TBC MPYA: Ushauri, Maoni na Mapendekezo ya ubora wa vipindi (Television Content)

Ndugu WanaJF,

Kumekuwepo na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi na hata hapa JF kuhusiana na changamoto ya vipindi vya Televisheni ya Taifa (TBC1). Malalamiko hayo yameegemea zaidi katika eneo la ubora wa vipindi na ubunifu.

Kwa bahati nzuri, Mkurugenzi pamoja na Watendaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) ni wadau wakubwa wa JamiiForums na huwa wanafuatilia taarifa na mijadala mbalimbali inayoendelea hapa. Hivyo tukiitumia vyema nafasi hii, tutawasaidia kuboresha maeneo ambayo yanatakiwa kurekebishwa kwa haraka.

Naomba tutumie uzi huu kutoa maoni, ushauri na mapendekezo kuhusu aina ya vipindi na ubunifu ambao ukitumiwa utasaidia kuifanya televisheni hii ya taifa kuvutia kutazamwa na kufurahiwa.

Tumeshalalamika sana. Sasa ni wakati wa kuchukua hatua na kutaja suluhu kwa mifano ili kuimaliza changamoto hii kabisa.

Karibuni sana.
Kwamuda mrefu nilishaacha kuangalia TBC kutokana na namna ambavyo wanaendesha vipindi ikiwemo taarifa ya habari. Siku mbili zilizopita nililazimika kuangalia TBC hasa taarifa ya habari ili kuona kama kuna jipya nikilinganisha na KBC, kwakweli TBC mjitathmini, haiwezekani taarifa ya habari nzima ni kusifia na kuelezea tu mambo mazuri yanayofanya na watendaji. Huenda wanalazimika kufanya hivyo ila nashauri TBC wajitahidini sana kujiweka kitaifa, inachosha na inaudhi sana kuona taarifa zilezile zenye mwelekeo uleule, kitu ingalau cha kunifanya labda niangalie labda ni michezo ila kwa kweli TBC kwa mtindo huu bado sana mnasafari
 
Heko TBC kwa kuanzisha channel ya TANZANIA SAFARI. Nawapongeza sana kwa kuanzisha channel hii, pia naomba mjitahidi kuuimarisha haswa kuifanya iache kusitasita yaani mnaita ku "scratch " kwenye kisimbuzi cha Azam. Ila nawapongeza sana huu ni mwanzo mzuri naamini wengi tutaitazama sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Heko TBC kwa kuanzisha channel ya TANZANIA SAFARI. Nawapongeza sana kwa kuanzisha channel hii, pia naomba mjitahidi kuuimarisha haswa kuifanya iache kusitasita yaani mnaita ku "scratch " kwenye kisimbuzi cha Azam. Ila nawapongeza sana huu ni mwanzo mzuri naamini wengi tutaitazama sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kweli wamejitahidi sana, ata muonekano wake ni mzuri. Uko ku scratch wapambane napo. Wajitahidi kuweka sub tittles za kizungu ili lengo la kutangaza utalii wa Tanzania duniani litimie.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tbc ya Tdo mhando n Bora kuliko itv au clouds ya sasa
Tdo alifanya Hadi ligi kuu uigereza Kuona bure
Tb n Bora kuliko tbc ya sasa
Vpnd hovyo,watangazaji ovyo
Mwanangu pekee ndo anaangalia tbc kile kipindi Cha Ubongo KIDS NA MAMA NDEGE
 
Nafikiri kwenye swala la uvaaji hii ni kutokana na tabia za mtu binafsi au iwe mishahara na posho zao ni ndogo kiasi wanakosa kuwa na bajeti nzuri kwaajili ya nguo
Tatizo kubwa sana la TBC ni kujiona kuwa wao ndo wasemaji wakubwa na watetezi wa CCM ndo maana imekosa mvuto kila kona ! Hovyo kabisa
watangazaji hawana swagga wanavaa utafikiri nini sjui... ovyo kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Website ya TBC haijitosheleze, wao wa google tu bbc.com, pale wataona wenzetu walivyosheheni mambo kede kede, mpaka LIVE link ya kutazama TBC..
Watangazaji wapunguze porojo, iwe kwenye Radio au TV, wakumbuke hawako kijiweni kwenye kahawa..
 
TBC kuwe na ubunifu.

Hiyo TBC2 bora iwe ya michezo tu.
Tangazeni hadi michezo ya bao, mpira wa miguu ligi ngazi zote, mpira wa pete, draft, pool, volleyball n k.

Pia mnaweza kuanzisha channel nyingine TBC3 ikawa ya mambo ya utamaduni tu ikiwa ni pamoja na singeli za kwenye vigodoro na ngoma za kienyeji.

Kuweni wabunifu banaaaa!
 
Maoni yangu ni kuhusu hii chaneli inayoitwa Tanzania Safari Chaneli. Nilifurahi sana kuiona hii chaneli ambayo inatangaza vivutio vya asili na utamaduni wa Tanzania.Awali muda mwingi nilikuwa na angalia chaneli za wanyama za Animax kutoka Star time tv na National Geo ya Azam.Lakini sasa kuna tatizo moja tu ambalo linapatikana kwenye Chaneli hiyo mpya ya Tanzania Safari.Tatizo hilo ni SCRATCHING muda wote. Sasa wahusika waliondoe tatizo hilo ambalo lipo kwenye chaneli hiyo moja tu.
Acheni kutumika kisiasa! Tunashindwa kuwelewa kama nyie ni Television ya Taifa au tawi la chama?
Ubora wa picha ni sifuri kabisa!
Nchi hii imejaa vijana zaidi ya 70% nyie asilimia 80 ya vipindi vyenu ni vya kizee!
Mnashindwa hata kuonesha mechi ya Taifa stars mmekalia ziara za viongozi wa chama wakitembelea matawi sijui kigoma gani huko!
Mmetangaza kufunga mitambo mipya ya kisasa na picha ndo kabisa zimerudi zile za kiwango cha chini kabisa!
Subirini na wengine wanakuja na mjiandae kwa POVU ZAIDI

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani niache kuangalia KTN au KBC niangalie TBC huhuhuh.......si bora niangalie katuni za Disney junior na wanangu.....!

Taarifa ya kusifia mwanzo mwisho badala ya kuripoti matukio.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mambo mengi huwa yanaendelea nchini na wadau wa nchi yetu wako dunia nzima. Kwa wadau walioko nje ya nchi sehemu muhimu ya kupata habari ni online streaming ya TBC ambayo kiukweli inakatisha tamaa.inastack as if wanacheza cd iliyojaa vumbi.mara nyingi nikiangalia AZAM tv habari iliyokwisha kuwa streamed na TBC naishiwa nguvu. Jaribuni kufanya uwekezaji unaoeleweka otherwise mjue online streaming yenu ina brand nchi yetu ila iko hoi bin taabani mjue TBC inapeperusha bendera ya nchi yetu sawa sawa na BBC kwa uingereza. Hebu tutolee hii aibu mtumie kodi zetu inavyotarajiwa.
 
Kuna mambo mengi huwa yanaendelea nchini na wadau wa nchi yetu wako dunia nzima. Kwa wadau walioko nje ya nchi sehemu muhimu ya kupata habari ni online streaming ya TBC ambayo kiukweli inakatisha tamaa.inastack as if wanacheza cd iliyojaa vumbi.mara nyingi nikiangalia AZAM tv habari iliyokwisha kuwa streamed na TBC naishiwa nguvu. Jaribuni kufanya uwekezaji unaoeleweka otherwise mjue online streaming yenu ina brand nchi yetu ila iko hoi bin taabani mjue TBC inapeperusha bendera ya nchi yetu sawa sawa na BBC kwa uingereza. Hebu tutolee hii aibu mtumie kodi zetu inavyotarajiwa.
Hiyo stesheni huwa naangalia kipindi cha katuni tu walahi, baada ya hapo narudi Azam 2 walahi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiacha kipindi cha marudio ya Rais na wachimbaji wa madini, sijawahi kufungua hii Channel kwasababu ya maudhui yasiyovutia.
 
Nimeona Channel E imejiimarisha kuwa tv ya kwanza ktk
Mfumo wa HD ukiacha sport channel ya Azam. TBC mnasubiri nini kujiweka ktk
Mfumo wa HD 1080 au 4k UHD manake tumechoka na picha zenu hafifu, muache pia kurusha taarifa ya habari kama
Documentary. Mjue kutofautisha hilo
 
Habari, kuna tatizo gani katika mfumo wa matangazo ya TBC Redio, mbona matangazo huwa yanasita mara kwa mara hasa mnapokuwa Mubashara Bungeni na Ikulu?
 
TBC.Nawashauri muandae vipindi vya watoto,cartoon na wanyama bila kusahau mikutano yoote ya Ccm.
Kiukweli niliisha acha kuangalia kabisa TBC naogopa kuisononesha nafsi yangu.

Tutamkumbuka Tido Muhando milele.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom