The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

Unajua kuna baadhi ya logic hutokana na level ya ufahamu aliyokuwa nayo mtu kwa wakati ule. Ukimwambia hiki kiko hivi au kimekuwa vile, atakataa kwa sababu logic zake zimeishia pale zilipochanganua, ni bora basi kwa mtu wa namna hii akaomba ushahidi japo wa kimazingira kuliko kubisha moja kwa moja. au ni bora akatoa benefit of doubt until itakapokuwa proved otherwise. ndio maana data ni za muhimu unapofanya analysis ya kisayansi, ingekuwa siyo data na ikawa logic peke yake basi humu duniani tungesema mambo kibao hayawezekani, watu wasingeweza kurusha ndege kwa sababu akili ya kawaida inagoma kwa chuma kupaa. watu wasingetabiri mvua kunyesha baada ya masiku tele, logic ingeuliza wewe umejuaje kama keshokutwa mvua itanyesha?. dataz na logic vyote muhimu wajomba, tusikatae nyuzi ya FMES kwa logic pekee unless kama mnatuletea dataz tofauti za kubatilisha info zake
 
Lakini si tuyliambiwa kuwa Chenge ni shahidi tu kwenye huu uchunguzi wa SFO? Sasa kwa nini shahidi anatiwa pingu?

Mpita Njia,

Kwa taarifa tu mimi nemeona watu wengi hapa UK wanafungwa pinga na bado polisi wanaendelea kusema ni mashahidi, wanakuwa searched na polisi wanaendelea kuwa mashahidi, mpaka siku polisi wakiamua wana ushahidi wa kutosha kuwapeleka mahakamani ndio huko kuitwa shahidi kunaondolewa.

Kwenye makosa hasa ya mauaji, kuna watu wengi wanakuwa shahidi kwa muda mrefu mno kabla ya kubadilika na kuwa watuhumiwa au washitakiwa.

Ukikamatwa, ukawa searched na kutokufunguliwa mashitaka, mara nyingi unabaki shahidi mpaka siku
wanapopata ushahidi zaidi.

Chenge kuwa shahidi kwa maana ya hapa UK, ni kwamba bado hawajaamua kumfungulia au kumwachia huru, anakuwa katikati, haina maana kabisa kwamba hana hatia. Vinginevyo ilitakiwa siku ile ile waliyomfanyia search wamkamate na kumfungulia mashitaka au wamwachie kabisa.
 
Unajua kuna baadhi ya logic hutokana na level ya ufahamu aliyokuwa nayo mtu kwa wakati ule. Ukimwambia hiki kiko hivi au kimekuwa vile, atakataa kwa sababu logic zake zimeishia pale zilipochanganua, ni bora basi kwa mtu wa namna hii akaomba ushahidi japo wa kimazingira kuliko kubisha moja kwa moja. au ni bora akatoa benefit of doubt until itakapokuwa proved otherwise. ndio maana data ni za muhimu unapofanya analysis ya kisayansi, ingekuwa siyo data na ikawa logic peke yake basi humu duniani tungesema mambo kibao hayawezekani, watu wasingeweza kurusha ndege kwa sababu akili ya kawaida inagoma kwa chuma kupaa. watu wasingetabiri mvua kunyesha baada ya masiku tele, logic ingeuliza wewe umejuaje kama keshokutwa mvua itanyesha?. dataz na logic vyote muhimu wajomba, tusikatae nyuzi ya FMES kwa logic pekee unless kama mnatuletea dataz tofauti za kubatilisha info zake

Gamba la Nyoka,

Kama unapanda juu kwenye madaraja ya shule wanasema forget about logic, forget about common sense and start thinking about un common sense.

Uvumbuzi wote wa maana unatokana na kwenda above logical thinking. Aliyesema logic ni za watoto hajakosea kwi kwi kwi!!! I f you want to think BIG! go beyond logic and common sense!

Sio wakati wote logic zinafanya kazi. Logic inatokana na group thinking na toka lini group thinking ilileta mawazo mapya au uvumbuzi?
 
Minaona si vibaya kuhoji data.
FMES, endelea kuweka data ila usi-mind wenzako wanapo hoji logic au uhalisi,hii ni kuhakikisha kwamba we are not taken for a ride. Kumbuka tulivyopata taarifa kwamba Chenge amekunywa sumu?!
Personally nadhani data zako zinaweza kuwa kweli lakini kuna holes in it, ambazo wengine wameuliza, hivyo inawezekana kwamba tukipata data kamili tunaweza kuamini data zako.
Sidhani kama Chenge kupelekwa London kuhojiwa itasaidia kitu cha maana kwetu sisi waBongo. Also nakubaliana na hoja ya kwamba kama ni kweli Muungwana yuko so determined angefanya shuguhli zote kwa uwazi. Otherwise data zako zinaonekana kutaka kumsafisha Mungwana na kumfanya aonekane anafanya kazi na kuwa yuko serious, kitu ambacho kinakuwa contradicted na actions zake anazotenda hadharani.
 
Minaona si vibaya kuhoji data.
FMES, endelea kuweka data ila usi-mind wenzako wanapo hoji logic au uhalisi,hii ni kuhakikisha kwamba we are not taken for a ride. Kumbuka tulivyopata taarifa kwamba Chenge amekunywa sumu?!
Personally nadhani data zako zinaweza kuwa kweli lakini kuna holes in it, ambazo wengine wameuliza, hivyo inawezekana kwamba tukipata data kamili tunaweza kuamini data zako.
Sidhani kama Chenge kupelekwa London kuhojiwa itasaidia kitu cha maana kwetu sisi waBongo. Also nakubaliana na hoja ya kwamba kama ni kweli Muungwana yuko so determined angefanya shuguhli zote kwa uwazi. Otherwise data zako zinaonekana kutaka kumsafisha Mungwana na kumfanya aonekane anafanya kazi na kuwa yuko serious, kitu ambacho kinakuwa contradicted na actions zake anazotenda hadharani.

Mkuu umenena!
 
.... Kwi kwi kwi... Wabongo bwana sasa mzee wa Vijisenti Akishughulikiwa tutakuwa tumemaliza matatizo yetu ya Uchumi wa Bongo?

... Mimi nilidhani hili tuwaachie vyombo vya usalama kwa sasa (aidha vya ndani au vya nje kwa sasa) tulete mawazo ya kukomboa nchi yetu kiuchumi jamani... haya mambo ya say TZS Billioni 800; ukiachilia mbali TZS Billioni (1) Moja ya Mzee wa Vijisenti hazileti kitu chochote significant kwenye taifa letu changa.

...Kama mawazo hayo ni kuwapa nchi akina Kitila, JJ Mnyika, Mwafrika wa Kike, Asha Abdallah tuangalie sasa namna gani tuwawezeshe...

...Kama ni kufanya kazi tuangalie namna gani ya kuwafanya waTanzania wafanye kazi kwa bidii na ufanisi!
 
.... Kwi kwi kwi... Wabongo bwana sasa mzee wa Vijisenti Akishughulikiwa tutakuwa tumemaliza matatizo yetu ya bongo?

Kwa hiyo Mkuu wewe unaonaje? Wamsamehe au Asurubiwe?

Hila Mkuu angalia na wewe nisije nikakuita Vijisenti, hivi Mkuu Nchi kama Tanzania ni nchi ya kuachia bilioni moja? Nisingependa kuendelea kufikiria kama kuna mtanzania ana mawazo ya kuachia kiasi hiki!
 
Mkuu Susuviri,

Na the likes, ninasema hivi hizi dataz hazina ubishi wala mikwaruzo, toka jana Media nzima ya bongo inanipigia magoti niwauzie, nimesema siuzii mtu kwa sababu ninaamini katika kuwaelemisha wananchi na pia siku zote kuweka heshima ya hii forum,

Kwa taarifa yako na wenzio, kama alivyosema Lunyungu, sijawahi ku-withdraw dataz na hazijawahi kuwa disputed na ukweli zaidi yake, lakini ni kweli kila ninapozitoa huwa kunakuwa na mashambulizi ya personal against me ambayo hayahusiani na the dataz, sababu huwa ni moja muhimu, nayo ni wivu na uwezo mdogo wa kufikiri kwa wahusika,

Nimesema mara nyingi sana na ninarudia kuwa think kabla hujaandika hapa, kwa mfano in the name of dataz, hapa JF ninawajua ndugu wa karibu na Chenge, angalau wawili ambao so far wametulia, meaning kwamba hata wao nimewasaidia maana walikuwa hawajui kuhusu hii ishu, I do not have to do this lakini ni vyema tukawasaidia wenye akili hapa, nilipoziweka hizi dataz Lunyungu ameenda kuzifuatilia na kuja na zake zaidi na kukubali ukweli wa dataz, mimi mtu yoyote akiweka dataz hapa kazi yangu ni kuzifuatilia na kuthibitisha kama nina-concern, na kumwambia ukweli wa ishu kwa kumuonyesha wapi amekosea na dataz zake, kwa mfano Chenge nimemuona jana yupo Dar, Rostam na Karamagi hawakusaifiri last week, ukweli ni one, two, and three, au kunyamaza kwa sababu kwenye maisha si kweli kwamba kama wewe hujui basi wengine wote hawajui,

Dataz ni dataz, I mean just dataz hatuna njia nyingine yoyote ya kuziweka, they are just dataz, kwa sababu tunapewa na watu ambao huwa wana-risk sana na kazi zao sasa ni wajibu wetu kutumia akili on how tunaziweka hapa, ndio maana nimesema kuwa ninajua hata jina la mahali huko London ambako hizi shughuli zinakofanyika,

na bado ninaendelea kuzikusanya more dataz, and more dataz yaaani ni just dataz tupu, asiyezitaka badili station tu lakini ninajua kuwa ni wengi wanaozitaka kwa sababu toka jana PM yangu imejaa mara mbili, halafu mind you PM yangu inachukua message 1000, sasa zote nimezi-print, mesage karibu 2500, leo nataka nijaribu kuzisoma, kwa wale wenye nia ya kuwa na ile DVD thing, ni kwamba nina vipande vinne, nimeangalaia viwili so far in full, bado vipande viwili vingine, kabla ya kuanza kuziweka zote nne in one master DVD, ili niweze kuzirudisha nilikoazimwa kwa muda, niliongea na Mkulu MMJ on what to do next ili kuiweka hapa, hilo halina ubishi itakuja when the time is right!

A Luta Na More Dataz Soon..........!
 
.... Kwi kwi kwi... Wabongo bwana sasa mzee wa Vijisenti Akishughulikiwa tutakuwa tumemaliza matatizo yetu ya Uchumi wa Bongo?

... Mimi nilidhani hili tuwaachie vyombo vya usalama kwa sasa (aidha vya ndani au vya nje kwa sasa) tulete mawazo ya kukomboa nchi yetu kiuchumi jamani... haya mambo ya say TZS Billioni 800; ukiachilia mbali TZS Billioni (1) Moja ya Mzee wa Vijisenti hazileti kitu chochote significant kwenye taifa letu changa.

...Kama mawazo hayo ni kuwapa nchi akina Kitila, JJ Mnyika, Mwafrika wa Kike, Asha Abdallah tuangalie sasa namna gani tuwawezeshe...

...Kama ni kufanya kazi tuangalie namna gani ya kuwafanya waTanzania wafanye kazi kwa bidii na ufanisi!


Kama kawaida yako uko kazini .Unapenda kuahirisha matatizo .Vyombo vya usalama vipi ? Vya Tanzania ama UK ? Maana unadhani kuahirisha matatizo ndiyo suluhu yake .
 
Halafu na hao paparazzi waliomuona Chenge ndani ya pingu hawana snap shots?
Ama hawakujishughulisha?
 
Kwa hiyo Mkuu wewe unaonaje? Wamsamehe au Asurubiwe?

Hila Mkuu angalia na wewe nisije nikakuita Vijisenti,
hivi Mkuu Nchi kama Tanzania ni nchi ya kuachia bilioni moja? Nisingependa kuendelea kufikiria kama kuna mtanzania ana mawazo ya kuachia kiasi hiki!

kakindomaster;

Kwi kwi kwi... si tayari hili linafanyiwa kazi... at least mutafute mwingine fisadi mwingine huyu yuko kwenye mikono salama as far as wananchi is concern... hili linafanyiwa kazi... twende mbele...

Kwa mawazo yangu Bill. 1 kwa uchumi wa nchi ni hela ndogo sana... tutafute tuchape kazi tulete mawazo mengine tujenge nchi....
 
.... Kwi kwi kwi... Wabongo bwana sasa mzee wa Vijisenti Akishughulikiwa tutakuwa tumemaliza matatizo yetu ya Uchumi wa Bongo?

... Mimi nilidhani hili tuwaachie vyombo vya usalama kwa sasa (aidha vya ndani au vya nje kwa sasa) tulete mawazo ya kukomboa nchi yetu kiuchumi jamani... haya mambo ya say TZS Billioni 800; ukiachilia mbali TZS Billioni (1) Moja ya Mzee wa Vijisenti hazileti kitu chochote significant kwenye taifa letu changa.

...Kama mawazo hayo ni kuwapa nchi akina Kitila, JJ Mnyika, Mwafrika wa Kike, Asha Abdallah tuangalie sasa namna gani tuwawezeshe...

...Kama ni kufanya kazi tuangalie namna gani ya kuwafanya waTanzania wafanye kazi kwa bidii na ufanisi!

Mkuu, natanguliza heshima. Mie siamini kama ulikuwa una-type huo ujumbe mind yako ikiwa AWAKE. Hivi kweli Billioni 1 haiwezi kufanya kitu Tanzania. Jamani tuache utani hapa. Sina haja ya kukushambulia au kukuvunjia heshima lakini kusema 1 Billion is nothing ni sawa na kuwatukana Watanzania. Hata kama ingekuwa ni Mia moja yes Tsh. 100 still ni mali ya Watanzania and they deserve it. Kusema 1 billion is nothing nitakuweka kundi moja na Mzee wa Vijisenti maana "kila mtu ana kipimo chake" Quote from Chenge. Tuacheni utani na kuwadhalilisha Watanzania. Wafanye kazi kwa bidii gani wakati mnawafukuza kwenye Machimbo yao ya madini mnawapa Meremeta????!! Wafanyeje wakati mnachukuwa pesa yao mnafanyia UFISADI?? Samahani kwa kutumia jumuisho maana naona wewe na Mzee wa Vijisenti are almost the same linapokuja suala la Pesa ya Watanzania.

Sorry kama nitakuwa nimekutonesha. I'm really sorry but that's THE TRUTH.
 
Nadhani sasa baada ya Chenge kutiwa nguvuni ni vyema kungojea kuona next move .Wambeya hapa wamenasa .Mimi nimezima sasa simu yangu baada ya kuwa kero .Wanataka kuuua ukweli lakini nimesema kesho nitakuwa ofisini tuonane huko leo napumzika .Ukweli umesimama na hata CCM na Ikulu kawaulize .They are all shocked kwamba habari hizo hazikulala na tunazo .ES
naujua unyonge wako mkuu lakini kwenye data no has disputed your data .Wamekuja hapa wambeya kibao akina GT na majungu lakini kila wasemalo mwisho ni fitina binafsi ama ku twist wakiwa kazini .

naomba tuwe focused sasa .Issue ni kukamatwa kwa Chenge na mali kibao za walafi kukamatwa .Sasa tumpe JK sifa ama hapana .Utaamua wewe .Mimi nampo kidogo kwa kuamua kutoa kibali cha Chenge kukamatwa na kumwambia Rostam na Karamagi kwenda kusema wanayo yajua .

Connection hapa ni kubwa Chenge si Rada pekee .Chenge amekiwa AG mwa kipindi kirefu namuda huo wote madhambi makubwa na mikataba kibao imewekwa .Hili pekee linaleta utata si UK pekee hata TZ kama kweli tuna utawala bora and unfortunately hatuna .
 
Swali:::

Issue nzima ya diplomatic immunity inatumika vipi ukiwa uko nje ya nchi??
Hawa MPs, CC mbrs status zao ziko vipi??
Je wamevuliwa??

Sheria za kimataifa zinasema vipi?? why mtu wa level ya Chenge akubali kwenda london kwa sheria ipi?? Au ilikuwa rendition??? SFO mipaka yao ni ipi???

Mzee ES nakuaminia siku zote endelea kutuletea dataz maana zinatusaidia kujua mengi.
 
LENYE MWANZO HALIKOSI MWISHO
According to the dataz, Chenge sasa yupo London akiwa chini ya ulinzi wa makachero wa UK, akiwasaidia kuhusiana na uchugnuzi wa Radar. Habari nyeti nilizozipaata jana ni kwamba Chenge aliondoka kwa siri hapa nyumbani bongo kuelekea London, majuzi usiku ambako alikuwa akitakiwa kisheria na wachunguzi wa huko ambao ndio walioibua kashfa ya zile "Vijisenti". Huko London, alipokewa na makachero hao mara tu alipofika kwenye uwanja wa ndege, ambao walimpokea na kutokomea naye kusikojulikana.

According to more dataz, ni kwamba Muungwana was approached na makachero hao wa UK, hata kabla ya kikao cha CCM Butiama, na kwamba hata alipokuwa anachagua baraza la mawaziri tayari alikuwa anazo habari za Chenge na "Vijisenti", lakini hakutaka pupa. Dataz hizo zinasema kuwa hata kabla ya kwenda India, muungwana alikuwa tayari ameshawapa makachero wa UK, kibali cha maandishi cha kumshika, na kum-search Chenge, as much as they wanted or see fit!

Kabla ya kwenda Butiama, Chenge was approached na makachero hao wa UK lakini akawajibu kijeuri sana kuwa yeye ni mtu mkubwa sana hawezi kutishwa na wakoloni, ndipo wazungu walipomuonyesha warrant maalum iliyoandikwa na kusainiwa na Muungwana, Chenge almost fainted, lakini akakubali na kuchukuliwa na makachero hao, walioi-search nyumba yake upside down kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa mbili suiku, na kupata ushahidi mwingi waliokuwa wakiutafuta na kuondoka nao, na muungwana alimpa order ya kuendelea kuwasaidia hadi watakapomaliza uchunguzi wao, na baada ya kujiuzulu Chenge aliambiwa ajitayarishe kwenda UK kushiriki kwenye kuwasaidia zaidi makachero hao wakizungu, ambako ndio alienda rasmi majuzi na yuko huko bado.

Halafu dataz zaidi pia zinasema kuwa mapesa mengi na mali za mafisadi zimeszuiwa na serikali kwa siri kubwa sana, the matter of fact hata nyumba za mafisadi wengi zilizoko SA ikiwemo ya Mkapa pia zimeshikwa na serikali tayari, ikiwa ni pamoja na mapesa yao yote yaliyopo hapa bongo.

Mafisadi wengi wamejaribu kumfuata Mkono ili awasadie, akiwemo Chenge pia, lakini according to the dataz hata Mkono amewaruka wote, baada ya kupewa a very strong warning na muungwana kuwa akae mbali nao, now mnyonge anyongwe, lakini haki apewe on this.

....More Dataz to Come Soon....


Siku zote lenye mwanzo halikosi mwisho. Kama kuna mwanzo wa kujitengenezea vijisent kuna mwisho wake pia. Namuunga mkono JK.
 
Mkuu, natanguliza heshima. Mie siamini kama ulikuwa una-type huo ujumbe mind yako ikiwa AWAKE. Hivi kweli Billioni 1 haiwezi kufanya kitu Tanzania. Jamani tuache utani hapa. Sina haja ya kukushambulia au kukuvunjia heshima lakini kusema 1 Billion is nothing ni sawa na kuwatukana Watanzania. Hata kama ingekuwa ni Mia moja yes Tsh. 100 still ni mali ya Watanzania and they deserve it. Kusema 1 billion is nothing nitakuweka kundi moja na Mzee wa Vijisenti maana "kila mtu ana kipimo chake" Quote from Chenge. Tuacheni utani na kuwadhalilisha Watanzania. Wafanye kazi kwa bidii gani wakati mnawafukuza kwenye Machimbo yao ya madini mnawapa Meremeta????!! Wafanyeje wakati mnachukuwa pesa yao mnafanyia UFISADI?? Samahani kwa kutumia jumuisho maana naona wewe na Mzee wa Vijisenti are almost the same linapokuja suala la Pesa ya Watanzania.

Sorry kama nitakuwa nimekutonesha. I'm really sorry but that's THE TRUTH.

Mkuu Indume Yene, umelonga. Bado ninazikumbuka makala za Samson Mwingamba ktk gazeti la Tanzania Daima zenye kichwa "Je Tanzania zipo nyingi?

Yaani viwango vimetofautiana mno, wakati mwananchi mwingine anahangaika kutafuta mlo wa baadaye, mwingine anaona 1bln siyo kitu. Wakati wengine wanatembea kilomita 10 kwenda zahanati, au shule hazina walimu, madawati wa vitabu, barabara mbovu hazipitiki kipindi cha mvua, mwingine anaona 1bln siyo kitu.

Naomba Watanzania wenzangu hasa mnaoishi nje ya nchi, mpatapo nafasi ya kutembelea bongo, tembeleeni vijijini na mitaa ya uswahili. 1bln inapowekezwa ktk huduma za jamii inaweza kuleta impact kubwa.

Tuache kuwatukana Watanzania, fikiria hata wafanyakazi wa Serikali tena wenye degree wanalipwa basic 300,000, take home 230,000 - 240,000 kwa mwezi, je utamwambiaje huyu 1bln si kitu?
 
Na tuliambiwa kwenye media kwamba safari yake ilikuwa "ya kawaida"... kwa hiyo anaendelea kututhibitishia kuwa kweli anazo hela nyingi zaidi ya alizokutwa nazo ktk account, yaani kwamba kweli ni "vijisenti", kwa kukutwa na SHILINGI BILIONI 1 ZA KITANZANIA NYUMBANI!! Mungu wangu!! Na kuna watu hata elfu 1 cash hawana ndani ya nyumba!! Dhambi iliyoje
 
Back
Top Bottom