kwanza hakikisheni umeme haukati ovyo ovyo!
kwa wastani umeme hukatika mara 4 kwa wiki ni sawa na wastani wa masaa 16 kwa mwezi, unaweza kupata jawabu la hasara tunayopata haswa kwa wenye viwanda vidogo. tasco tanescoo!!!
 
kwanza hakikisheni umeme haukati ovyo ovyo!
kwa wastani umeme hukatika mara 4 kwa wiki ni sawa na wastani wa masaa 16 kwa mwezi, unaweza kupata jawabu la hasara tunayopata haswa kwa wenye viwanda vidogo. tasco tanescoo!!!
Eneo gani na namba yako ya simu mpendwa mteja,je huwa unapata taarifa zetu za kazi ya uboreshaji miundombinu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza niwashukuru kwa kujizatiti na kuamua kufungua akaunti ili kurahisisha zaidi huduma na kuwafikia watumiaji.
Mimi ni mkazi wa Temeke kata ya Buza mtaa wa kwa lulenge lakini hapa mtaani kwetu kuna shida kubwa sana ya kukatika umeme pasipo kua na sababu za msingi. Weekend tunakosa umeme siku nzima jumamosi na jumapili ukiuliza vipi kuna mgao? Majibu ni hakuna. Mpaka hivi sasa tupo njia panda. Kila siku ni lazima umeme ukatike lakini mbaya zaidi ni eneo la mitaa ya kwa lulenge tu lakini maeneo ya jirani huduma wanaendelea kupata kama kawaida. Hili tatizo ni la muda mrefu takribani miezi 4 sasa. Tunaomba ufafanuzi chanzo cha tatizo ni nn? Alafu pili marekebisho ya kulitatua hili tatizo yatafanyika lini? Na tutegemee yatachukua muda gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
Tunaomba namba yako ya simu mpendwa mteja,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
*TAARIFA KUHUSU DAWATI LA DHARURA MBAGALA*

Tunawaomba ndugu wateja wetu unapokuwa na suala la dharura, au kupata taarifa ya kukosekana kwa umeme, kutokea kwa hitilafu ya umeme katika eneo lako, na mengineyo.

Tafadhali usisite kuwasiliana na *Dawati la dharura TANESCO Mbagala* kwa namba za simu zifuatazo:
+255 714 073 588
+255 786 975 538
Au
Kituo cha miito ya simu TANESCO makao makuu:
+255 768 985 100
+255 22 219 4400

Tunawaomba mzingatie hilo ili muweze kupata taarifa kwa wakati kutokana na wakati mwingine kutokuwepo online kwa muda kutokana na mujukumu ya wakati huo.

*Imetolewa Na:*
Ofisi ya uhusiano
TANESCO Mbagala

TANESCO "Tunayaangaza maisha"
 
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani tarehe 20/8/2017 amefanya ziara katika Kituo cha Kupozea Umeme cha KIA mkoani Kilimanjaro kinachotoa Umeme wa kiasi cha megawati 18.

Kituo hicho kilijengwa chini ya Mradi wa TEDAP uliohusisha ujenzi wa Transfoma mbili zenye uwezo wa MVA 20 kila moja pamoja na jengo la kuendeshea mitambo ambapo Kituo kinasambaza umeme kwa wateja kupitia njia 6 za msongo wa kilovoti 33.

kituo hicho kilikamilika mwaka 2014 na kuimarisha upatikanaji wa umeme katika mikoa ya Kilimanjaro na Arusha.

Kwa kuwa utekelezaji wa Mradi huo wa KIA ulienda sambamba na ujenzi wa vituo vya kupozea umeme vya Mbagala na Kurasini, Dkt Kalemani aliwataka watendaji wa TANESCO kuhakikisha kuwa vituo hivyo navyo vinakamilika haraka ili kuboresha upatikanaji wa Umeme katika Jiji la Dar es Salaam.

Mradi wa TEDAP chini ya Wizara ya Nishati na Madini unahusisha Ujenzi wa njia za kusafirishia umeme wa msongo wa kilovolti 132, ujenzi wa vituo vitano vya kupozea umeme jijini Dar es salaam pamoja na Kituo cha kupozea Umeme cha KIA.
6fd17396439291b0eb28ab70e3289a78.jpg
3adf3accc46f2d810f66659c7275201a.jpg
a4f869fa382786407e3bcd21f51ee946.jpg
3ef14ec10f366875fe262fd4391334cd.jpg


TANESCO "Tunayaangaza maisha"
 
Tarif 1 wanaotumia umeme chininya 75 unitd kwa mwezi na zaidinya hapo mpaka 7500 units ni tarif 1
Nilikuwa tarif 4,Julai mwaka jana nikarudishwa tarif 1 kwa kuwa nilikuwa nanunua umeme wa sh.10,000 kwa mwezi. Nilienda ofisi za TANESCO mkoa,nikaambiwa nitarudishwa tarif 4 na system. Lakini ni zaidi ya mwaka sasa sijarudishwa tarif 4 japo matumizi yangu kwa mwezi ni chini ya unit 75. Je,nifanye nini kurudishwa tarif 4?
 
