Serikali kutumia kigezo cha kupitia JKT ili kupata nafasi za kazi wakati si vijana wote huchaguliwa kujiunga na JKT ni ubaguzi wa wazi

Kumekuwa na tabia za hivi karibuni, kwamba ili upate nafasi za kazi kwa vyombo vya ulinzi na usalama, mojawapo ya sifa ya waombaji ni kupitia mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa. Huu ni ubaguzi wa wazi kabisa.

Hivi toka lini vijana wote waliohitimu kidato cha sita waliitwa wote kujiunga na jeshi la kujenga Taifa? Ina maana hata wale ambao hawakuchaguliwa kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa, pasipo hiari yao, wameondolewa sifa za kuwa watumishi wa vyombo hivi vya Ulinzi na Usalama.

Kufanya kigezo cha kupitia mafunzo ya JKT kama moja ya sifa ya kupata kazi Polisi, Magereza, Uhamiaji na TAKUKURU ni ubaguzi wa wazi kwa watu ambao hawakuchaguliwa kujiunga na vyombo hivyo na pia ni mwendelezo wa upendeleo kwa watu waliopendelewa kujiunga na kozi hizi za JKT.
Naunga mkono hoja
 
Afrika bado kuna ujinga mwingi Sana baada ya kupata uhuru miaka ya 1960s bado watu wanatumia sifa primitive kabisa za kupata ajira mfano sifa moja wapo ya askari wa kikoloni ilikuwa kutojua kusoma na kuandika Leo hii sifa ya kuwa police lazima uwe umefeli 4m 4

60% ya viongozi waliopo serikalini Wana uwezo mdogo"Prof Assad
 
Uzalendo unafundishwa
Acha kukariri mkuu kwamba uzalendo unafundishwa.Mataifa ya ulaya hakuna habari za jkt kama huku kwetu lakini watu wanazipenda nchi zao kutoka mioyoni mwao na ufisadi aidha hakuna kabisa ama kwa asilimia chache.

Huku Africa ufisadi ni mkubwa sana na ndo tunaolazimisha watu wakajifunze uzalendo.Uzalendo upo moyoni mwa mtu sio
ufundishwa.
 
Acha kukariri mkuu kwamba uzalendo unafundishwa.Mataifa ya ulaya hakuna habari za jkt kama huku kwetu lakini watu wanazipenda nchi zao kutoka mioyoni mwao na ufisadi aidha hakuna kabisa ama kwa asilimia chache.

Huku Africa ufisadi ni mkubwa sana na ndo tunaolazimisha watu wakajifunze uzalendo.Uzalendo upo moyoni mwa mtu sio
ufundishwa.
Wanafundishwa shule kuipenda nchi yao,historia yao,akina milambo wao,utamaduni wao,hawawi wazalendo from no where,hapo isike humjui,abushiri humjui,gen mayunga humjui,twalipo humjui
 
Wanafundishwa shule kuipenda nchi yao,historia yao,akina milambo wao,utamaduni wao,hawawi wazalendo from no where,hapo isike humjui,abushiri humjui,gen mayunga humjui,twalipo humjui
Mbona blaah blah nyingi mkuu.Jibu swali kama uzalendo unafundishwa mbona ufisadi hauishi tena watu wanaiba mchana kweupe.

Mbona hata sisi tunafundishwa kuhusu ukasiri wa kina Mkwawa,Isike,Mirambo nakadhalika lakini wizi na ufisadi haviishi.
 
Ndomana mkatakiwa muende,sababu mmepitia malezi ya kibwege Sana,mmelegea,Hamna nidhamu,Hamna uzalendo
Hivi watu wengine huwa mnaelewa mkilewa au? Mleta mada kasema Wazi si vijana wote wanaohtimu form 6 wanachaguliwa kwenda JKT. Kwa hiyo kutumia dhana hiyo kama kigezo muhimu ni ubaguzi, halafu wewe unakuja unasema nendeni JKT utafikiri kwenda huko Mtu anajipeleka.
 
Kumekuwa na tabia za hivi karibuni, kwamba ili upate nafasi za kazi kwa vyombo vya ulinzi na usalama, mojawapo ya sifa ya waombaji ni kupitia mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa. Huu ni ubaguzi wa wazi kabisa.

Hivi toka lini vijana wote waliohitimu kidato cha sita waliitwa wote kujiunga na jeshi la kujenga Taifa? Ina maana hata wale ambao hawakuchaguliwa kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa, pasipo hiari yao, wameondolewa sifa za kuwa watumishi wa vyombo hivi vya Ulinzi na Usalama.

Kufanya kigezo cha kupitia mafunzo ya JKT kama moja ya sifa ya kupata kazi Polisi, Magereza, Uhamiaji na TAKUKURU ni ubaguzi wa wazi kwa watu ambao hawakuchaguliwa kujiunga na vyombo hivyo na pia ni mwendelezo wa upendeleo kwa watu waliopendelewa kujiunga na kozi hizi za JKT.
Ila kiukweli, kama Nchi tunatatizo kubwa sana la watoa maamuzi. Kuna watu wamewekwa ktk nafasi mbalimbali za maamuzi, lakini ni zero kabisa. Sijui hili tatizo litakwisha lini...mie sijui.....
 
Mimi sikuchaguliwa jkt lakini nilijipeleka pale kanembwe wakanipokea Kwa mikono miwili Na posho nkawa Napokea kama kawaida....Ni uzembe wako kutoenda jkt wazi?
 
Hivi watu wengine huwa mnaelewa mkilewa au? Mleta mada kasema Wazi si vijana wote wanaohtimu form 6 wanachaguliwa kwenda JKT. Kwa hiyo kutumia dhana hiyo kama kigezo muhimu ni ubaguzi, halafu wewe unakuja unasema nendeni JKT utafikiri kwenda huko Mtu anajipeleka.
Una uhakika so vijana wote huenda jkt
 
Back
Top Bottom