Sophia Simba ambwaga Anne Kilango uenyekiti UWT

Nazungumza na jamaa yangu ndani ya uchaguzi wa UWT kwa kura zilizokwisha hesabiwa mama Sophia Simba anaelekea kuchukua ushindi, habari hii ni ya uhakika toka kwenye chumba cha kuhesabia kura, Anne Kilango anaponzwa na undumila kuwili wake mara anapinga ufisadi mara anametetea Ngereja , haeleweki, akina mama wamempa fundisho.
 
Huu ndio ulikuwa msimamo wangu kuhusu Uchaguzi wa UWT kwenye uzi wangu huu Uenyekiti wa UWT: Ni Vita Kati ya Ukweli na Ubatili!


quote_icon.png
By Pasco
Wanabodi,
Kipenga cha kugombea nafasi ya Uenyekiti wa UWT kimepulizwa na wa kwanza kukimbilia fomu ni Mwenyekiti wa sasa Mhe. Sofia Simba akijiaminisha atapata kwa mteremko wa kupita bila kupingwa maana CCM inatawaliwa na nidhamu ya woga kwa jina la "utii". Lakini hali haikuwa hivyo kwani Mhe. Mama Anne Kilango Malecela ametia timu kumpinga Mama Simba ambae "she is good for nothing"!. Mama Kilango ni just an opportunist mpiga kelele kila anapoongea as if ana uchungu wa kweli na anachopigia kelele!.

Ila kumlinganisha na mama Simba, Kilango ni mpiganaji wa kweli kwani baada ya kubebwa pale mwanzoni, sasa amejibeba na kubebeka zaidi wakati Simba yeye ni kubebwa tuu mwanzo mwisho!.

Leo kuna binti kijana, msomi wa haja ambaye yuko very bright upstairs kwa jina la Bi. Mayrose Kavura Majinge, naye atatupa karata yake!. Huyu ni "very promising" kuibadili UWT toka hapo ilipo na kuipaisha to the next level!.

Sasa subirini tushuhudie sarakasi za kama CCM inaendelea kuchagua "good for nothing" na kuisindikiza rasmi kaburini, au wana CCM wata opt for "oportunistic" ili kuendeleza ulaji na kupeana au this time watachagua "promising leadership" kujaribu kuiokoa CCM ambayo imeshaonyesha dalili zote za mkao wa kifo?!.

Kwa vile sio siri, its open secret kuwa members wengi wa jf ni washabiki wa CDM, wakiwa na matumaini kuwa 2015 its their time, wajue kuwa wapiga kura wengi zaidi Tanzania ni wanawake, I doubt kama BAWACHA does realy exist!, hivyo majaaliwa ya Chadema kushinda uchaguzi wa 2015, itategemea kura za wanawake hivyo ni nani anashinda uchaguzi wa UWT!. Akirudi Mama Simba au Mama Kilango, ushindi wa Chadema ni dhahiri, ila akishinda Mayrose Kavura!, amini msiamini, ikulu mtaishia kuisikia tuu!.
Mark my words!.

Pasco!.

NB. Kwa vile mimi namshabikia EL ateuliwe CCM, na kwa CDM naisupport move ya ZZK, bado nasisitiza sina chama!. Ila wale mnao amini mimi ni gamba, endeleeni kuamini hivyo kwa sababu kuwa mwana CCM sio dhambi wala kuishabikia CCM sio kosa!.



Uchaguzi umemalizika matokeo yametoka!, ubatili umeshinda!. Sasa tuendelee na mengine huku tukisubiria yatokanayo!.

P.​
......
......huyu Pasco yupo kweli
 
Asante Mungu, Pasco uwt tumeshamaliza kazi njia ya mtukufu Lowasa ni nyeupe sasa. Wapi Le Mutuz? Je Mzee Malecela ataendelea yeye mwanae kusema CCM itaendelea kutawala miaka 50 ijayo?
Hizi kauli bwana leo hii mnamuitaje?kweli gamba ni lilelile
 
Pasco, tangu siku ulipotoa posti thread hii nilikwambia namjua vema sana huyu uliyemuita msomi na mtu stahiki UWT Mayrose. Nilikwambia namjua fika ni dhaifu kupindukia. Ningeshangaa kama hata angekuwa wa pili. Kwa wagombea waliokuwepo wote watatu, hakukuwa na mtu muafaka kwa wanawake wa Tanzania, vyote ni vinyago vilivyokuwa vnachongwa tu na hatimaye kinyago kizuri kimevishinda vingine.

Lakini kwakuwa Mshindi Sofia simba yuko katika kambi yako ya EL, naomba nikupe hongera kwa niaba yake. Mnajiandaa vema kwa 2015
 
Hii kauli yako hii.Kama vigezo vilivyotumika ambavyo viliwekwa wazi kabisa vilijikuta vimeelekeza kupitishwa dada,wake na hata vimada wa vigogo basi hao ndiyo wanaofaa.Huwezi kukubali vigezo halafu ukakataa matokeo yaliyotokana na vigezo!
Ben 1400
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom