The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

Dr.WHO,

Yote tisa..kumi ni kwamba wachunguzi toka nje huja TZ mara kwa mara kuchunguza mambo kibao na mengi yanahusiana sana na mikopo ama misaada yao!..it doesn't matter huwa wanakuja kabla ya utoaji wa fedha yoyote ile. Chini ya mikataba yao ya misaada kila nchi imetuma wawakilishi wake kufanya uchunguzi nchini tena mara nyingine kwa gharama yetu sisi (walipa kodi).

Pili, sielewi kwa nini bado unadai kuwepo kwa charitable organisation hali swala hili lilifka hadi bunge la Uingereza kabla kabisa rada haijanunuliwa. na ilikuwa scandal kubwa kwa Blair right from the start na hata baadhi wabunge wachunguzi walikuja TZ na kuzungumza na baadhi ya viongozi wetu -Wakiwemo hao uliowataja hapo juu.
Sasa kuandikwa kwa barua hii kutasaidia sana kwa vyama vya upinzani Uingereza kupata sababu na msukumo toka kwa wananchi wa Tanzania na kizuri zaidi ni kwamba upelelezi uliokwisha fanyika kabla na baada ya ununuzi umepitia vyombo vya juu. Hii ni sauti ya wananchi ambayo hawajawahi kuisikia kabisa!
Kumbuka pia ile scandal ya Iran-Contra ilivuma sana kutokana na wapepelezi wa nje na hasa waandishi wa habari ambao walikwenda huko South kupeleleza na kuziweka wazi.

Who knows, Dr.WHO kujaribu kitu ni bora kuliko kukaa kimya tukitegemea kuwa na maelezo yote ambayo hayawezi kupatikana. Scandal za watergate na kadhalika zote zimetokana na viamsho vidogo sana lakini baada ya uchunguzi mkubwa mambo mengi yalikuja bainika tena kortini.

Mimi naamini kabisa kuwa vyama vya upinzani Uingereza vinahitaji kiamsho sio lazima tuwe na ukweli wote lakini ikiwa madai yetu yatakuwa na nguvu ya kumwangusha Blair they will go for it. Fedha, Power, na sheria zote wanazo wao. haiwezekani kabisa fedha za ununuzi wa rada kuwa ni charitable org. kwani bunge la Uingereza wenyewe walipinga sana wakisema rada hiyo ina-cost Tanzania zaidi ya USd 40/m, nchi ambayo ni maskini kupindukia.
 
Mkandara

FYI Blair anaachia hatamu kabla ya mwezi August, hivi sasa yupo katika harakati za kukabidhi madaraka kwa Brown.
 
DrWho, nashukuru kwa majibu yako hata hivyo maswali yangu bado yanabakia:

- Kwanini Tanzania iliamua kununua rada hii ya matumizi ya kijeshi na kiraia?

Hili sina jibu ambalo ni conclusive lakini inawezekana kuwa ma consultants waliwaambia kuwa ni bora kwani tutakuwa tunaua ndege wawili kwa jiwe moja na itakuwa ni bargain nzuri tuu....vile vile usisahau kuwa inawezekana ikawa WU(Wizara ya Ulinzi) waliulizwa msimamo wao wa kushare lakin kwa jinsi ninavyowajua wanajeshi sidhani kama hili walikubaliana nalo nadhani unaelewa wanajeshi wanavyopenda kufanya mambo kivyao bila kucompromise kazi zao


- Ni tishio gani la anga ambalo lililazimisha serikali kung'ang'ania lazima iwe ni rada hii? Ni nchi gani iliyotupa tishio hilo na kwanini Watanzania hawakuambiwa kuwa tunatishiwa kijeshi!?

Yeah hili ni rahsi sana kwani tumezungukwa a maadui wa kila namna mfano MUSEVENI na pesa zake za mafuta kila kukicha ananunua militari kits toka CZECH REPUBLIC,CHINA,UKRAINE pamoja na ISRAEL sasa kwa hali ya kawaida sisi kama majirani tuna kila sababu ya kuwa attention kwani tuna historia ya kwenda vitani na hawa jamaa,the same applies to KENYA na hao magaidi ambao sasa hivi wanauwezo mkubwa sana tu wa kijeshi.

La kwa nini hatukuambiwa kuwa tunatishiwa kijeshi linatofautiana kwani kuna issue zingine za kiusalama wa Taifa ambazo hazihitaji kuwa katika PUBLIC DOMAIN unless necessary,pili nchi yetu hatuna culture ya kuwa transparent na issue kama hizi,tatu uzembe wa wabunge wetu kuuliza mambo haya bungeni sasa waliopo juu nao wanaona hakuna haja ya kudisclose mambo haya...nadhani mtiririko mzima unavyofanya kazi ndio wenye matatizo kwani naamini sheria ziko ambazo zinawapa wananchi right ya kujua haya lakini of course kuna namna ya kuget around them


- Ni kwanini rada hiyo imegharimu Dola milioni 40 wakati kuna mabenki na wafadhili wengine ambao walikuwa tayari kutusaidia kupata rada ya kiraia, ya kisasa na ambayo ingetupa usalama wa anga kwa bei ya robo ya hiyo?


Kwa sababu hiii ilikuwa ni BILATERAL agreement kati ya serikali yetu na serikali ya UK, na hiii ingetupunguzia mzigo mkubwa wakugo around kubeg kwa benki zingine ambazo zingetutoza interest rates kubwa zaidi ya Barclays,pili be very wary na hao wanaoitwa waWAFADHILI kwani huwa wanakuja na smal prints ambazo zinatumaliza zaidi kuliko initial deal.Vile vile sisi tunauhusiano mzuri na wasikunyingi wa kununua kits toka kwa waingereza sasa hili nalo nadhani walilitake into consideration lakini sisemi ni excuse ya sisi kupata bad side of of the deal (kama ni hivyo)

- Katika ununuzi unaomhusisha dalali, dalali hulipwa aidha na mnunuzi au na muuzaji. Hadi hivi sasa dalali amekiri kupokea malipo ya dola milioni 12 toka kwa muuzaji. Je mnunuzi (Tanzania) alimlipa dalali huyo malipo yoyote, kiasi gani, na nje ya hizo Dola milioni 40?

Hii sitegemei kama inaweza kutoka japo bwana Mwanakijiji IDEALISTICALLY uko right lakini REALISTICALLY uko wrong kwani hii ni business na siku zote kuna kitu kinaitwa confidentiality ambayo sheria zipo kuilinda hii hivyo usitegemee kama information hii ikawa disclosed kwani kuna watu wata SUE na COUNTER SUE na matokeo yake tutapoteza pesa nyingi kuliko ambazo tayari tumeshapoteza na hili la kulipa kamisheni kwa jamaa ni halali yao kwani ni sisi ndio tuliongia contract nao na tulijua kuwa we have to honor oursede of the deal

sasa kama hili ni kosa au la hilo si tatizo la dalali



- Je, kuna ofisa yeyote wa Tanzania ambaye amepokea malipo toka kwa dalali huyo nje ya nchi na maofisa waliohusika na ununuzi wako tayari serikali iwatake waidhinishe akaunti zao nje ya nchi zichunguzwe kujua pesa walizonazo humo zimetoka wapi?


Hili nilishakujibu katika post yangu hiyo hapo juu kuna hiyo BANKING CODE huwezi kupata kitu na kwa taarifa yako siku hizi si lazima ulipwe pesa inawezekana ikawa pesa ziko interms of STOCKS au PREMIUM BONDS sasa mabenki nao hawataki kuwa sued kwa sababu wamebreach CONFIDENTIALITY AGREEMENT kwa sababu y uzembe wa serikali


- Wakati wa ununuzi wa rada hii aliyekuwa Waziri waa Mambo ya nchi za nje alitetea kwa kusema kuwa tunahitaji rada hii kwani itatuongezea mapato na kuongeza utalii. Je tangu rada hii inunuliwe ni kiasi gani kimekusanywa kwa sababu ya rada hii (tukikusanya mapato toka nchi zinazopita katika anga letu). Je ni watalii kiasi gani ambao wameongezeka sababu ya matumizi ya rada hii?

HII NISHAIJIBU KATIKA POST YANGU YA AWALI HAPO JUU

- Lengo la rada hii tuliambiwa na Rais Mkapa ni kuongeza usalama wa anga. Je kabla ya kununuliwa kwa rada hii ni ajali ngapi zimetokea au nusura kutokea angani, na kununuliwa kwake kumepunguza ajali hizo kwa kiasi gani?

Details ainzaweza kupatikana toka idara ya Anga ambao nao ni part ya seriakali lakini usisahau kuwa viwanja vyetu vingi havina mitambo ya kisasa ya anga ,na evidence ziko za kuonyesha near miss incidents lakini sijui kama zilitokana na uzembe wa RUBANI wetu au RADA. vile vile nadhani unaelewa kuwa haya juzi tu tumempoteza naibu waziri(ofisa mkubwa serikalini) kwenye ajali ya ndege


- Rada hii tuliyoinunua ina uwezo wa kuangali theluthi moja tu ya nchi na hususan viwanja vya ndege vya Mwalimu Nyerere na kile cha KIA. Ili kuweka ulinzi na usalama kwa nchi nzima tunahitaji rada nyingine mbili zenye uwezo kama huo. Je tuko tayari kununua rada nyingine kwa gharama hiyo hiyo kila moja ili kutimiza lengo la kuilinda anga letu na kutupa usalama? Tuko tayari kutumia dola milioni 80 kufanya hivyo?



Capability ya rada hii iko QUESTIONABLE lakini vile vile usisahau kuwa suala hili linahitaji consultation toka idara mbali mbali za serikali na personally nadhani dola milioni 80 ni ndogo sana when it comes to national security lakini hii si semi kuwa nina ENDORSE rushwa na mabaya mengineyo AMBAYO INAWEZEKANA YALITOKEA


- Kuna uhusiano gani kati ya kununua ndege ya Rais kwa karibu kiasi hicho hicho cha rada na kumtumia dalali yule yule, dalali ambaye anafanya biashara ya silaha na serikali yetu kwa muda mrefu? Ni nani anampa dili hizo dalali huyo na mtu huyo ananufaishwa vipi?

Hii ni biashara na pale mjini wako jamaa wengi ambao nao wanadeals zao, sasa kama huyu mhindi anacontacts zake ambazo yeye anazitazama na anawatake care vizuri sidhani kama ni tatizo kwake kupata access...ni biashara na yeye ni mtafutaji hivyo siwezi kumlaumu kwa hilo

- Kama tumeweza kumfikisha mahakama Balozi kwa kughushi na kutumia vibaya nafasi yake na kununua nyumba ya ubalozi kwa bei ya chini wakati akitoa stakabadhi za kuonesha bei ya juu, ni kwanini hatufikiri kuwa kuna mtu katika serikali ambaye inawezekana kabisa amefanya jambo hilo kwenye rada? Mtu huyo ni nani?

Kumfikisha mtu mahakamani hakumaanishi kuwa kafanya kosa kwani sheria bado inamlinda as HE IS STILL INNOCENT UNTIL PROVED OTHERWISE BY THE COURT OF LAW....na huwezi kuwafikisha watu waserikali mahakamani kwa kuwa na hiyo CISRCUMSTANTIAL EVIDENCE...otherwise wanaweza kucounter sue na itaicost serikali zaidi sasa cha muhimu ni kuziba hiyo mianya ambayo inapelekea hali hiiikutokea

- Uchunguzi wa SFO ni kwa ajili ya serikali ya Uingereza. Uchunguzi huo hata kidogo hautuzuii sisi kuanzisha uchunguzi wetu wenyewe. Je serikali iko tayari kufungua uchunguzi huru? Je kuna chombo chochote kinachoweza kuanzisha uchunguzi bila ya kutaka ruhusa kwa Rais?

Hili nakubaliana na wewe na last time niliambiwa kuwa uchunguzi unafanyika na labda tu jamaa hawajaiweka katika public domain lakini uchunguzi tayari uko mbioni


Hayo ni maswali yangu na ya Watanzania wengine wengi.

na maswali valid na kama mwenye uchungu na nchi yake nafurahi kuona kuwa sio kila mtu amegive up
 
Nilikuwa sijawahi kusema kitu kwenye hili maana nilikuwa sina ukweli, sasa finally ukweli unaaanza kujitokeza na huku bongo moto unawaka,

leo serikali ya US imeamua kujitosa na hii issue wameleta watu wa FBI kufuatilia kwa kina, Muungwana anawalaumu UK,

hapa bongo leo nilipata bahati ya kuongea na mhindi mmoja anayehusika, inasemakana kuwa kuna mhindi mmoja tu ambaye amekuwa middleman wa milo yote kuanzia Richmond, Radar, mpaka ndege za rais, huyo mhindi nimeonyeshwa lakini nilipomgusa akakataa kabisa kuongelea hizo deals, nina wasi wasi kuwa huyu mhindi atapotea very sooon,

lakini finally, ukweli unaanza kukaribiwa, Mzee Mahalu kesi ni nzito, maana ni afadhali kushitakiwa na polisi lakini sio PCB na get ready kusikia majina mengine mazito yakitajwa maana Mahalu aliapa kuwa hakul;a peke yake, tunafuatilia kwa makini yote!
 
Quote mkandara
Dr.WHO,

Yote tisa..kumi ni kwamba wachunguzi toka nje huja TZ mara kwa mara kuchunguza mambo kibao na mengi yanahusiana sana na mikopo ama misaada yao!..it doesn't matter huwa wanakuja kabla ya utoaji wa fedha yoyote ile. Chini ya mikataba yao ya misaada kila nchi imetuma wawakilishi wake kufanya uchunguzi nchini tena mara nyingine kwa gharama yetu sisi (walipa kodi).

kwa sbabu serikali zao zina kitu kinaitwa CKECKS AND BALANCE ambazo ziko transparent na wananch wana access ya kujua ni kiasi gani serikali inaspend kwenye kuwasaidia watu Africa na kadhalika vile vile kuna umuhumi wa kujua hawa jamaa wanatuwahi katika kuweka masharti ambayo sisi kama wenye shida huwa mara nyingi hatuquestion


Pili, sielewi kwa nini bado unadai kuwepo kwa charitable organisation hali swala hili lilifka hadi bunge la Uingereza kabla kabisa rada haijanunuliwa. na ilikuwa scandal kubwa kwa Blair right from the start na hata baadhi wabunge wachunguzi walikuja TZ na kuzungumza na baadhi ya viongozi wetu -Wakiwemo hao uliowataja hapo juu.

Samahani ni wapi nimeandika kuhusu charitable organisation?

