The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

na muhogo,...mwa na pilipili mwa inakolea ko singo!!!! nakikubali msosi wa kwa mama pale ferry magogoni au holiday inn annexe jirani na kwa prof shaba..we si matani mzee!!! unajua mara nyingine hawa warungu wanadharau misosi yetu so wakifungua outlets wanatujazia ma sandwich na ma hotdog ,,wapi na wapi...ukiwa pale annexe utagundua hata mabosi wamatumbi wenzetu wanakuja...wale wanaogopa protocal wanawatuma madereva na hotpot..ugali ,matembele na dagaa la kigoma topped with maharage ya mbeya,....tsh 600 tu[cents 0.45 usd/belly bursting lunch]..usisahau na ndizi mbivu au parachichi la moro...
 
kikwete alikataa maswali hapa uk kwa kuogopa kuhulizwa hili swala,lakini namkumbusha alipo hulizwa akiwa waziri wa mambo ya nje na bbc world services na alivyotetea hilo swala. swali langu kwake je mpaka sasa anaendelea kuitetea hiyo deal kama alivyofanya mwanzo?
 
Kama kweli tungalikuwa na watu Serious ana tukawa na private prosecutor leo hii mahakamani JK asingalipona . Leo hakuna uchunguzi wa mana utafanyika ambao yeye kasema hawezi kuingilia kwa kuwa JK anahusika moja kwa moja na ununuzi wa Rada. Kumbuka maamuzi yalitoka baraza la Mawaziri ambalo yeye alikuwemo. JK ni mnafiki sana na mfano wake ni ununuzi wa nyumba za serikali . Je hakununua ? Mbona alikaa kimya hadi mwisho ?
 
Duh mazee ununuzi wa nyumba za serikali hebu tuwekee wazi unajua tena wengina tuko mbali na upeo wa macho itakua bomba kama utatoa ya ununuzi wa nyumba za serikali kwa kirefu..
 
nakuambia si mchezo ila mazishi yale sasa ndio nini kupiga picha kwenye maji..
pale mie sijamfagilia hata kwa nini..ila mzee unyanyasaji kweli..kula hela..ya walipa kodi..inauma wangu..kuna siku pale tutaanza kuchinjana kama iraqi wee acha tu
 
Shemzigwa,

hapa ndipo napokoma na viongozi wetu.. hiyo picha pamoja na ile alopiga na Michuzi wakivuka kwa mashua nilidhani ni kampeni moja kubwa kuwa atajenga daraja akichaguliwa, lakini ndio hivyo tenaaa..anaonyesha kuwa yeye pia anaweza kuvuka kama wenyeji.
 
hehehe mzee hapo alikua kazi hana akaona akunje maji avuke surual au huwenda alimiss kuvuka maji si unajua tena...ukizoea kitu inakua tabu kukiacha hahaha ni mzozo ndani ya bongo
 
Lets keep to the point RUSHWA YA RADAR !RUSHWA YA RADAR !RUSHWA YA RADAR !RUSHWA YA RADAR !RUSHWA YA RADAR !RUSHWA YA RADAR !.Wanajambo what is the way forward?
 
Mzee MKJJ
Vyombo vya habari hata kusema maandamano yamefanyika wamesindwa wataweza kupokea pesa na kufanya matangazo ? Serikali ya JK na EL ni serikali fedhuli . Wamehakikisha ujumbe haufiki mbali na hivyo vyombo vya habafri ni waoga kupokea ujumbe huo na kuusambaza . Haya ni maoni yangu lakini pia ndiyo hali halisi . Vyombo vimebanwa na kumbuka vingi owned na supporters wa CCM ambao wao Nchi si muhimu bali CCM na maslahi yao na wake zao .QUOTE] WELL SAID. JAMANI NASISITIZA TENA....BARUA HIYO YA KUZUNGUSHA KWENYE MTANDAO HAYO MAMANDAMANO TAYARI NI HISTORIA. LEO ASUBUHI KILA MVUJA JASHO ANATAFUTA CHAKULA CHAKE NA WATOTO WAKE. WENZETU WALE "AKAUNTI ZAO ZIMESHANENEPA WANA UHAKIKA WA KILA KITU ....HADI VITUKUU WAO"!
Wana jambo....lets agree on way forward na sisi tufanye nini ...."kuendeleza effectya maandamano"
 
Jamani, tusifanya mambo kwa haraka, kila kitu its about timing. Sasa, kwanza kabisa kabla hatujafanya lolote, lazime tudefine lengo letu ni nini. Vingine vinakuja baada ya hapo. Mama Lu, lengo la waraka huo ni nini?
 
Jamani, tusifanya mambo kwa haraka, kila kitu its about timing. Sasa, kwanza kabisa kabla hatujafanya lolote, lazime tudefine lengo letu ni nini. Vingine vinakuja baada ya hapo. Mama Lu, lengo la waraka huo ni nini?


Mimi nafikiri mama Lulu ana hoja. Iandikwe barua (au ile uliyokwishaandika) ya kulitaka bunge lianzishe uchunguzi juu ya manunuzi ya radar hasa katika mambo mawili:

i) kama bei iliyonunuliwa ilikuwa ni halali
ii) ni akina nani Tanzania walipewa hizo $30m

Hiyo barua izunguke watu tuweke majina yetu halisi iende kwa speaker na kila mbunge wa bunge letu pamoja na ubalozi wetu uingereza.

Vipi hapo?
 
Iandikwe barua (au ile uliyokwishaandika) ya kulitaka bunge lianzishe uchunguzi juu ya manunuzi ya radar hasa katika mambo mawili:

i) kama bei iliyonunuliwa ilikuwa ni halali
ii) ni akina nani Tanzania walipewa hizo $30m

Hiyo barua izunguke watu tuweke majina yetu halisi iende kwa speaker na kila mbunge wa bunge letu ?
Naona naanza kueleweka.......pia iende balozi zote nyeti...USA, Uingereza, Scandinavian Countries etc
 
Mzee Mwanakiji...hii barua iwe na maelezo ya kina kuhusu huu "uozo". Magazeti ya bongo hayaelezei hizi details kama humu yenyewe yanakuwa ni watu wa "headlines " ili wauze at the same time ...wapendwe na serikali.In simple terms watu waelewe kuwa "tumeibiwa, tumedanganywa na kuna rushwa imeendelea!". Tu waambie wananchi hizi pesa zingewezaje kutumika vizuri zaidi nchini(examples).Na tuseme what we need...waliohusika wawe put to task! NDIO MAANA YA UTAWALA BORA!!!!!!!!!PUT PRESSURE TO THE PUBLIC.
.....PRESSURE PRESSURE WALIOKULA MLUNGULA WAWEZE KUWA PUT TO TASK..AU SIVYO HAWA WAFADHILI WASIMAMISHE HIYO MISAADA INAYOWANUAFAISHA WACHACHE.KAMA TUNAWEZA KU ENTERTAIN ONE PERSON KUPATA 12 BILLIONI WAKATI HOSPITALI HAZINA VITANDA ....
 
Sasa iwe ni barua ya Kiingereza (walengwa ni wafadhili na nchi za nje) au ya Kiswahili (walengwa ni Watanzania wenzetu)?
 
It can be the same letter......in both languages.Ikishindikana kabisa...tuandike ya kiswahili si wana translators?
 
WAFADHILI SI NDIO WALIOSHINIKIZA TUNUNUE HIYO RADA?


Kuna uchunguzi unaofanywa na SFO huko London kwa nini hao jamaa wasipewe nafasi wafikie mahali waseme either wameshindwa au wame-uncover anything...ndio then tulalamike.

Kwa sasa kupeleka barua kwa Wafadhili mimi naona ni sawa na kumpa kesi ya nyani ngedele.
 
Jamani. Pamoja na kwamba naunga mkono suala hili, tusisahau hizi issue tatu nazo ni IPTL, SONGAS na RICHMONDULI. Malipo ya IPTL na SONGAS kwa miezi minne tu (capacity charges) yanafikia "cha juu" alichopata mhindi huyo kama si kuzidi, tukiassume kwamba rada tunaitaka. RICHMONDULI ni zaidi sana ya hizi fedha za rada. Nadhani mikataba hiyo ya umeme (I+S) bado inadai si chini ya miaka 15 ijayo ili iishe. Sasa ukisikia mikataba ya uozo ambayo inabidi irekebishwe, ndio kama hii. hapo bado madini.
 
Back
Top Bottom