walimu

  1. A

    JamiiForums Tanzania KERO Walimu wa Shule ya Shekilango Sinza wanang'ang'ania kutoa watoto wa la saba saa 1 usiku. Wizara tusaidieni kukomesha hii

    Wakuu, Kuna ndugu yangu wangu la 7 ndo anarudi shule leo karudi saa 1 usiku. Muda wa kutoka shule ni saa 10 lakini hawa la 7 wanakalishwa hadi saa 1 usiku Nilivyouliza kwanini wanabaki hadi muda huo nimeambiwa wanasoma masomo ya ziada ili kujiandaa na mtihani wa taifa. Lakini kwenye kubaki...
  2. A

    JamiiForums Tanzania KERO Umoja wa Walimu wasio na ajira (NETO) tumewasilisha taarifa kuhusu kutotekelezwa kwa ahadi za Serikali na kutopatiwa majibu ya changamoto

    Umoja wa Walimu Wasio na Ajira (NETO) uliwasilisha taarifa kupitia vyombo mbalimbali vya habari kuhusu kutotekelezwa kwa ahadi za Serikali na kutopatiwa majibu kuhusu changamoto zinazowakabili. Katika kikao chetu cha tarehe 12 Machi 2025, tulishangazwa kuona baadhi ya vyombo vya habari...
  3. A

    JamiiForums Tanzania HOJA Kwanini Walimu wa shule binafsi Wilaya ya Ngara hatuteuliwi kusimamia mitihani ya NECTA tangu 2021?

    Tunaomba ufafanuzi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI kuhusu uteuzi wa walimu wa shule binafsi kusimamia mitihani ya NECTA. Kabla ya mwaka 2021, walimu wa shule binafsi walikuwa wakiteuliwa kushiriki katika usimamizi wa mitihani ya NECTA. Hata hivyo, tangu mwaka 2021 hadi sasa, walimu wa...
  4. Mtu na nusu

    JamiiForums Tanzania Kama maslahi ya walimu nchini ni madogo, kwanini walimu wasiombe ajira kwenye nchi za kimataifa zinazolipa vizuri?!

    Nimejaribu kupitia na kuangalia maslahi ya walimu kwenye nchi za wenzetu(botswana, South Africa, Rwanda, Qatar n.k) nikagundua walimu wanalipwa vizuri mno kuliko wanavyolipwa kwetu Nikaangalia vigezo na taratibu za kuomba ajira nikaona vyote ni rahisi na vinawezekana. Nilichojilaumu ni mimi...
  5. H

    JamiiForums Tanzania KERO Walimu ajira mpya Bariadi Vijijini hatujalipwa fedha za kujikimu tangu tuajiriwe mwaka 2025

    Habari za muda huu, JF. Mimi ni mwalimu wa ajira mpya na ninawakilisha walimu wenzangu wa ajira mpya katika Halmashauri ya Bariadi Vijijini. Tunaomba msaada wako katika kufikisha kero yetu kuhusu kutolipwa fedha zetu za kujikimu tangu tulipoajiriwa mwaka 2025. Tumejaribu kufuatilia suala hili...
  6. A

    JamiiForums Tanzania KERO Watumishi wa Kwimba wamelipwa fedha za kujikimu, mbona Walimu wa ajira mpya bado?

    Leo nimeona taarifa kwamba baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba wamelipwa fedha zao za kujikimu. Swali langu ni, kwa nini sisi walimu wa ajira mpya bado hatujalipwa fedha zetu za kujikimu? Je, kuna sababu yoyote ya tofauti hii katika malipo? Tunaomba mamlaka husika...
  7. A

    JamiiForums Tanzania KERO Watumishi wa Halmashauri ya Kyela walioajiriwa 2022 hatujapandishwa madaraja, wengine tayari

    Watumishi wa Halmashauri ya Kyela walioajiriwa mwaka 2022 bado hatujapandishwa madaraja, wakati watumishi wa halmashauri nyingine tayari wamefanyiwa utaratibu huo. Tunapofuatilia suala hili hatupati majibu ya kueleweka. Tunaomba msaada ili wahusika watoe ufafanuzi na kuhakikisha haki yetu...
  8. ndege JOHN

    JamiiForums Tanzania Una mpango wa kurudi kuwasalimia Walimu wako wa Primary na Sekondari au ndiyo basi ishapita NO shobo tena?

    kila mtu anajua hili kuna walimu walituvumilia sana mpaka tukafika hapa tulipo leo. Lakini wengi wetu tukishamaliza shule hatukanyagi tena hata kwenda kusema Asante mwalimu. Je, wewe una mpango wa siku moja kurudi kuwasalimia walimu wako wa primary na sekondari, au unaona muda umeshapita na...
  9. Fbn

    JamiiForums Tanzania Walimu wa afrika wamezima ndoto za wanafunzi wengi ndio maana afrika kuendelea ngumu.

    Leo mjinga ndio anakuwa na cheo na kila kitu. Kwa nini dotto magari kafikia kuziaki wenye elimu wakati anachokitumia kimetengenezwa na wenye elimu. Tanzania kama mzazi kumbatia mawazo ya mtoto wako na ndoto zake. Walimu wengi wameharibu ndoto za watoto hata mliopo hapa JF mnaweza kutoa...
  10. V

    JamiiForums Tanzania Walimu wa arts na lugha waanza kuitwa kazini #kiswahili, English,htm

  11. MWL WALTER

    JamiiForums Tanzania KUBADILISHANA WALIMU VITUO VYA KAZI MSINGI

    Ndugu Admin, Napenda kuwataarifu kuwa nimerudi tena katika kundi letu. Naomba tuendelee kuzingatia lengo letu kuu la uhamisho. Aidha, natafuta mwalimu wa kubadilishana vituo vya kazi aje KONDOA DC Mimi nije katika idara ya elimu ya msingi, hususan katika wilaya za Morogoro:🔴 GAIRO🔴 KILOSA🔴...
  12. K

    JamiiForums Tanzania Watuhumiwa CWT wasubiri uamuzi wa mahakama

    VIONGOZI waliosimamishwa na Baraza la Taifa la Chama cha Walimu Tanzania (CWT) wataendelea kuwa nje ya nafasi zao za uongozi hadi Mahakama ya Mkoa wa Dodoma itakapotoa uamuzi katika kesi inayowakabili. Waliosimamishwa ni aliyekuwa Rais wa CWT, Leah Ulaya, Rais Dkt. Suleiman Ikomba, Maganga...
  13. Roving Journalist

    JamiiForums Tanzania Walimu wa Mkataba (Mradi wa GPE-TSSP): Tunafanya kazi katika mazingira magumu, hakuna usawa, tunabaguliwa, hatupewi stahiki zetu

    Walimu wa Mkataba (Mradi wa GPE-TSSP): Mikataba inaonesha tumeajiriwa na Wazazi na si TAMISEMI, tuna mazingira magumu. Ujumbe wa Walimu wa Mkataba chini ya mradi wa GPE-TSSP, Juni 26, 2026: Napenda kuwasilisha kwenu baadhi ya changamoto kubwa tunazokabiliana nazo sisi walimu wa mkataba chini...
  14. T

    JamiiForums Tanzania Hakuna kundi la waajiriwa wa serikali linalonyanyaswa na kuonewa kama walimu. Siku wakisanuka, CCM bye bye

    Waalimu wana malalamiko mengi sana. CCM imeiteka CWT ili iwacontrol waalimu na kuwapumbaza. Cwt inawakata waalimu hela asilimia 2% kila mmoja kwa idadi ya waalimu tulionao karibia laki 4 hadi 5 ambapo kwa uchache karibia bilion 2 hadi 3 kila mwezi. Kundi hili ndilo kundi linaloongoza kwa...
  15. A

    JamiiForums Tanzania KERO Walimu wa Ajira Mpya 2026 tunahitaji Haki sawa ya Malipo ya Fedha za Kujikimu

    Sisi walimu wa ajira mpya 2026 tunaonyesha masikitiko yetu kutokana na kutopatiwa fedha za kujikimu, ilhali watumishi wa ajira mpya wa kada ya afya tayari wamepata stahiki hizo kupitia TAMISEMI. Tunaiomba Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI kutoa ufafanuzi kuhusu tofauti hii ya utoaji wa stahiki...
  16. M

    JamiiForums Tanzania Ridhiwani Kikwete ameikudu wizara nyeti. Walimu na watumishi wengine tumpongeze. Najua anachukiwa kwa mambo yake mengine ila...

    Ukweli lazima usemwe. Hii ni wizara ambayo inagusa maisha ya kila mtanzania. Kuna vijimtu vipuuzi na vipumbavu kuwa wasimamizi vinadhania vimemaliza maisha. Vinanyanyasa watumishi na kuwatukana kama housegirls wao. Tangu Rizimoko aingie madarakano kama waziri wa menejimenti ya utumishi na...
  17. A

    JamiiForums Tanzania DOKEZO Ma-DED, maofisa Utumishi wadaiwa kuzuia walimu kujitoa CWT, kujiunga na vyama vingine

    Katiba ya Jamhuri ya Muungano ibara ya 20(1) inasema, “Kila mtu anao uhuru wa kukutana na watu wengine kwa hiari yake na kwa amani, kuchanganyika, kushirikiana na watu wengine, na kwa ajili hiyo kutoa mawazo yake hadharani na kuanzisha na kujiunga na vyama au mashirika yaliyoanzishwa kwa...
  18. A

    JamiiForums Tanzania KERO Changamoto Sekondari Mchungaji Mwema: Walimu, Mishahara na Utawala

    KERO Mimi kama mzazi na mdau wa elimu shule ya sekondari mchungaji mwema iliyoko chini ya dayosisi ya Kagera nakelwa na mambo kama haya 1. Walimu KUNYIMWA MKATABA ambao ni silaha ya kulinda ajira yao Kwa mujibu wa SHERIA. 2. Mishahara ya kusuasua Kwa WAFANYAKAZI na kulipwa kinyume na SHERIA...
  19. Wakusoma 12

    JamiiForums Tanzania Kwanini walimu wenye Shahada za elimu katika masomo ya sanaa wasiajiriwe shule za msingi ili kupunguza idadi ya wahitimu wa fani hizo mitaani?

    Huu ni mjadala huru : Wahitimu wa taaluma ya elimu katika masomo ya sanaa nchini Tanzania wanapitia kwenye kaa la moto kwa muda mrefu sasa, watu wamesota miaka zaidi ya kumi lakini hakuna anayehisi maumivu yao. Serikali na mamlaka tatizo si kulimaliza bali hata kulipunguza haijatoa mwelekeo...
  20. A

    JamiiForums Tanzania KERO Mbeya Jiji: Nusu ya fedha za kujikimu kwa ajira za Walimu wa mwaka 2025 hatujalipwa

    Ni zaidi ya mwaka sasa tangu walimu tuliopata ajira mwaka 2025 turipoti kazini, lakini bado hatujalipwa fedha za kujikimu ambazo ni stahiki ya kila mtumishi wa umma. Kwa mujibu wa taratibu za utumishi wa umma, fedha hizi zinapaswa kulipwa ndani ya siku saba baada ya mtumishi kuripoti katika...
Back
Top Bottom