Baadhi ya mapungufu yaliyojitokeza kwenye ajira za ualimu 2021

Jensen salamone

JF-Expert Member
Sep 28, 2019
320
639
Kwanza nianze kwa kuwapongeza wizara ya Tamisemi chini ya waziri ummy, katibu mkuu na wote waliohusika kwenye mchakato mzima wa uchambuzi na utoaji ajira

Ofcourse wanastahili kupewa pongezi kwa kazi nzuri waliyofanya kwani kwa asilimia kubwa wametenda haki kwa waombaji hasa kwa kutoa kipaumbele kwa vijana waliomaliza vyuo na kukaa mtaani kwa muda mrefu. Mbali na kutenda haki pia wamejitahidi kuwa wawazi hususani kwenye kuainisha kiwango cha elimu kwa kila mwombaji kwa sababu kulikuwa na uvumi kwamba walimu wenye digrii hawaajiriwi lakini hivi sasa tumeshuhudia kwa macho wakiajiriwa.

Pamoja na pongezi hizo nzuri kuna mambo machache ambayo naona hayajaenda sawa kwenye mchakato wa hizo ajira nayo ni kama yafuatayo,

1. Kuna waombaji kiwango chao cha elimu kinaonyesha wamemaliza elimu ya digrii mwaka 2019 lakini index zao za kidato cha nne zinaonyesha wamehitimu kidato cha nne 2014 ambapo kwa kuzingatia mwaka wao wa kumaliza kidato cha nne kwa mujibu wa TCU ilibidi digrii yao ya kwanza ya ualimu waipate kuanzia 2020 kwani digrii ya ualimu minimum ni miaka mitatu kwa vyuo vyote nchini. Miongoni mwa waombaji hao ni wenye index zifuatazo
(i) S4463-0023/2014 -kuhitimu degree(2019)
(ii) S3065-0009/2013-kuhitimu degree(2016)
(iii) S1183-0035/2014- kuhitimu degree(2019)
(iii) S4507-0035/2014 -kuhitimu degree(2019)
(iv) S1229-0068/2014-kuhitimu degree(2019)

2. Mwombaji mwenye index no S4166-0038/2014 taarifa zinaonyesha hakufanya mtihani wa kidato cha nne
20210627124530.jpg


3. Watu wenye ulemavu (PWD's) walioajiriwa ni 145 kati ya 1000 maana yake ile 3% haijafikiwa kwani kwa idadi yao ilibidi waajiriwe angalau 208 ili kufikia lengo la 3%. Kwahiyo mnapokuwa mnaajiri ni vyema mkazingatia hilo kwa sababu PWD's tunaishi nao kwenye jamii zetu na tunajua wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo kutengwa, kudharauliwa na wengine huficha ulemavu wao kwa hofu ya kubaguliwa na hivyo huishi kwa taabu sana

4. Mwombaji mwenye index no S0660-1409/2019 haitambuliki kwenye baraza la mitihani (NECTA) kwahiyo ni vema mka link mifumo yenu na necta ili kasoro ndogo ndogo kama hizi sijirudie

5. Halmashauri ya muheza imepelekewa walimu wengi kulinganisha na halmashauri zingine. Kwahiyo ni vema mnapokuwa mnagawa walimu kuwepo na uwiano mzuri angalau kila halmashauri ipate watumishi kuliko kupeleka walimu wengi sehemu moja huku halmashauri zingine zikibaki na uhaba mkubwa.

Otherwise jitahidini kuomba vibali vya kuajiri walimu mara kwa mara kwakuwa bado tatizo la uhaba wa walimu ni kubwa kupita maelezo.
 
Kwanza nianze kwa kuwapongeza wizara ya Tamisemi chini ya waziri ummy, katibu mkuu na wote waliohusika kwenye mchakato mzima wa uchambuzi na utoaji ajira

Ofcourse wanastahili kupewa pongezi kwa kazi nzuri waliyofanya kwani kwa asilimia kubwa wametenda haki kwa waombaji hasa kwa kutoa kipaumbele kwa vijana waliomaliza vyuo na kukaa mtaani kwa muda mrefu. Mbali na kutenda haki pia wamejitahidi kuwa wawazi hususani kwenye kuainisha kiwango cha elimu kwa kila mwombaji kwa sababu kulikuwa na uvumi kwamba walimu wenye digrii hawaajiriwi lakini hivi sasa tumeshuhudia kwa macho wakiajiriwa.

