Tazama baadhi ya mapungufu yaliyojitokeza katika majina ya ajira za Ualimu yaliyotolewa. Jina la 'ABADALLAH LEONARD SHONDE lajirudia mara 196

IMG_8172.jpg

TAMISEMI HAWAKUONYESHA UMAKINI KWENYE MCHAKATO WA AJIRA ZA WALIMU ?

Mimi kama mdau wa elimu hapa nchini nimekuwa nikifatilia mchakato mzima wa hizi ajira za ualimu yaani tokea kuomba mpaka kutangazwa kwake na haya ndio machache niliyo yagundua;

1.Mfumo wa kuomba ajira yaani OTEAS ulizidiwa pale pale mwanzo na kufanya ugumu katika kuomba ajira hizo kwa zaidi ya siku 15.

2. Udanganyifu wa idadi ya watakao ajiriwa na walio ajiriwa ( ajira walitangaza ni 13,000 lakini wameajiri 9,000 +, je kama kibali cha ajira kilikua ni cha watu 13,000 hao watu wengine wameajiliwa wapi au wanabana matumizi?).

3. Mchakato sio wazi na shindani (non competitive and lack of transparent). Hawakusema wametumia kigezo gani kuajiri waliowaajiri na kuwaacha wengine kati ya wengi walio omba hizo ajira.

4. Uzembe na Uvivu. hii imejidhihirisha wazi kabsa kwa jina moja kujitokeza mara 196 inamaana wameprint tu na kuzitoa wameshindwa kuyapitia hayo majina na pia kushindwa kuweka namba kwenye majina hayo ili watu washindwe kutambua idadi halisi.

5. Kutoainisha majina kama mahitaji yalivyokua yakionesha kwenye tangazo la kazi yaani kwa taaluma mbali mbali kama lab technician 10 na majina yao haya au walimu daraja la 111 A 150 na majina yao haya wa 111 C. 670 na majina yao. Kuliko kuyachanganya na kufanya mkanganyiko kwa waliomba na jamii kwa ujumla.

6.Wasi wasi wa utendaji wao wa kazi na kazi yao kwa ujumla ( kwa waombaji )

IMG_8171.jpg

IMG_8170.jpg

IMG_8173.jpg
 
Kusema ukweli hizi ajira ni MAGUMASHI, hazina uhalisia wowote. Jina moja linajirudia mara nyngi na kituo ni kilekile.

Kuna wengine wamemaliza fom4 mwaka 2019 eti na wao wameajiriwa.

Swali: Kwanini hawajaandika vyuo walivyosomea? Kwanini hawajaweka serial number?

MUNGU TUNUSURU


---

---

---


PIA SOMA:
= > TAMISEMI yatangaza ajira za walimu shule za msingi na sekondari. Walimu waliopata ajira watakiwa kuripoti kuanzia Desemba mosi, 2020
Sasa toka 1997 anaajiriwa leo ? Hatari na nusu.
 
Tumeomba Takukuru ipelekewa majina yote yaliyopitishwa kuajiriwa kabla hawajaripoti kwenye vitu vya kazi. Tanzania Kuna watu wanatumia fursaya mfumo kupiga deal au kuiba.kuna ufisadi mkubwa Sana Tamisemi hasa kupitia ajira za wasalimu wapya 2020.
Mkuu maisha yanaedelea ujue hilo
 
Wee nae kilaza kweli embu angalia index no yake ya form inaonyesha kamaliza shule mwaka 2019
Au mwenzetu hukufika hata form 4 ila kama umefika utaona mfano S.101.202.2017 huyu unajua kamaliza 2017 sasa mtoa mada anamaanisha index no ya huyo Halima inaishia na 2019 je alisoma chuo kwa miaka mi ngapi na kumaliza hiyo kozi iwe certificate au diploma
Hebu mkubali kujulishwa vitu na sisi walimu kwenye hili

Ipo hivi Ukiona namba ya mtihani ya mtahiniwa inaanzia na S01860.....Jua kuwa huyu mtahiniwa ndio Mara yake ya kwanza kufanya huo mtihani wa kidato Cha nne ,lakin Ukiona namba yake ya mtihani inaanzia na P01860.... Fahamu huyu alishawahi kufanya huko nyuma na sasa ameamua kurudia Tena huo mtihani wa kidato Cha nne

Hivvyo huyo anaweza kuwa alikwenda kusoma ualimu na Sasa ameamua kusafisha cheti chake kimatokeo mazuri zaidi
 
Anarudia mtihani wa form four wa nini kama alishafika chuo na akasomea ualimu? How can people be this foolish hata kuchambua vitu virahisi? So kasomaje chuo hadi aje aresit saivi smh
Hjjawahi kusikia mtu ana PhD lakini anasomea certificate ya kitu kingine?
Mbona unaonekana Kama c mtanzania mwezutu vile!
 
Kwanzia baba mpaka watoto wote wadanganyifu. Hamna pakukimbilia Ni kuwa wapolee tuu. Ukihoji Sana utaambiwa umetumwa na mabeberu.
 
Bado najiuliza ni rushwa ,kujuana au maagizo.
Katika ajira zilizotoka jana za ualimu limetokea jina la Bint Halima Saidi Mohamed na amepangiwa kituo cha kazi mkoa wa Lindi wilaya ya Kilwa katika shule ya msingi Nandembo...

Ukistaajabu ya Halima utashangaa ya Mahera Kupokea Majina ya Covid19 tar 19 kutoka chadema huku Nusrat akiwa ndani na tar 20 Mahela akakanusha kwamba hawajapokea majina.
 
We boya mtahiniwa anakuwa identified na Index number hata ufanye mtihani mara 100.. Sijui kwa nn mnashindwa kujielimisha kabla ya kuropoka
Tatizo udumavu wa akili mkuu, akili ikidumaa reasoning inashuka Sanaa....
 
Back
Top Bottom