Ukishaangia leba kanuni ni moja tu fanya kila atakachokwambia mkunga huku ukimuomba Mungu wako kimoyomoyo !

Ukifanya hivyo hutachelewa nakwambia Mungu anakufanyia wepesi ajabu!
Unapopiga Makelele hayakusaidii na unajichelewesha mwenyewe!
 
Hili ndo jibu lililosababisha niufufue uzi huu

Mtu anabisha eti uchungu hauleti bond kati ya mama na mtoto
NI KWELI KABISA KABISA KABISA mwanamke aliezaa na uchungu hata malezi ya mwanae ni tofauti na ya mama aliezaa kwa kisu..Nimelishuhudia hilo kwa macho yangu mawili ya nyama.

Mke wangu mtoto wa kwanza alijifungua kwa kisu...ki ukweli mwanangu yule nilikua namhangaikia mimi kiasi kwamba hadi nikawa nahisi huyu mke wangu WALINIBADILISHIA HOSPITALI NINI mbona hamjali mtoto kabisa? Basi nikapuuzia kwakua muda mwingi waifu anakaa na mtoto nkajua anakua anachoka na yeye so haikunipa shda kumuhudumia mwanangu.

Afya ya mwanangu wa kwanza haiku vile nitakavyo,mtoto akikataaa kula mke wangu hamlazimishi kula yani anaishi na mtoto the way mtoto anavyotaka...bhas miaka ikaenda kwa shda ivyo ivyo had mtoto amekua na sasa ana afya nzuri maana anakula mwenyewe nk.

MTOTO WA PILI WAIFU KAJIFUNGUA KWA UCHUNGU

Jamani Jamani Jamani sijawahi kuona upendo na caring ile ya uzazi aliyokua nayo mke wangu kwa mtoto,ki ukweli mtoto wangu wa pili anapendwa na mke wangu hadi mi namwambiaga ukweli BABE HUYU MTOTO UNAMPENDA BWANA basi ananijibu simple "HUJUI MAUMIVU YA UCHUNGU WEWE" natamanigi nimrudishie jibu moja hilooooo Sema namstahi namwachaga.

so kusema ukweli mwanamke zaaa kwa UCHUNGU tu...najua ina uma lakini kama unataka mtoto wako umpende 100+100+100% zaa kwa uchungu...Kuzaa kwa opareshen tusidanganyane MAMA atakua na upendo lakini nasema hiviiiii upendo wa MAMA kwa mtoto wake aliemzaa kwa oparesheni Unapitwa na upendo wa BABA kwa mtoto.

nina uhakika asilimia 100000 mimi nampenda first born wangu kuliko mke wangu anavyompenda...na hii ni sababu first born alikuja kwa kisu...ila nina uhakika 100000 pia mke wangu anampenda sec born wangu kunipita hata mimi hilo nakiri kwakweli.
 
Fika leba kaka ndo utajua nini wanawake tunapitia

Mkeo ni bahati yake tu wapo wasioumwa uchungu ule mkali upo wa kawaida na upo komesha yenyewe na wa muda mrefu na kuna tofauti kati ya uchungu wa mtoto wa kike na wa kiume....wa kike nasikia unazidi wa kiume
nyie nashangaa mnalalamika uchungu mtoto mwenyewe wa kwanza,mi wife kajifungua watoto wa3 kwa mpigo yuko kawaida tu,hongera sana msambaa wangu
 
Morogoro Hosp nikienda kujifungua pale, ukilia unapigwa kama mtoto, wale waupe mpaka wa napata wekundu kwa makofi. Mi hawakunipiga ila waliniulia mtoto.


Unanyanyaswa mpaka unaona hiki nini,,,sitasahau pale uchungu umekolea naambiwa nenda kafate dawa nje( sikujua kumbe wanataka rushwa) nikaanza kutambaa kwenda( kumbuka sakafu ya leba na serikalini uchafu wake) nilipofika mlangoni nikaskia we vipi wewe rudi,,utaendaje sasa


Aiseee I have a tale to tell
Pole sana
 
Manesi wa kike wengi roho mbaya tu, nilizalishwa na mwanaume nzao ya pili kwa huduma alonipa nakuhakikishia dunia ingeshajaa hii
Kuna watu wanapenda kesi balaa, hata ukimtazama anaweza kukushtaki. Manesi hutoa maneno ya kebehi ili uwahi kujifungua.
 
Aisee pole tena kwa mara nyingine

Story km yangu ya first born,, huyo nesi shombo zake km nilizopewa mimi, nilisaidiwa na mfanya usafi tu, nilikuwa nimezungukwa na wakunga wanne wote wanaogopa kunigusa kwa hofu ya kuwafia mikononi mwao ndipo huyo mfanya usafi kuingia akakuta nahaha nguvu sina uchungu unapoa na mtoto hajatoka, akavaa gloves na kunibinya chini ya kifua kwa nguvu mtoto akatoka,

Alilia kidogo tu ilikuwa asubuhi alikuja kulia tena usiku saa tatu ni wazi nilimtolea padogo tu ....angekufa,,,
Sasa hiyo trela,,,kuna kubwa mbili ndo nikikumbuka naliaga tuu

Ntakusimulia moja.
Unajua uzazi wa kwanza unakua hujui vitu ,,sasa ikafika muda nimeshikwa haja ndogo lakini haitoki,( naskia mtoto anaweza gandamiza pale kwenye kibofu)kila nikienda haja haitoki,,nikaanza kuhisi maumivu makali sana,,nikaita nesi,,akaja kwa ukali,, nini?? Nikamwambia nesi tangia Jana usiku sijakojoa mkojo hautoki ( tangia SAA mbili usiku mpaka saa mbili asbh) akanambia pumbavu wewe kwa hiyo Mimi Nije kukukojolesha Nina kazi zangu usiniite ,,akaondoka. Kufika saa NNE nikaona kama sasa nakufa,, kama nataka kupasuka,,nikaita kwa yowe kubwa kwa uchungu sana,,,nilikua na mwenzangu mmoja( tuliweka chumba chetu Tulikua na pressure) akaita nesi njoo naye akawa anaogopa akajua nakufa,nesi akaja nikamwambia tena akafyonza akaondoka, ,Bahati muda ule kuna kijana wa field akapita ( Mungu ambariki aliko) nikamwambia akasema nipe hela nikanunulie mpira nje,,akaja akaniwekea ,,yani pale pale kifuko kikajaaa,,akasema Dada ulikua unapasuka kibofu,,SITASAHAU ,,,
 
Samahani ila wengi huumia tu kwa kutojua matumizi sahihi ya midomo yao,ukijua nesi ana frastresheni zake wala hupati taabu.!utajua namna gani useme naye na kauli nzuri hulainisha moyo mgumu.
Ni jukumu lao mbona wakunga wa kiume au wa kike ambae hajazaa huwa na huruma na wanatimiza majukumu yao pasipo tatizo lolote?
 
Hospital za serikali nyingi huduma ni hizo sio huko moro tu mpaka inaonekana kama kuzaa salama ni muujiza kumbe sio
Badae nilikuja kuanza kuhisi labda ni mawakala wa mashetani, ,sio kawaida,, ingawa Morogoro Hosp hayo mambo ni kawaida sana
 
Mimi nilivyofika Leba ,nikapelekwa sehemu ya mapumziko walikuwepo wajawazito wengii,sasa uchungu ulikuwa haujanishika kivile nilikuwa natokwa na maji tu, daktari akanipima akasema bado,,sasa mle kwenye ukumbi kulikuwa na wamama wengi mwingine anaruka, mwingine anajivuta vuta chini, si nikaanza kuwacheka nikasema mbona mimi siumwii.

kKumbe bana uchungu unakuja taratibu, nikawa nashangaa kila muda unavyozidi kwenda maumivu yananizidia wale niliokuwa nawacheka wao wanajifungua wananiacha tu, kukakucha asubuhi niliona ni mwaka na nikasema sirudiii ,kama nilikuwa natembea uchungua ukaja ghafla naganda kama sanamu kama kuna mti ntaung'ang'ania kweli, ilifikia muda sitaki kuja kusalimiwa wala kuonwa na mtu yeyote maana watu wanavyozidi kuja kuniona ndivyo uchungu unazidi kuwa mkali nikawazuia.

Niliita majina yote ya Mungu nikawa namshika mama yangu namuambia aniombee haraka uchungu upoe kiuno changu kilikuwa cha moto nauchukua mkono wa mama nauweka kiunoni kwangu namwambia aniombee mama yangu mpaka alilia nilivyokuwa nahangaika nyie acheni jamani.

Usiku ulipofika saa 2 nikasikia kusukuma nikapelekwa chumbani nimefika kule kila nikisukuma hola,,wakaniwekea maji ya uchungu wapiii wakasema huyu anatakiwa kisu tu nikajitahidi kusukuma wakaja madaktari na manesi wamenizunguka mwingine kanishika kichwa ,mwingine tumbo anabinya,mwingine anaangalia njia ya mtoto (sitasahau)mtoto alitoka saa 8 nanusu kuamkia tarehe 8 na mwaka ....8 loo kazi niliipata

Sasa najiuliza wanaozaa watoto 7 au 8 wanawezaje?maana mim toka nizae sina hamu tena halaf sijawah pata maumivu kama yale toka nizaliwe sema na ukweli
Mama Aheshimiwe ,maana wanaume wangepewa huu uchungu hata dakika wangeukataa na wangetuheshimu sana
Nimecheka huku nakuona huruma sana aise, nimepara pic wife alivyoteseka kunizalia vidume vyangu viwili! Pole na hongera,
 
huu ndo ujinga wenyewe!
manesi wanahitajika kubadilika we unaleta maombi!!.. ni mara ngapi watu wameshaliombea taifa lakini hayo maombi hayafui dafu..?
inatakiwa tuishi maisha ya kweli si kuimagine!,unatenda hivi unadhibitiwa ili usitende si hizi lomolomo.. kuna mwanamke kakomenti kuwa ilikuwa amebakiza kidogo tu kibofu kipasuke,asingekuja huyo kijana akamtibia hicho kibofu kingelipona?
hayo mambo ya maombi watz tufute kichwani huo si uhalisia,we need to change our way,we will get changes.
Yawezekana maombi ndiyo yalimleta huyo kijana aliyetoa msaada acha watu waabudu kwa imani zao kuzaa ni kujitoa uhai maana yake kifo kinakuwa karibu,,, acheni waombe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom