TLS: Kwa Mujibu wa Katiba, sasa Tanzania haina baraza la Mawaziri, Rais Samia atakiwa kuteua Waziri Mkuu ndani ya siku 14

Mnamo tarehe 19 Machi 2021, aliyekuwa Makamu wa Raisi wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, aliapishwa kuwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, kufuatia kifo cha Raisi Dr. John Pombe Joseph Magufuli. Kuapishwa kwake kunaibua suala la msingi la kikatiba juu ya kuendelea au kutoendelea kuwapo kwa Baraza la Mawaziri lililoteuliwa na Hayati Raisi John Magufuli...
Asante sana TLS.

Mmetupa mwongozo murua.

Hii ndio tunataka kuona inafanyika Tanzania. Wataalamu wa fani husika wawe mstari wa mbele na huru kutoa maoni, mapendekezo na ushauri kulingana na jambo husika linalotatiza nchi.

Kwa kifupi kabisa, kisheria kwa sasa hatuna waziri mkuu, hatuna baraza la mawaziri.
 
Rais mwenyewe leo amekubali kuingia kwenye kikao cha baraza la mawaziri, na Rais huyo huyo mwanzo alitangaza siku 14 za maombolezo badala ya 21 zinazotambulika kisheria.

Hata wasaidizi wake nao wanaonekana bado wamelala, hawajui kama tupo kwenye utawala mwingine.
 
Akikosea tu kufuata muongozo huo, ndio kitakuwa chanzo cha kuparangana kwa serikali yake... na mwanzo wa watendaji wake kutokuwa na nguzu za kisheria kufanya kazi zao... na hata wakitoa maamuzi, hayo maamuzi yatakuwa ni null and void ab nitio.

Ushauri wa bure, Mheshimiwa SS usome na uufanyie kazi.
 
Hongereni TLS.
Nahisi ndio maana mh Rais alisita kidogo kumtaja majaliwa kama waziri mkuu wa Tz wakati anatoa heshima zake kwa viongozi wengine kabla ya hotuba yake kwa wananchi.
Hata mimi nilishangaa! Alimtaja baada ya kuwataja viongozi wengi tu kwanza ndipo baadae akamtaja yeye.

Sasa nimepata clue.
 
Tumechoka kuona masuala haya yanajadiliwa, kuchambuliwa kwa niaba yetu nje ya mipaka ya nchi yetu Tanzania.

Mfano vyombo vya habari, vyama vya kitaaluma na wananchi wenye uzoefu Kenya wamekuwa mstari wa mbele kutuchambulia hali iliyopo Tanzania kumbe kuna wadau wazalendo kabisa wanaweza kutoa mchango tena kwa lugha adhimu ya kiswahili kizuri na kila mtanzania akaelewa.
 
Kama baraza la mawaziri halipo, leo kile kikao cha baraza la mawaziri kilikuwa kinafanya nini? Nadhani kama Mama Samia hatatengua Majaliwa baraza linabaki hai, atakachofanya ni kubadilisha wachache kutokana na matakwa yake.
 
Mnamo tarehe 19 Machi 2021, aliyekuwa Makamu wa Raisi wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, aliapishwa kuwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, kufuatia kifo cha Raisi Dr. John Pombe Joseph Magufuli. Kuapishwa kwake kunaibua suala la msingi la kikatiba juu ya kuendelea au kutoendelea kuwapo kwa Baraza la Mawaziri lililoteuliwa na Hayati Raisi John Magufuli...
Tunawashukuru sana kwa huu ufafanuzi. Kumbe hadi sasa hakuna Baraza la Mawaziri
 
Ccm hujiamulia tuu hawajui katiba. Bunge lenyewe linalo tajwa ni nani aliwacgagua. Hata mwenda zake alikuwa akiwaambia hawakuchaguliwa na wananchi. Hilo ni bunge la tume ya uchaguzi na baadhi ya vyombo vya dola. Usishangae wakamwambia Mh Mama Samia aendelee na mawaziri ambao hawaja apa mbele yake

Hawa lazima wabanwe, maana tunaanza upya na hii ni nafasi ya mabadiliko ktk masuala ya kisiasa na kijamii tuachane na "desturi au taratibu" za kuvunja katiba na sheria za nchi.
 
Nimeona pia leo amerekebisha muda wa maombolezo kuwa siku 21 kwa mujibu wa katiba, baada ya kufanya makosa kwenye ile taarifa ya awali kuea ni siku 14. Rais aliyepita alikuwa sio mfuataji wa katiba, na TLS wakawa waoga kusema katiba inasema nini. Mfano rais alipokea wanaccm kwenye kamisheni ya jeshi huko Arusha, wakati jeshi limetengwa kikatiba na jeshi/vyombo vya dola.
Anaonekana ni msikivu kwa vitendo, ngoja tuendelee kumfuatilia maana anaonesha mwanga mpya wa matumaini mapya kuachana na uvunjifu wa katiba
 
Tanganyika Law Society muongozo wenu unanipa ukakasi Sana... Inamaanisha baada ya kifo Cha rais serikali yote inakoma?

Basi Makamu wa raisi aliendesha kikao Cha LEO Kimakosa maana aliendesha na Baraza ambalo limekwisha vunjika.

Nionavyo Mimi katiba yetu iliacha ombwe juu ya hii issue, ndio maana nchi nyingine wanaitisha uchaguzi ili kuunda serikali mpya.

Ninavyo sema hivi ninaona mbele yangu shida nyingi za kisheria, matharani uteuzi wa wabunge. Je wabunge walio ingia bungeni kwa tiketi ya raisi watatenguliwa ili Mama Samia akidhi takwa la kisheria la kuwa na nafasi 10?

TLs inaonaje hili ni awamu ya tano au awamu ya 6?

Karibuni kwa mtifuano
 
Hivi ndivyo inatakiwa wadau, wananchi wenye uzoefu au vyama vya kitaaluma n.k kuchangia mawazo na ushauri wao kwa uwazi ili serikali iliyopo madarakani iweze kuwajibika na kutekeleza majukumu yake ipasavyo. Ni mwanzo mzuri. Tunaanza vizuri kwa kutoa ushauri ni mategemeo serikali itakuwa sikivu na shirikishi kwa kukubali ushauri murua kama huu...
Very good!!!!!😆😆😆😆 usimikaji wa mamlaka za nchi kwa kufuata; sheria, kanuni na taratibu inasaidia sana ku-avoid kuwa na the so called BANANA REPUBLIC!!!!😆😆😆

Asante sana TLS kwa guidance yenu hiyo nzuri itakayotufanya tuwe among the modern societies tukiufuata!!
 
Tanganyika Law Society muongozo wenu unanipa ukakasi Sana... Inamaanisha baada ya kifo Cha rais serikali yote inakoma?
Basi Makamu wa raisi aliendesha kikao Cha LEO Kimakosa maana aliendesha na Baraza ambalo limekwisha vunjika...
Lile siyo Baraza la Mawaziri. Ni kikao tu cha marafiki. Ndiyo maana kina Abbas alihudhuria wakati siyo wajumbe wa Baraza
 
Back
Top Bottom