Wanawake tujikumbushie vituko vya leba

Wanawake tujikumbushie vituko vya leba

Hakuna,, havihusiani.kuna Dada niliyekua naye,,alikua na tumbo limekaa km Chungu afu liko juu halijashuka na siku zimefika,,waliitana wanacheka njooni muone tumbo gani hili,,,tumbo kibuyu,,aisee nilijionea maajabu ya dunia,,,
Jamani poleni. Mnahaki ya kuwafichua hawa
 
Asee wahanga poleni sana kwa kweli.....
Kweli cc wababa wa baadae tujpange na wake zetu tuone hii changamoto tunaikabili VP...

Ahsanten kwa kufunguka..wenye stories pia wekeni...we learn a lot from you

[HASHTAG]#thanksJF[/HASHTAG]
 
Naomba nichangie hivi.
Ktk HOSPITALI ZA SERIKALI
-Kumuwajibisha muhudumu wa afya ni long process
-Hakuna hasara ambayo kituo husika kitapata kwa wewe kuto enda kupata huduma pale.
-wengi wanao enda hudumiwa katika vituo hivi ni watu wa dalaja la chini hivyo hawana ujasili wa kwashtaki wahudumu hawa.
 
Morogoro Hosp nikienda kujifungua pale, ukilia unapigwa kama mtoto, wale waupe mpaka wa napata wekundu kwa makofi. Mi hawakunipiga ila waliniulia mtoto.


Unanyanyaswa mpaka unaona hiki nini,,,sitasahau pale uchungu umekolea naambiwa nenda kafate dawa nje( sikujua kumbe wanataka rushwa) nikaanza kutambaa kwenda( kumbuka sakafu ya leba na serikalini uchafu wake) nilipofika mlangoni nikaskia we vipi wewe rudi,,utaendaje sasa


Aiseee I have a tale to tell
sad to hear
 
Kama ulikuwa hujui basi chukua hii
Mgonjwa akienda kumshitaki mtoa huduma, yeye husikilizwa zaudi maana ndie mtendewa jambo. Lakini hatakama mtoa huduma hoto fukuzwa kazi kwa mudahu basi huwekwa chini ya uangalizi ili kubaini tabia hiyo kama anayo hivyo hawezi rudia kufanya vitendo viovu akijua atanyang'anywa leseni.
 
Da!! Mie nkikumbuka niliteseka acha kabsa , nlkua na mapacha wakiume, mmoja akatoka ametanguliza miguu na mwingine mkono, ila wapili akafariki, pindi hajatoka wapl nilhis kufa, yaan mpka Leo hii Picha ya mtoto yule haijafutika machoni najitahid kumtoa akilin nashindwa
 
Najua picha haidanganyi sasa bora wangenipa wote nikawazike maana wife aliishiwa nguvu hata hakujielewa but am sure hawakunipa mtoto mmoja though wanadai alikuwa mmoja ila taarifa za picha walizoandika ktk kadi ziliendelea kuwaumbua.
Ipo siku Mungu ataonekana.
pole sana mkuu,

I can feel how unaumia!, hakika Mungu naamini kuna jambo atafanya ndani ya maisha yako.
 
Naomba nichangie hivi.
Ktk HOSPITALI ZA SERIKALI
-Kumuwajibisha muhudumu wa afya ni long process
-Hakuna hasara ambayo kituo husika kitapata kwa wewe kuto enda kupata huduma pale.
-wengi wanao enda hudumiwa katika vituo hivi ni watu wa dalaja la chini hivyo hawana ujasili wa kwashtaki wahudumu hawa.
unaposema ni watu wa daraja la chini hivyo hawawezi kuwashitaki unamaanisha nini mkuu? je kuna freedom of expression hapo?
 
Sasa hiyo trela,,,kuna kubwa mbili ndo nikikumbuka naliaga tuu

Ntakusimulia moja.
Unajua uzazi wa kwanza unakua hujui vitu ,,sasa ikafika muda nimeshikwa haja ndogo lakini haitoki,( naskia mtoto anaweza gandamiza pale kwenye kibofu)kila nikienda haja haitoki,,nikaanza kuhisi maumivu makali sana,,nikaita nesi,,akaja kwa ukali,, nini?? Nikamwambia nesi tangia Jana usiku sijakojoa mkojo hautoki ( tangia SAA mbili usiku mpaka saa mbili asbh) akanambia pumbavu wewe kwa hiyo Mimi Nije kukukojolesha Nina kazi zangu usiniite ,,akaondoka. Kufika saa NNE nikaona kama sasa nakufa,, kama nataka kupasuka,,nikaita kwa yowe kubwa kwa uchungu sana,,,nilikua na mwenzangu mmoja( tuliweka chumba chetu Tulikua na pressure) akaita nesi njoo naye akawa anaogopa akajua nakufa,nesi akaja nikamwambia tena akafyonza akaondoka, ,Bahati muda ule kuna kijana wa field akapita ( Mungu ambariki aliko) nikamwambia akasema nipe hela nikanunulie mpira nje,,akaja akaniwekea ,,yani pale pale kifuko kikajaaa,,akasema Dada ulikua unapasuka kibofu,,SITASAHAU ,,,
Dah!nimeskia kulia,Pole sana,pole tena
 
Da!! Mie nkikumbuka niliteseka acha kabsa , nlkua na mapacha wakiume, mmoja akatoka ametanguliza miguu na mwingine mkono, ila wapili akafariki, pindi hajatoka wapl nilhis kufa, yaan mpka Leo hii Picha ya mtoto yule haijafutika machoni najitahid kumtoa akilin nashindwa
Pole sana, na poleni wote mliopitia manyanyaso
 
Morogoro Hosp nikienda kujifungua pale, ukilia unapigwa kama mtoto, wale waupe mpaka wa napata wekundu kwa makofi. Mi hawakunipiga ila waliniulia mtoto.


Unanyanyaswa mpaka unaona hiki nini,,,sitasahau pale uchungu umekolea naambiwa nenda kafate dawa nje( sikujua kumbe wanataka rushwa) nikaanza kutambaa kwenda( kumbuka sakafu ya leba na serikalini uchafu wake) nilipofika mlangoni nikaskia we vipi wewe rudi,,utaendaje sasa


Aiseee I have a tale to tell
Pole Sana, nyie wanawake huwa hampendani, sidhani kama angekuwa nurse mwanaume angefanya hivyo, I hope ulijifungua salama
 
Sasa hiyo trela,,,kuna kubwa mbili ndo nikikumbuka naliaga tuu

Ntakusimulia moja.
Unajua uzazi wa kwanza unakua hujui vitu ,,sasa ikafika muda nimeshikwa haja ndogo lakini haitoki,( naskia mtoto anaweza gandamiza pale kwenye kibofu)kila nikienda haja haitoki,,nikaanza kuhisi maumivu makali sana,,nikaita nesi,,akaja kwa ukali,, nini?? Nikamwambia nesi tangia Jana usiku sijakojoa mkojo hautoki ( tangia SAA mbili usiku mpaka saa mbili asbh) akanambia pumbavu wewe kwa hiyo Mimi Nije kukukojolesha Nina kazi zangu usiniite ,,akaondoka. Kufika saa NNE nikaona kama sasa nakufa,, kama nataka kupasuka,,nikaita kwa yowe kubwa kwa uchungu sana,,,nilikua na mwenzangu mmoja( tuliweka chumba chetu Tulikua na pressure) akaita nesi njoo naye akawa anaogopa akajua nakufa,nesi akaja nikamwambia tena akafyonza akaondoka, ,Bahati muda ule kuna kijana wa field akapita ( Mungu ambariki aliko) nikamwambia akasema nipe hela nikanunulie mpira nje,,akaja akaniwekea ,,yani pale pale kifuko kikajaaa,,akasema Dada ulikua unapasuka kibofu,,SITASAHAU ,,,
Mmmmhhhh!!!! Hizo habari mumeo anazijua sipati Picha ningekuwa mumeo hao manesi wangekuwa kaburini Muda mrefu tu
 
Iliwahi tokea mke wangu kapigwa picha kaambiwa ana mapacha but mwisho wa siku akapewa mtoto mmoja mfu tena kwa ukatili wa hali ya juu.Hadi leo nikiangaliaga ile kadi na mimba ilivyokuwa kubwa na kumtesa hadi namuogesha nakumbuka mengi.Manesi wengine siyo kabisa.Duuuh.
Ulichukua hatua gani???? Ilibidi ule nao sahani moja
 
Da!! Mie nkikumbuka niliteseka acha kabsa , nlkua na mapacha wakiume, mmoja akatoka ametanguliza miguu na mwingine mkono, ila wapili akafariki, pindi hajatoka wapl nilhis kufa, yaan mpka Leo hii Picha ya mtoto yule haijafutika machoni najitahid kumtoa akilin nashindwa
Pole sana aiseee, hospital ya serikali au Private
 
Ulichukua hatua gani???? Ilibidi ule nao sahani moja
Wao wenyewe wakaanza kujifanya kushangaa na kumtupia lawama mtu wa picha lakin akawaambia ana uhakika na majibu yake.Ukweli niliishia kuumia hadi leo sikuchukua hatua yoyote ukizingatia hata pesa nilikuwa sina for that time.
Hiyo hospital inaitwa Igogwe.
 
Pole Sana, mimi pia ni mchanga wa hospitali zetu za serikali. Ila hakikisha kama mkeo ni mjamzito uwe unamweka kwenye maombi Sana. Pia kumbuka kuombea hao watakaomuhudumia mkeo. Ni jambo dogo lakini limetusaidia Sana. Mungu anasikia na atajibu. Usiku mwema.
huu ndo ujinga wenyewe!
manesi wanahitajika kubadilika we unaleta maombi!!.. ni mara ngapi watu wameshaliombea taifa lakini hayo maombi hayafui dafu..?
inatakiwa tuishi maisha ya kweli si kuimagine!,unatenda hivi unadhibitiwa ili usitende si hizi lomolomo.. kuna mwanamke kakomenti kuwa ilikuwa amebakiza kidogo tu kibofu kipasuke,asingekuja huyo kijana akamtibia hicho kibofu kingelipona?
hayo mambo ya maombi watz tufute kichwani huo si uhalisia,we need to change our way,we will get changes.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom