Licha ya kwenda JKT wizi wa mali za umma ndio umeshamiri zaidi

Nyamesocho

JF-Expert Member
May 5, 2023
476
1,244
Serikali ilianzisha utaratibu wa vijana kujiunga na Jeshi la kujenga Taifa (JKT) pamoja na malengo mengine ilikuwa kuwajengea vijana moyo wa uzalendo na kuipenda nchi yao na kuwa vijana wa kujituma, waadilifu wenye nidhamu na kujitolea kuisaidia jamii.

Lakini ni tofauti sana licha ya watanzania wengi kupitia JKT na kupata mafunzo ya uzalendo kwa nchi yake ndo wizi wa mali za umma umekithiri zaidi na mbaya zaidi wanaohusika ndo walipata mafunzo ya JKT.

Uadilifu na uzalendo wa mtu hutabadilishwa na JKT hata siku moja bali kwenye jamii alipokulia.

Mtanzania hawezi kuwa mzalendo kama alikulia kwenye mazingira yafuatayo;

1. Alipokuwa mtoto alikuwa anadokoa vitu, madaftari ya wanafunzi, nyumbani na mtaani na mbaya zaidi jamii wakimfuatilia wazazi wake humkingia kifua, usitegemee JKT itambadilisha tabia.

2. Kama amekulia mazingira ya umimi, hali ya kutothamini watu wengine haikuwepo usitegemee JKT itambadilisha.

3. Alisoma shule zaidi ya 4 kwa sababu ya nidhamu usitegemee JKT itambadilisha.

4. Kama shule ya msingi na sekondari alikuwa na kiburi na akipewa adhabu wazazi wake wanakuja juu usitegemee JKT itambadilisha.

5. Viboko vitembee kwa wanafunzi visipotembea usifikiri JKT itambadilisha tabia.

Ushauri kwa serikali, inapoajiri iangalie pia historia ya utotoni msingi na sekondari.
 
Wivu huo acha upuuz wewe
Naona umenyimwa asali una lia lia
Shaur yako komaa ulambe asali kwanza
Kila mtu apambane na hali yake

Ngoja nichukue buyu langu la asali
255627593160_status_953b1dcddec5412e9e8e18e3572b884d.jpg
 
JKT ni mateso na karaha tupu, tena kwa wasio na wito wa mambo ya Jeshi ni mzigo na upotevu wa muda tyuuh.

Sijaona umuhimu wake, miezi 3 nilipoteza buree tyuuh.
Hata huo uzalendo unakuwepo ukiwa kambini, ukishatoka bas kila kitu kwishney.

Labda kuna 7bu zingne za msingi, zaidi ya uzalendo.
 
JKT ni mateso na karaha tupu, tena kwa wasio na wito wa mambo ya Jeshi ni mzigo na upotevu wa muda tyuuh.

Sijaona umuhimu wake, miezi 3 nilipoteza buree tyuuh.
Hata huo uzalendo unakuwepo ukiwa kambini, ukishatoka bas kila kitu kwishney.

Labda kuna 7bu zingne za msingi, zaidi ya uzalendo.
Mkuu wew umewahi kuhudhuria mafunzo hayo,vipi kuna moduli yoyote ya wizi wa mali za umma maana sasa hivi ni hatari zaidi
 
Serikali ilianzisha utaratibu wa vijana kujiunga na Jeshi la kujenga Taifa (JKT) pamoja na malengo mengine ilikuwa kuwajengea vijana moyo wa uzalendo na kuipenda nchi yao na kuwa vijana wa kujituma, waadilifu wenye nidhamu na kujitolea kuisaidia jamii.

Lakini ni tofauti sana licha ya watanzania wengi kupitia JKT na kupata mafunzo ya uzalendo kwa nchi yake ndo wizi wa mali za umma umekithiri zaidi na mbaya zaidi wanaohusika ndo walipata mafunzo ya JKT.

Uadilifu na uzalendo wa mtu hutabadilishwa na JKT hata siku moja bali kwenye jamii alipokulia.

Mtanzania hawezi kuwa mzalendo kama alikulia kwenye mazingira yafuatayo;

1. Alipokuwa mtoto alikuwa anadokoa vitu, madaftari ya wanafunzi, nyumbani na mtaani na mbaya zaidi jamii wakimfuatilia wazazi wake humkingia kifua, usitegemee JKT itambadilisha tabia.

2. Kama amekulia mazingira ya umimi, hali ya kutothamini watu wengine haikuwepo usitegemee JKT itambadilisha.

3. Alisoma shule zaidi ya 4 kwa sababu ya nidhamu usitegemee JKT itambadilisha.

4. Kama shule ya msingi na sekondari alikuwa na kiburi na akipewa adhabu wazazi wake wanakuja juu usitegemee JKT itambadilisha.

5. Viboko vitembee kwa wanafunzi visipotembea usifikiri JKT itambadilisha tabia.

Ushauri kwa serikali, inapoajiri iangalie pia historia ya utotoni msingi na sekondari.
Kwa taarifa yako hata hao wakufunzi huko JKT ni kwakuwa hawako kwenye vitengo vya upigaji, lakini ukiwaaingiza kwenye maeneo ya upigaji utakuta na wao wanavua uzalendo wanavaa upigaji. Hakuna uzalendo boss Bali ni kukosa tu angle za upigaji.
 
Kwa taarifa yako hata hao wakufunzi huko JKT ni kwakuwa hawako kwenye vitengo vya upigaji, lakini ukiwaaingiza kwenye maeneo ya upigaji utakuta na wao wanavua uzalendo wanavaa upigaji. Hakuna uzalendo boss Bali ni kukosa tu angle za upigaji.
JkT ifutwe
 
Inaweza kubaki tu kama sehemu ya kutoa ajira, lakini ni wendawazimu kuamini Kuna uzalendo utapatikana kwa mtu kwenda JKT.
Sasa uzalendo ukajifunziwe wapi? Vyuo vya vyama vimeshindwa, jkt zimeshindwa, Dini zetu nazo zimeshindwa kutujengea uaminifu, shule zetu ndiyo usiseme kabisa! Sasa twende wapi? Wanafilosofia ebu tusaidieni.
 
Sasa uzalendo ukajifunziwe wapi? Vyuo vya vyama vimeshindwa, jkt zimeshindwa, Dini zetu nazo zimeshindwa kutujengea uaminifu, shule zetu ndiyo usiseme kabisa! Sasa twende wapi? Wanafilosofia ebu tusaidieni.
Kama wanaopaswa kuwa kioo kwenye jamii, wengi wao ndio wale wanaotoa maagizo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri kuiba Kura Kisha kuwatangaza Washindi. Baadae Washindi wale wakipata nafasi za Uwaziri unategemea nn zaidi ya Business as Usual?? Atakuwa na Uzalendo vipi kwa nchi yake ktk kulinda Mali za Umma?? Atakuwa na ubavu upi wa kumkea Mkurugezi wa Halmashauri kwenye matumizi Mabaya ya fedha za Umma zaidi ya kushirikiana nae kwenye wizi??

Uzalendo kwa Vijana waliopitia JKT uliishia miaka ya 92 kurudi nyuma. Walikuwa wakipewa kazi ya kulinda mgodi wanalinda kweli. Hawa wa sasa wanashirikiana na Wachimbaji kutorosha madini yetu. Uzalendo wao utatoka wapi hapo??
 
Back
Top Bottom