The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

Mzee MKJJ
Vyombo vya habari hata kusema maandamano yamefanyika wamesindwa wataweza kupokea pesa na kufanya matangazo ? Serikali ya JK na EL ni serikali fedhuli . Wamehakikisha ujumbe haufiki mbali na hivyo vyombo vya habafri ni waoga kupokea ujumbe huo na kuusambaza . Haya ni maoni yangu lakini pia ndiyo hali halisi . Vyombo vimebanwa na kumbuka vingi owned na supporters wa CCM ambao wao Nchi si muhimu bali CCM na maslahi yao na wake zao .


Mzee MKJJ habari ya Rada na wizi huu umesha wafikia wananchi kule kijijini kwetu .Maana Radio yao ya Taifa wanayoipata sana ni BBC Swahili service . RTD hadi wapande mlimani kuipata . Sasa ujumbe wanao kisa ni masanda yao yale na kugubikwa na ujinga na kuweka ushabiki mbele na kuto kuelewa Rada ni kitu gani na 40m ni kiasi cha pesa na 12m na Banki ya Uswisi ni kitu maana CCM walifanikiwa kuwanyima Elimu .Ila wanaweka speed ya kuwapa maguo yale ya rangi za Hamas na Hezbolla
 
r2709628724.jpg


Kina mama wakiandamana mapema leo (picha na AP)

rada1.jpg


Watanzania wakiandamana (picha na M.I. Michuzi)

rada3.jpg


Wanadai kujua kuhusu ununuzi wa rada (Picha na M.I. Michuzi)
Tembelea tovuti ya Michuzi kwa picha za mambo mbalimbali http://www.issamichuzi.blogspot.com

wapinzanimroki.jpg


Watanzania wakiandamana kuihoji serikali yao kuhusu ununuzi wa rada ya shilingi bilioni 40. Kutoka kulia Mbatia, Mrema, Lipumba na Cheyo (Picha na Mroki Mroki) Tembelea tovuti ya Mroki hapa http://www.blog.co.tz/mrocky
 
Du babake Umefanya la maana nilikua nasikiliza BBc mahojiano yake naona anatoa nje...kuhusu Rada anasema Bongo Rada...ila huyu jamaa ni msanii tu nae...
 
Shem weka link haoa ya Mahojiano hayo ya Rada ndiyo maana tuko hapa. Bandika na wengine wapate kusikia na kujenga hoja
 
poa mazee nimecheliwa unajua tena Bi mkubwa alikuja hapa nikawa naangalia tv nae kucheki kumbe ushatuma kitu..Ila huyu Jk mizinguo kweli yani..anadai tz tunahitaji rada na imetusaidia hatupangii mtu majukumu yetu..serikali ya Uk kujadili suala lile..kwa vile walikua wana chunguza shirika lenyewe zaidi wee Gonga hapa BBc amka na africa jitahidi kabla hawajaamka tena kesho http://www.bbc.co.uk/swahili/
 
Rada tunahitaji lakini iwepo transparency na pili nadhani kuna suala zima la consultation na kuangalia kama ni value for money
 
DrWho, ni kweli rada tunahihitaji, lakini kwanini rada ya kijeshi? kwanini rada isiyoangalia nchi nzima bali sehemu ya nchi? Rada kwa ajili ya ulinzi wa anga, tuna tishio la nani na toka nchi gani? Rais Kikwete alisema rada itatuongezea mapato na utalii je, imetuongezea mapato kiasi gani, na watalii wameongezeka kiasi gani kwa sababu ya rada hiyo? Ili kuweza kuangalia nchi nzima na kutupa ulinzi kamili tunahitaji rada nyingine mbili zenye uwezo kama huo, je tuzinunue kwa bei ya dola milioni 80 kwa vile tunazihitaji? Dalali hulipwa na mnunuzi au muuzaji, katika hili inaonekana amelipwa na muuzaji. Lakini tuna uhakika mnunuzi hakumlipa pia kwa kumtafutia chombo kizuri kama hicho? Kama amelipwa na mnunuzi pia, amelipwa kiasi gani? Ili dalali aweze kuiuzia serikali ya JMT bila ya shaka kuna mkataba hapo mkataba huo unasema nini kuhusu malipo hayo, na uliingiwa na nani?
 