Nilikuwa tarif 4,Julai mwaka jana nikarudishwa tarif 1 kwa kuwa nilikuwa nanunua umeme wa sh.10,000 kwa mwezi. Nilienda ofisi za TANESCO mkoa,nikaambiwa nitarudishwa tarif 4 na system. Lakini ni zaidi ya mwaka sasa sijarudishwa tarif 4 japo matumizi yangu kwa mwezi ni chini ya unit 75. Je,nifanye nini kurudishwa tarif 4?
Sheria inakutaka ununue umeme wa tsh 9150 ambao ninujit 75 kwa mwezi wewe ulikuwa unanunua unit 77 hivyo ulivuka takwa hilo na sasa upo tarif inayoendana na matumizi yako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shirika la Umeme Tanzania - (Tanzania Electric Supply Company Limited - TANESCO), Tunaomba mtupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri kupitia huu uzi nasi tutawajibu.

Tunawaomba mzingatie yafuatayo ili kurahisisha ufafanuzi na ufumbuzi wa tatizo au taarifa husika;

1.ENEO HUSIKA

(Mnaweza kuwa eneo moja lakini mnahudumiwa na transfoma au njia ya kusambaza umeme (feeder) tofauti)

2.NAMBA YA SIMU

(Wakati mwingine umeme upo kote isipokuwa kwako hivyo na rahisi kuwasiliana na wewe)

3.KARIBU NA NINI

(Kuna alama vitu au watu mashuhuri karibu na eneo lako mfano ofisi ya Serikali ya Mtaa, Mahakama, Kituo cha Polisi nk)

4.JINSI YA KUFIKA MAKAZI YAKO

(Toa ufafanuzi wa jinsi ya kufika makazi yako,chukulia unamuelekeza mtu ambaya hajawahi kufika kabisa)

5.MKOA,WILAYA NA KITONGOJI/KIJIJI

(Taarifa hii ni muhimu sana kusaidia kubaini eneo husika lipo wapi kwani yapo maeneo yanayofanana kwa majina lakini yapo Mikoa tofauti mfano Magomeni ipo Dar es Salaam na Mkoa wa Mtwara pia.)

6.KAMA NI TATIZO LA MITA NINI KINATOKEA UKIWEKA UMEME

(Kila mita ina ujumbe wake unaoashiria kitu fulani hivyo kubainisha ujumbe kunamsaidia mpokea taarifa kukupatia maelezo sahihi mfano mita namba 24339173921 inaonyesha error 77)

7.KAMA NI KUSHINDWA KUNUNUNUA UMEME UNAPATA UJUMBE GANI NA UNANUNUA KWA NJIA GANI

(Ujumbe huu ni muhimu sana kuweza kubaini chanzo cha tatizo pamoja na njia iliyotumika kununulia umeme mfamo Mpesa, Tigopesa, Maxcom nk)

TUNAENDELEA KUWASIHII WATEJA WETU KUZINGATIA UTOAJI WA TAARIFA SAHIHI NA FASAHA KWA HUDUMA BORA ZAIDI KUTOKA TANESCO.

ENDELEA KUFURAHIA HUDUMA BORA KUTOKA TANESCO

Kw mawasiliano Kituo cha Miito ya Simu (+255) 22194400 or (+255) 768 985 100 Mitandao ya kijamii Tanescoyetu (@tanescoyetu) | Twitter Facebook: Tanesco Yetu

HAPA CHINI NI NAMBA ZA SIMU ZA MIKOA

Ofisi ya Mkoa wa Mbeya Simu ya Mkononi (+255) 757 529 380 ya Mezani (+255) 252 504 219

Ofisi ya Mkoa wa Ilala Simu ya Mkononi (+255) 784 768 586 ya Mezani (+255) 222 133 330

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kusini (Magomeni) Simu ya Mkononi (+255) 715 271 461/ (+255) 784 271 461

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kaskazini (Mikocheni) Simu ya Mkononi (+255) 784 768 584 / (+255) 716 768 584 ya Mezani (+255) 222 700 367/ (+255) 222 701 602 / (+255) 222 774 098

Ofisi ya Mkoa wa Temeke Simu ya Mkononi (+255) 712 052720 / (+255) 758 880155 / (+255) 732 997361

Ofisi ya Mkoa wa Pwani Simu ya Mkononi (+255) 78 5122020 / (+255) 65 7108782ya Mezani (+255) 23 2 402 386

Ofisi ya Mkoa wa Arusha Simu ya Mkononi (+255) 75 8 174 343 Mezani (+255) 272 506 110

Ofisi ya Mkoa wa Tanga Simu ya Mkononi (+255) 658 122 412/ (+255) 687 677 667 Mezani (+255) 27 2 646 779

Ofisi ya Mkoa wa Kilimanjaro Simu ya Mkononi (+255) 765 397 925/ (+255) 682 771 310 Mezani (+255) 272 755 007/8

Ofisi ya Mkoa wa Manyara Simu ya Mkononi (+255) 689 795 599 / (+255) 75 9 534 130 Mezani (+255) 272 530 590

Ofisi ya Mkoa wa Mwanza Simu ya Mkononi (+255) 759 777 786 / (+255) 687 910 202 Mezani (+255) 282 501 060 / (+255) 282 500 090

Ofisi ya Mkoa wa Geita Simu ya Mkononi (+255) 744 085 696 Mezani (+255) 28 2520330

Ofisi ya Mkoa wa Kagera Simu ya Mkononi (+255) 78 5 787 898 / (+255) 75 3 120 701 Mezani (+255) 282 220 061

Ofisi ya Mkoa wa Mara Simu ya Mkononi (+255) 762 165 087 / (+255) 732 985 672

Ofisi ya Mkoa wa Simiyu Simu ya Mezani (+255) 282 700 180

Ofisi ya Mkoa wa Dodoma Simu ya Mkononi (+255) 782 161 643 Mezani (+255) 262 321 728

Ofisi ya Mkoa wa Morogoro Simu ya Mkononi (+255) 68 4889272 / (+255) 65 4829046 Mezani (+255) 232 613 501/2

Ofisi ya Mkoa wa Singida Simu ya Mkononi (+255) 71 4 477 445 / (+255) 732 960 924 / (+255) 689 373 757 Mezani (+255) 262 502 133

Ofisi ya Mkoa wa Tabora Simu ya Mkononi (+255) 786 558 510 / (+255) 763 162 868

Ofisi ya Mkoa wa Shinyanga Simu ya Mkononi (+255) 754 521 070 Mezani (+255) 28 2762120

Ofisi ya Mkoa wa Kigoma Simu ya Mkononi (+255) 78 3720598 Mezani (+255) 28 2802668

Ofisi ya Mkoa wa Katavi Simu ya Mkononi (+255) 68 8345200

IMETOLEWA NA:- Ofisi ya Uhusiano

TANESCO Makao Makauu.

Vilevile pitia threads hizi kupata Maelezo ya ziada;

LUKU:Mfumo wenye Tija kwa Wateja na TANESCO

Fahamu mita za LUKU zinazofungwa majumbani

Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO
habari za kazi
nina swali moja kidogo hivi nikitaka kuvuta umeme kwenye nyumba yangu nini haswa mnahitaji kutoka kwangu kama mteja mtarajiwa? mnafanya vipi na watu wa ardhi kuhusu kupeleka umeme sehemu zilizopimwa na ambazo hazijapimwa?

vipi kuhusu maeneo ambayo hayatakiwi kujengwa au yaliyojengwa kwenye hifadhi ya barabara,mito nakadhalika kwani ni mnapeleka umeme?
 
habari za kazi
nina swali moja kidogo hivi nikitaka kuvuta umeme kwenye nyumba yangu nini haswa mnahitaji kutoka kwangu kama mteja mtarajiwa? mnafanya vipi na watu wa ardhi kuhusu kupeleka umeme sehemu zilizopimwa na ambazo hazijapimwa? vipi kuhusu maeneo ambayo hayatakiwi kujengwa au yaliyojengwa kwenye hifadhi ya barabara,mito nakadhalika kwani ni mnapeleka umeme?
Ukitaka umeme kwanza hakikisha nguzo za kusambaza umeme zimefika eneo lako kisha mtafute mkandarasi aliyesajiliwa akufanyia kazi ya kutandaza nyaya ndani ya nyumba yako (wiring) kisha uje na kitambulisho utapewa fomu bure ofisi yeyote ile hapa nchini kisha tutakufanyia vipomo ( survey) na kukuambia kwa barua ulipe kiasi gani, ukilipa unafungiwa


Kuhusu maeneo yasiyopimwa , Utaratibu upo wazi kwa kuwa maeneo mengi nchini hayajapimwa tukisema hiki kiwe kigezo umeme utatembea maeneo machache sana utakubaliana nasisi hata hapa Dar es Salaam maeneo kama kimara na Mbezi Luis ndio yanapimwa saivi hivyo huduma inaenda kwa wateja huku upimaji ukiendelea.


Kuhusu maeneo yasiyotakiwa kujengwa, ikumbukwe kuwa maeneo ambayo hayajapimwa ni ngumu sana kusema hapa hapafai kujenga au laa na tungeongeza kigezo kuwa ukitaka umeme uende aridhi kwanza nadhani ungeona mlolongo wa malalamiko na ucheleweshaji wa huduma.aitha maeneo ambayo hayapaswi kujenga yakibainiswa na wahusika sisi tunaondoa miundombinu yetu mara moja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sheria inakutaka ununue umeme wa tsh 9150 ambao ninujit 75 kwa mwezi wewe ulikuwa unanunua unit 77 hivyo ulivuka takwa hilo na sasa upo tarif inayoendana na matumizi yako

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwahiyo natakiwa kufanya nini ili nirudi tarif 4? Maana matumizi yangu ni chini ya unit 75. Au ndo siwezi kurudishwa tena tarif 4?
 
Karibu TANESCO Masasi mkoa wa Mtwara kwa msaada wa dharura wasiliana nasi kwa namba 0789999924 tutakuhudumia

2f95afe2d98bde93e858d90a65bac1e0.jpg
21778b8819300fb69faae055b8a1b5c1.jpg
d1638f76aa0754ad656f13d990de7d20.jpg
7eea797f84c64c74d4829765d3b5ef2e.jpg


TANESCO "Tunayaangaza maisha"
 
Uzinduzi wa miradi ya REA III mkoa wa Mtwara wilaya Namyumbu


c604decf7cae4f07a62e9b8055d6a249.jpg
243462255a2c6a5dd51fb012135351c2.jpg
7fdaa70d6fc36a8d4691b61b68bd0765.jpg
7cb799ebd814957351528c1fed137e2e.jpg
568d49683e3a50ae82c9710901188357.jpg
 
Tanesco, kiukweli nimefadhaika sana baada ya kufata process zote za kufungiwa umeme na baadae kukamilisha malipo
Baada ya kutajiwa gharama na kukamilisha malipo ndani ya siku iyo iyo na kungojea kufunguwa umeme ndani ya siku 30 za kazi badala yake imegeuka kuwa kero tu,

badala ya kupewa huduma yangu stahiki naambiwa nisubiri mpaka pale vitu vitakapopatikana wakati siku 30 zimeshayoyoma mnanitumia sms za kukatisha tamaa kabisa

Mbona wakati mnachukua pesa yangu imeingia faster kwenye account yenu ila umeme kwangu ndo imekuwa kero kiasi ichi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ndio sms yenu mmenitumia kwenye simu yangu

HABARI NDUGU MTEJA TUNAOMBA RADHI KWA KUKUCHELEWESHEA KUPATA HUDUMA YA KUUNGANISHIWA UMEME, KUTOKANA NA UHABA WA VIFAA. TUNAFANYIA KAZI SUALA HILI PINDI TUTAKAPO PATA VIFAA TUTAKUPIGIA SIMU KWA AJILI YA KUKUJENGEA! ASANTE KWA KUWA MILIVU.. NI SHIRIKA LA UMEME TANESCO KINONDONI KUSINI [MBEZI].

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ndio sms yenu mmenitumia kwenye simu yangu

HABARI NDUGU MTEJA TUNAOMBA RADHI KWA KUKUCHELEWESHEA KUPATA HUDUMA YA KUUNGANISHIWA UMEME, KUTOKANA NA UHABA WA VIFAA. TUNAFANYIA KAZI SUALA HILI PINDI TUTAKAPO PATA VIFAA TUTAKUPIGIA SIMU KWA AJILI YA KUKUJENGEA! ASANTE KWA KUWA MILIVU.. NI SHIRIKA LA UMEME TANESCO KINONDONI KUSINI [MBEZI].

Sent using Jamii Forums mobile app
Si ushukuru hata umepewa taarifa mkuu? Wangekaa kimya je
 
Back
Top Bottom