Pamoja na pongezi hizo nzuri kuna mambo machache ambayo naona hayajaenda sawa kwenye mchakato wa hizo ajira nayo ni kama yafuatayo,

1. Kuna waombaji kiwango chao cha elimu kinaonyesha wamemaliza elimu ya digrii mwaka 2019 lakini index zao za kidato cha nne zinaonyesha wamehitimu kidato cha nne 2014 ambapo kwa kuzingatia mwaka wao wa kumaliza kidato cha nne kwa mujibu wa TCU ilibidi digrii yao ya kwanza ya ualimu waipate kuanzia 2020 kwani digrii ya ualimu minimum ni miaka mitatu kwa vyuo vyote nchini. Miongoni mwa waombaji hao ni wenye index zifuatazo
(i) S4463-0023/2014 -kuhitimu degree(2019)
(ii) S3065-0009/2013-kuhitimu degree(2016)
(iii) S1183-0035/2014- kuhitimu degree(2019)
(iii) S4507-0035/2014 -kuhitimu degree(2019)
(iv) S1229-0068/2014-kuhitimu degree(2019)
Mkuu mimi ninachojua mtu siyo lazima aende chuo direct. Kuna kumaliza form six halafu mtu anakaa kwanza nyumbani, chuo anaenda baadaye.
2. Mwombaji mwenye index no S4166-0038/2014 taarifa zinaonyesha hakufanya mtihani wa kidato cha nne
3. Watu wenye ulemavu (PWD's) walioajiriwa ni 145 kati ya 1000 maana yake 3% haijafikiwa. Kwahiyo mnapokuwa mnaajiri ni vyema mkazingatia hilo kwa sababu PWD's tunaishi nao kwenye jamii zetu na tunajua wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo kutengwa na kudharaulika.

4. Mwombaji mwenye index no S0660-1409/2019 haitambuliki kwenye baraza la mitihani (NECTA) kwahiyo ni vema mka link mifumo yenu na necta ili kasoro ndogo ndogo kama hizi sijirudie
Kama hakufanya mtihani wa form 4 ataripoti vipi bila cheti?
5. Halmashauri ya muheza imepelekewa walimu wengi kulinganisha na halmashauri zingine. Kwahiyo ni vema mnapokuwa mnagawa walimu kuwepo na uwiano mzuri angalau kila halmashauri ipate watumishi kuliko kupeleka walimu wengi sehemu moja huku halmashauri zingine zikibaki na uhaba mkubwa.

Otherwise jitahidini kuomba vibali vya kuajiri walimu mara kwa mara kwakuwa bado tatizo la uhaba wa walimu ni kubwa kupita maelezo.
💯
 
MHESHIMIWA WAZIRI SALAM
awali yote nipende kukupongeza kwa Kazi nzito unayoifanya Mheshimiwa Waziri Mungu akupe nguvu na hekima
Mheshimiwa Waziri utakapopata muda Tafadhari naomba upitie tena PDF ya ajira za walimu kuna mambo hayajakaa vizuri kiasi kwamba yamezusha mjadala hususani sisi tuliokosa

Mheshimiwa Waziri
Kuna Mwalimu namba 4115 na Namba 4116 Christina Edward Luhunga Index number S2324-0013/2010 na S2324-0014/2010 Kapangwa Kigoma wilaya Kasulu Dc
Index number S2324-0023 Kapangwa Mayonga Sekondari na
S2324-0014 Kapangwa Nyakitonta Shule ya Sekondari
Mheshimiwa Waziri Mwalimu mwenye index number S2324-0014 huyu anaitwa Chuki Mtaki Lucas na kwa mjibu wa NECTA ana division zero point 35 akiwa na F Kwa Masomo aliyofanyia mitihani

Mheshimiwa Waziri mwingine ni Mwalimu namba 6571 NICHOLOUS DEUSDEDITH index number S0660-1409/2019 Mwalimu wa Physics na Biology Shida iko hapo kwenye taaluma yake Diploma yake ya ualimu kapata kwa wakati mmoja na Elimu ya Kidato cha Nne ? Na Kama ndiyo hivyo huo mfumo ulianza lini ?