Lipumba amshika pabaya Ben Mkapa



na Charles Mullinda


VIONGOZI wa vyama vitano vya upinzani, wamesema wana wasiwasi na utetezi uliokuwa ukitolewa na Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, katika ununuzi wa rada iliyoibua kashfa nzito nchini Uingereza.


Wamesema Mkapa anapaswa kueleza anachokijua kuhusiana na ununuzi wa rada hiyo ili ajisafishe machoni mwa Watanzania na jumuiya ya kimataifa kama hakuhusika katika amana hiyo.


Wamemtaka atangaze mali alizochuma kwa muda wa miaka kumi, kipindi alichokuwa madarakani kama alivyofanya wakati akiingia madarakani ili Watanzania wajue utajiri alionao sasa, ili ulinganishwe na mali alizoingia nazo madarakani.


Wakizungumza katika mkutano wa hadhara uliotanguliwa na maandamano ya kulaani ununuzi wa rada hiyo jana, katika viwanja vya jangwani, Dar es Salaam, viongozi hao, walisema Mkapa alitetea kwa nguvu ununuzi wa rada hiyo na kueleza kwamba tenda yake haikuwa na chembe ya rushwa.


Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, alisema ya kuwa wakati wa mchakato wa ununuzi wa rada hiyo, wananchi, vyama vya upinzani na nchi wahisani walipinga kununuliwa kwa rada hiyo, lakini hawakufanikiwa kwa sababu Mkapa aliziba pamba masikioni.


“Wahisani, wananchi na vyama vya upinzani vilipinga kununuliwa kwa rada hii, lakini Rais Mkapa akiwa Australia alitetea inunuliwe na kueleza kuwa mpango mzima haukuwa na chembe ya rushwa.


“Sasa imebainika kuwa rushwa iligubika mpango mzima, tunataka kujua kama Mkapa hakuhusika na rushwa hii, ni vizuri ajitokeze awaeleze Watanzania kwa nini alitetea sana inunuliwe!


“Pia tunataka atangaze mali zake kama alivyofanya wakati akiingia madarakani, alipoutangazia umma kuwa ana nyumba moja hapa Dar, moja Masasi, miche 100 ya korosho na shamba ambalo halijaendelezwa nje ya jiji la Dar es Salaam, tunataka kujua baada ya miaka 10 ya urais amechuma mali kiasi gani ili tulinganishe na ile aliyoingia nayo madarakani.


“Tunasema hivi kwa sababu kashfa hii ilitokea wakati wa Awamu ya Tatu aliyokuwa akiiongoza, na pesa iliyoibiwa ni nyingi mno, kwa vile baada ya kuachia madaraka aliwaomba radhi Watanzania kuwa wamsamehe kwa aliyowakosea, itakuwa vizuri kama atatusaidia kuzirejesha nchini hizo sh bilioni 15,” alisema Lipumba.


Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour, Augustine Mrema, alisema mwaka 1991 ndipo alianza kujua jinsi Tanzania inajengwa na wenye moyo na inavyoliwa na wenye meno.


Alisema katika kipindi cha utawala wa Awamu ya Tatu aliandamwa na kesi nyingi ambazo maelekezo ya kuziendesha yalikuwa yakitoka Ikulu, lakini alifanikiwa kujinasua kwa sababu alikuwa na kinga iliyotolewa na Bunge ya kutoshitakiwa.


Baadhi ya wanakamati wa kamati ya Bunge iliyokuwa ikisikiliza kesi yake ya kuwahutumu baadhi ya vigogo wa serikali kuhongwa sh milioni 900 walizadiwa vyeo mbalimbali, ukiwamo uwaziri na Rais mstaafu Mkapa.


Alisema vyeo hivyo walipewa baada ya kumkingia kifua Mkapa ili asihojiwe na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na alikuwa amemtaja katika sakata hilo.


Viongozi wengine wa vyama vya upinzani waliounga mkono maneno ya Lipumba na Mrema, ni Mwenyekiti wa UDP, John Cheyo, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, na Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Shaibu Akwilombe.


Kadhalika, viongozi hao walimshangaa Rais Jakaya Kikwete kutokasirishwa na taarifa za kuwapo kwa rushwa katika ununuzi wa rada na kueleza kuwa hatua yake hiyo inatia shaka.


Mwenyekiti wa UDP, Cheyo, alisema alitegemea kusikia Rais Kikwete akitoa kauli ya kukasirishwa na taarifa za kuwapo kwa rushwa katika ununuzi wa rada, lakini anamshangaa kusema kuwa aibu hiyo ni ya Waingereza.


“Nilitegemea kumsikia Rais Kikwete akisema amekasirishwa na tuhuma za kuwapo kwa rushwa ya sh bilioni 15 katika ununuzi wa rada hiyo, fedha ambazo zilifaa kwenda kwenye ujenzi wa shule, ajabu anasema hiyo ni aibu ya Waingereza.


“Ninawaomba Watanzania wamuonyeshe Rais Kikwete kuwa wamekasirishwa na rushwa hii, tofauti na yeye. Kama Wazungu wameweza kumkarisha chini Brair ambaye nchi yake imechukua pesa za Watanzania maskini, kwa nini sisi tusikasirike?” alihoji Cheyo.


Alionya kuwa kitendo cha Rais Kikwete kutokerwa na ufisadi unaofanywa na baadhi ya watu, kitaipeleka nchi pabaya na itabaki kuwa tegemezi milele.


Mrema yeye alimponda Rais Kikwete kuwa kazi kubwa anayoweza kuifanya kwa ufasaha ni kutembelea wagonjwa hospitali na wafungwa gerezani.


“Hatutaki rais mzuri, uzuri wake unatusaidia nini? Anacheka cheka tu, anakwenda hospitali kutembelea wagonjwa, anawaombea wapone, hivi tulimchagua kuombea wagonjwa? Rais huyu ni sheikh? Kama kweli ni mwanamume arejeshe hizo sh bilioni 15 ziliporwa,” alisema Mrema aliyezungumza kwa hisia kali jana.


Alisema kwa mujibu wa uchunguzi alioufanya amegundua rada hiyo ilinunuliwa kwa shinikizo la Serikali ya Marekani ambayo Tanzania sasa ni mshirika wake wa karibu.


Mrema alisema kuwa Marekani iliishinikiza Tanzania kununua rada hiyo ili kuweza kuona sehemu zote za Afrika Mashariki pamoja na Pembe ya Afrika, lengo kuu likiwa kupambana na ugaidi.


Alishangaa kuwa Tanzania imekubali kutekeleza masilahi ya Marekani kwa kutumia pesa za Watanzania ambao ni masikini wa kutupwa tofauti na wananchi wa Marekani.


Naye Prof. Lipumba alisema kashfa ya rada iko wazi na Rais Kikwete anapaswa achukue hatua za haraka kuwashughulikia wote waliohusika na kashfa hiyo ili wananchi wasimnyoshee kidole kuwa na yeye alihusika katika mpango huo.


Akizungumzia historia ya mpango wa kununuliwa kwa rada hiyo, Profesa Lipumba alisema mpango mzima ulianza kupangwa mwaka 1995 lakini viongozi waliokuwa wakihusika waliogopa kuutekeleza kwa kumuhofia Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere aliyefariki dunia Oktoba 14, mwaka 1999.


“Waliogopa kwa sababu walijua kuwa angeupinga kwa nguvu,” alisema Profesa Lipumba.


Alisema baada ya kufa kwa Mwalimu mwaka 1999, mpango huo ulianza kutekelezwa na alidai kwamba dola milioni nane za Marekani ziliwekezwa kwa ajili ya utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mpango huo.


Profesa Lipumba alisema kwamba ingawa viongozi waliohusika walijua kuwa rada hiyo ina teknolojia ya kizamani na ilikuwa imeshindwa kununuliwa popote duniani kutokana na ubovu iliokuwa nao, waliendelea na mpango huo bila kujali madhara hayo.


“Mimi baada ya kujua mpango huo nililiandikia barua Bunge nikiliomba lizuie ununuzi wa rada hiyo, lakini Waziri wa Fedha wa wakati huo alinijubu kuwa pilipili iliyoko shamba inakuwashia nini?


“Bi Claire Short wa Uingereza naye kwa kutambua ubovu wa rada hiyo na kuwaonea huruma Watanzania alipinga kwa nguvu kununuliwa kwake na akasafiri hadi hapa nchini, akakutana na Mkapa ili am-support kupinga kununuliwa rada hiyo.


“Ajabu Mkapa alisema Watanzania wanataka rada hiyo hiyo, akaishiwa nguvu, rada ikanunuliwa, kamisheni iliyotengwa kwanza ilikuwa asilimia moja lakini dili lilipofanikiwa ikawa asilimia 30,” alisema Profesa Lipumba.


