Sophia Simba ambwaga Anne Kilango uenyekiti UWT

Sophia Simba ambwaga Anne Kilango uenyekiti UWT

Ukisikia mtu wa CCM kaibuka kidedea ujue amemzidi mwenzake kwa rushwa na mizengwe tu.Huko hakuna kidedea wa siasa za kistaarabu wala hoja.

Ukisikika mtu kaibuka kidedea Chadema jua fika baba mkwe Mtei kaweka zengwe!

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Lowasa kanunua nchi nzima viongozi wa ccm muulize Sumaye
 
A road to Damascus.... CCM is Lowassa & Lowassa is CCM.... Thats it... JOB DONE.... Sasa ili Lowassa asiwe RAIS wa nchi hii ni either augue UPUNGUFU wa AKILI (WEHU) au AFARIKI........ Otherwise jamaa ndo hivyo tena... hakuna ubishi... Kifupi ni kuwa jamaa yupo Barabara Shaaban Robert (maeneo ya Shule ya Bunge) anapiga Jaramba aingie Magogoni kama PREZDAA...Chezea Pesa nini!!!!
 
Jaman huyu mama akiwa tena mwenyekiti hakika ccm imekufa. Hana sifa za uwongozi na hatuwez kuanika kwanin hafai ila anabebwa kwa manufaa yawanao mbeba. Ila tisubiri cc ya J. K.
 
Huu ndio ulikuwa msimamo wangu kuhusu Uchaguzi wa UWT kwenye uzi wangu huu Uenyekiti wa UWT: Ni Vita Kati ya Ukweli na Ubatili!

Wanabodi,
Kipenga cha kugombea nafasi ya Uenyekiti wa UWT kimepulizwa na wa kwanza kukimbilia fomu ni Mwenyekiti wa sasa Mhe. Sofia Simba akijiaminisha atapata kwa mteremko wa kupita bila kupingwa maana CCM inatawaliwa na nidhamu ya woga kwa jina la "utii". Lakini hali haikuwa hivyo kwani Mhe. Mama Anne Kilango Malecela ametia timu kumpinga Mama Simba ambae "she is good for nothing"!. Mama Kilango ni just an opportunist mpiga kelele kila anapoongea as if ana uchungu wa kweli na anachopigia kelele!.

Ila kumlinganisha na mama Simba, Kilango ni mpiganaji wa kweli kwani baada ya kubebwa pale mwanzoni, sasa amejibeba na kubebeka zaidi wakati Simba yeye ni kubebwa tuu mwanzo mwisho!.

Leo kuna binti kijana, msomi wa haja ambaye yuko very bright upstairs kwa jina la Bi. Mayrose Kavura Majinge, naye atatupa karata yake!. Huyu ni "very promising" kuibadili UWT toka hapo ilipo na kuipaisha to the next level!.

Sasa subirini tushuhudie sarakasi za kama CCM inaendelea kuchagua "good for nothing" na kuisindikiza rasmi kaburini, au wana CCM wata opt for "oportunistic" ili kuendeleza ulaji na kupeana au this time watachagua "promising leadership" kujaribu kuiokoa CCM ambayo imeshaonyesha dalili zote za mkao wa kifo?!.

Kwa vile sio siri, its open secret kuwa members wengi wa jf ni washabiki wa CDM, wakiwa na matumaini kuwa 2015 its their time, wajue kuwa wapiga kura wengi zaidi Tanzania ni wanawake, I doubt kama BAWACHA does realy exist!, hivyo majaaliwa ya Chadema kushinda uchaguzi wa 2015, itategemea kura za wanawake hivyo ni nani anashinda uchaguzi wa UWT!. Akirudi Mama Simba au Mama Kilango, ushindi wa Chadema ni dhahiri, ila akishinda Mayrose Kavura!, amini msiamini, ikulu mtaishia kuisikia tuu!.
Mark my words!.

Pasco!.

NB. Kwa vile mimi namshabikia EL ateuliwe CCM, na kwa CDM naisupport move ya ZZK, bado nasisitiza sina chama!. Ila wale mnao amini mimi ni gamba, endeleeni kuamini hivyo kwa sababu kuwa mwana CCM sio dhambi wala kuishabikia CCM sio kosa!.
Uchaguzi umemalizika matokeo yametoka!, ubatili umeshinda!. Sasa tuendelee na mengine huku tukisubiria yatokanayo!.
 
Nilifikiri CCM is dying?
na kwambayeyote ndani ya CCM hawezi kuwa tishio?

sasa mbona watu wako busy na Mwenyekiti wa UWT na sio BAWACHA?

au hii ni ishara ya CCM kuwa ni very strong?
 
Kwa mujibu wa vyanzo vya uhakika mhe Anna Kilango aliyepigiwa chapuo na mhe Banji akambulia kuchambwa hajui siasa za chini, ambazo mhe Sophia hakuzifafanua na juzijuzi wamempa nafasi awawakilishe ubunge wa Africa mashariki baada ya kuulizwa ana mikakati gani ccm ishinde 2015 wakati mpaka sasa amekuwa kiongoz wa umoja huo hamna alilofanya.

Licha ya majibu mepesi na kejeli na vituko ambapo alishuka meza kuu banji akaokolewa na watu wa usalama.

Habari za uhakika zinasubiri kutangazwa mhe Anna Kilango na Wapambe wake wakiwakilishwa na Mhe. Banji wameangukia pua wameshindwa. Ndivyo ilivyokuwa kwa mtoto au Mwanafamilia Willium Malechela "Lemutuz".

Wanabodi walimpa ushauri ndio uzuri wa jamii ukishinda hawakosi cha kusema na pia ukishindwa hawakubani mawazo.

Naomba mods msiiunganishe yamemfika na Mama wanajamvi tusiwanyime maoni, ushauri mawazo kwa huu upepo huu kwa familia ya Malechela na hata zecomed iliyoonyeshwa na Wagombea na Wapiga kura katika uchaguzi wa jumuiya hii ya Wanawake CCM.
 
Hakuna tunda bovu linaweza endelea kuwa mtini lazima lianguke
 
Kwa mujibu wa vyanzo vya uhakika mhe Anna Kilango aliyepigiwa chapuo na mhe Banji akambulia kuchambwa hajui siasa za chini, ambazo mhe Sophia hakuzifafanua na juzijuzi wamempa nafasi awawakilishe ubunge wa Africa mashariki baada ya kuulizwa ana mikakati gani ccm ishinde 2015 wakati mpaka sasa amekuwa kiongoz wa umoja huo hamna alilofanya.
Licha ya majibu mepesi na kejeli na vituko ambapo alishuka meza kuu banji akaokolewa na watu wa usalama.
Habari za uhakika zinasubiri kutangazwa mhe Anna Kilango na Wapambe wake wakiwakilishwa na Mhe. Banji wameangukia pua wameshindwa. Ndivyo ilivyokuwa kwa mtoto au Mwanafamilia Willium Malechela "Lemutuz"
Wanabodi walimpa ushauri ndio uzuri wa jamii ukishinda hawakosi cha kusema na pia ukishindwa hawakubani mawazo.
Naomba mods msiiunganishe yamemfika na Mama wanajamvi tusiwanyime maoni, ushauri mawazo kwa huu upepo huu kwa familia ya Malechela na hata zecomed iliyoonyeshwa na Wagombea na Wapiga kura katika uchaguzi wa jumuiya hii ya Wanawake CCM.


Kwahiyo WILLIAM MALECELA kaanguka PIA?
NI LINI TUTAPATA HABARI za UKWELI... Hii imekaa kiushabiki zaidi ya HABARI

Shy-ROSE kupata UBUNGE wa EA ni kushukuru kambi ya UPINZANI haswa CHADEMA ndio Waliompa kura za kufikia # 2; CCM wachache sana walimpigia KURA sio ZAIDI ya 25
 
Japo si mfuasi wao, naunga mkono kambi ya Lowasa.
 
lowassa in action towards 2015, mtasoma plate number.....
 
Nape amekiri kuwa mtu akijaza watu CC na NEC sio sifa ya kuwa mgombea urais. Embu tufanye utafiti tujue ni nani ambaye kambi yake ina watu wengi NEC na CC? Mimi sio mwanaCCM hivyo siwezi jua nani ni nani japo hisia zinanituma kuwa ni yuleyule ambaye Sophia Simba aliwahi kusema ndoo mwanaume kama yeye katika CCM
 
kama kweli mama Sofia SImba kaibuka kidedea, basi kura yangu toka moyoni aliipata. nampenda saana huyu mama kwa kuwa ni muwazi si mnafiki, kama wengine mama yuko straight kwenye maamuzi, ndugu zangu tukubaliane ktk chaguzi kama watu hawakutaki hata ukitoa fedha hupati ushindi fedha zinakwenda kwa waanaokupenda ukiona mtu anapiga kelele ujue fedha zake zimekataliwa au zimeliwa na yy kashindwa. jiulize Sofia huyu aliyempiga chini katibu wake kuwa hana uwezo wa kuongoza, Sofia huyu aliyewaambia wabunge wa kuteuliwa kupitia UWT mwisho vipindi viwili baada bya hapo waende kugombea kwenye majimbo ashinde kwa kutoa fedha ampe nani? kama katoa na zimepokelewa basi kwa wanaomkubali .
 
Nilifikiri CCM is dying?
na kwambayeyote ndani ya CCM hawezi kuwa tishio?

sasa mbona watu wako busy na Mwenyekiti wa UWT na sio BAWACHA?

au hii ni ishara ya CCM kuwa ni very strong?
You noted the knot. Be my guest!!
 
Nazungumza na jamaa yangu ndani ya uchaguzi wa UWT kwa kura zilizokwisha hesabiwa mama Sophia Simba anaelekea kuchukua ushindi, habari hii ni ya uhakika toka kwenye chumba cha kuhesabia kura, Anne Kilango anaponzwa na undumila kuwili wake mara anapinga ufisadi mara anametetea Ngereja , haeleweki, akina mama wamempa fundisho.

Nakala kwa william j Malecela
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom