Walimu kuajiriwa na TSC badala ya Wizara kunaenda kutengeneza rushwa, undugu na kujuana kwenye ajira. Rais litazame hili linaenda kukuharibia

msovero

JF-Expert Member
Jun 30, 2019
839
1,472
Waziri wa nchi, ofisi ya Rais-Tamisemi ameiagiza tume ya utumishi wa walimu 'TSC' kuandaa utaratibu wa kuanza kuajiri walimu kupitia halmashauri kwa niaba ya wizara ya ofisi ya Rais-Tamisemi.

Japo utaratibu wa kuomba hizo ajira bado haujafahamika lakini nadhani maombi yatakuwa yanatumwa moja kwa moja kwenye ofisi za tume ya utumishi wa walimu(TSC) zilizopo kwenye kila wilaya.

Baada ya utaratibu huu kuanza kutumika tutarajie rushwa kuwa moja ya kigezo kwenye upatikanaji wa ajira. Maana yake kama unatokea familia duni sasa sahau kupata ajira ya ualimu.

Najua kwa sasa naweza nisieleweke lakini ukweli ndio huo kwa sababu watumishi wa TSC nao ni binadamu wana ndugu zao. Je, unadhani wataacha kuchomeka ndugu zao wakupe ajira wewe mtu baki?

Tukumbuke kuwa ofisi za TSC zipo kila wilaya kwenye majengo ya halmashauri ambako kuna watendaji na maafisa wa idara mbali mbali na hawa watu wana fanya kazi kwa ukaribu sana. Sasa tuchukulie baada ya ajira kutangazwa, mkurugenzi wa halmashauri achomeke watu wake, DC achomeke watu wake, afisa mipango achomeke watu wake, afisa utumishi achomeke mtu wake, afisa elimu achomeke mtu wake, afisa ardhi achomeke mtu wake, afisa tehama naye achomeke wakwake katika mgawanyo kama huu ajira zitaishia kuwa za watu wa halmashauri na wenye ukaribu na watumishi wa TSC kwahiyo mtoto wa mkulima hatakuwa na nafasi ya kupata ajira tena.

Pia tukumbuke baada ya ajira kurudishwa TSC kuna vigezo vipya vitaibuka moja wapo kitakuwa kigezo cha kujitolea, ufaulu, chuo ulichosoma, umri, jinsia nakadhalika. Kimsingi vigezo hivi vitawekwa kimkakati ili kutengeneza mianya ya rushwa ili kwa yoyote atakayeshindwa kuvitimiza atoe pesa ili apatiwe ajira.

Sasa kwakuwa hili ni jambo la kitaifa na linagusa maslahi ya wananchi naomba kushauri mambo yafuatayo,

1. Namuomba waziri wa Tamisemi, ummy mwalimu asitishe mchakato huu kwani unaenda kutengeneza undugu, kujuana na rushwa kwenye ajira.

2. Nashauri utaratibu unaotumika sasa kuajiri walimu uendelee kama kawaida kwani kwa kiasi fulani umesaidia kupunguza kama sio kuondosha kabisa urasimu kwenye ajira. Na katika hili napendekeza pia utaratibu uliotumika kwenye ajira zilizopita wa kutumia kigezo cha mwaka wa kuhitimu chuo ndio uendelee kwani kuna vijana wamemaliza chuo muda mrefu na wameanza kukata tamaa hata kukosa matumaini kwa serikali yao.

3. Namuomba mheshimiwa Rais mama yetu Samia aliangalie hili kwa uzito wake kwani linaenda kumchonganisha yeye binafsi na serikali anayoiongoza kwa wananchi wake.

4. Namuomba mheshimiwa Rais atafakari upya na kurudisha usimamizi wa masula ya elimu kwenye wizara husika(wizara ya elimu) kwani mapendekezo haya ya waziri ni dalili kwamba TAMISEMI imeanza kuelemewa kutokana na mzigo wa kimajukumu iliyonayo ya kuhudumia sekta nyingi kwa wakati mmoja.

5. Kwakuwa waziri wa Tamisemi, ummy mwalimu alianza vizuri na hapa kati kati ameanza kulega nilikuwa nashauri amwombe mheshimiwa Rais ambadilishie wizara kabla mambo hayajaharibika kwa sababu huku anakotaka kwenda siko.

Mwisho kabisa natoa Rai kwa ndugu wazazi na vijana mnaotarajia kuomba ajira ya ualimu kukataa utaratibu huu kwani unaenda kuwaumiza zaidi badala ya kuwaponya. Hata mimi binafsi naupinga kwa nguvu zote kwani umewahi kutumika miaka ya nyuma na rushwa ilikuwa inatembea sana ndipo serikali ikabadili utaratibu wa kuajiri sasa nashangaa leo serikali inataka kuturudisha kulekule. Katika hili tuseme HAPANA kwa sauti kubwa
 
Mawaziri wengine,wanakua kama hawaijui Tanzania na watu wake,yaani hapo rushwa ya kila aina itatamakaki.
Nashindwa kuimagine upachikwaji wa watu utakavyokua.
 
Kuna kipindi mdau mmoja humu JF aliwahi kutoa hili wazo, naona limefanyiwa kazi.

Mkuu kwanza elewa tu RUSHWA HAIWEZI KUISHA TANZANIA KAMWE.

Fanya sarakasi zote ila rushwa huwezi komesha na kuimaliza.

Hii njia naona itasaidia Shule kupata waalimu wahitajika kuliko ile mara ya kwanza wanapangwa bila kujali shule fulani ina uhitaji wa mwalimu wa somo gani.

Kuhusu rushwa, hiyo haiwezi kuisha kamwe.
 
Kuna kipindi mdau mmoja humu JF aliwahi kutoa hili wazo, naona limefanyiwa kazi.

Mkuu kwanza elewa tu RUSHWA HAIWEZI KUISHA TANZANIA KAMWE.

Fanya sarakasi zote ila rushwa huwezi komesha na kuimaliza.

Hii njia naona itasaidia Shule kupata waalimu wahitajika kuliko ile mara ya kwanza wanapangwa bila kujali shule fulani ina uhitaji wa mwalimu wa somo gani.

Kuhusu rushwa, hiyo haiwezi kuisha kamwe.
Nakubali rushwa haiwezi kuisha lakini angalau kutuma maombi kwa njia ya kielektroniki na maombi hayo kusimamiwa na wizara kulipunguza sana urasimu kwenye ajira tofauti na mfumo wanaotaka kuanzisha. Kuhusu uhitaji wa walimu kimasomo takwimu huwa zinatumwa TAMISEMI labda ni wao ndio huwa hawazifanyii kazi kwenye upangaji wa ajira
 
Nikweli halimashauri zinapewa nguvu (serikali zamitaa)lakini hao ndowaliajiri zilehewa alizokataa magufuli wetu wao

Mungu wangu wambinguni na mahali pote ulimwenguni tunaomba utusimamie

Sent from my TECNO F2 using JamiiForums mobile app
 
Mawaziri wengine,wanakua kama hawaijui Tanzania na watu wake,yaani hapo rushwa ya kila aina itatamakaki.
Nashindwa kuimagine upachikwaji wa watu utakavyokua.
Rushwa itatembea balaa na watakaoumia zaidi ni wale wanaotokea familia maskini sijui nani kamshauri waziri huu utumbo
 
Kuna kipindi mdau mmoja humu JF aliwahi kutoa hili wazo, naona limefanyiwa kazi.

Mkuu kwanza elewa tu RUSHWA HAIWEZI KUISHA TANZANIA KAMWE.

Fanya sarakasi zote ila rushwa huwezi komesha na kuimaliza.

Hii njia naona itasaidia Shule kupata waalimu wahitajika kuliko ile mara ya kwanza wanapangwa bila kujali shule fulani ina uhitaji wa mwalimu wa somo gani.

Kuhusu rushwa, hiyo haiwezi kuisha kamwe.
Kuna waratibu elimu kata.
Kuna maafisa elimu wilaya taaluma.
Kuna mnyororo mrefu sana wa elimu nchini.
Hawa wote kama hawajui shule fulani hitaji lake ni nini,wanafanya kazi gani sasa!!??
Yaani kama TAMISEMI pamoja na "human resource" yote kubwa waliyonayo wanashindwa kufanyia kazi changamoto za elimu nchini,basi tutegemee Tanzania kuondokana na maadui wetu miaka 100 ijayo.
Mke wangu ni Katibu wa TSC halmashauri moja, najua ninachokiandika.
Hii ya ajira kufanywa na TSC ni bonge moja la tusi kwa walimu, elimu na ajira kwa ujumla.
 
Waziri wa nchi, ofisi ya Rais-Tamisemi ameiagiza tume ya utumishi wa walimu 'TSC' kuandaa utaratibu wa kuanza kuajiri walimu kupitia halmashauri kwa niaba ya wizara ya ofisi ya Rais-Tamisemi.

Japo utaratibu wa kuomba hizo ajira bado haujafahamika lakini nadhani maombi yatakuwa yanatumwa moja kwa moja kwenye ofisi za tume ya utumishi wa walimu(TSC) zilizopo kwenye kila wilaya.

Baada ya utaratibu huu kuanza kutumika tutarajie rushwa kuwa moja ya kigezo kwenye upatikanaji wa ajira. Maana yake kama unatokea familia duni sasa sahau kupata ajira ya ualimu.

Najua kwa sasa naweza nisieleweke lakini ukweli ndio huo kwa sababu watumishi wa TSC nao ni binadamu wana ndugu zao. Je, unadhani wataacha kuchomeka ndugu zao wakupe ajira wewe mtu baki?

Tukumbuke kuwa ofisi za TSC zipo kila wilaya kwenye majengo ya halmashauri ambako kuna watendaji na maafisa wa idara mbali mbali na hawa watu wana fanya kazi kwa ukaribu sana. Sasa tuchukulie baada ya ajira kutangazwa, mkurugenzi wa halmashauri achomeke watu wake, DC achomeke watu wake, afisa mipango achomeke watu wake, afisa utumishi achomeke mtu wake, afisa elimu achomeke mtu wake, afisa ardhi achomeke mtu wake, afisa tehama naye achomeke wakwake katika mgawanyo kama huu ajira zitaishia kuwa za watu wa halmashauri na wenye ukaribu na watumishi wa TSC kwahiyo mtoto wa mkulima hatakuwa na nafasi ya kupata ajira tena.

Pia tukumbuke baada ya ajira kurudishwa TSC kuna vigezo vipya vitaibuka moja wapo kitakuwa kigezo cha kujitolea, ufaulu, chuo ulichosoma, umri, jinsia nakadhalika. Kimsingi vigezo hivi vitawekwa kimkakati ili kutengeneza mianya ya rushwa ili kwa yoyote atakayeshindwa kuvitimiza atoe pesa ili apatiwe ajira.

Sasa kwakuwa hili ni jambo la kitaifa na linagusa maslahi ya wananchi naomba kushauri mambo yafuatayo,

1. Namuomba waziri wa Tamisemi, ummy mwalimu asitishe mchakato huu kwani unaenda kutengeneza undugu, kujuana na rushwa kwenye ajira.

2. Nashauri utaratibu unaotumika sasa kuajiri walimu uendelee kama kawaida kwani kwa kiasi fulani umesaidia kupunguza kama sio kuondosha kabisa urasimu kwenye ajira. Na katika hili napendekeza pia utaratibu uliotumika kwenye ajira zilizopita wa kutumia kigezo cha mwaka wa kuhitimu chuo ndio uendelee kwani kuna vijana wamemaliza chuo muda mrefu na wameanza kukata tamaa hata kukosa matumaini kwa serikali yao.

3. Namuomba mheshimiwa Rais mama yetu Samia aliangalie hili kwa uzito wake kwani linaenda kumchonganisha yeye binafsi na serikali anayoiongoza kwa wananchi wake.

4. Namuomba mheshimiwa Rais atafakari upya na kurudisha usimamizi wa masula ya elimu kwenye wizara husika(wizara ya elimu) kwani mapendekezo haya ya waziri ni dalili kwamba TAMISEMI imeanza kuelemewa kutokana na mzigo wa kimajukumu iliyonayo ya kuhudumia sekta nyingi kwa wakati mmoja.

5. Kwakuwa waziri wa Tamisemi, ummy mwalimu alianza vizuri na hapa kati kati ameanza kulega nilikuwa nashauri amwombe mheshimiwa Rais ambadilishie wizara kabla mambo hayajaharibika kwa sababu huku anakotaka kwenda siko.

Mwisho kabisa natoa Rai kwa ndugu wazazi na vijana mnaotarajia kuomba ajira ya ualimu kukataa utaratibu huu kwani unaenda kuwaumiza zaidi badala ya kuwaponya. Hata mimi binafsi naupinga kwa nguvu zote kwani umewahi kutumika miaka ya nyuma na rushwa ilikuwa inatembea sana ndipo serikali ikabadili utaratibu wa kuajiri sasa nashangaa leo serikali inataka kuturudisha kulekule. Katika hili tuseme HAPANA kwa sauti kubwa
Tutalajie wenye vyeti feki kurudi kwa kishindo pia
 
Tutalajie wenye vyeti feki kurudi kwa kishindo pia
Badala ya kusonga mbele tunarudi kwenye zama za toa kitu upate kitu, watumishi hewa na vyeti feki na hapa ndipo tunalazimika kumkumbuka hayati magufuli japokuwa hatukumpenda
 
Kuna waratibu elimu kata.
Kuna maafisa elimu wilaya taaluma.
Kuna mnyororo mrefu sana wa elimu nchini.
Hawa wote kama hawajui shule fulani hitaji lake ni nini,wanafanya kazi gani sasa!!??
Yaani kama TAMISEMI pamoja na "human resource" yote kubwa waliyonayo wanashindwa kufanyia kazi changamoto za elimu nchini,basi tutegemee Tanzania kuondokana na maadui wetu miaka 100 ijayo.
Mke wangu ni Katibu wa TSC halmashauri moja, najua ninachokiandika.
Hii ya ajira kufanywa na TSC ni bonge moja la tusi kwa walimu, elimu na ajira kwa ujumla.
Umesomeka mkuu kama asipoelewa na hapa atakuwa na matatizo binafsi
 
Kweli haina Afya kabisa hii
Haina mantiki na kama ndivyo alivyoshauriwa ummy basi kuanzia sasa atambue ameingizwa mkenge na watanzania hawatakubali kama haamini aendelee na huo mchakato tuone mwisho wake
 
Mfumo wa maombi kwa njia ya mtandao wa OTEAS ulikuwa unatoa fursa sawa kwa mtu yeyote kuajiriwa bila kujali status ya familia anayotoka!

Lakini huu mfumo mpya unaotaka kuanzishwa utatengeneza ajira za matabaka na rushwa kwa kisingizio cha kujitolea!

Mama yetu hangaya atunusuru waja wake na huu ukiritimba unaotaka kufanyika! Lol..!
 
Mfumo wa maombi kwa njia ya mtandao wa OTEAS ulikuwa unatoa fursa sawa kwa mtu yeyote kuajiriwa bila kujali status ya familia anayotoka!

Lakini huu mfumo mpya unaotaka kuanzishwa utatengeneza ajira za matabaka na rushwa kwa kisingizio cha kujitolea!

Mama yetu hangaya atunusuru waja wake na huu ukiritimba unaotaka kufanyika! Lol..!
Hivi ulishawahi kuamini utendaji kazi wa ummy mwalimu? Kuna watu wanabahati ya kupata ila utendaji zero pamoja na mwigulu!
 
Hivi ulishawahi kuamini utendaji kazi wa ummy mwalimu? Kuna watu wanabahati ya kupata ila utendaji zero pamoja na mwigulu!
Ummy mwalimu alifanya vizuri akiwa waziri wa afya hususani katika mapambano ya corona na alisifiwa sana!

Sasa naona sifa alizozipata akiwa waziri wa afya zimeanza kumlewesha kwa matamko yake ya hovyo hovyo yasiyo zingatia matakwa ya kisheria!

Watangulizi wake walitengeneza mfumo mzuri wa kuajiri na umekuwa na matokeo chanya licha ya changamoto za hapa na pale. Yeye amekuja sasa anataka kuubomoa aturudishe nyuma tulikotoka!

Kwangu naona ni bora akarudishwa wizara ya afya huku Tamisemi hapamfai ana haribu mno!!
 
Back
Top Bottom