Tofauti kati ya Yesu na Nabii Issa
Kwaio wewe ni Lukwangu? Sasa kuna faida gani ukitumia ID mbili? au ndio ionekane una wafuasi wengi kama kawaida yenu wakiristo 😀 😀 😀
hahaha mimi sio huyo mdau. siwezi kufanya usanii kwenye mambo ya Mungu mkui. Bora nitoke kabisa jukwaa hili kuliko kuwa mnafiki kiasi hicho.
nilikuta notification (Quotes) zaidi ya 12 nikafungua moja baada ya nyingine kwenye tab na kuanza kurespond.
hiyo niliishtukia baada ya kuwa nimeandika nikaona kumbe kuna jamaa mwinhine huyo anakomaa na yeye nikaamua kupotezea.

usihofu sijafikia hatua hizo mkuu, usiwe na wasiwasi wala shaka.
 
Lam yalid walam yulad"HAKUZAA(MUNGU)WALA HAKUZALIWA",unawezaje kumuita mwana wa mungu.
Inamaana mungu alioa?alimtia mimba kwa kumjamii Mariam?hufahamu kuwa Mariam alikuwa bikira?je na sisi ni wana wa mungu?
Mtume, wake zake, rafiki zake wote na waislam wote huitwa kwa ubin Wa baba. Hata wote kwenye taurat,zabur,injil, hakuna anayetumia jina la mama.
Mfano Juma Bin Said.

Kwa nini Sio Issa Bin Yusufu?

Je mnakubali kisirisiri kuwa Yesu ni Mungu aliyekuja kupitia Marian na sip trndo la ndoa kati ya Mariam na Yusufu?


UPDATES
Tumegundua Yesu hakuwa na Baba Binadamu. Tumegundua Yesu hakuanzia Tumboni mwa Mariam ila alipitia Tumboni mwa Mariam. Waislam wako sahihi Kumuita Issa Bin Mariam ila watakuwa sahihi saizi wakimuita Mwana Wa Mungu ambaye ni Mungu.
 
yesu wa biblia nani kakuambia mwana wa mariam anaitwa yesu.....swali ni ili.....mariam alimuita jina gani mwanae namaanisha birth name sio mlilomuita waswahili
Aliitwa Yesu Kristo. Sasa vitabu vya mpinga kristo vilivyokuna miaka zaidi ya 700 baada ya yeye kwenda mbinguni ndio vimekuja na uongo kama ilivyo tabiriwa. Ndio maana mnawaaminisha anaitwa issa tena kazaliwa chini ya mtende.
 
Lam yalid walam yulad"HAKUZAA(MUNGU)WALA HAKUZALIWA",unawezaje kumuita mwana wa mungu.
Inamaana mungu alioa?alimtia mimba kwa kumjamii Mariam?hufahamu kuwa Mariam alikuwa bikira?je na sisi ni wana wa mungu?
Ukiambiwa allah wa quraan ni kajini unabisha. Sasa umeongea pointi gani hapo.
 
Aliitwa Yesu Kristo. Sasa vitabu vya mpinga kristo vilivyokuna miaka zaidi ya 700 baada ya yeye kwenda mbinguni ndio vimekuja na uongo kama ilivyo tabiriwa. Ndio maana mnawaaminisha anaitwa issa tena kazaliwa chini ya mtende.

Kwani hicho Kitabu unachokiamini wewe kimeandikwa miaka mingapi baada Yesu kuondoka?
 
Katika Islam, Yesu anaitwa Issa Bin Maryam kwa sababu hakuwa na 'biological father' na Mungu katika Quran ameamrisha watoto waitwe kwa majina/ubini wa baba zao. Hivyo, kwa kuwa Maryam hakuingiliana na mwanaume yeyote kabla hajamzaa Yesu, nasaba ya Issa inaanzia moja kwa moja kwa Maryam mwenyewe. Isitoshe, ili mtoto azaliwe ni lazima pawepo na muunganiko wa mbegu za uzazi za mwanamke na mwanaume. Kwa muktadha huo, Maryam (kwa uwezo wa Mungu) alizalisha mbegu zote mbili ndani yake. Mbegu ya kiume na kike. Nasisitiza, kwa uwezo wa Mungu. Hivyo, Yesu au Issa kuitwa Issa Bin Maryam maana yake ni kwamba Maryam ni baba na Maryam ni Mama kwa Yesu/Issa.

Ninadhani mojawapo ya malengo ya Mungu kufanya hivyo, ni kuvunja unasaba wa Yesu na Makabila fulani ambayo hayakuwa yametakasika endapo Yesu angezaliwa kwa Maryam kuingiliana na mumewe. Hiyo ni assumption tu ambayo yafaa ichunguze kihistoria ili kujua yule mume wa Maryam, Yusufu, alitokana na kabila gani na kama kabila hilo lilikuwa na historia isiyo nzuri kwa nabii kutokea kwao au la. Nasisitiza tu, hii ni assumption yenye kifaa kuchunguzwa.
Mtume, wake zake, rafiki zake wote na waislam wote huitwa kwa ubin Wa baba. Hata wote kwenye taurat,zabur,injil, hakuna anayetumia jina la mama.
Mfano Juma Bin Said.

Kwa nini Sio Issa Bin Yusufu?

Je mnakubali kisirisiri kuwa Yesu ni Mungu aliyekuja kupitia Marian na sip trndo la ndoa kati ya Mariam na Yusufu?


UPDATES
Tumegundua Yesu hakuwa na Baba Binadamu. Tumegundua Yesu hakuanzia Tumboni mwa Mariam ila alipitia Tumboni mwa Mariam. Waislam wako sahihi Kumuita Issa Bin Mariam ila watakuwa sahihi saizi wakimuita Mwana Wa Mungu ambaye ni Mungu.
 
Yesu hakuumnwa.
Yeye ndiye aliyeumba, na Pasipo yeye Hakikufanyika chochote ambacho kilifanyika Yohana 1:1-3.
Ufunuo 5: mwishoninanaabudiwa na viumne wote wa mbinguni yeye pamoja na ababa Yake.
Mimi nawewe si rahisi kuelewana. Yesu kazaliwa na Mariamu halafu tena unasema yeye ndiye aliyeumba, haieleweki.
 
mitale na midimu


Nnaomba tafsiri ya huu mstari wa biblia...

Zaburi 137:
9 Heri yeye atakayewakamata wadogo wako, Na kuwaseta wao juu ya mwamba
hii zaburi ni ukumbusho wa utumwa wa wayahudi Babeli, na furaha ya maadui zao (Wana wa Edom) walipoona babeli ikiwashughulikia.

Hapa mwisho 8, 9 ni utabiri pia wa mabaya yatakayowapata hao wababeli chini ya mjukuu wa Nebukadneza Belshaza. Kuwa hata wao ubaya waliowatendea watakomeshwa kwa ubaya huohuo na maadui wao wengine. Kumbuka Dola ya Babeli ilidhani itatawala dunia milele lkn mwaka 539 Jeshi la Wairan (Waajemi) chini ya mtawala Masihi kupitia lango la mashariki baada ya Kudivert mto yaliingia babeli siku hiyo mfalme na jeshi wakiwa wamelewa pombe. Ndio Siku aliyopewa Onyo na Dqniel '' Mene mene Tekel na Peresi'' wakaingia na kufanya maangmamizi makubwa na kuchukua utawala wa dunia ya wakati huo.


Wayahudi walijua maana ilikuwa imetabiriwa na Nabii Isaya, Kuwa Koreshi atazaliwa na ataongoza hayo majeshi kuangusha babeli ambayo imetesa watu wa Mungu. Mungu alimgeuza Koreshi kama fimbo ya kuuzima utawwla wa Babeli.

Maneno hayo sio ya Kwanza, ni utimilivu wa maneno hayohayo nabii isaya alotabiri. Isaya 13:16. Hata Koreshi alitabiriwa kabla hata ya Kuzaliwa.

Hizo lugha za fungu la 8,9 ni matukio ya siku ya kuangamia kwa babeli.
Ni huyu Koreshi ndiye aloyetoa tamko la wayahdi watoke utumwani warudi kwao, Baadae amri hiyo ilitekelezwa zamani za mfalme Altashasta.
 
Mimi nawewe si rahisi kuelewana. Yesu kazaliwa na Mariamu halafu tena unasema yeye ndiye aliyeumba, haieleweki.
Kwa Mariam ilikuwa ni njia.
Alikuja Duniani Kupitia njia hiyo sio kwamba alianzia kwa mariam.
Mbona ametoa kauli nyingi kuwa yeye sio wa dunia hii amekuja.
Na alikuwepo hata kabla ya mariam wala bibi yake mariam kuwepo.

'Kabl ya Ibrahim baba yenu kiwako , mimi niko au YHWH, Maana nyingine kabla ya Ibrahim Yeye ni Mungu.
Wayahudi wakataka Kumuua kwa sababu wameona kakufuru kwa kujiita Mungu, Ila Yeye akawaambia mnataka kuniua kwa sababu nimewaambia ukweli?


mkuu Yesu mtamu ukimsoma kwa kutulia
 
Kwa Mariam ilikuwa ni njia.
Alikuja Duniani Kupitia njia hiyo sio kwamba alianzia kwa mariam.
Mbona ametoa kauli nyingi kuwa yeye sio wa dunia hii amekuja.
Na alikuwepo hata kabla ya mariam wala bibi yake mariam kuwepo.

'Kabl ya Ibrahim baba yenu kiwako , mimi niko au YHWH, Maana nyingine kabla ya Ibrahim Yeye ni Mungu.
Wayahudi wakataka Kumuua kwa sababu wameona kakufuru kwa kujiita Mungu, Ila Yeye akawaambia mnataka kuniua kwa sababu nimewaambia ukweli?


mkuu Yesu mtamu ukimsoma kwa kutulia
Je mtu asiye na mwanzo wala mwisho, asiye na baba wala mama mbona hajapewa cheo cha uungu?
 
Hapa hatuna jibu, ngoja tukamuone sheikh Ponda kwa msaada zaidi
 
hajaumba, pasipo Yesu hakikufanyika chochote kilichofanyika mbinguni na duniani.
Miujiza aliyopewa Yesu na Mungu ni pamoja na kuumba ndege kwa idhini ya Mungu, hakujamfanya kuwa Mungu. Kwenye Biblia nzima hakuna sehemu Yesu anasema "Mimi ni Mungu na niabuduni" bali baadhi ya wakristo wanaungaunga aya ili wathibitishe Uungu wa Yesu.
 
Aliitwa Yesu Kristo. Sasa vitabu vya mpinga kristo vilivyokuna miaka zaidi ya 700 baada ya yeye kwenda mbinguni ndio vimekuja na uongo kama ilivyo tabiriwa. Ndio maana mnawaaminisha anaitwa issa tena kazaliwa chini ya mtende.

Yeye mwenyewe kakataza asiitwe Kristo mbona unampakazia Yesu? Au husomi Biblia?
 
Back
Top Bottom