Wanawake tujikumbushie vituko vya leba

Wanawake tujikumbushie vituko vya leba

Mi niliwekewa kidonge cha uchungu siku moja kabla ya due date. Nikawaaga rafiki zangu wale wa karibu kuwa naenda labor. Basi kila mara namuuliza nurse saa ngapi dawa itareact maana nilikua nishachoka nataka tu nimuone mtoto.

Niliwekewa saa saba mchana. Nikala mchana kama kawaida yangu nikawa busy nachat mwenyewe kwenye groups. Mama angu alikuwepo akakaa mpaka saa moja na nusu akasema ngoja arudi nyumbani akaniandalie chakula cha kesho asubuhi kama itakua sijajifungua.

Mama alivyotoka tu kule wodini nikaanza kusikia kama tumbo la period. Nakumbuka nilikua nimevaa wig nimepaka na lipstick mwenyewe. Mara nikawa sielewi elewi. Akaja nurse nikamwambia naumwa tumbo halafu kama najisikia kwenda kujisaidia haja kubwa. Akaniambia vua nguo zako jifunge tenge. Ile kujifunga tenge ndo kama nilimzindua huyu mkurya tumboni. Kutoka ward kwenda labor ni kama hatua kumi tu. Kufika nikakuta mama mtu mzima nae anasubiri kujifungua. Sasa nikaanza kutapika. Nikaanza kulia. Nikatupa wig kule maana niliona linanibana. Nilisali baba yetu mara kumi kumi. Nilikua nashikilia kitanda siachii. Nilijuta majuto yote. Nilijuta kwanini sikutoa mimba tu kuliko shida ninazopata. Nilijuta kuumwa mwanamke. Nilifikia hatua naomba Mungu anichukue tu kuliko maumivu ninayopitia.

Manurse walikoma na mimi mpaka wananiuliza mzigua gani muoga hivyo. Nilikua kiuno kikikaza sana nawaita wakija wanasema njia bado. Yule mama niliemkuta leba nikamuuliza mtoto wake wa ngapi yule anasema eti wa nne. Nikawa namuuliza unawezaje kuzaa watoto wote hao na maumivu yote haya. Ikafikia point wakanihamishia kitanda cha kujifungulia sasa.

Kitendo cha kutoka kitanda nilicholala mwanzo mpaka kitanda cha kujifungulia niliona ni kama natoka Dar Moro kwa miguu japo ilikua ni kitanda cha tatu toka nilipokua. Nikaishiwa nguvu. Nikawekewa dripu. Sasa mkono niliokua nautumia kujisugua kiuno ukawa umewekwa dripu. Nikaambiwa nikae pozi moja tu. Pale ndo nikazidisha sala za Mungu kunichukua duniani.

Hapo nishajaribu kupush kama mara nne hamna kitu. Nurses wakatoka nje wakaniambia nikijisikia haja nijisaidie tu. Sijui nilijuaje muda umefika ila niliita kwa sauti manesi kuja wakasema sasa tayari anza kupush. Hapo nimeshakata tamaa ya kuishi mmoja akawa amekaa anasubiri mtoto atoke mwingine akawa anamsukuma tumboni anamleta chini.
Mungu wa ajabu sana the moment mtoto ametoka maumivu yote yalikata.

Hata wakati wa kushonwa nyuzi wala sikuogopa sana na uoga wangu wote. Huyu mtoto mzuri nilie nae hapa nikimuangalia naona yale maumivu ya leba ni sawa tu kama nilipitia kumpata malaika mzuri hivi. Wanaume wangejua tunachokipitia leba wangetuheshimu sana.
Siyo kuwa hatuyajui wengine tunawasaidia kupokea vitoto vyenu cha msingi acheni vituko acheni kabisa

Kama uliweza kupanua mapaja usindweje kupushi tu
 
Na ulivyo na kidomo hahahaha watakupiga masingi mpaka uchukie dudu haahahh nakutania tu mdogo wangu mzuri mzuri

Ni kawaida usiogope sana sie si unaona tumo tunachekelea na mbwembwe zote hizo hapa natamani kupata kichanga
Jamani mpaka nimeogopa.... Uwiiii sijui itakuwaje mwaka wa mimi kuingia huko nadhani manesi watanipiga makofi
 
mnaogopa kuzaa lakin cha ajabu amuachi kunaniii na akina nanii.

Alafu sahiv amuna wanawake kuna wasanii tu....zamani ndo kulikuepo wanawake wa ukweli kama Mama Yangu
Maana wanawake wasahivi kutwa mnawaza nanii .
Hiki ni kitu gani
Kuna hakim alipeleka mke wake kujifungua general hospital, mkewe alikuwa headmistress shule moja, basi kampeleka usiku hadi asubuhi hajajifungua, mida ya saa nne akaenda na mkate na chai, akakuta mambo yamepamba moto. Ilr anaingia tu mke kusikia sauti ya mumewe akaanza kuporomosha matusi ya nguon akaona haitoshi akatoka uschi wa mnyama na mfagio anataka ampige mh. Hakimu hadi getini. Ndo mara ya kwanza naona mwanamke akiwa uchi, nlikiwa formfour
 
Mimi nilivyofika Leba ,nikapelekwa sehemu ya mapumziko walikuwepo wajawazito wengii,sasa uchungu ulikuwa haujanishika kivile nilikuwa natokwa na maji tu, daktari akanipima akasema bado,,sasa mle kwenye ukumbi kulikuwa na wamama wengi mwingine anaruka, mwingine anajivuta vuta chini, si nikaanza kuwacheka nikasema mbona mimi siumwii.

kKumbe bana uchungu unakuja taratibu, nikawa nashangaa kila muda unavyozidi kwenda maumivu yananizidia wale niliokuwa nawacheka wao wanajifungua wananiacha tu, kukakucha asubuhi niliona ni mwaka na nikasema sirudiii ,kama nilikuwa natembea uchungua ukaja ghafla naganda kama sanamu kama kuna mti ntaung'ang'ania kweli, ilifikia muda sitaki kuja kusalimiwa wala kuonwa na mtu yeyote maana watu wanavyozidi kuja kuniona ndivyo uchungu unazidi kuwa mkali nikawazuia.

Niliita majina yote ya Mungu nikawa namshika mama yangu namuambia aniombee haraka uchungu upoe kiuno changu kilikuwa cha moto nauchukua mkono wa mama nauweka kiunoni kwangu namwambia aniombee mama yangu mpaka alilia nilivyokuwa nahangaika nyie acheni jamani.

Usiku ulipofika saa 2 nikasikia kusukuma nikapelekwa chumbani nimefika kule kila nikisukuma hola,,wakaniwekea maji ya uchungu wapiii wakasema huyu anatakiwa kisu tu nikajitahidi kusukuma wakaja madaktari na manesi wamenizunguka mwingine kanishika kichwa ,mwingine tumbo anabinya,mwingine anaangalia njia ya mtoto (sitasahau)mtoto alitoka saa 8 nanusu kuamkia tarehe 8 na mwaka ....8 loo kazi niliipata

Sasa najiuliza wanaozaa watoto 7 au 8 wanawezaje?maana mim toka nizae sina hamu tena halaf sijawah pata maumivu kama yale toka nizaliwe sema na ukweli
Mama Aheshimiwe ,maana wanaume wangepewa huu uchungu hata dakika wangeukataa na wangetuheshimu sana
Pole my love ulivyoelezea nimeyahisi maumivu yake
 
yani wewe mwanamke umenitoa machozi na umenifurahisha pia,all an all natamani sana kuitwa mama
Mmmhh shikamooh mama mie nilivyoenda leba nasikia nilisema "uwiii wanaume wote wafe" manesi wakanijibu afe wa kwangu tu maana waume zao bado wanawapenda hahahhaha sitaki kusikia leba maana akili haikuwa yangu mweehh shkamooh mama
 
Naona Nyie amjui maumivu ya kuumia zile kengele zetu mbili..napita tu
 
Kuna dada alikuwa anatukana balaa huku anaita manesi wampe maji ya kunywa,hakuna aliekuwa anamjali..Alimaliza matusi yote.Nilikuwa na uchungu lkn matusi ya yule dd yalinivunja mbavu.Ilipofika zamu yangu sasa ya kujifungua mwili hauna nguvu .mapigo ya moyo yako juu,jasho,machozi na kamasi vilitoka kwa wakati mmoja.

Nilisali sala zote za kiroma na kiluther zooote nikazimaliza.Nilikosa nguvu kbs kiasi cha kushindwa ku-push na kichwa cha mtt kilianza kuonekana lakini nguvu sina.Ilifika wakt nika-give up kabisa nikaanza kunyoosha miguu nikamuambia nesi"Nesi siwezi tena"
Nesi alinisihii kujitahidi otherwise mtoto atakufa kwa kukosa hewa na kunywa maji machafu..Nilishindwa kabisa ilibidi nesi aongeze njia na nilijifungua mtt mrembo sana wa kilo 4.This time nililia machozi ya furaha na kumshukuru Mungu.
 
Tuongeze mtoto mmoja basi
Kuna dada alikuwa anatukana balaa huku anaita manesi wampe maji ya kunywa,hakuna aliekuwa anamjali..Alimaliza matusi yote.Nilikuwa na uchungu lkn matusi ya yule dd yalinivunja mbavu.Ilipofika zamu yangu sasa ya kujifungua mwili hauna nguvu .mapigo ya moyo yako juu,jasho,machozi na kamasi vilitoka kwa wakati mmoja.

Nilisali sala zote za kiroma na kiluther zooote nikazimaliza.Nilikosa nguvu kbs kiasi cha kushindwa ku-push na kichwa cha mtt kilianza kuonekana lakini nguvu sina.Ilifika wakt nika-give up kabisa nikaanza kunyoosha miguu nikamuambia nesi"Nesi siwezi tena"
Nesi alinisihii kujitahidi otherwise mtoto atakufa kwa kukosa hewa na kunywa maji machafu..Nilishindwa kabisa ilibidi nesi aongeze njia na nilijifungua mtt mrembo sana wa kilo 4.This time nililia machozi ya furaha na kumshukuru Mungu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom