TLS: Kwa Mujibu wa Katiba, sasa Tanzania haina baraza la Mawaziri, Rais Samia atakiwa kuteua Waziri Mkuu ndani ya siku 14

Kwa maana hiyo hata hawa kina Pole pole walioteuliwa kuwa wabunge na rais Magufuli nao inatakiwa wasiwe wabunge tena?

Hapa hawa TLS inaonekana nao hawana wanachojua
 
Shukrani sana TLS Kwa mwongozo huu.
Imani yetu rais ameapa kuilinda na kuitetea katiba yetu, naamini pia atakiishi kiapo chake, kama hakutakua na mashinikizo yalio juu ya uweza wake kwa wakati huu.
Rais anaweza wote. Akiwa weak the hayo mashinikizo yatamsumbua.
 
Kwa maana hiyo hata hawa kina Pole pole walioteuliwa kuwa wabunge na rais Magufuli nao inatakiwa wasiwe wabunge tena?

Hapa hawa TLS inaonekana nao hawana wanachojua
Katiba haijatamka waziwazi kuhusu suala la baraza la mawaziri na kifo cha Rais aliyekuwepo madarakani.
 
Hata iweje watarudi walewale ilikumuenzi mtangulizi lakini mama kasema tugange yajayo
 
Hawa lazima wabanwe, maana tunaanza upya na hii ni nafasi ya mabadiliko ktk masuala ya kisiasa na kijamii tuachane na "desturi au taratibu" za kuvunja katiba na sheria za nchi.
naona unaanza kumfundisha kazi.. Sasa mh raisi.. Unadhani yeye na jiwe wanautofauti huyu yeye anafanya kimya kimya tofauti na aliepita aliekuwa anasemaa hadharani... Anaposema atailinda na kuisimamia katiba si katiba tu hata ba matakwa ya chama chake kibaki madarakani ni mpuuzi gani akubali arahisihe sheria ili CCM Ikose nguvu? never ever..
 
Akiapa raisi mpya harithi kiapo cha aliyemtangulia.

Magufuli alipoapa November 2020, uwaziri mkuu wa Majaliwa ulikoma siku hiyo, hata yeye alisema, Japo alikuja kumteua tena kuendelea nae
We umezungumzia kiapo wanachoapa.

Ni wapi kwenye katiba ambapo panasema Rais aliyepo madarakani akikoma kuwa Rais basi baraza la mawaziri nalo linavunjika automatically?
 
Bado sheria ina ombwe kidogo,je ni kweli mh Rais aliendesha kikao cha Baraza la mawaziri ambalo halipo au aliwachagua watu alioona washauriane?
Alichagua sura za watu wachache watete kidogo. Ukiangalia vyema utaona sura za watu wasio mawaziri, labda watakuwa makatibu wakuu.
 
naona unaanza kumfundisha kazi.. Sasa mh raisi.. Unadhani yeye na jiwe wanautofauti huyu yeye anafanya kimya kimya tofauti na aliepita aliekuwa anasemaa hadharani... Anaposema atailinda na kuisimamia katiba si katiba tu hata ba matakwa ya chama chake kibaki madarakani ni mpuuzi gani akubali arahisihe sheria ili CCM Ikose nguvu? never ever..

Kiongozi, tunakumbushana umuhimu wa kufuata katiba na sheria. Tunataka kumsaidia kwa kumpa ushauri ulio sahihi bila kupepesa macho.
 
Sawa, hiyo ni kuhusu waziri mkuu.

Lakini, ni wapi panapotamka hivyo kuhusu Rais aliyepo madarakani?
Iko hivi
1.Raisi akila kiapo cha uraisi waziri mkuu anaacha kuwa waziri mkuu immediately-Rejea Magufuli alipoapishwa the second time, siku hiyo akamwambia PM kuwa siyo PM tena mpaka alipomwapisha tena some few days later (Kifungu kipo itafute kwenye katiba)

2.Na waziri mkuu akiacha kuwa waziri mkuu basi baraza la mawaziri linavunjika - rejea kujiuzulu kwa Lowasa kuliondoka na baraza lote la mawaziri, Kikwete alikuja kuliunda upya baada ya kumwapisha Pinda)

Kwa hiyo kuingia kwa Samia Suluhu Hassan, huyu ni Rais Mpya na kiapo kipya.
 
hongeren TLS kwa kutimiza wajibu wenu sasa ni muda wa wahusiku kufanya yaliyoshauriwa 👏
Yale yaa kika
Asante sana TLS.
Mmetupa mwongozo murua.
Hii ndio tunataka kuona inafanyika Tanzania. Wataalamu wa fani husika wawe mstari wa mbele na huru kutoa maoni, mapendekezo na ushauri kulingana na jambo husika linalotatiza nchi.

Kwa kifupi kabisa, kisheria kwa sasa hatuna waziri mkuu, hatuna baraza la mawaziri.
Yale ya kikatiba yatafuatwa lakini yale aliyochomekea ya kiuanaharakati hayatafuatwa. Nimeiona sauti ya Tundu Lisu kwake! Amerukia kueleza taratibu za kufuata kwenye janga hili la korona! Hilo si eneo lake! Amwachie waziri mwenye dhamana hiyo!
 
Iko hivi
1.Raisi akila kiapo cha uraisi waziri mkuu anaacha kuwa waziri mkuu immediately-Rejea Magufuli alipoapishwa the second time, siku hiyo akamwambia PM kuwa siyo PM tena mpaka alipomwapisha tena some few days later (Kifungu kipo itafute kwenye katiba)

2.Na waziri mkuu akiacha kuwa waziri mkuu basi baraza la mawaziri linavunjika - rejea kujiuzulu kwa Lowasa kuliondoka na baraza lote la mawaziri, Kikwete alikuja kuliunda upya baada ya kumwapisha Pinda)

Kwa hiyo kuingia kwa Samia Suluhu Hassan, huyu ni Rais Mpya na kiapo kipya.
Sawa.

Lakini hakuna mahali panaposema waziwazi kuwa rais mpya akila kiapo basi baraza zima la mawaziri nalo linavunjika, siyo?

Umenielewa?
 
Back
Top Bottom