Alionya kuwa mipango yote inayofanywa na serikali kwa kushirikiana na Kampuni ya BAE System na wakala wake aliyeko Jijini Dar inapaswa kuchunguzwa ili kujua pesa ya Watanzania iliyopotea.


Aliitaja baadhi ya mipango hiyo kuwa ni pamoja na ununuaji wa ndege ya rais na mpango unaoendelea sasa wa kununua helikopta.
 
Sasa hivi nibano tu hakuna kupumua hadi swala hili liishe...

DrWHO,

Kweli kabisa maneno yako. Mimi binafsi sioni kabisa tatizo la kuwepo rada nchini ... ni kweli yawezekana tunaihitaji sana lakini kwa kiasi gani zaidi ya ustawi wa jamii? hilo sina hakika maanake miaka ya nyuma ukanda wa mashariki kulikuwa na vurugu nyingi sana na hatari kwa usalama wa nchi yetu.
Kinacho nivuta zaidi ktk hoja hii ni RUSHWA, rushwa iliyotumika ni nafasi nzuri sana kwa uongozi wa sasa kuweza ku-deal na tatizo letu kubwa sana. RUSHWA..
Kwa hiyo kama ilivyokuwa muhimu kuwa na hiyo rada, ni muhimu pia sasa hivi kupambana na Rushwa kwani hii ni moja ya athari kubwa inayoturudisha nyuma. Ukimfumani mwenza (mke/mme) ni nafasi tosha kabisa ya kuvunja ndoa mbaya lakini ukiacha na kusamehe basi utakuwa umekubali zinaa ndani ya nyumba yako.
Ni hiyo commission ya USd millioni 12/- inayogomba...
 
Mzee Mwawado,

hebu tupe nyeti kidogo kuhusu what is behind this RADAR
 
DrWHO

Radar ni muhimu na ilikuwa inatakiwa lakini sio ya kijeshi ambayo gharama ni kubwa.
Consultation ya Bongo ni kuandika kwenye vyombo vya habari and then bila hata kujua nani aliulizwa inatekelezwa, sio kama ziile consultation ambazo zinafanyika Ulaya.

Mfano consultation ya kuwakaribisha Rwanda na Burundi kwenye jumuiya ya Afrika Mashariki, Je umeona matokeo yake; Hiyo consultation ilifanywa baina ya JK, M7 na Kibaki, sasa kweli hii ni consultation?

Vile vile ipo hii mpya ya kuunda Umoja wa siasa wanajiconsult wale ambao wanataka kula na kushiba, what a joke?
 
mimi ninafikiri kwa sasa safari za JK asitishe kidogo kwa sababu amejitambulisha sana sasa kuhusu rada inampunguzia sana uwaminifu na ujasiri aliyo kuwa nao wakati akijitambulisha katika mataifa mengine pia wawekezaji sasa wakiona ni mtu wanamuona hivyo basi imani ina pungua sana sasa huyu rais wetu mbona amashikwa na kigugumizi alipokuwa anahujiwa na BBC kuhusu rada na matembezi yake ya kila siku na watanzania wanapenda kumuona ofisini mimi nina jua kitu JK na Lowassa wanapenda zile zawadi wanazopewa huku safarini hii ni ...... kwa kiongozi au ikulu kuna kunguni?

Haya ni malalamikokutoka kwa wasomi wa TZ waishio UK JK umejishusha sana pia maongezi yako ukiongea na wawekezaji unaongea kama unaongea na watu wa Ruvuma wakati wa kampani sijui bwana kama ni kweli..
kuwa sirizi basi!!!! ninajua unaweza,

jingine ni hao wafanyabiashara unao tembea nao ni pumba tupu hata kujieleza hawajui, wanaakili za kizamani hawajui mfumo wa biashara wa ulaya, marekani na nchi nyingine, hawana pesa, siyo wabunifu, ni watu wenye bahati tu wachimba madini. mwana apolo mererani ambaye ofisi iko mfukoni,mimi sioni kama ni msaada kwao ,

kwa sababu wawekezaji wamekwenda shule unaenda kumkutanisha na mtu ambaye ajasoma eti kwasababu alitoa mchango mkubwa kwenye kampani ya CCM sasa wewe kama Rais unawasaidia nini ,na wao wanajisifia wanakula na Rais na kulala hotel moja na Rais ndicho walicho kwenda kukitafuta? .

Ushauri kwa RAIS WA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MUHESHIMIWA JAKAYA M. KIKWETE. kama umampango wa kusafiri na wafanyabiashara wa Tanzania fanya hivi tafuta mshauri wa biashara wa kimataifa awafundishe jinsi ya kuongea, mfumo wa biashara wa kimataifa,jinsi ya kumshawishi mwekezaji, pasonalite,
lugha,apiarensi, wengine ni walevi muda wote sasa wako vokasheni au na mengine mengi kama nimekosea ninaomba marekebisho,

Hii ni aibu kubwa Rais siyo mfanyabiashara hajui haya mambo, yeye kazi yake nikuwatambulisha tu sasa ninakumbuka wamekuja wengi tu na Rais Mkapa hakuambulia muwekezaji hata mmoja sasa hawa watu wetu bado hawako kimataifa wanajua Dubai tu kwenda kununua bidhaa.

Wawekezaji wanao kuja Tanzania wanakuja wenyewe na ndiyo uoni wazawa ndani ya kampuni zao sasa safari za nini? angalia kampuni zote za wawekezaji niambie nani mzawa kama siyo mwajiriwa, hii inaonyesha wafanya biashara wetu hawana ushawishi katika biashara za kimataifa.

kuna majina nikutajia hapa wametembea na Rais kama bodigadi au mpambe wa JK

hawa wengine hawana pesa wana manyumba,mashamba,migodi, na hati ziko bank wamekopa mamilioni mwekezaji awezi kuingia tu sehemu kuna deni wanatujua style yetu ya biashara ndiyo maana wakija hawataki mzawa sasa muwekezaji akitaka kuona hati za mali yake atafanya nini au atamuonyesha nini? ili waanza biashara

JK saa nyingine unalipa fazila kishanba sana unatembea na watu siyo waelewa wao wanaona sifa kuwa na Rais safarini wengine wamesha zoea kila safari ya Rais nao wapo wanatowa wapi pesa zakutembea na wewe,Rais anatumia pesa za walipa kodi, wao kila safari wapo hawani majambazi na wauza madawa ya kulevia ambao unaogopa kuwataja majina yao,

sasa jamani sisi tujiulize mtu wakawaida hawezi kutembea akacha familia yake eti anatafuta wawekezaji wakati lugha inampashida anatembea na vijarida,vipeperushi, kweli tuna kazi .....

elimu kwanza .......
 
Maneno haya si ya Hasara hata mara moja . Ni faida tupu na shule kubwa kwa wale wajinga Mtetezi na Mtoa Ukweli na Rais wa Nchi .JK unakula vubaya Nchi yetu tafadhali ona aibu na kumbuka kuna mwisho wa haya .
 
mmenigusa sana ,well tatizo la jk kupata kigugumizi kwenye rada ni wazi,yeye kama waziri wa zamani wa mambo ya nje hii radar hawezi kukwepa kuhusika ,so akikubali kuwa palikuwa na rushwa ni sawa ma kusema alipata mugawo..sasa tunaomba mtu mwenye majina maafisa ya watu waliojadili kwa niaba ya tanzania,ooffcourse chenge [mwanamtandawo] kwa nafasi yake kama mwanasheria mkuu kwenye list hatakosa ..

kuhusu suala la wafanyabiashara ,nilishawahi kutahadharisha wakati waziara ya america ,kuwa tuwe makini tusije peleka wasanii ..kama hakuna wafanyabiashara wenye hadhi ya kuwa kwenye presidential tour ni bora wasiende..au bora kupeleka wachache,nashauri tuwe wazi na tuwe na utaratibu wa kuwa na list ya wafanyabiashara wazawa wanaoheshimika [most respected business people in tanzania ] kenya wanayo hiyo na pia kila mwaka kwa kushirikiana na price water huandaa most respected componies in east africa...tanzania pia kuna wafanyabishara wanoheshimika kimataifa mf bakhresa na wengine.
pia katika hili la wafanyabishara waliokuja london kama kuna mtu anayo list atupe hapa isije kuwa walienda watoto wa mjini wa salamander
 
Phillemon mikael,
eeeh bwana wee mbona umetudharau sana vijana wa Salamadar!...