Mheshimiwa Waziri mtu mwingine ni walimu Namba
5919 mwenye index number S4507-0035/2014
Namba 5857 index number S4166-0038/2014
Namba 5798 index number S1183-0035/2014
Namba 5791 index number S4463-0023/2014

Hao ni baadhi tu niliowaona mheshimiwa Hawa walimu ni walimu wa degree kwa Masomo yao
Mheshimiwa shida yangu na Hawa walimu ni kwamba wamemaliza Bachelor degree of education 2019 kitu ambacho siyo ukweli

Kwani walimu Hawa 2015 -2016 ni Kidato cha tano
2016 - 2017 ni Kidato cha sita

CHUO
Mwaka wa kwanza ni
2017- 2018
Mwaka wa pili
2018-2019
Mwaka wa tatu
2019-2020

Maana yake ni kwamba ofisi inatudanganya sisi kuwa Hawa watu wamemaliza Bachelor degree 2019 kitu ambacho siyo ukweli na hakuna Tanzania hii degree ya miaka miwili Mheshimiwa Waziri naomba uliangalie hilo

Kwa mjibu wa professor Karibu mkuu amesema wamechukua mwisho 2019 sasa hao wanatafuta nini ?

Mheshimiwa Waziri naomba hilo suala liangaliwe upya Watu tunakosa fursa kumbe Kuna watu wanapeana tu kindugu

Naomba kuwakilisha

Nategemea feedback mheshimiwa Waziri
 
Nachoshangaa ni kwanini vyuo vya elimu ya juu hawaajiri walimu wakati hali ni mbaya zaidi. Kuna baadhi ya programs waalimu wote ni part time hadi unajiuliza kama kuna waziri wa elimu
 
Hiko hivi Mimi na washikaji wangu tulimaliza nao degree 2020 kwenye hizi ajira 2020 walikua hawaruhusiwi,so wakaamua kuomba kwa lazima lakini mwaka wa kumaliza chuo waliandika 2019 hawakuandika ile halisi ambayo ni 2020.
Kumbuka ni system walikua wana command kwamba 2020 tuwaondoe ndio maana 2020 hayupo hata mmoja ila wa 2020 alieandika 2019 basi alikua yupo kwenye chance moja na waliopo kwenye system.
Nadhani kosa lililofanyika haawezi kufatilia kwamba huyu kamaliza 2014 form four basi 2020 ndio awe amemaliza degree huo mda hawana.
Usiwasagie kunguni waache wale cake ya taifa mzee..
 
Hizo index zenye matokeo ya division zero na zile ambazo watahiniwa hawakufanya mtihani kabisa ni mkakati maalumu wa kuwaweka makusudi ili kutimiza lengo la kuongeza idadi ya ajira ambazo kimsingi ni fake hiyo yote ni kuupumbaza umma wa Mtanzania na uhuni wote huo ulianzia kwa jiwe na kama wataendelea hivo mama ataharibu sana.
 
ni changamoto ila nimegundua bora kutafuta pesa utengeneze connections, ufanye investment ili upate urahisi wa watoto kuajirika pia😀🙏
Bodi ya Mikopo na hizi ajira za magumashi, zituamshe wazazi kuwaandalia watoto wetu miradi ya kuja kuisimamia baada ya kuhitimu masomo yao lakini pia kupatikakana kww ada ya kuwasomeshea vyuoni.

Katika hiyo orodha, huwezi kukuta watoto wa matajiri! Ni watoto wa Watanzania maskini pekee! Na bado wananyanyapaliwa! Yaani waombaji elfu 90, wanaajiriwa elfu 7 kasoro!

Halafu bado eti Wizara iliongeza muda zaidi kwa waombaji kuendelea kuomba hizo ajira! Kama siyo dharau ni nini hizi!!
 
Mkuu mimi ninachojua mtu siyo lazima aende chuo direct. Kuna kumaliza form six halafu mtu anakaa kwanza nyumbani, chuo anaenda baadaye.


Kama hakufanya mtihani wa form 4 ataripoti vipi bila cheti?

💯
Mkaruka nadhani bado hujaelewa hoja yangu ni hivi kwa mwanafunzi aliyemaliza form four 2014 kama alienda direct ilibidi digrii yake ya kwanza ya ualimu aipate 2020 lakini wao inaonyesha wameipata 2019. Je ni chuo gani kinachotoa shahada ya ualimu kwa miaka miwili???
 
Binafsi yangu nimeona nijifukize tu na kujikinga na wimbi la tatu la coronya nimeshagundua bila mchongo hupati ajira
 
Hizo index zenye matokeo ya division zero na zile ambazo watahiniwa hawakufanya mtihani kabisa ni mkakati maalumu wa kuwaweka makusudi ili kutimiza lengo la kuongeza idadi ya ajira ambazo kimsingi ni fake hiyo yote ni kuupumbaza umma wa Mtanzania na uhuni wote huo ulianzia kwa jiwe na kama wataendelea hivo mama ataharibu sana.
Haya mambo nikafikiri yalikufa na mwendazake kumbe bado yapo..hehehe!! Mama awe makini sana asikubali uhuni huu wa kutafuta kiki na sifa za kisiasa kwenye mambo ya kitaifa
 
Kuna diploma iliyosahaulika diploma in secondary kwa masomo ya art 2015 hawajawai kuwekwa kwenye vigezo vya kuomba ajira tangu mwenda zake akiwepo mpaka sasa yaan vijana hawa wanateseka na kujiona labda hawakusoma serikal iliangalie hili.
 
Mnapotoa kasoro mkumbuke mambo mawili

Moja Kuna mtihani unaitwa qt five six kwa mwaka mmoja

Pili kuna mtu kupata zero na akareset mtihani

Mimi naona ha jalifikilia hilo
 
Kwa namna yoyote ile lazima kuna shida sehemu fulani..makosa yaliyoahinishwa hapo yanaonyesha udhaifu mkubwa kweny mfumo..pia inaonesha hakuna coordination kati ya taasisi zinazohusika na elimu pamoja na ajira..na kama hali itakuwa hivihivi uwezekano wa kuajiri watumishi hewa utakuwepo
 
Ajira hizi ni changamoto ukiachwa bila kuchaghuliwa unatafuta kasoro kwa wezako. Kubali matokeo subiria awamu nyingine unaweza ukachanghuliwa.
 
MHESHIMIWA WAZIRI SALAM
awali yote nipende kukupongeza kwa Kazi nzito unayoifanya Mheshimiwa Waziri Mungu akupe nguvu na hekima
Mheshimiwa Waziri utakapopata muda Tafadhari naomba upitie tena PDF ya ajira za walimu kuna mambo hayajakaa vizuri kiasi kwamba yamezusha mjadala hususani sisi tuliokosa

Mheshimiwa Waziri
Kuna Mwalimu namba 4115 na Namba 4116 Christina Edward Luhunga Index number S2324-0013/2010 na S2324-0014/2010 Kapangwa Kigoma wilaya Kasulu Dc
Index number S2324-0023 Kapangwa Mayonga Sekondari na
S2324-0014 Kapangwa Nyakitonta Shule ya Sekondari
Mheshimiwa Waziri Mwalimu mwenye index number S2324-0014 huyu anaitwa Chuki Mtaki Lucas na kwa mjibu wa NECTA ana division zero point 35 akiwa na F Kwa Masomo aliyofanyia mitihani

Mheshimiwa Waziri mwingine ni Mwalimu namba 6571 NICHOLOUS DEUSDEDITH index number S0660-1409/2019 Mwalimu wa Physics na Biology Shida iko hapo kwenye taaluma yake Diploma yake ya ualimu kapata kwa wakati mmoja na Elimu ya Kidato cha Nne ? Na Kama ndiyo hivyo huo mfumo ulianza lini ?

Mheshimiwa Waziri mtu mwingine ni walimu Namba
5919 mwenye index number S4507-0035/2014
Namba 5857 index number S4166-0038/2014
Namba 5798 index number S1183-0035/2014
Namba 5791 index number S4463-0023/2014

Hao ni baadhi tu niliowaona mheshimiwa Hawa walimu ni walimu wa degree kwa Masomo yao
Mheshimiwa shida yangu na Hawa walimu ni kwamba wamemaliza Bachelor degree of education 2019 kitu ambacho siyo ukweli

Kwani walimu Hawa 2015 -2016 ni Kidato cha tano
2016 - 2017 ni Kidato cha sita

CHUO
Mwaka wa kwanza ni
2017- 2018
Mwaka wa pili
2018-2019
Mwaka wa tatu
2019-2020

Maana yake ni kwamba ofisi inatudanganya sisi kuwa Hawa watu wamemaliza Bachelor degree 2019 kitu ambacho siyo ukweli na hakuna Tanzania hii degree ya miaka miwili Mheshimiwa Waziri naomba uliangalie hilo

Kwa mjibu wa professor Karibu mkuu amesema wamechukua mwisho 2019 sasa hao wanatafuta nini ?

Mheshimiwa Waziri naomba hilo suala liangaliwe upya Watu tunakosa fursa kumbe Kuna watu wanapeana tu kindugu

Naomba kuwakilisha

Nategemea feedback mheshimiwa Waziri
Five six mwaka mmoja mkuu
 
Back
Top Bottom