Ndio wabunge walikuja na mimi binafsi nilikutana na Clare Short kipindi hicho hicho na baada ya kuresign na kama miezi miwili iliyopita nilipata nafasi ya kumuuliza aliyechukuwa nafasi yake bwana HILLARY BENN kwenye hafla pale DFID na akaniambia kuwa what comes first ni kuwa waingereza wanaoni ni responsibility yao kuisaidia nchimaskini kama Tanzania na pili issue ambayo ni bilateral agreement basi wao waaona ni bora zaidi kwa kampuni ya kiingerea kuchukua tenda hiyo, na mama Short alipoambiwa hiyo hakubisha kwani hii ilikuwa political minefield kwake, na pili lazima uelewe kuwa CLARE SHORT na TONI BLAIR walikuwa na bado ni PAKA na MBWA na SHORT alihakikishiwa kuwa kutakuwa fairness kuhusu hili na GORDON BROWN ambaye alikuwa naelewana naye zaidi

Vile vile usisahu kuwa SHORT hana uhusiano mzuri na media hapa na angeletamatatizo basi ilikuwa rahisi kumharibia not necessarily kupitia issue hii ya RADA bali hiyo ya kumtupa mtoto wake,hana interest na wafanyakazi wa kule BAE systems and so on


Sasa kuandikwa kwa barua hii kutasaidia sana kwa vyama vya upinzani Uingereza kupata sababu na msukumo toka kwa wananchi wa Tanzania na kizuri zaidi ni kwamba upelelezi uliokwisha fanyika kabla na baada ya ununuzi umepitia vyombo vya juu. Hii ni sauti ya wananchi ambayo hawajawahi kuisikia kabisa!

Vyama vya upinzani sio issue lakini ujue kuwa network ya BAE SYSTEM ni kubwa kuliko unavyofikiri i wish nigeweza kukupostia majina ya mashare holders wakubwa pale BAE SYSTEMS, kwa taarifa yako wengi wao ni conservatives na Lib dema...(hata hivyo Ming Campbell wa LIBERAL DEMOCRATS) aliliuliza hili bungeni na akajibuwa kuwa hakuna anayeweza toa statment kwani bado issue inafanyiwa chunguzi na for legal reasons hawawezi kutoa matamshi zaidi ya hayo

Labda kazi ingekuwa rahisi kwa CHADEMA ambao wana uhusiano wa karibu na CONSERVATIVES lakini hii nayo ni ngumu kwani nadhani unajua kuwa akina MYIKA mpaka leo wameshindwa kufafanua kuhusu uhusiano wao na CONSERVATIVES ulivyo sasa dont expect much from opposition kuhusu hili

Kumbuka pia ile scandal ya Iran-Contra ilivuma sana kutokana na wapepelezi wa nje na hasa waandishi wa habari ambao walikwenda huko South kupeleleza na kuziweka wazi.


No, IRAN-CONTRA leaks zilitokea kule kule Pentagon ambako kamaa waliamua kuileak kabala huyo OLIVER NORTH na wenzie hawajaharibu lakini ili backfire kwa sababu Washington Post tayari walishaipata na hata hao jamaa wa LATIMES na wengine walipojimwaga huko Nicaragua it was too late pentagon walishaweza kuicontain lakini sisemi kama haikuwa big embarassment kwa akina Brezinski kule state department

Who knows, Dr.WHO kujaribu kitu ni bora kuliko kukaa kimya tukitegemea kuwa na maelezo yote ambayo hayawezi kupatikana. Scandal za watergate na kadhalika zote zimetokana na viamsho vidogo sana lakini baada ya uchunguzi mkubwa mambo mengi yalikuja bainika tena kortini.

Tofauti kati ya scandal za watergate na hii ni kuwa kule watergate akina DEEP THROAT walikuwa na evidence ya kutosha na akina Bob Woodward walikuwa hawana haraka ya kuipublish mpaka walipokuwa na uhakika na source yao.kujaribu zi mbaya lakini kujaribu kuendane na ushahidi wa kutosha isije kuwa yale yale ya CUF -LONDON/UK kuishitaki serikali ya Tanzania house of Lords in 90's matokeo yake nadhani unayajua

Mimi naamini kabisa kuwa vyama vya upinzani Uingereza vinahitaji kiamsho sio lazima tuwe na ukweli wote lakini ikiwa madai yetu yatakuwa na nguvu ya kumwangusha Blair they will go for it. Fedha, Power, na sheria zote wanazo wao. haiwezekani kabisa fedha za ununuzi wa rada kuwa ni charitable org. kwani bunge la Uingereza wenyewe walipinga sana wakisema rada hiyo ina-cost Tanzania zaidi ya USd 40/m, nchi ambayo ni maskini kupindukia.


Hili nilishakujibu na naweza kukupa mfano mdogo sana

Tazma kwa undani deal ya AL YAMAMA iliendaje wakati huo huo wasaudi wanawauwa wanajeshi wa UK kule Afghanistan na Iraq,Saudi Arabia serikali yake haina Demokrasi na wanawake hawana rights zozote za maana kama binadamu lakini waingereza walifumia mabo yote haya wakaamua kuwuzia hiyo ndege at a cost of 40 billion pounds

Never underestimate the power of money na hilo wazungu wanalijua sana tuu
 
Confidentiality agreements and banking codes absolutely rubbish, hizi ndio zile tunaita janja ya Nyau tikisa Makia. Mbona wameweza ku-freeze pesa za Osama and company kule tora Bora? Mbona wameweza ku-freeze pesa za Robert Mugabe and company?

We know the West better than that, at least the September 11 was an eye opener. Mwalimu (R.I.P.) alisema wakati mwingine huhitaji sheria wakati watu wanajifanya wajanja kukwepa sheria, ndio maana kuna presidential powers. Lets not cheat ourselves.

UK wameanzisha SOCA hivi karibuni haina zaidi ya mwaka mmoja, (kama unapenda unaweza kutembelea hapa kujua kazi zao n.k. http://www.soca.gov.uk/index.html) hawa wakikushitukia wana power ya kuchukua mali yako yoyote wakati wowote mpaka u-prove kwamba umenunua kihalali na umelipa kodi kihalali, mbona hawakufungulii kesi mahakamani na ni jukumu lako ku-prove sio wao waende mahakamani. Hata hawa BAE sasa hivi wanahaha kwa sababu ya deal zao nyingi duniani ni rushwa tupu. kama hawa vibaka wangekuwa UK wangeozea jela na kufilisiwa.
 
Nilikuwa sijawahi kusema kitu kwenye hili maana nilikuwa sina ukweli, sasa finally ukweli unaaanza kujitokeza na huku bongo moto unawaka,

leo serikali ya US imeamua kujitosa na hii issue wameleta watu wa FBI kufuatilia kwa kina, Muungwana anawalaumu UK,

hapa bongo leo nilipata bahati ya kuongea na mhindi mmoja anayehusika, inasemakana kuwa kuna mhindi mmoja tu ambaye amekuwa middleman wa milo yote kuanzia Richmond, Radar, mpaka ndege za rais, huyo mhindi nimeonyeshwa lakini nilipomgusa akakataa kabisa kuongelea hizo deals, nina wasi wasi kuwa huyu mhindi atapotea very sooon,

lakini finally, ukweli unaanza kukaribiwa, Mzee Mahalu kesi ni nzito, maana ni afadhali kushitakiwa na polisi lakini sio PCB na get ready kusikia majina mengine mazito yakitajwa maana Mahalu aliapa kuwa hakul;a peke yake, tunafuatilia kwa makini yote!

Usisahu kuwa sisi tuko notorious kwa kuchelewesha kesi

Hatutokuja na conclusion mpaka hao ninao waita SERIOUS FARCE OFFICE watakapomaliza yao

lakini hii siyo excuse yetu kuwa so incompetent
 
Lunyungu,
Mshikaji inaonyesha wewe una kimeo fulani hapa...
sasa hawa watu wanaoishi nje mbona huwaulizi kwa nini wanachangia mada hizi!..Kwa uchungu gani waliokuwa nao ikiwa wao sio Watanzania?
Mshikaji unashindwa kuunganisha vitu na kufahamu kuwa hiyo dual inahusiana sana na wakazi wa Uingereza na ndiyo inayowapeni nyie nafasi ya kuweka sahihi ktk hiyo petition yenu ya Uingereza!.

Jamani nyie wabongo ama kweli roho za kikorosho haziwaishi.. Mimi nakuuliza wewe hapo!...
Una haki gani ya kuwa Mtanzania kuliko sisi hapa! Kama sio sheria mbovu za kidikteta hizo ambazo tunapingana nazo humu kuziondoa.

Mkandara,
Take a deep breath brother. Hilo suala la dual citizenship litakuja ama halitakuja kutegemea na watawala wetu jinsi watakavyoamka siku hiyo. Hadi sasa hivi hawalipi kipaumbele kwa sababu kama kawaida yao wanachoangalia ni maslahi binafsi. Wao, watoto wao, vimada wao na mabuzi yao wanaweza kwenda kokote nakufanya chochote bila huo uraia wa nchi mbili. Wanaona hakuna cha ziada cha kufaidi ndio maana wanaona bora wakimbilie shirikisho la Afrika Mashariki sababu siku zote wanawaza madaraka tu. Wana uhakika wa tu vyeo kule ndio mana hilo kwao ni muhimu.
Ndio maana mimi kila siku nasisitiza tunahitaji bunge, bunge, bunge lisilo la chama kimoja. Ni kuchukua wabunge kadhaa tu na kulipeleka bungeni na tayari tuna dual citizenship. Lakini leo hii tutasaini hiyo petition halafu itaenda wapi? Ikifika kwa watu wawili watu nani wataipatia msukumo unaofaa? Labda tufanye mchango tuwahonge wabunge wetu maana bila rushwa mambo hayaendi. 🙂 Nitakusanya huo mchango (rushwa).
 
Neither of the two

Kwa hiyo ni maoni yako tu hayana msingi katika ukweli. Nataka nikujibu lakini kama ni maoni yako tu sina ulazima ila umenipa mwanga of possible answers from the government. Miye natafuta mtu mwenye majibu rasmi.
 
DrWho, nashukuru kwa majibu yako hata hivyo maswali yangu bado yanabakia:

- Kwanini Tanzania iliamua kununua rada hii ya matumizi ya kijeshi na kiraia?

- Ni tishio gani la anga ambalo lililazimisha serikali kung'ang'ania lazima iwe ni rada hii? Ni nchi gani iliyotupa tishio hilo na kwanini Watanzania hawakuambiwa kuwa tunatishiwa kijeshi!?

- Ni kwanini rada hiyo imegharimu Dola milioni 40 wakati kuna mabenki na wafadhili wengine ambao walikuwa tayari kutusaidia kupata rada ya kiraia, ya kisasa na ambayo ingetupa usalama wa anga kwa bei ya robo ya hiyo?

- Katika ununuzi unaomhusisha dalali, dalali hulipwa aidha na mnunuzi au na muuzaji. Hadi hivi sasa dalali amekiri kupokea malipo ya dola milioni 12 toka kwa muuzaji. Je mnunuzi (Tanzania) alimlipa dalali huyo malipo yoyote, kiasi gani, na nje ya hizo Dola milioni 40?

- Je, kuna ofisa yeyote wa Tanzania ambaye amepokea malipo toka kwa dalali huyo nje ya nchi na maofisa waliohusika na ununuzi wako tayari serikali iwatake waidhinishe akaunti zao nje ya nchi zichunguzwe kujua pesa walizonazo humo zimetoka wapi?

- Wakati wa ununuzi wa rada hii aliyekuwa Waziri waa Mambo ya nchi za nje alitetea kwa kusema kuwa tunahitaji rada hii kwani itatuongezea mapato na kuongeza utalii. Je tangu rada hii inunuliwe ni kiasi gani kimekusanywa kwa sababu ya rada hii (tukikusanya mapato toka nchi zinazopita katika anga letu). Je ni watalii kiasi gani ambao wameongezeka sababu ya matumizi ya rada hii?

- Lengo la rada hii tuliambiwa na Rais Mkapa ni kuongeza usalama wa anga. Je kabla ya kununuliwa kwa rada hii ni ajali ngapi zimetokea au nusura kutokea angani, na kununuliwa kwake kumepunguza ajali hizo kwa kiasi gani?

- Rada hii tuliyoinunua ina uwezo wa kuangali theluthi moja tu ya nchi na hususan viwanja vya ndege vya Mwalimu Nyerere na kile cha KIA. Ili kuweka ulinzi na usalama kwa nchi nzima tunahitaji rada nyingine mbili zenye uwezo kama huo. Je tuko tayari kununua rada nyingine kwa gharama hiyo hiyo kila moja ili kutimiza lengo la kuilinda anga letu na kutupa usalama? Tuko tayari kutumia dola milioni 80 kufanya hivyo?

- Kuna uhusiano gani kati ya kununua ndege ya Rais kwa karibu kiasi hicho hicho cha rada na kumtumia dalali yule yule, dalali ambaye anafanya biashara ya silaha na serikali yetu kwa muda mrefu? Ni nani anampa dili hizo dalali huyo na mtu huyo ananufaishwa vipi?

- Kama tumeweza kumfikisha mahakama Balozi kwa kughushi na kutumia vibaya nafasi yake na kununua nyumba ya ubalozi kwa bei ya chini wakati akitoa stakabadhi za kuonesha bei ya juu, ni kwanini hatufikiri kuwa kuna mtu katika serikali ambaye inawezekana kabisa amefanya jambo hilo kwenye rada? Mtu huyo ni nani?

- Uchunguzi wa SFO ni kwa ajili ya serikali ya Uingereza. Uchunguzi huo hata kidogo hautuzuii sisi kuanzisha uchunguzi wetu wenyewe. Je serikali iko tayari kufungua uchunguzi huru? Je kuna chombo chochote kinachoweza kuanzisha uchunguzi bila ya kutaka ruhusa kwa Rais?

Hayo ni maswali yangu na ya Watanzania wengine wengi.

MKJJ mchango wangu kwa baadhi ya maswali yako:

Tukiweka masuala ya rushwa pembeni:

1. Rada ilikuwa muhimu na itabaki kuwa muhimu. Kwamba rada hiyo ina uwezo wa kutumika kijeshi na kiraia naona kama ni faida badala ya hasara kwani ni sawa na kuua ndege wawili kwa jiwe moja. Itakuwa kosa kiuchumi endapo kwa kununua rada mbili tofauti (ya kiraia na ya kijeshi) tutakuwa tumetumia pesa nyingi zaidi, lakini endapo kwa kununua hiyo moja tutakuwa tumeokoa pesa basi ni sawa. Tatizo liwe labda liwe la kiufundi kuwa "upande wa kijeshi wa rada" ukiharibika basi na "upande wa kiraia" ushindwe kufanya kazi. Baadhi ya wanajeshi wa anga (nikiozungumza nao wakati ule) walifurahia sana ununuzi huo ambao kwao waliona kama ukombozi kwani wanasema kwa muda mrefu tulikuwa tunanyanyasika na tusingekaa vizuri tungekuja kuadhiriwa siku moja. Baada ya vita ya Kagera hatukuwa tumenunua nyenzo muhimu kwa muda mrefu kutokana na kuyumba kwa uchumi. Na hata wakati vita inaanza tulikuwa almost off-guard na ndiyo maana mwanzoni tulipigwa vibaya sana. Ingekuwa kosa kurudia kosa.

2. Kumbuka tumezungukwa na nchi zenye migogoro na vita. Wenye kujua wanakwambia Rwanda na Uganda wamelimbikiza silaha kibao na ndiyo maana walipata hata jeuri ya kwenda DRC. Kwa nini tudhani siku moja hawawezi kutugeuka na sisi na wakati watu wanazungumzia Hima Empire? Ni wakati mzuri zaidi wa kujiandaa kwa vita kama si wa amani? If you want peace prepare for war!

3. Teknolojia inabadilika na hivyo ni muhimu kwa ulinzi kwenda na wakati pia ikiwa ni pamoja na kujipatia zana na vifaa vya kisasa!

4. Hiyo bei inayosemwa ya robo ni kwa ajili ya rada yenye matumizi ya kijeshi na kiraia pia au ni kwa ajili ya matumizi ya kiraia pekee? Isije ikawa watu wanazungumzia vitu viwili tofauti.

5. Kuhusu kuongezeka kwa watalii huenda ni vigumu kusema idadi iliyoongezeka kwa hakika kuwa ni kwa sababu ya rada. Kiujumla watalii wa kuja Tanzania wamekuwa wakiongezeka kila mwaka na kwa miaka kumi iliyopita, kwa mfano, idadi yao imeongezeka kutoka 295,300 mwaka 1995 mpaka 613,000 mwaka 2005. Lakini ni wazi kuwa watalii na mashirika ya ndege yanataka uhakika wa usalama wa anga. Kuna wakati Tanzania na nchi kadhaa zilionywa na ICAO kuhusu usalama wa anga zake na baadhi ya mashirika yalitishia kusitisha safari zao kwa kile kilichoitwa "African unsafe skies".

6. Madai kwamba rada hiyo inaona theluthi moja nadhani si kweli kwani katika mambo ya anga inatakiwa rada zetu zione mpaka kwa jirani na jirani aone mpaka kwetu ili kusaidiana katika mawasiliano. Ikumbukwe kuwa ishasemwa kuwa rada hiyo ilinunuliwa pia kutokana na shinikizo la Marekani ili kupambana na ugaidi katika eneo la Afrika Mashariki. Kwa mantiki hiyo, Marekani wangetaka Tanzania iwe na rada yenye uwezo wa kuona mpaka nje ya mipaka yake. Wajuzi wengine wanadai kwa hakika kuwa rada hiyo inaona eneo lote la Afrika Mashariki mpaka Djibouti! Wengine pia wanasema hivi sasa wanaotumia anga letu wanajulikana kwa hakika na hivyo wanatumiwa invoice kutulipa kila wanapofanya hivyo tofauti na zamani. Hayo madai kuwa rada hiyo si mali kitu ni danganya toto kuwa Tanzania hamna kitu lakini ni moto wa kuotea mbali!

Pamoja na maelezo yote, sina majibu kuhusu maswali mengine yahusuyo rushwa, na kamwe mchango wangu usichukuliwe kuwa natetea uozo wa Uingereza na uzembe na uvivu wa baadhi ya watendaji katika serikali yetu.
Mungi Ibariki Tanzania.
 
Dua Wrote
Confidentiality agreements and banking codes absolutely rubbish, hizi ndio zile tunaita janja ya Nyau tikisa Makia. Mbona wameweza ku-freeze pesa za Osama and company kule tora Bora? Mbona wameweza ku-freeze pesa za Robert Mugabe and company?

Well hapo umekosea kidogo.Mmambo ya kuweza pesa kwenye akaunt sikuhizi yamepitwa na wakati. pili Osama alikuwa hana akaunti kule TORA BORA na pesa nyingi alikuwa hana yey binafsi basi ulikuwa na fungu lake alilopata toka BIN LADEN CONSTRUCTION GROUP. na hawaja jamaa mpaka leo wanakula contracts middle east na hivi ninavyoongea na wewe wengine walioa na kuolewa nadi ya Royal Family ya Saudi au House of Saud. As far as Mugabe is concerned ndiyo walifrezebaadhi ya pesa lakini ma lawyer wake walishazineutralize pesa zake na still jamaa anazo nyumba zeke kule Scotland japo haziko kwenye jina lake na usisahu kuwa UK haikustawi hivi hivi walistawi kutokana na kweli ni wanafiki na wanaijuia fitna kuliko wamarekani



We know the West better than that, at least the September 11 was an eye opener. Mwalimu (R.I.P.) alisema wakati mwingine huhitaji sheria wakati watu wanajifanya wajanja kukwepa sheria, ndio maana kuna presidential powers. Lets not cheat ourselves.


Unfortunatelly some of us knew these westerners since they landed in our countries and we didnt need 9/11 to be an eye opener for us. Yeah hata kama zipo presidental powers lakini hiyo hairuhusu yeye rais kuwa ABOVE THE LAW ndio maana exective office ikiwa wrong basi wanaweza wakawa OVERULED na JUDICIARY na hata Mugabe kule zimbabwe SUPREME COURT saa zingine inaoverule decisions za Ikulu au Rais

UK wameanzisha SOCA hivi karibuni haina zaidi ya mwaka mmoja, (kama unapenda unaweza kutembelea hapa kujua kazi zao n.k. http://www.soca.gov.uk/index.html) hawa wakikushitukia wana power ya kuchukua mali yako yoyote wakati wowote mpaka u-prove kwamba umenunua kihalali na umelipa kodi kihalali, mbona hawakufungulii kesi mahakamani na ni jukumu lako ku-prove sio wao waende mahakamani. Hata hawa BAE sasa hivi wanahaha kwa sababu ya deal zao nyingi duniani ni rushwa tupu. kama hawa vibaka wangekuwa UK wangeozea jela na kufilisiwa.

Nafahamu sana kuhusu soca lakini umesahu kitu kuwa mbona hawa SOCA walitolewa nishai na jaji baada ya kuset up a sting operation kumkamata jamaa muuza unga mwingereza spain ..na waliambwa kuwa methods zao ni illegal, pili kulikuwa na skendo la watu kula pesa za VAT na serikali iliingia gharama zaidi ya 40 billion kwa miezi miwili..saka wakawafikisha jamaa mahakamani wakashindwa kwa sababu walikuwa ma gang ho katika upelelezi wao,tatu jana ilitoka report kuwa Special Branch walikuwa wanafumbia macho mauaji ya jamaa wa Unionists kule NOTHERN IREALAND na infact kes jana ilianguka baada ya kujulikana kuwa ma HIT MEN walikuwa wako kwenye payroll ya SPECIAL BRANCH sasa leo unaliza sheria ziko wapi?, Nnne SFO waliambiwa wa STOP upelelezi wa deal ya BAE na SAUDI ARABIA baada ya kuambiwa na waarabu kuwa SFO wakiendelea then wao watawapa deal hiyo wa FARANSA...matokeo yake ni nini? SFO waliambiwa kuwa investigation yao is not in national interest..haya kiko wapi?
 
Mwanagenzi, majibu yako ni rasmi kiasi gani? Je rada hiyo ina uwezo wa kiasi gani kutupa usalama wa anga na ulinzi wa anga?
 
Kwa hiyo ni maoni yako tu hayana msingi katika ukweli. Nataka nikujibu lakini kama ni maoni yako tu sina ulazima ila umenipa mwanga of possible answers from the government. Miye natafuta mtu mwenye majibu rasmi.



Depends definition yako ya kuwa yana msingi au la

wewe umenipa option mbili ambazo nimekujibu kuwa neither of them na nilitegemea ungenuliza ni ipi lakini looks like you have made your conclusion which is fair enough

Nilitaka ulitazame hili katika angle kubwa zaidi na ndio maana ya mjadala huu

lakini majibu rasmi hutopata kwani ukitaka ni either seriali ya UK ambaye last week kwenye Prime Ministers Question Time alichomoa for legal reasons, BAE ambao nao wako tight liped, SFO ambao watakuambia bado wanafanya Investigation, Huyo Mhindi ambaye naamini yuko njiani kurudu nyumbani kwake huo Hertforshire,Ubalozi wa Tanzania UK ambao watakuambia wanasuiri instructions toka Foreign,ambao wao watakuambia wanasubiri tamko toka Ikulu ambayo itakuambia waku suala hili bado linafanyiwa uchunguzi

lakini si mbaya kujaribu
 
DrWHO

Hiyo ya kuandika Tora Bora nilikuwa sitaki kuandika hilo jina lake kwani big brother huwa na mazoea ya kufuatilia jina kutaka kujua nini kinaendelea na connection ya Saudi Arabia naifahamu fika - the bottom line is The West can do whatever they want in their own countries and beyond but we can't do the same even in our own countries.
 
Dua,

Usiwe na wasi wasi

hujafanya kosa lolote lakini

nakubaliana na statement yako ya mwisho kwani uchumi wetu tegemezi unaendeshwa na pesa za walipa kosi walioko nchi za maghabribi

na hapo sisi hatuna la zaidi
 
Mwanagenzi, majibu yako ni rasmi kiasi gani? Je rada hiyo ina uwezo wa kiasi gani kutupa usalama wa anga na ulinzi wa anga?

On a light note, ni rasmi kwa kadri yanavyopatikana kwa njia zisizo rasmi! Bado nakumbuka msemo wako "Read at your own peril!"

Taarifa nyingine hizo za uwezo etc ni nyeti bro
 
Dr.WHO,
Charity umeiweka ktk assumption zako! tazama kipengele cha Assumption!

Wanabodi,
Mbona mnaanza kunichanganya hapa?

Kinachozungumziwa kuhusu rada ni RUSHWA lililotumika au sio? au tunazungumzia umuhimu wa rada!.. Jamani hata hizo ndege, Richmond, IPTL zote ni muhimu hakuna ubishi isipokuwa tunachozungumza hapa ni rushwa lililotumika. Tusipoteze mwlekeo wetu jamani kwani kufanikisha ama kutofanikisha ni kesi nyingine kabisa.
Kuhusu uwezo wa hiyo rada sidhani kabisa ni deal kwetu wala kwa waingereza ila hapa tunazungumzia sawa na mtu kununua gari hali watoto hawana chakula, pia gari lenyewe sio kwa bei iliyokuwa halali..Sasa kuna ndugu wanaojali watoto (uingereza) na sisi watoto tunayajali yote ila kinachotupa sheria zaidi ni hiyo thamani ya gari lenyewe.

Rushwa la Kiafrika siku zote ni kubomoa uchumi wa nchi yako hali wenzetu rushwa kwao ni kuchukua commission ukitumia wadhifa wako serikalini otherwise it is legal. Huwezi hata siku mohja kuona rushwa la kubomoa nchi Ulaya.. hii ni kesi isiyokwisha na inampeleka mtu jela hata kama mtu huyo ni rais.
 
Back
Top Bottom