Hujui kwamba pale ndio maskani yanayounganisha wafanyabiashara wa nje na nchini. Pale kuna vijana wenye exposure kubwa ya nje na wanafahamu kinachokwenda nje badala ya ndani tu.
Biashara ndugu yangu Ujanja, Bakhresa na fedha yake anaweza kuchemsha viabya vibaya inapofikia kutangaza mazao yetu. Kuna mtu alikuja na viatu vyake vya kibongo hapa ati anatafuta soko. Sasa unafikiri bila vijana wa mjini ataweza kweli?...

Subiri basi nikupe tip ya kutoka Salamandar, kama ningekuwa huyu jamaa ningemshika koo Jay Z na Biyonce (walivyokuja Bongo) waweze kutumia majina yao ktk lebel ya viatu vyangu. Design yote inafanyika US na watu wake kisha Bongo mnatengeneza viatu hivyo vya ngozi ya nyoka sijui mamba. Huhitaji faida kubwa gawana na watu utaendelea lakini kutangaza mali ya Bongo Ulaya bila kuwa na kifua mshikaji ni kujidanyanya... yale yale ya kahawa ya Ethiopia. Siku hizi uzuri wa kitu jina!... quality ni matokeo.

Kibaya Hujitembeza na kizuri hujiuza!...
 
bw. Mkandara.. Business ni Art!
Especially International Business!
Sio lazima mmiliki wa biashara ndo ufunge safari na JK!
Wabongo inabidi tuamke tujifunze namna ya ku-deal na dunia hii ya utandawazi!
matokeo yake ndo haya mtu anaandamana na Rais halafu anabeba buti za ngozi ya Chatu. Hivi akitokea mwekezaji akamaindi hiyo biashara.. jamaa anaweza ku-supply buti za kutosha kweli?
na hao 'Vyatu" watatoka wapi?
 
kaka mkandara ,siku hizi baada ya manji kununua salamander ,wanataka kuivunja though watu wa antiquities wamekataa...siku hizi job less coner imehamia stears..yes unanunua kahawa unazugia hadi jioni..wengine na vitendea kazi . unadhifu kwanza hadi lap top siku hizi vijana wanakua nazo busy wanachapa kazi..sasa je ,,lunch time unaenda ferry kuna mama ntilie poaa ...
so braza vijana wa mjini wengi nawakubali tena wamesoma au wengine ni wastaafu wasomi na redundant wanaoshinda wakipata tembo pale georges grill[nbc club],sasa kama una ishu za kisanii utawapata wataalaam pale ,wale wangewezeshwa na wakaacha ishu za kupiga tungefika mbali kijasiriamali...

sasa nitasikitika sana kama kwenye list ya safari tunapeleka watu dizaini ya papaa..tuweke targets za investments ie commercial farming na tu advertise globally badala ya kubeba vihiyo na maimunas
 
Brutus,

Nakubali kabisa kuwa biashara ni art!... hii haina kipingamizi lakini pia kubmka Bongo bado kabisa hatujafikia umri huo kibiashara. Wabongo watakutia mchanga wa macho na kujitangaza wao ama kuuza deal.. Unajua tena Bongo watu hutafuta penyu za kujitarijisha kwa kubomoa badala ya kujenga.
Ni vugumu sana kufanya biashara nje ktk mila zetu, hujui wa kumwamini. Ukimpa mtu mtaji fumba macho na mara nyingi mtaji haurudi hesabu hiyo kama sadaka.
Mimi nilijaribu tu kumwonyesha ndugu yangu Phillemon mikael kuwa nafasi kama hizi zimetolewa kwa Watanzania wote wenye viwanda vyao na watapenda kujiendeleza zaidi. Mwenye mali awe mtu wa Salamandar au Bakhresa, kikubwa ni umuhimu wa mali hiyo ktk kuuza nje na pengine faida kwa nchi. Mwenye viatu vya chatu ndio hivyo, dunia hii imekuwa wa biashara labda inabidi kuanzisha ufugaji wa chatu vilevile!... Unajua tena nyama yake huko Asia ya mbali ni soko vilevile!
Ukisikitikia Chatu mbona kondoo na mbuzi hatuna wakili? heee! heee! heee!
 
Ufugaji wa Chatu!
Kondoo na Mbuzi hatuna Lawyers sio!?
Dah kaka mkandara leo si mchezo!
 
Mikael tuombe Msamaha sisi tunao kula ferry .Watumishi wengi wa Serikali tunakula huko tunapaitwa HILTON HOTEL

Una pesa kidogo unashiba sana .
 
Back
Top Bottom