upcoming tycoon
JF-Expert Member
- Apr 16, 2018
- 353
- 468
TAMISEMI HAWAKUONYESHA UMAKINI KWENYE MCHAKATO WA AJIRA ZA WALIMU ?
Mimi kama mdau wa elimu hapa nchini nimekuwa nikifatilia mchakato mzima wa hizi ajira za ualimu yaani tokea kuomba mpaka kutangazwa kwake na haya ndio machache niliyo yagundua;
1.Mfumo wa kuomba ajira yaani OTEAS ulizidiwa pale pale mwanzo na kufanya ugumu katika kuomba ajira hizo kwa zaidi ya siku 15.
2. Udanganyifu wa idadi ya watakao ajiriwa na walio ajiriwa ( ajira walitangaza ni 13,000 lakini wameajiri 9,000 +, je kama kibali cha ajira kilikua ni cha watu 13,000 hao watu wengine wameajiliwa wapi au wanabana matumizi?).
3. Mchakato sio wazi na shindani (non competitive and lack of transparent). Hawakusema wametumia kigezo gani kuajiri waliowaajiri na kuwaacha wengine kati ya wengi walio omba hizo ajira.
4. Uzembe na Uvivu. hii imejidhihirisha wazi kabsa kwa jina moja kujitokeza mara 196 inamaana wameprint tu na kuzitoa wameshindwa kuyapitia hayo majina na pia kushindwa kuweka namba kwenye majina hayo ili watu washindwe kutambua idadi halisi.
5. Kutoainisha majina kama mahitaji yalivyokua yakionesha kwenye tangazo la kazi yaani kwa taaluma mbali mbali kama lab technician 10 na majina yao haya au walimu daraja la 111 A 150 na majina yao haya wa 111 C. 670 na majina yao. Kuliko kuyachanganya na kufanya mkanganyiko kwa waliomba na jamii kwa ujumla.
6.Wasi wasi wa utendaji wao wa kazi na kazi yao kwa ujumla ( kwa waombaji )